Unakumbuka mwaka 1994 Wazanzibar walivyokasirika Rais wa Zanzibar kuondolewa kuwa Makamu wa Rais wa Muungano?

MdogoWenu

JF-Expert Member
Dec 23, 2009
555
915
Kabla ya vyama vingi kuja Rais wa Zanzibar alikuwa moja kwa moja ni makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Vilipoanza vyama vingi ilibidi kubadili katiba tume ya Bomani (RIP) ikapendekeza kuwe na makamu wawili na wagombee pamoja uchaguzini na watoke chama kimoja.

Mapendekezo yakasema kwamba Rais wa Zanzibar asiwe tena makamu wa Rais kama ilivyokuwa.

CCM wakapokea mapendekezo hayo, wakayakubali na Julius Nyerere.

Lakini kumbe mapendekezo yale wana CCM wa Zanzibar hawakuyapenda. Sababu ni kwamba walitaka Rais wa Zanzibar aendelee kuwa Makamu wa Rais.

Wazanzibar walikasirika hadi wakashinikiza yasipitishwe na hayakupitishwa mwaka 1992.

Hatimaye Nyerere akakasirika hadi akaandika kitabu kiitwacho UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA.

Katika kitabu kile alisema mfumo wa Rais wa Zanzibar akiwa moja kwa moja makamu wa Rais hata kwa wakati ule ingeweza kuleta shida.

Kwamba kazi ya makamu wa Rais ni kwamba Rais akiondoka madarakani kwa sababu yoyote kama kifo au kujiuzulu au ugonjwa basi makamu wa Rais anachukua Urais.

Sasa tungeendelea na mtindo wa Rais wa Zanzibar kuwa makamu basi siku Rais wa muungano akifa au lolote basi huyu makamu na Rais wa Zanzibar anarithi Urais.

Nyerere akasema hilo lilikuwa ni tatizo kwa sababu Rais wa Zanzibar anachaguliwa na wazanzibar tu.

Sasa huyu akiwa Rais wa muungano wakati watanganyika hawakumchagua itakuwa tatizo.

Hoja hii ya Nyerere ndiyo ilisababisha wazanzibari wakubali kwa shingo upande, hata hivyo Salmin Amour aligoma kuhudhuria baraza la mawaziri hadi anaondoka madarakani.

Hivyo iko siku tutaona ukweli wa alichosema Nyerere. Iko siku Rais wa muungano ataweza kupata tatizo ikabidi makamu wa Rais achukue Urais ndipo wazanzibari wenye akili ngumu waelewe.

Jadili
 
Nyerere na Bomani waliku right kabisa. Katiba ya tanzania haijawahi kuwa wazi kuhusu kupokeana madaraka wakati Rais akifa; kwa mfano wakati Karume alipofariki, Makamu wa wa pili wa Rais wakati huo alikuwa Kawawa, lakini yeye hakuwa promoted kuwa makamu wa kwanza wa Rais, badala yake aliletwa Jumbe ambaye alikuwa waziri wa nchi kwenye ofisi ya Makamu wa kwanza Rais wakati huo.

Halafu Nyerere alipostaafu, Mwinyi hakuwa automatic choice bali kulikuwa kampeini kubwa sana ya "huyu ni mwenzetu" iliyofanywa na Nyerere ili kumkubali Mwinyi kama mrithi wa Nyerere, kulikuwa na uwezekano mkubwa sana wa watu wengine kuiwania nafasi hiyo.

Bado kulikuwa na woga wa "Treason Act 1351" kuhusu kuongelea uwezekano wa rais kufia madarakani.
 
Ila hata hivyo makamu wa raisi si huwa anatokea zenji?

Ila tukumbuke tuliambiwaView attachment 1724312
Kama nimemuelewa vizuri mwandishi wa uzi hu (kama ni kweli huo ndio msimamo wa Nyerere ) ni hivi; yule rais wa Zanzibar, Watanganyika hatukushiriki kumchagua (though still is too theoretical cause rais wa Zanzibar anachaguliwa na Dodoma) kachaguliwa na Wapemba na Waunguja, huyu makamo wa rais wa muungano anachaguliwa pamoja na rais aliyeko madarakani; Ingawa tuombe Mungu apishilie mbali mawazo ya wachangiaji wengi, Mungu atuepushe kabisa.
 
Watu mna mawazo ya ajabu kweli!! Anyway ni maoni yako kwa mujibu wa utashi wako ila Watz wenye nia njema wanaliombea taifa na viongozi wao.

Mwal. Nyerere hakutoa Hilo pendekezo kwa maslahi ya wazanzibar,au kutaka fair kwa wazanzibar.

Naona mleta mada umewapoint Wazanzibar, suala la makamu wa Rais ni kwa maslahi ya stability ya jamhuri ya muungano wa tanzania. Hapa labda ungesema ipo siku watanzania tutamuelewa 6au ulikuwa unawachenga mods wasing'amue target yako!!?

stop yr sarcastic,stop mocking yr country.
 
Kama nimemuelewa vizuri mwandishi wa uzi hu (kama ni kweli huo ndio msimamo wa Nyerere ) ni hivi; yule rais wa Zanzibar, Watanganyika hatukushiriki kumchagua ( though still is too theoretical cause rais wa Zanzibar anachaguliwa na Dodoma ) kachaguliwa na Wapemba na Waunguja, huyu makamo wa rais wa muungano anachaguliwa pamoja na rais aliyeko madarakani; Ingawa tuombe Mungu apishilie mbali mawazo ya wachangiaji wengi, Mungu atuepushe kabisa


Kwani Rais waTanganyika huwa tunamchagua au TUME ya uchaguzi ndo inamuweka madarakani?
 
Hatujawahi kuacha na hatutaacha kujadili kuhusu nchi yetu.

Nyerere alitabiri mwaka 1993 kuwa tatizo kama alilotabiri linaeza kutokea hata iwe miaka 60 ijayo.

Nyerere hakujua litatokea lini, na mimi sijui na wewe unayeuliza hujui.

Nini msingi wa bandiko lako? Unatabiri nini labda?
 
Nyerere akasema hilo lilikuwa ni tatizo kwa sababu Rais wa Zanzibar anachaguliwa na wazanzibar tu.
Hoja za kitoto hizo, makamu wa Rais anapigiwa kura na nchi nzima kushika nafasi ya umakamo. Tena na gharama zingekuwa nafuu, kwa vile kusingekuwa na makamo wa Rais, badala yake nafasi hii ingekuwa nearly empty kwa vile Rais wa tz akiwa hai makamu anashughulika kazi zake za Urais Zanzibar.
 
Back
Top Bottom