Unajua kwanini blogger wa nje wanapiga hela za adsense sana?

miamiatz

JF-Expert Member
Dec 4, 2017
504
927
Kuna blogger mmoja muhindi ni best yangu sana. Ubest wetu ulianzia kule freelancer.com tukawa tunachat mara kwa mara mpaka tumekuwa mabest akaja Tanzania kutembelea Arusha na Kilimanjaro.

Jamaa ana blog yake na kwa mwezi anaingiza dola 2,300. Ameniambia siri yake kubwa ni kuwa kule kwao watu wanapeana support sana. Bloggers wengi wana mfumo wa ku exchange traffic na watumiaji wengi wana mfumo wa kuappreciate kile ambacho bloggers wanaandika.

Mtu unakuta anasoma makala kwenye blog na anapenda sana ile makala anajua hawezi kuchangia kwenye donation kwaiyo anaamua kudonate kwa njia mbadala. Ana click ad na anascroll scroll hapa na pale then anasepa. Akija tena kutembelea blog hiyo anaclick ad flani.

Basi unakuta kwa siku anapata more than 800 clicks kati ya 20,000 users wanaotembelea blog yake. Anasema tatizo la afrika mtu hata akisoma kitu akakipenda mtandaoni hawazi hata kuwa clicking an ad ni njia ya kusupport kazi ya msanii aliyebuni blog hiyo.

#KukuzaMaarifa #KuongezaUstawi
 
Kuna kitu huwa kinanikatisha tamaa kwenye blogs za bongo; yaani unakuta kichwa cha habari ni cha kuvutia, lakini ukifungua habari ni tofauti.

Sasa, kwa mtindo huo unategemea nitaclick ads zake ukizingatia amenidanganya?! Bloggers wa Tanzania wawe serious na content zao.
 
Ni hela nyingi mkuu, mana unaingiza bila kutumia nguvu, ni wew na laptop, tablet, au simu yako tu.
Umesema blogger wa nje wanapiga sana hela..
Sasa mbona blogger wa kino go wengi tu wanapata zaidi ya hizo??
 
Umkonto, Tukubali tu kuwa few bloggers are doing well ila hatuwapi support.

Utakuta blog ni nzuri ila mwishoni inapotea. Mfano kuna hii blog ilikuwaga miaka ya 2011 ambayo pia ilikuwa ikichapisha vijarida vya maswali na majibu yahusuyo kodi. Hii hapa moja ya kijarida kilichowahi chapishwa. Kijarida hicho kilipata umaarufu mkubwa sana ila hakikudumu mana hakukuwa na support ya aina yoyote kwa blogger.

Kuna bloggers wanaojitahidi kuandika makala za afya unasoma mpaka unakinai ila no support from readers.

Blogger akipata hata angalau 200 clicks kwa siku na CPC ikawa 0.1 anapata USD 20 kwa siku kwa mwaka ni wastani wa 17m hii itamsaidia kulipia server, kulipia subscriptions za paid pluggins, kulipa wakusanya taarifa na hata japo nayeye kupata ela ndogo ndogo za nauli etc.

Akikua akapata sponsorships za makampuni then anaweza pata more than four times that 17m kwa mwaka.

Kiufupi bloggers wa kitanzania kwanza wenyewe kwa wenyewe hawapendani. Hawana positive competition.
 
Umesema blogger wa nje wanapiga sana hela..
Sasa mbona blogger wa kino go wengi tu wanapata zaidi ya hizo??
Hapa tusichanganye madesa kuna wanaotengeneza ela za ads tz zaidi ya 10m kwa mwezi ila unakuta ni ads za kwenye blog na kwenye youtube videos not just blogs.
 
tena unakuta lijitu linaclick mara nyingi nyingi mda huo huo ili upigwe ban, wafunge account
Sure yan hyo ndio wabongo wengi imewakaa yaan anaCLICK kama sifa ili GOOGLE wakupige BAN account yako but itafika tu muda wengi watabadilika.

Ila kusema ukweli Bloggers wengi wa Tanzania ni copy and paste without editing even a single line yaani habari kama sasahivi ni Forex basi kila sehemu ni hiyo hiyo, kipindi ilikuwa inabamba kilimo kila sehem kilimo cha tikiti yaani hakuna change yoyote tena kuna master wao mmoja wa copy and pate anaitwa Muungwana huyu jamaa ni hatari yaani anacopy nakala za watu hatari.

Ni bora kama umeamua kuwa blogger chagua niche yako moja utakayozungumzia na usimame hapo hapo ni bora kwa week uwe unatoa nakala 2 lakini iwe motivated na ata mtu akisoma next time lazima aje.

Kuna jamaa mhindi anablog yake inaitwa SHOUTMELOUD kipindi najifunza ishu za blogging and affiliate marketing huyu jamaa nilimweka kama mentor wangu yaan ukiingia kwenye site yake ilikuw lazima upate Nondo ya ukweli mpaka mtu unashawishika kuingia kwenye full time blogging.

TZ bloggers u must change sio ukipata vijiADS kwenye vikampuni viwil vitatu basi ndio research imeisha haponi mwendo wa copy, ujue unakuwa unajimaliza mwenyewe lazima utengeneze mazingira ya kukua kama unatumia .COM na unapost ENGLISH contents Lazima uhakikishe unapost vitu kuntu ili ujiwekee mazingira ya kupata ADS DUNIANI maana kule malipo ni makubwa sana ya ads tofauti na Tanzania.

I wish you all the best!

If you want .COM domain just check me for only 20,000
0656540271
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom