Mwenda_Pole
JF-Expert Member
- Jul 5, 2008
- 281
- 66
Maroon Commandos kutoka Kenya - Charonyi ni wasi
[ame="http://www.youtube.com/watch?v=zqIJNJB73Ug"]http://www.youtube.com/watch?v=zqIJNJB73Ug[/ame]
Mpongo Love - Ndaya
[ame="http://www.youtube.com/watch?v=6F7lHM90KwI"]http://www.youtube.com/watch?v=6F7lHM90KwI[/ame]
Macho yanacheka Moyo unalia
http://www.eastafricantube.com/media/1414/Taarab_-_Macho_Yanacheka_Moyo_Unalia/
Binafsi nakumbuka mbali sana enzi hizo radio zilikuwa ni National na Philips tu na zilikuwa zinauzwa kwenye maduka ya RTC.
Nakumbuka maduka yale yalikuwa yanaitwa Bora yalikuwa karibu kila mkoa, walikuwa wanauza viatu vikiitwa safari boot, pamoja na raba mtoni zilikuwa zinaitwa Bora.
Nakumbuka enzi hizo daftari za mistari mikubwa na midogo kwa ajili ya kujifunza mwandiko kwa wanafunzi zilikuwa zinapatikana maduka ya Tanzania Elimu Supplies tu.
Nakumbuka pia tulikuwa tunapewa madaftari bure shuleni kila mwaka shule ikifunguliwa na likiisha unakwenda kumuonyesha mwalimu anakupa jingine jipya.
Nakumbuka enzi hizo kulikuwa na mashirika ya uchukuzi kila mkoa Mwanza ilikuwa KAUMA, Kagera ilikuwa KAGERA RETCO, Iringa ilikuwa IRINGA RETCO, Dodoma ilikuwa KAUDO, wadau mtaongezea.. Morogoro, Rukwa na kule kaskazini yalikuwa yanaitwaje..
Namkumbuka nakumbuka radio Tanzania ya enzi hizo na vipindi vyake kama Kahawa ni Mali, sikiliza Bwana Umeme, TTCL simu kwa Maendeleo, General Tyre, Starehe na BP, Malenga wetu.... wadau ongezeeni vipindi mlivyokuwa mnakumbuka enzi hizo...
Nakumbuka enzi hizo kulikuwa hakuna TV watu walikuwa wanakwenda kwenye kumbi za sinema tu kuangalia movies, Dar zilikuwepo kumbi kama Avalon,Drive Inn n.k Dodoma kulikuwa na N.K Disco Teques
Nakumbuka enzi hizo mabasi yalikuwa yakisafiri usiku tu na kulikuwa hakuna ajali nyingi kama sasa. Nakumbuka pia Mabasi maarufu enzi hizo kama SIRI YAKO, SUPER STAR, NGORIKA na wale mliokuwa Dodoma mtakumbuka mabasi yale ya kwenda Tanga kama SIMBA MTOTO, AMEET na zile honi zao kimadaha.
Nakumbuka pia watu walikuwa na ushirikiano sana, jirani alikuwa ni kama ndugu yako.
Mdau unakumbuka nini enzi hizo...??????
Mwenda Pole
Mdau wa Dodoma
[ame="http://www.youtube.com/watch?v=zqIJNJB73Ug"]http://www.youtube.com/watch?v=zqIJNJB73Ug[/ame]
Mpongo Love - Ndaya
[ame="http://www.youtube.com/watch?v=6F7lHM90KwI"]http://www.youtube.com/watch?v=6F7lHM90KwI[/ame]
Macho yanacheka Moyo unalia
http://www.eastafricantube.com/media/1414/Taarab_-_Macho_Yanacheka_Moyo_Unalia/
Binafsi nakumbuka mbali sana enzi hizo radio zilikuwa ni National na Philips tu na zilikuwa zinauzwa kwenye maduka ya RTC.
Nakumbuka maduka yale yalikuwa yanaitwa Bora yalikuwa karibu kila mkoa, walikuwa wanauza viatu vikiitwa safari boot, pamoja na raba mtoni zilikuwa zinaitwa Bora.
Nakumbuka enzi hizo daftari za mistari mikubwa na midogo kwa ajili ya kujifunza mwandiko kwa wanafunzi zilikuwa zinapatikana maduka ya Tanzania Elimu Supplies tu.
Nakumbuka pia tulikuwa tunapewa madaftari bure shuleni kila mwaka shule ikifunguliwa na likiisha unakwenda kumuonyesha mwalimu anakupa jingine jipya.
Nakumbuka enzi hizo kulikuwa na mashirika ya uchukuzi kila mkoa Mwanza ilikuwa KAUMA, Kagera ilikuwa KAGERA RETCO, Iringa ilikuwa IRINGA RETCO, Dodoma ilikuwa KAUDO, wadau mtaongezea.. Morogoro, Rukwa na kule kaskazini yalikuwa yanaitwaje..
Namkumbuka nakumbuka radio Tanzania ya enzi hizo na vipindi vyake kama Kahawa ni Mali, sikiliza Bwana Umeme, TTCL simu kwa Maendeleo, General Tyre, Starehe na BP, Malenga wetu.... wadau ongezeeni vipindi mlivyokuwa mnakumbuka enzi hizo...
Nakumbuka enzi hizo kulikuwa hakuna TV watu walikuwa wanakwenda kwenye kumbi za sinema tu kuangalia movies, Dar zilikuwepo kumbi kama Avalon,Drive Inn n.k Dodoma kulikuwa na N.K Disco Teques
Nakumbuka enzi hizo mabasi yalikuwa yakisafiri usiku tu na kulikuwa hakuna ajali nyingi kama sasa. Nakumbuka pia Mabasi maarufu enzi hizo kama SIRI YAKO, SUPER STAR, NGORIKA na wale mliokuwa Dodoma mtakumbuka mabasi yale ya kwenda Tanga kama SIMBA MTOTO, AMEET na zile honi zao kimadaha.
Nakumbuka pia watu walikuwa na ushirikiano sana, jirani alikuwa ni kama ndugu yako.
Mdau unakumbuka nini enzi hizo...??????
Mwenda Pole
Mdau wa Dodoma