Unajua kwamba ukitaka kukarabati nyumba yako au kuijengea uzio ni lazima uombe kibali Serikali za Mitaa kabla ya kufanya hivyo?

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279
Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imetilia mkazo sheria ya ardhi na upangaji miji ambayo inamtaka kila mkazi katika eneo lake anapotaka kufanya ukarabati wa nyumba yake, kupaka rangi ama kujenga uzio lazima awe na kibali kutoka halmashauri.

Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni, Aron Kagulumjuli amesema kibali hicho hakitolewi bure bali kinalipiwa, kwamba kuhusu kiasi inategemea na aina ya ukarabati unaofanya.

Amesema kuwa watu wamezoea kufanya kazi kwa mazoea bila usimamizi wa sheria, kwamba sheria hiyo kwa sasa inatekelezwa.

==========================

Kwa mujibu wa Vifungu 124 na 125 vya Kanuni za Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) (Udhibiti Uendelezaji), Sura 288 (GN 242 ya mwaka 2008), Ujenzi wowote ndani ya Mamlaka za Upangaji ambazo ni Mamlaka za Miji Midogo, Halmashauri za Miji, Manispaa na Ma-jijini lazima upate kibali cha Ujenzi kutoka kwenye Mamlaka husika.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 35 (i) cha Sheriaya Mipangomiji Na. 8 ya mwaka 2007,Mamlaka ya Upangaji inatakiwa kutoa kibali cha Ujenzi katika kipindi kisichozidi siku 60 kuanzia tarehe mwombaji alipowasilisha maombi yake. Aidha, ndani ya muda huo mamlaka inatakiwa kumjulisha mwombaji kuwa amekubaliwa au amekataliwa ombi lake na kutaja sababu zilizopelekea ombi lake kukataliwa.
 
Kwa mijini hii ni sawa ila kwa maeneo mfano miji ambayo bado kutangazwa wilaya taratibu kama hizi zinadumaza maendeleo maana kama nimepata 1,000,000 nataka kuanza hata msingi nilazimike kuanza kutafuta ofisi za halmashauri nipunguze hiyo million kwa nauli na ada za kulipia kibali wengi tutaishia kuamua kuzinywa hizo pesa.
 
Hivi nyumba yako ikiezuliwa na upepo unatakiwa pia kungoja hadi utakapopata kibali ndio uweke mabati mapya? Kibali kinachoweza kutoka baada ya siku 59! Mimi nadhani badala ya kuwawekea vizingiti wakazi wake Manispaa ilitakiwa kuwatia moyo ili wakarabati nyumba ambazo zinaweza kusababisha maafa si tu kwa wanaoishi ndani mwake bali pia kwa majirani na wapiga njia.

Amandla
 
Huku kwetu ukijenga bila kibali unakutana na maneno haya kwenye jengo unalojenga, ya rangi nyekundu, fonti size kubwaaa

BOMOA/SITISHA UJENZI, WASILISHA KIBALI CHA UJENZI MANISPAA YA ILEMELA KABLA YA TAREHE 12/4/2020...
 
Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imetilia mkazo sheria ya ardhi na upangaji miji ambayo inamtaka kila mkazi katika eneo lake anapotaka kufanya ukarabati wa nyumba yake, kupaka rangi ama kujenga uzio lazima awe na kibali kutoka halmashauri.

Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni, Aron Kagulumjuli amesema kibali hicho hakitolewi bure bali kinalipiwa, kwamba kuhusu kiasi inategemea na aina ya ukarabati unaofanya.

Amesema kuwa watu wamezoea kufanya kazi kwa mazoea bila usimamizi wa sheria, kwamba sheria hiyo kwa sasa inatekelezwa.

==========================

Kwa mujibu wa Vifungu 124 na 125 vya Kanuni za Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) (Udhibiti Uendelezaji), Sura 288 (GN 242 ya mwaka 2008), Ujenzi wowote ndani ya Mamlaka za Upangaji ambazo ni Mamlaka za Miji Midogo, Halmashauri za Miji, Manispaa na Ma-jijini lazima upate kibali cha Ujenzi kutoka kwenye Mamlaka husika.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 35 (i) cha Sheriaya Mipangomiji Na. 8 ya mwaka 2007,Mamlaka ya Upangaji inatakiwa kutoa kibali cha Ujenzi katika kipindi kisichozidi siku 60 kuanzia tarehe mwombaji alipowasilisha maombi yake. Aidha, ndani ya muda huo mamlaka inatakiwa kumjulisha mwombaji kuwa amekubaliwa au amekataliwa ombi lake na kutaja sababu zilizopelekea ombi lake kukataliwa.
Endeleeni kutukamua mpaka ngama, naona zoezi linaendelea la kamua kamua wananchi wa donaz kantri
 
Hivi nyumba yako ikiezuliwa na upepo unatakiwa pia kungoja hadi utakapopata kibali ndio uweke mabati mapya? Kibali kinachoweza kutoka baada ya siku 59! Mimi nadhani badala ya kuwawekea vizingiti wakazi wake Manispaa ilitakiwa kuwatia moyo ili wakarabati nyumba ambazo zinaweza kusababisha maafa si tu kwa wanaoishi ndani mwake bali pia kwa majirani na wapiga njia.

Amandla
Hata rangi inayotaka nusu saa utumie masiku. Kujenga sawa lakini rangi au kuweka dirisha jipya au mlango

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom