Kumekuwa na malalamiko mengi sana kuhusu wanawake kuolewa halafu Wanaambiw waache kazi na waume zao. Yaani mfano mwanamke ni mwalimu akishaolewa anaambiwa acha kazi ukae nyumbani nitakuhudumia kwa kila kitu, na yeye anakubali kuacha kazi.
Hivi kweli mtu umesoma na wakati mwingine kazi hiyo kuipata nguvu imetumika, halafu unakubali kirahisi rahisi tu kuacha kazi ili ukae nyumbani ulee watoto, mwisho wa siku ukikubali kuacha kazi unapewa huduma kwa muda mambo yanabadilika mnaanza kulia lia, huu ni ujinga usio na mfano.
Lakini pia na nyie wanaume huwa mnafikria nini kumuachisha mkeo kazi ili akae nyumbani? Huku ni kutokujiamini, uoga na wivu kijinga, kwanza mwanamke akifanya kazi anakuwa na uwezo wa kujihudumia na kukupunguzia mzigo, Vilevile ni rahisi kuepuka vishwawishi tofauti na wale waliokaa tu bila kazi. Lakini pia hakuna aijuaye kesho yake, mwanamke akiwa na kazi ni rahisi kuhudumia familia pindi Mungu akikuchukua tofauti na yule ambae hana kazi.
Hivi kweli mtu umesoma na wakati mwingine kazi hiyo kuipata nguvu imetumika, halafu unakubali kirahisi rahisi tu kuacha kazi ili ukae nyumbani ulee watoto, mwisho wa siku ukikubali kuacha kazi unapewa huduma kwa muda mambo yanabadilika mnaanza kulia lia, huu ni ujinga usio na mfano.
Lakini pia na nyie wanaume huwa mnafikria nini kumuachisha mkeo kazi ili akae nyumbani? Huku ni kutokujiamini, uoga na wivu kijinga, kwanza mwanamke akifanya kazi anakuwa na uwezo wa kujihudumia na kukupunguzia mzigo, Vilevile ni rahisi kuepuka vishwawishi tofauti na wale waliokaa tu bila kazi. Lakini pia hakuna aijuaye kesho yake, mwanamke akiwa na kazi ni rahisi kuhudumia familia pindi Mungu akikuchukua tofauti na yule ambae hana kazi.