Unaishi vipi na jirani anayependa dezo na kuombaomba?

Kuna mpangaji mwenzangu hapa ana mume wake bodaboda hajamaliza hata wiki picha linaanza asubhi anamtoa mtoto wake aje kuomba uji au chai yaan yy hapiki sana sana ataenda kununua chai au uji, ukifika mchana hapiki chochote mnachopika anataka mumpatia na yy , yaan wiki tu tushamchoka namuonea huruma sana binti yao maana wakat mwingine hata hawajui amekula nn na Yuko wapi....

Wanaume tuangalie sana wanawake wa kuoa jamani.
Aisee

Hii mbona hatari!
 
Najua jirani ni ndugu wa karibu ila kuna mengine yamezidi.

Jirani alikua anakuja kuomba chaji nikaona sio kesi nimenunua nyingine nikamuachia atumie.

Bado basi yake imeharibika hana mpango wa kuitengeneza wala kununua nikaona sikesi usumbufu umezidi nichukue nyingine, sasa naona haajiongezi, chaji ile sijui imekuaje anakuja tena kugonga nimuwekee chaji, waungwana ujirani huu unafanyaje?
Chunguza vizuri, huenda kuna "agenda" ya ziada. Jirani yako ni wa jinsia tofauti na yako?
 
Kuna mmoja alikuja kuazima pasi akaunguza waya nikakausha bahati nzuri nilikuanayo nyingine ambayo niliinunua nikiwa kwrnye safari moja hivi, so kila akija kuomba nampa ile mbovu na sijui anaitumiaje!? Maana haipeleki moto

Hahahahah kuna watu wamakiti humu
 
Natengwa na majirani sababu ya mmea, kuna kisa fulani nikikumbuka mpaka nacheka kuna siku nilikuwa naelekea dukani usiku kununua mkate maana kesho yake nilikuwa nawahi asubuhi sana kutoka.

Kuna mama fulani wa makamo alikuwa anaelekea njia moja na mimi ila yupo mbele yangu ndio anaenda nyumbani kwake sasa nikiongeza mwendo na yeye anaongeza mwendo nisimkaribie mpaka akakata sandals alizokuwa amevaa.

Kumsemesha namuona ana hofu kama anatetemeka na hasira, alibahatisha kuna toyo ilikuwa inapita akaichukua na kwenda nayo umbali haufiki hata nusu kilomita kesho yake nilikuja kusikia stori mtaani eti alinusurika kukabwa na wavuta bangi wa mtaani duh nikajua kumbe najulikana mtaani na na kuogopwa kabisa, hamna mtu mwenye time na mimi wanajua ni mhuni tu anayepuliza mmea kila saa, na mimi nawaacha wanichukulie hivyo hivyo sitaki mazoea
nimecheka sana
 
Noma sna acha tu Mkuu
Hapa ninavo type kuna jirani yangu yupo ndani kashika na remote zote za screen na king’amuzi yani imebidi nitoke tu nje nimwache lakini ikifika mida ya mechi za mpila naenda kumtoa..yan mtu ukimcheki mnaheshimiana lakini mambo yake ukiyatafakari unakuwa unajiuliza inamaana yeye haoni majirani zake wanaishi vipi..
 
Kuna mmoja alikuja kuazima pasi akaunguza waya nikakausha bahati nzuri nilikuanayo nyingine ambayo niliinunua nikiwa kwrnye safari moja hivi, so kila akija kuomba nampa ile mbovu na sijui anaitumiaje!? Maana haipeleki moto
Lahaulaaa... Mkuu! Umeniacha hoi...
 
Shuleni tulikuwa tukifungua mtu anapewa pocket money ananunua Air Force, mi nanunua mahitaji yote na ya ziada. Baadae anakuja kuomba dawa ya meno, namjibu kavae Air Force hata usiswaki bro si umeona ndio muhimu

Mwingine anazoea kuomba omba peanut au makorokoro gani. Jibu langu ni kama huumwi kwa kuikosa ujue peanut kwako sio lazima. Ingekuwa muhimu ungelazwa, mimi ni muhimu ndio maana nimenunua

Tabia za kuwapa watu wenye uwezo vitu inalemaza mno. Nilijua hili mapema baada ya kuona ndugu wa mtu fulani maarufu hapa nchini hawana mbele wala nyuma kisa tu ndugu yao anawapa hela wakihitaji. Hawafanyi kazi, ikafika siku jamaa akawa na kesi na TAKUKURU ndugu zake mibaba mizima ilikuwa kama yatima ikakosa hata hela kulisha familia
 
Natengwa na majirani sababu ya mmea, kuna kisa fulani nikikumbuka mpaka nacheka kuna siku nilikuwa naelekea dukani usiku kununua mkate maana kesho yake nilikuwa nawahi asubuhi sana kutoka.

Kuna mama fulani wa makamo alikuwa anaelekea njia moja na mimi ila yupo mbele yangu ndio anaenda nyumbani kwake sasa nikiongeza mwendo na yeye anaongeza mwendo nisimkaribie mpaka akakata sandals alizokuwa amevaa.

Kumsemesha namuona ana hofu kama anatetemeka na hasira, alibahatisha kuna toyo ilikuwa inapita akaichukua na kwenda nayo umbali haufiki hata nusu kilomita kesho yake nilikuja kusikia stori mtaani eti alinusurika kukabwa na wavuta bangi wa mtaani duh nikajua kumbe najulikana mtaani na na kuogopwa kabisa, hamna mtu mwenye time na mimi wanajua ni mhuni tu anayepuliza mmea kila saa, na mimi nawaacha wanichukulie hivyo hivyo sitaki mazoea
Watu bana
 
Kuna mpangaji mwenzangu hapa ana mume wake bodaboda hajamaliza hata wiki picha linaanza asubhi anamtoa mtoto wake aje kuomba uji au chai yaan yy hapiki sana sana ataenda kununua chai au uji, ukifika mchana hapiki chochote mnachopika anataka mumpatia na yy , yaan wiki tu tushamchoka namuonea huruma sana binti yao maana wakat mwingine hata hawajui amekula nn na Yuko wapi....

Wanaume tuangalie sana wanawake wa kuoa jamani.
Duu kumbe wako wengi, kwakweli hii hali inatia hasira, na kibaya unakuta hata ukisema umuoneshe mtu kua umekasirika ila yeye hajiongezi, atarudi tena
 
Someni hapa mnaoombwa
%E8%B6%85%E7%BA%A7%E6%88%AA%E5%B1%8F_20210828_000503.jpg


Sent from my vivo X6D using JamiiForums mobile app
 
Najua jirani ni ndugu wa karibu ila kuna mengine yamezidi.

Jirani alikua anakuja kuomba chaji nikaona sio kesi nimenunua nyingine nikamuachia atumie.

Bado basi yake imeharibika hana mpango wa kuitengeneza wala kununua nikaona sikesi usumbufu umezidi nichukue nyingine, sasa naona haajiongezi, chaji ile sijui imekuaje anakuja tena kugonga nimuwekee chaji, waungwana ujirani huu unafanyaje?
Kama ni jinsia tofauti na wewe Kuna anachohitaji zaidi ya hiyo charger !!
 
Kuna mtu unamsaidia akiwa nashida akipata kidogo tu anakuaona ww ninadui yake! Hii kitu hua inanipatabu kidogo ila mungu kanipa moyo wa ushujaaa akirudi na mpokea tunaendelea na maisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom