LUS0MYA
JF-Expert Member
- Aug 4, 2011
- 851
- 1,077
Waziri anayehusika atoe amri ya ukaguzi wa dharura na kutumia vyombo vya usalama na TAKUKURU kwa kuwa kuna viashiria vikubwa ya matumizi mabaya ya fedha na utoaji mikopo mwaka huu licha ya serikali kusema kuwa imetenga bajeti kubwa zaidi kuliko miaka mingine.
1. Idadi ya wanafunzi walioomba mikopo wakakosa ni wengi sana na hata waliopata wengi wao ni asilimia 40 kushuka chini.
2. Msimu huu ulishuhudia kuongezeka kwa idadi kubwa ya waombaji walioomba kukata rufaa ya kunyimwa mikopo kulinganisha na miaka mingine.
Swali la kujiuliza hii pesa iliyotengwa imelipwa kwa nani?isije yakaibuka yale mambo ya kulipa waombaji hewa" Kama serikali haikutoa fedha ya kutosha basi taarifa iwekwe wazi.
Ushauri wa mwisho ni bodi kuchapisha majina ya waombaji mkopo hasas wa mara ya kwanza waliopata na kiasi walichopata kupitia gazeti la serikali au vyombo vingine.
Kama ilivyotolewa na chuo cha udaktari Bugando. Vyuo pia vitoe taarifa ya idadi ya wanafunzi waliodahiliwa na wale walioshindwa kuendelea na masomo kwa kukosa mkopo.
Nawakilisha.
1. Idadi ya wanafunzi walioomba mikopo wakakosa ni wengi sana na hata waliopata wengi wao ni asilimia 40 kushuka chini.
2. Msimu huu ulishuhudia kuongezeka kwa idadi kubwa ya waombaji walioomba kukata rufaa ya kunyimwa mikopo kulinganisha na miaka mingine.
Swali la kujiuliza hii pesa iliyotengwa imelipwa kwa nani?isije yakaibuka yale mambo ya kulipa waombaji hewa" Kama serikali haikutoa fedha ya kutosha basi taarifa iwekwe wazi.
Ushauri wa mwisho ni bodi kuchapisha majina ya waombaji mkopo hasas wa mara ya kwanza waliopata na kiasi walichopata kupitia gazeti la serikali au vyombo vingine.
Kama ilivyotolewa na chuo cha udaktari Bugando. Vyuo pia vitoe taarifa ya idadi ya wanafunzi waliodahiliwa na wale walioshindwa kuendelea na masomo kwa kukosa mkopo.
Nawakilisha.