Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kwenye safari kwa sisi ambao bado tunatumia usafiri wa Umma, kuna kero mbili ambazo zinatukabili wasafiri. La kwanza ni ukosefu wa vyoo kwenye njia tunazotumia kusafiria matokeo yake hujisaidia maporini kwa mtindo wa kuchimba dawa. Kwa kweli hii staili inakera ingawa kwa wengine huwa ni kama faraja kwao kwani huitumia kwa kunyoosha miguu kutokana na kutokuwa na uwezo wa kukaa muda mrefu wakiwa wamekunja miguu!!
Kero nyingine ni ya hawa abiria wenzetu ambao wanapenda kula kula lakini hawana uwezo wa kuhimili misuko suko ya safari matokeo yake huishia kutapika garini wakati safari inaendelea. Unakerwa na nini unaposafiri na mabasi yaendayo mikoani??
Kero nyingine ni ya hawa abiria wenzetu ambao wanapenda kula kula lakini hawana uwezo wa kuhimili misuko suko ya safari matokeo yake huishia kutapika garini wakati safari inaendelea. Unakerwa na nini unaposafiri na mabasi yaendayo mikoani??