Unajua Nini Kuhusu Crack

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Kwa sasa hivi sio ajabu kabisa kwenda katika kampuni yenye watu zaidi ya 60 mfano ukakuta wanatumia programu ambazo hazina leseni , ambazo zina crack na vitu kama hivyo .

Wakurugenzi wa kampuni hizi sijui kama wanajua madhara yake kwa kuruhusu hizo programu kutumika pale , hata sijui walimu wa vyuo wanafundisha nini wanafunzi wao haswa wale technician na administrator wa baadaye kuhusu vitu hivi .

Ni kawaida kabisa kukuta administrator ameacha system yake iwekwe programu hizi na zitumike bila wasi wasi na tatizo lolote , shida ikitokea si anaformat tu ? kwanza hata installation cd anazotumia sio licenced yeye anashida gani ??

Wakati Fulani rafiki yangu mmoja aliwahi kuniomba programu Fulani kwa ajili ya kazi zake , nikamwambia ninayo lakini yangu ina leseni ambayo ni kwa ajili ya mtu mmoja au computer moja tu .

Akaniuliza siwezi kumkopia au siwezi kumtafutia programu kama hiyo hiyo ya bure ambayo ni cracked ( iliyofanyiwa usanii ili ifanye kazi ) nikamwambia huo ni uhalifu siwezi kufanya hivyo , akaniuliza kama kuna tovuti yoyote wanazotoa serial number au crack au keygen zake .

Unaweza kuchanganyikiwa kidogo ninavyotaja crack , keygen na serial number na licence key hivi ni vitu tofauti .

Crack – Ni aina ya njia haramu ya kuifanya programu Fulani ifanye kazi , lakini programu hiyo inakuwa haina baadhi ya vitu na ni ngumu sana kujua labda likitokea tatizo Fulani , ila mara nyingi crack huwa na virus ndani yake na spyware .

Keygen – Hii ni programu inayotumika kutengeneza serial number katika programu husika , mfano programu nyingi za adobe zina keygen au nero 7 ina keygen au Autocad , maana yake ukisha install inabidi kufungua keygen ili ugenerate serial number kwa ajili ya programu yako .

Serial Number – Hizi ni namba maalumu unazotakiwa uingize katika programu yako ili ihalalishwe katika matumizi yako ya kawaida , sasa Keygen inaweza kugenerate hiyo serial number .

Licence Key – hizi nazo ni namba pia lakini mara nyingi hizi licence key unatakiwa uimport katika programu yako ili iweze kufanya kazi na hizi zinatumika zaidi katika programu kama za Autocad 2008 na kuendelea .

Hayo ni maelezo mafupi kuhusu baadhi ya mambo muhimu ambayo ni muhimu kujua unapokutana na vitu kama hivi .

1 – Programu nyingi ambazo ni cracked zinakuwa na virus katika baadhi ya file zake kwahiyo haitafanya kazi ipasavyo ingawa sio zote .

2 – zingine zinakulazimisha usijiunga na internet ukifanya hivyo wenye programu ni rahisi kuifunga au kukutambua kwamba unatumia kitu haramu na kuzifungia mfano wake ni Microsoft Windows Xp na Windows Vista .

3 – Ni rahisi kushambuliwa kwa njia ya mtandao kama unatumia Antivirus au Firewall ambazo ni cracked kwa sababu baadhi ya vitenda kazi vinaweza kuwa havifanyi kazi au vimezimwa ingawa sio zote .

4 – Kama unatumia programu za uhasibu , au mahesabu ni rahisi kupoteza data , au kuchanganya baadhi ya mahesabu kutokana na hivi yaani programu kutokufanya kile inachotakiwa kutokana na mapungufu wakati wa cracking .

5 – Kwa programu kama Adobe Acrobat Profesianal 6 na kuendelea , ukitumia crack hizi , unapojaribu kugeuza Kitu toka Word kwenda Pdf au PDF kwenda Word , baadhi ya maandishi yanaweza kupotea au kutokea madhara mengine yoyote katika Document husika .

6 – Ni rahisi kuforge vitu vilivyotengenezwa kwa kutumia programu hizi kwa sababu zinakuwa hazina protection ya kutosha au protection hizi hazifanyi kazi zikiwekwa.

Hayo ni baadhi ya madhara tu ingawa kuna madhara mengi na mambo mengi unayoweza kukumbana nayo unapotumia programu ambazo sio halali .

Nakushauri usitependee sana kutumia programu ambazo sio halali kwa sababu madhara yake ni ya muda mrefu , unaweza kuharibu data za watu huko makazini , au unaweza kusababisha madhara yoyote yale yatakayoleta hasara katika jamii yako unayofanya nayo kazi .

Kama unanunua programu ambazo si halali na ukafurahia wakati unajua sio halali na ni makosa , basi hata mafisadi usiwalalamikie , unasababisha hasara kwa watu waliowekeza katika kutengeneza programu husika ,utambue na wao wanatakiwa kuishi na kudhaminiwa kutokana na ujuzi wao wa kukuletea programu hiyo husika .

Mwisho kabisa programu nyingi zinakuwa na kitu kinaitwa Terms Of Use , Disclaimer na Fair Use , kwahiyo unatakiwa uwe makini sana unavyojaribu ku install hizi programu , soma ujue kampuni husika inasema nini kuhusu bidhaa yake hiyo .

Ingawa sheria nyingi zinazotumika ni za marekani na nchi zingine za ulaya sio kwamba Huwezi kushitakiwa unavyotumia kinyume chake , kwa sababu kuna sheria za kimataifa zinazoweza kutumika kuku hukumu .
 
..umasikini ndio unaofanya baadhi ya watu watumie cracked programs.

..lakini pia kuna dhana iliyopo kwa wanao-crack copy za hizo apps,kuwa watengenezaji wanaziuza kwa bei mbaya na inabidi watu wazipate ili maisha yao nao yawe bora!

..ukweli ni kuwa,matumizi yake ni risk hasa kwa usalama wa pc na data za mhusika!ni vyema kuwa makini.

..simply usitumie anti-virus iliyokuwa cracked. ni sawa na kutembea na mwathirika hata kama unatumia protection!

..hizo nyingine ni moral and ethics za mtu! kwa mfano,ms office is a fair deal if u ask me! hawa jamaa wa microsoft wangetoa copy ya bure [ambayo haina vitu professional]angalau hata mwanafunzi wa africa akaweza chapisha ripoti na kusoma docs zake!

..otherwise,open source is getting better!
 
Wazo lako ni zuri, lakini mimi nionavyo ni wajibu wa wenye software husika kujua kuwa kazi zao zinaibwa hivyo kutafuta namna m badala ya kudhibiti uizi huo, mfano mmoja wapo ni ku validate software kabla haijaanza kutumika.

kuna maeneo watu wanazitaka software flani lakini hazipatikani wanaona njia rahisi ni kuzipata tokea kwa watu wengine ambao tayari wanazo. mfano Africa nchi zilizo nyingi hakuna software vandors watu watazipataje kama sio kupitia hizo namna nyingine?

Nakubaliana na wewe kwa hayo makampuni yenye uwezo wa kuagiza software tokea huko ulaya wafanye hivyo, lakini vipi wale wasioweza na wanazitaka hizo software?

cha msingi hao wenye software wahakikishe wanazifikisha product zao kote duniani na zipatikane kwa urahisi na bei poa.

hao crackers wakidhibitiwa nani ataweza kufoji sotfware? kuna Website nyingi tu tena za kibiashara zina promote cracked software ukitaka mifano naweza kukupa maana ni maarufu sana kwanini wenye software wasidhibiti hizo sources?

No one will use cracked software kama hazipo. Tatizo na hao programmers wanaachia source code zao kirahisi hivyo kuwafanya crackers kujenga modification kirahisi.

Mimi nadhani tusiwalaumu watumiaji bali hao wanaozitengeneza na kuzi publish kwenye web. Na hao wanaoona software zao zimekuwa attacked na wanakaa kimya bila kuwachukulia hatua hao waharibifu.

Mwisho nakupongeza kwa kuwatahadharisha hao watumia cracked software, nikweli baadhi yake hazifanyi kazi kiukamilifu na baadhi ya crack zinaambatanishwa na viruses. Hivyo wanatumia cracks kuweni macho na hizo cracked zenu.
 
Tunashkuru kwa Ushauri juu ya cracked software..

Siku hizi kuna sharing system torrent system,japo wanasema Haram lkn kuna vita vikubwa. Umaskini ndio unaotusumbua. so far anae install program anafanya hivyo on his own risk.

Kuzuia ngumu lkn JUU ya KILA MWENYE ELIMU basi AJUE KUNA WENGINE WAJUZI JUU YAO.
 
Is this a discussion about cracked software? or a crack?

I think you should read between the lines.

Shy has thorough discussed about the people who crack softwares and computer users who often use cracked softwares which they buy from crackers.

So the idea is to alert all of us the dangers of using cracked softwares.

We in Europe we call cracked softwares "pirate softwares" and the process of cracking them- software piracy.

Software piracy means duplicating and selling software illegally. It can take many forms, including unlicensed copying, counterfeit products and hard-disk loading.

I think it is simple as that.
 
Thanks Richard infact there is a strong need to stop software piracy so that common man may able to afford the software on the web which are so very high priced due to software piracy.
 
Tunashkuru kwa Ushauri juu ya cracked software..

Siku hizi kuna sharing system torrent system,japo wanasema Haram lkn kuna vita vikubwa. Umaskini ndio unaotusumbua. so far anae install program anafanya hivyo on his own risk.

Kuzuia ngumu lkn JUU ya KILA MWENYE ELIMU basi AJUE KUNA WENGINE WAJUZI JUU YAO.
BInafsi nilishazoea kutonunua software.PC yangu naitumia mwenyewe na kila nikitoka natoka nayo.Na mara kwa mara huwa naishusha injini ili kuifanya iwe imara zaidi.
Kama nafanya uharifu bora huu ninaofanya mimi.Na kama kuna mtu anajua mbinu mpya za ku crack na kutafuta key log anai PM
 
Thanks Richard infact there is a strong need to stop software piracy so that common man may able to afford the software on the web which are so very high priced due to software piracy.

..picassa, infact the opposite is true!the high price of softs [and so costs] is causing some people to pirate.
 
BInafsi nilishazoea kutonunua software.PC yangu naitumia mwenyewe na kila nikitoka natoka nayo.Na mara kwa mara huwa naishusha injini ili kuifanya iwe imara zaidi.
Kama nafanya uharifu bora huu ninaofanya mimi.Na kama kuna mtu anajua mbinu mpya za ku crack na kutafuta key log anai PM

..si lazima utumie os ya kununua,unaweza weka one of the open source distros. inategemea unatumia pc kufanyia nini hasa.

..huko kushusha engine ndio nini?fafanua,si unajua hilo neno ni tata!ha!ha!ha!
 
Kuna crack moja ya idm dah hatari kwa kweli mkuu hakuna namna.
 
Nishajiapia kua kwenye ishu ya software gharama yangu ni bundle tu hii ya kulipia licence sijui token keys nishakataaga

Kwa kampuni lenye nyaraka za siri kwa upande wao wanasababu ya mashiko kabisa hata kiusalama, kwanza kampuni unakuaje unapita kitonga wakati fast jet unaweza kuimudu?

Lakini mtu kama mimi hata kama kweli hiyo package imeambatana na virus ambao wanabeba taarifa, zitamsaidia nini huyo mdukuzi?

Cracker ni mhindi ndani ya hiyo crack kaweka spymalware ambao wanachukua password, imagine ndio kadukua account yangu ya jf anakutana na kiswahili naye ni muhindi atafanya nini cha maana kitachomnufaisha yeye aonekane ile crack yake imemsaidia kupata jambo fulani la muhimu?

Na atadukua watu wangapi maana crack ishakua new trend watu zaidi ya laki wamedonwload hiyo crack atakua anafanya kazi ya kumpitia kila mmoja ili acgukue taarifa zake za siri ataweza?

Nimeshakua addicted kiasi program yeyote ambayo iko free bila kua na crack nahisi kua haitafanya kazi ipasavyo nikiipakua
 
Ni risk ila hakuna namna siwezi nikanunua software aisee...kidogo nikijitahidi nitanunua Kaspersky antivirus pekee.
 
Pc yangu ina softwares kama 80 na zote ziko cracked! - Siwezi kununua maji ya bomba ili niogee wakati bahari iko mbele ya nyumba yangu.

R.i.p mtoa mada btw.
 
Nishajiapia kua kwenye ishu ya software gharama yangu ni bundle tu hii ya kulipia licence sijui token keys nishakataaga

Kwa kampuni lenye nyaraka za siri kwa upande wao wanasababu ya mashiko kabisa hata kiusalama, kwanza kampuni unakuaje unapita kitonga wakati fast jet unaweza kuimudu?

Lakini mtu kama mimi hata kama kweli hiyo package imeambatana na virus ambao wanabeba taarifa, zitamsaidia nini huyo mdukuzi?

Cracker ni mhindi ndani ya hiyo crack kaweka spymalware ambao wanachukua password, imagine ndio kadukua account yangu ya jf anakutana na kiswahili naye ni muhindi atafanya nini cha maana kitachomnufaisha yeye aonekane ile crack yake imemsaidia kupata jambo fulani la muhimu?

Na atadukua watu wangapi maana crack ishakua new trend watu zaidi ya laki wamedonwload hiyo crack atakua anafanya kazi ya kumpitia kila mmoja ili acgukue taarifa zake za siri ataweza?

Nimeshakua addicted kiasi program yeyote ambayo iko free bila kua na crack nahisi kua haitafanya kazi ipasavyo nikiipakua
hahaha no way mkuu..
alafu nina shida kama naweza kupata crack ya easeus recovery nina flash yangu nilimuazima mtu apige windo akaiharibu haifomatiki inaandika RAW sasa nimeona kama hii software inaeeza kunisaidia ila naona inahitaji linsens key au kama ipo namna ya kufanya nikaactivate bila key tupeane ujuz au kama ipo njia nyingine ya kufomat hii flash..

nishatumia disk manager,cmd,format ya kawaida ile ya this pc Right click, zote olaa
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom