Unakumbuka Siku ile ya machozi...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Imepita miaka mingi na kumbukumbu zetu zimeanza kufifia; wengine hawana kumbukumbu kabisa lakini kwa wengine siku ile iko kama jana... kwa mara ya kwanza Tanzania bara ilimpoteza kiongozi wake wa kitaifa, na likawa pigo la kwanza kwa wananchi wa bara kumpoteza kiongozi wa juu wa kitaifa akiwa bado madarakani na bado inabakia ndio tukio pekee ingawa kama Taifa, lilitanguliwa na tukio la kuuawa kwa Karume.

Siku ile ya Alhamisi ya tarehe 12, 1984 ni siku ya kukumbuka kwa wengine machozi na kwa wengine siku ambapo yawezekana kabisa mafisadi walipojua kuwa huko mbeleni hakutakuwa tena na kiongozi hodari na jasiri kama yule. Mwaka mmoja baadaye Rais Nyerere alistaafu na mabadiliko makubwa yalitokea. Taifa likajikuta halina mtu kwenye uongozi wa juu mwenye uwezo wa kusimamia ukweli na kuwaambia viongozi wenzie ukweli...

Pamoja na mapungufu yake mengi na labda jazba kubwa ya kuwatafuta "wahujumu uchumi na walanguzi" alijijengea maadui au aligusa makasri yasiyoguswa; lakini hadi leo hii tukimlinganisha na waliokuja baada yake na viongozi wengine ni wazi kuwa bado anasimama kwenye kundi la peke yake.

Tunapoendelea na mapambano haya dhidi ya mafisadi najikuta leo nikikumbuka na kummiss Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine na nikiamini yaliyosemwa wakati ule kuwa "pengo aliloliacha haliwezi kuzibika". Yanayoendelea sasa nchini yanathibitisha kabisa kuwa watu kama Sokoine wanakuja mara moja kila nusu karne!

Mhe. Edward Moringe Sokoine... watu bado wanakukumbuka hasa wale wanyonge wa Taifa hili..
 
Yule Dereva pia aliyehusika nasikia anakana kabisa kabisa mpaka sasa kuwa hakuhusika alisingiziwa tu, hata yeye hakujua kilichotokea.

Madereva kwa kusingiziwa bwana!
 
Yule Dereva pia aliyehusika nasikia anakana kabisa kabisa mpaka sasa kuwa hakuhusika alisingiziwa tu, hata yeye hakujua kilichotokea.

Madereva kwa kusingiziwa bwana!

Ni kweli lazima akane Bwana. Unajua kilichompata Dr. Fupi wa Morogoro ambaye alifanya postmoterm? Hii ndiyo Tanzania, hata hivyo katika Tanzania hii tunao viongozi wenye uchungu halisi nanchi yao ambao kwasasa hatunao tena. Wish them RIP.
 
http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2007/04/12/88230.html][/url]

Edward Moringe Sokoine was a darling to all patriots because he was a great patriot, to all honest people because he was the most honest man, to all hard working people because he was himself the epitome of hard work, to all practical people because he was a man of few words. He was action-oriented. He wanted to see things done and done now, not tomorrow.

But Edward Moringe Sokoine was a terror to majambazi (bandits) because he hated them like poison, he was poison itself to embezzlers; and saboteurs feared him like death.

.


May God Almighty rest his soul in eternal bliss. Amen.
 


Dr Fupi alipatwa na nini?

Alipotaka kuandika report ya postmoterm kuwa alipigwa risasi hawa watu wausalama wakamlazimisha aandike kuwa amefariki kwa ajali. Kwa shingo upande akaandika kulingana na matakwa yao. Sasa ukitaka kujua yuko wapi sikia kama bado jina lake linatajwa kwamba kuna Dr Fupi. Alishabadilishwa jina siku nyingi katika mazingira ya kutatanisha si unajua tena TZ hiyo.
 
Kama aliwachukia kiasi kile wahujumu wa sukari,sabuni nk,sijui leo angekuwepo akawaona hawa wa EPA,Richmond,Kiwira nk na jinsi tunavyo washughulikia kishikaji nina hakika angejitoa uhai.
RIP MORINGE
 
Alipotaka kuandika report ya postmoterm kuwa alipigwa risasi hawa watu wausalama wakamlazimisha aandike kuwa amefariki kwa ajali. Kwa shingo upande akaandika kulingana na matakwa yao. Sasa ukitaka kujua yuko wapi sikia kama bado jina lake linatajwa kwamba kuna Dr Fupi. Alishabadilishwa jina siku nyingi katika mazingira ya kutatanisha si unajua tena TZ hiyo.


R.I.P. Edward Moringe Sokoine.
Kuna wengine walisema kuwa Prof. Philemon Sarungi alihusika pia kwenye postmoterm ya Sokoine, eti hili nalo ni kweli?
 
Alipotaka kuandika report ya postmoterm kuwa alipigwa risasi hawa watu wausalama wakamlazimisha aandike kuwa amefariki kwa ajali. Kwa shingo upande akaandika kulingana na matakwa yao. Sasa ukitaka kujua yuko wapi sikia kama bado jina lake linatajwa kwamba kuna Dr Fupi. Alishabadilishwa jina siku nyingi katika mazingira ya kutatanisha si unajua tena TZ hiyo.

Nahisi hapa unamaanisha kuwa walimsokoine pia
 
Tanzania tunachukulia mambo kirahisi rahisi tu. Sokoine, Karume, Kombe wamekufa lakini hakuna uchunguzi wa Serikali uliofanyika tukajua ilikuwaje kuwaje. Sijui kwa nini uongozi wa wakati huo uliona ni bora mambo yabaki siri mpaka kesho.
 
Na ndo maana hata viongozi wa UFISADI hakuna anayedhubutu kuwagusa, maana yeyote atakayeelekea kufanya mambo ya kutafuta haki na sheria kifo kinamyemelea kutoka kwa Mafisadi, na viongozi wengine wa serikali??

Sasa kifanyike nini jamani?
Mimi naona hapa solution pekee, ni kuanzisha vita jamani? Vita yenyewe, sio ya ukabila au udini kama zilivyo nchi zingine, ila ni vita kati ya wanyonge na Mafisadi, vita hii inalenga kuhakikisha kuwa mali zote za wananchi zinarudi mikononi mwa wananchi!! au mnasemaje wakuu, hivi hivi tutakaa kuongea tu mpaka basi, na hakuna kitakachofanyika kwa sababu hata kikwete anaogopa anaweza kuuliwa muda wowote, sasa ni sisi kuhakikisha mafisadi wote tunawamaliza na kuanza kuijenga Tanzania mpya jamani

Kumbe tulitekwa zamani? Hata kabla Mwalimu hajafariki?
 
Na ndo maana hata viongozi wa UFISADI hakuna anayedhubutu kuwagusa, maana yeyote atakayeelekea kufanya mambo ya kutafuta haki na sheria kifo kinamyemelea kutoka kwa Mafisadi, na viongozi wengine wa serikali??

Sasa kifanyike nini jamani?
Mimi naona hapa solution pekee, ni kuanzisha vita jamani? Vita yenyewe, sio ya ukabila au udini kama zilivyo nchi zingine, ila ni vita kati ya wanyonge na Mafisadi, vita hii inalenga kuhakikisha kuwa mali zote za wananchi zinarudi mikononi mwa wananchi!! au mnasemaje wakuu, hivi hivi tutakaa kuongea tu mpaka basi, na hakuna kitakachofanyika kwa sababu hata kikwete anaogopa anaweza kuuliwa muda wowote, sasa ni sisi kuhakikisha mafisadi wote tunawamaliza na kuanza kuijenga Tanzania mpya jamani

Hakika IKO SIKU BUBU WATASEMA, VIZIWI WATASIKIA NA MOTO UTAZIMWA KWA NJITI YA KIBIRITI.
 
Solution ya vita sio nzuri, watu wapewe uwezo wa kujua mabaya ya viongozi wao ili hata kama wakionga na pesa za EPA wasipigiwe kura. Tatizo ni sisi wapiga kura bado hatujaamua kuwatoa madarakani kwani wakionga sh. na sinia za pilau watanzania wanawapigia kura.
 
Solution ya vita sio nzuri, watu wapewe uwezo wa kujua mabaya ya viongozi wao ili hata kama wakionga na pesa za EPA wasipigiwe kura. Tatizo ni sisi wapiga kura bado hatujaamua kuwatoa madarakani kwani wakionga sh. na sinia za pilau watanzania wanawapigia kura.

Wananchi wetu bado wana elimu ndogo katika suala zima la upigaji kura. Kinachoweza kuvunja mtandao huu ni kuua CCM. Ikifa inakufa na kila kitu.
 
Alipotaka kuandika report ya postmoterm kuwa alipigwa risasi hawa watu wausalama wakamlazimisha aandike kuwa amefariki kwa ajali. Kwa shingo upande akaandika kulingana na matakwa yao. Sasa ukitaka kujua yuko wapi sikia kama bado jina lake linatajwa kwamba kuna Dr Fupi. Alishabadilishwa jina siku nyingi katika mazingira ya kutatanisha si unajua tena TZ hiyo.

Bubu nadhani umechanganya masuala kidogo hapa. Dr Fupi (Ferdinand, MD) hadi hivi karibuni alikuwepo Morogoro kwa kadiri ya kumbukumbu yangu, na kuna wakati miaka michache iliyopita nilikutana nae huko katika vikazi vyangu vya "ungwini". Dr Fupi "aliyepotezwa" ni yule aliyekuwa mkemia mkuu wa serikali miaka ya 1990, enzi ya lile sakata la uingizaji wa vyakula vibovu, aliweka msimamo mkali sana juu ya maelfu ya tani za vyakula hivyo vilivyoagizwa kutoka nje kifisadi kuwa havifai kwa matumizi ya binadamu, na alikuwa shahidi muhimu mahakamani. Alifariki katika mazingira ya kutatanisha kabla hajatoa ushahidi huo.
 
Wananchi wetu bado wana elimu ndogo katika suala zima la upigaji kura. Kinachoweza kuvunja mtandao huu ni kuua CCM. Ikifa inakufa na kila kitu.

kuua ccm sio suluhisho, maana upinzani ukiwaachia nchi hapatokalika, maana bado hawajaiva kabisa.


suluhisho kuimarisha somo la uraia na kuwaandaa wananchi wetu wote up9inzani na ccm kuwa tanzania ni nchi yetu na ss ndio tunajukumu la kuilinda, kuijenga na kuitumikia.


kuwasomesha upendo wa nchi na kujitolea sio kama chadema wamejali viposho wamerudi bungeni wakawaacha wenzao mataani
 
Mimi nijuavyo ni kuwa Dr. Shaba ndite alifanya postmotem ya Moringe na ripoti ilikuwa siri sana kwa kweli. Kwa mara ya kwanza nilimuona Kambarage akitoa machozi hadharani pale Karimjee (bunge la zamani).

Niliambiwa kuwa Lowassa alikuwa na mpango kuwa baada ya Kikwete urais ungehamia Monduli kwa miaka 20 maana yeye angechukua kwa miaka 10 na kisha kumpisha mtoto wa Marehemu Sokoine ambaye yuko Marekanai kwa miaka mingine 10. Wakati yeye (Lowassa) akiwa rais mtoto wa Moringe angekuja kugombea ubunge wa Monduli (ambao angeupata kirahisi kutokana na jina la baba yake) na kisha baadaye kuwa waziri kwa miaka 10 ya uongozi wa Lowassa. Hiyo ingempa uzoefu wa kuwa rais baada ya Lowassa kumaliza kipindi chake.

Sasa mambo kidogo yamebadilika sijui itakuwaje.
 
Na ndo maana hata viongozi wa UFISADI hakuna anayedhubutu kuwagusa, maana yeyote atakayeelekea kufanya mambo ya kutafuta haki na sheria kifo kinamyemelea kutoka kwa Mafisadi, na viongozi wengine wa serikali??

Sasa kifanyike nini jamani?
Mimi naona hapa solution pekee, ni kuanzisha vita jamani? Vita yenyewe, sio ya ukabila au udini kama zilivyo nchi zingine, ila ni vita kati ya wanyonge na Mafisadi, vita hii inalenga kuhakikisha kuwa mali zote za wananchi zinarudi mikononi mwa wananchi!! au mnasemaje wakuu, hivi hivi tutakaa kuongea tu mpaka basi, na hakuna kitakachofanyika kwa sababu hata kikwete anaogopa anaweza kuuliwa muda wowote, sasa ni sisi kuhakikisha mafisadi wote tunawamaliza na kuanza kuijenga Tanzania mpya jamani

Mara zote vita huwa ni suluhu ya mwisho kabisa na hii haipangwi ila huja automatically. Ukisema uanzishe vita utajikuta uko peke yako unavunja ukuta wa nyumba ya Lowasa wenzio wako majumbani. Tatizo tulilo nalo TZ ni ukosefu wa elimu hasa ya kujua haki zetu za msingi kutoka kwa watawala tuliowapa dhamana ya kutuongoza. Bado tunawaza kuwa kupiga kura ni kutimiza wajibu na hatuoni thamani ya kura tunayopiga. Siku tutajua thamani ya kura ndipo hata vita itakuwa ni rahisi kuwepo kama hiyo kura yangu ya thamani haijatendewa haki.

Siku mwananchi amejua thamani ya kura yake ndipo mambo yatakuwa ktk mstari. Ninayo mifano mingi kutoka kwa rafiki na ndugu wa karibu wakati wa kupiga kura wanasema hawaendi au hata kujiandikisha wanaona ni usumbufu kwao. huu ni ushahidi tosha kuwa mtu huyu hajui thamani ya kura yake. Hata wewe mwana JF inawezekana unao watu wa hivyo au hata wewe mwenyewe wanadharau u-thamani wa kura zao. Hili ni hatari na linahitaji msukumo wa kipekee kwani hata wasomi wengine ni Ma-prof siku ya kura hawaendi wako busy na reseach zao bila kujua hizo reseach haziwezi kutekelezwa bila kuwa na kiongozi muadilifu.

MTANZANIA THAMINI KURA YAKO KUANZIA LEO, USIKOSE KUPIGA KURA, UJUE UMUHUMU WA KUWEPO HAPA DUNIANI, JITHAMINI KWANZA WEWE KUWA UNAWEZA KULETA MABADILIKO. JIANDIKISHE KUPIGA KURA, NAFASI YA KUJIANDIKISHA UMEPEWA, FANYA HIVYO TAFADHARI.

MUNGU AWABARIKI
 
Back
Top Bottom