Unajua unaongea na nani?

Ukifuatilia kwa ukaribu utabaini kuwa watu wa namna hiyo wametoka kwenye maisha duni sana na wakati mwingine nguo za ndani wameanza kuvaa baada ya kupata huto tuvyeo wanatonyanyasia wenzao
 
Cheo ni dhamana. Sitakitumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yoyote.
Emmanuel Nchimbi na Yule aliyemtangulia almaaruf Masha. na yule msukuma wa ATM.
 
Hizi zinatokeaga sana pale unagongana au kuchunana magari, anashuka dereva na kuanza kukuambia hivyo!
 
Kuna day moja niko maeneo ya makumbusho nacheki mechi ligi ya uingereza kaja jamaa mmoja kakalia siti ya mtu alienda chooni mara moja ,mwenye siti anarudi anataka akae jamaa, akaanza unajua mi nani unataka kuniinua hapa !! Jamaa akamuambia sitaki kujua we nani ile kwa hapa makumbusho hamna wa kumtisha kwa hicho unachotaka kusema labda uwe umeajiriwa juzi juzi, si unataka kuniambia we usalama wa taifa sio naomba siti yangu !! Jamaa alikua mdogo kama priton !!!
 
Ni kawaida kwa viongozi -wa Tz... Kuna aliyekuwa waziri wa uvuvi Mr. David Mathayo hataki kusubirishwa na 'shikamoo' hataki yule baba..utasikia unaninyima nini mtoto mzuri... Khaaaa!
 
Tatizo la watanzani ni hapa kuficha majina ya wahusika. Mleta uzi ulipaswa ku-disclose majina yote ya wenye hiyo tabia uliokutana nao na wadau wengine wangefuata
 
Kuna siku dereva wa Nchimbi alipaki gari mbele yangu Barclays sehemu ya kutokea gari yangu ikiwa nyuma yake kupiga honi mara tatu akaja jamaa mmoja akaniambia wewe tulia mjini hapa unamjua aliyepaki gari nikasema hapana akasema waziri wa mambo ya ndani. Du tena ilikuwa Noah, nilichoka.
 
Niliwahi kukutana na swali kama hilo na mimi nikamjibu kijeuri “ Najua Wewe ni Jambazi Sugu”.
 
Aisee usinikumbushe...kuna siku nilikua bar moja kule kigamboni kuna jamaa akaja akawa anaongea ovyo, nikajifanya kumwambia aongee taratibu tunaangali mpira....jamaa akaniuliza kama namjua yeye ni nani, mimi si nikamjibu mbovu...yalaa, nilichezea kichapo, na msamaa nikamuomba. Kumbe jamaa ni mjeshi tena mwenye vyeo.
 
kuna waziri anaitwa Dr Tizeba jamani Mungu anisamehe huyu jamaa kwakweli mimi ni jirani yangu kwa maana tunatoka kijiji kimoja huko jimboni kwake lakini jamaa ukimpigia cm kwanza hapokei na hata ukituma meseji hawezi kujibu,cm yake iko hewani lakini hata ukipiga kwa nyakati tofautitofauti hapokei, na mara zote anadhani labda unataka kumpiga bomu kwa maana ya kumwomba msaada wakati unataka kumpatia shida za wananchi. Mfano mwaka jana nilikwenda jimboni kwake nikakuta njaa hatari mihogo inaugonjwa kwa takribani mwaka na hakuna msaidizi,nilijitahidi kwenda wilayani kwa DALDO lakini sikupata msaada,nikampigia simu mbunge hakupokea nikamtumia sms kama sita hivi hakujibu nikampigia mdogo wake naye kiburi hakupokea ,HALI HII YA KUJIONA VICHWA KAKA YAKE MBUNGE ALIAMUA KUJITOA CCM NA KUHAMIA CHADEMA akiwa diwani coz hasikilizwi na mbunge, 2015..........KAZI ANAYO......CCM HESABUNI MAUMIVU BUCHOSA mbunge labda kama atajirekebisha kupita watu bila salaam na kulazimi ferry kumsubili jioni nyakarilo hata kama yuko mwanza anakuja eti coz ni mbunge hiyo hata kidogo ni utemi wa ajabu..........hudumia watu utawajua..........
 
Aisee usinikumbushe...kuna siku nilikua bar moja kule kigamboni kuna jamaa akaja akawa anaongea ovyo, nikajifanya kumwambia aongee taratibu tunaangali mpira....jamaa akaniuliza kama namjua yeye ni nani, mimi si nikamjibu mbovu...yalaa, nilichezea kichapo, na msamaa nikamuomba. Kumbe jamaa ni mjeshi tena mwenye vyeo.

Aaaah wanajeshi achana nao
 
Kuna hii tabia ya watu kuingia kwenye maofisi ya watu, hawataki kufuata utaratibu ukimuuliza anakwambia unajua unaongea na nani.

Hii tabia inanikumbusha aliyewahi kuwa Waziri wa nishati na madini, siku alipoingia kwenye ATM na kuanza kuongea na simu muda mrefu yule mlinzi alipomfuata "jamaa" akampiga makofi.

Tukio lingine ni aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa mambo ya ndani na hivi majuzi amejiuzulua akiwa Waziri wa Maliasili, huyu jamaa alipita maeneo ya Kijitonyama akiwa kwenye gari linaloendeshwa na dereva wake, walipokuta foleni ikabidi "watanue" askari wa kike alipowasimamisha akajibiwa "unajua unaongea na nani" kisha baada ya hapo yaliyomkuta huyo askari anajua Mungu mawazo yangu kama we ni nani au ni nani unaeshimu taratibu na pia ueshimu kazi za watu bila kujali cheo.:mad:

Mungu ni mkubwa hao wote niliowataja walisitisha au kusitishiwa ajira zao baada ya kashfa kwa sasa kuna "jamaa" fulani ambaye ki cheo ni Waziri huyu "jamaa" huwa anakuja sana ofisini kwetu akifika hasalimii watu pale mapokezi ye huingia tu kule back office ambako kuna boss wetu rafiki yake sasa juzi nilifurahi kwa sababu ofisini pale kwenye corridor kulikuwa kumefanyiwa fumigation.

Mheshimiwa alirudi mbio huyo wenzetu wenye vyeo acheni tabia hizi ni za kishamba.

Kweli Mungu ni Mkubwa!! huyo mjamaa nasikia alipowasili Maliasili akasema YEYE NI MBUYU na mtu yeyeto anayefikiria kumwangusha atakuwa futi sita chini kabla hajaanguka! sasa akaanguka mwenyewe! chini kulikuwa hamna miti. Huyu jamaa nadhani anajihami kwa kutisha watu ili wamuogope.POLE zake
 
kuna waziri anaitwa Dr Tizeba jamani Mungu anisamehe huyu jamaa kwakweli mimi ni jirani yangu kwa maana tunatoka kijiji kimoja huko jimboni kwake lakini jamaa ukimpigia cm kwanza hapokei na hata ukituma meseji hawezi kujibu,cm yake iko hewani lakini hata ukipiga kwa nyakati tofautitofauti hapokei, na mara zote anadhani labda unataka kumpiga bomu kwa maana ya kumwomba msaada wakati unataka kumpatia shida za wananchi. Mfano mwaka jana nilikwenda jimboni kwake nikakuta njaa hatari mihogo inaugonjwa kwa takribani mwaka na hakuna msaidizi,nilijitahidi kwenda wilayani kwa DALDO lakini sikupata msaada,nikampigia simu mbunge hakupokea nikamtumia sms kama sita hivi hakujibu nikampigia mdogo wake naye kiburi hakupokea ,HALI HII YA KUJIONA VICHWA KAKA YAKE MBUNGE ALIAMUA KUJITOA CCM NA KUHAMIA CHADEMA akiwa diwani coz hasikilizwi na mbunge, 2015..........KAZI ANAYO......CCM HESABUNI MAUMIVU BUCHOSA mbunge labda kama atajirekebisha kupita watu bila salaam na kulazimi ferry kumsubili jioni nyakarilo hata kama yuko mwanza anakuja eti coz ni mbunge hiyo hata kidogo ni utemi wa ajabu..........hudumia watu utawajua..........

Ni kweli mkuu, ila kipindi anaomba kura huo ukarimu na ustaarabu aliokua anaonesha ulikua wa hali ya juu mno. Jamaa sa hivi kawa mwingine kabisa.
 
Hii yote ni ulevi wa madaraka. Wakishapata tuvyeo wanageuka kuwa miungu watu!
Wakuu kalamu ya chuma na NYEHUNGE nipeni updates za huko jimboni Buchosa, 2015 tumejipanga vipi kuwakabidhi wapinzani jimbo letu ili kuchochea maendeleo kwa wananchi? msiniambie habari za kumkabidhi yule zungu wa mbilimbi Shigongo make mijiudenda ya kitejateja kila kukicha inamtoka kuwania ubunge kupitia CCM! Aisee msifanye makosa kumpa huyu shetani keshauwa wenzetu wengi sana. Msifanye akalewa sifa na kuona kila akitakacho hapa Duniani kinawezekana!
Uchafu aliofanya unatosha sasa hatumtaki.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kisima nikuhakikishie kabisa jimbo letu la buchosa linarudi UKAWA kwani mpaka sasa hakuna jipya,kuanzia kome kisiwani,nyakaliro,mpaka nyehunge,rudi huku bupandwa pote mpaka Luhama,hakuna jipya,barabara hakuna,kilimo cha uhakika na maendeleo ya kuibuliwa kuokoa umasikini hakuna,mimi naona fursa nikipita naibadilisha buchosa,nimekwisa asses nini hitaji la jimbo kupitia marafiki majirani wa Kenya nitashangaza,CCM KWISHA KABISA.
 
Hii nayo imekaa vp wandugu. Hv ktk foleni ya kupata huduma flani may be ni bank,hsptl au popote pale panapobidi kuwe na foleni. Akaja either askari,nurse ama denti yupo ktk sare. Je,wanaweza kupita pasi kupanga foleni.?!
 
Hakuna kauli nisiyoipenda kama hii... mtu wa aina hii akiingia kwenye anga zangu is nobody to me, cheo chake anakiacha ofisini kwake....

Kweli si lugha ya kiungwana,sawa na mjamaa anakuwa sehemu anamwona demu na kuingiza nyimbo,mrembo akikataa anamwambia,unajua unaongea na nani?Binti kichwa tikiti na mpenda pesa kwa tamaa atalainika na kuingia king,lakini kuna wale mademu ambao huwa hawataki kusikia status ya mtu kwa kweli unaweza aibika.Kwani wao hutaka kipenda roho hula nyama mbichi,na hasa wadada wenye FWEZA ZAO na WENYE KIPATO CHA UHAKIKA tofauti na hao wengine lakini WAREMBO HASWA.:A S 109:
 
Back
Top Bottom