Nawatania
Senior Member
- Jul 13, 2021
- 148
- 549
Fursa maana yake ulione tatizo na utafute njia za kulitatua huku ukitengeneza pesa.
Ndio maana watu wengi ushindwa kuziona fursa maana hawapendi kutatua matatizo.
Daktari anatibu mgonjwa na anapata pesa
Mwalimu anapelekewa mwanafunzi hasiyejua kusoma wala kuandika anamtengeneza yeye kuwa Dactari, Mwalimu wake na mwalimu au injinia.
Niende kwenye mada; Tanzania ni kama nchi zingine ambazo zinaendea hivyo Tanzania ina fursa nyingi sana kama ambavyo nchi zote zinazoendelea zilivyojaa fursa.
Kwa kutumia technojia ya habari na mawasiliano kuna fursa kubwa naenda kukupa hapa chini.
Unaanzaje? Zunguka mitaa yote ya Tanzania hasa mijini utakutana na matangazo ya karatasi mtaani huyu anatangaza Shule, huyu anatangaza Chuo, huyu anatangaza ajira, huyu anatangaza tenda, wengine wanajitangaza nyakati za uchaguzi lakini zile Karatasi uwa zinaacha uchafuzi mkubwa wa mazingira hasa kuta mbalimbali za majengo maeneo mbali mbali mijini.
Hii ni fursa kwa sababu zifuatazo
1: Hakuna serikali yeyote duniani inayopenda mazingira yake yachafuliwe
2: Serikali itailinda biashara yako kwa sababu itapanua wigo wa ukusanyaji kodi
3: Makampuni wanatumia gharama kubwa sana kutangaza maana wanachapisha wenyewe matangazo, Wanayasambaza wenyewe na wanayalinda wenyewe yasibanduliwe yalipowekwa utawashawishi kwa kuwafanyia kila kitu.
4: Watu wengi utapeliwa pesa na baadhi ya makampuni hewa ambayo utangaza fursa hewa kwa sababu hakuna monitoring kwa makampuni husika.
Hizi hoja tatu zitakufanya upate pesa wewe kwa kutumia fursa hii ipasavyo.
Jinsi ya kuanza: Kasajili kampuni BRELA ambayo inajihusisha na mambo ya tekinolojia ya mawasiano, Pata Till namba na Reseni ya biashara anza kazi hivi.
Zitumie halimashauri za miji na majiji na uhakikishe unapata eneo la kujenga note board ambayo nitaonyesha picha yake hapo chini, Notes board zako ziwekewe taa ( electrical instillation) yaani wakati wa usiku iwake na waambie halimashauri ya kampuni yako itakapoanzia kwamba unahitaji tenda za matangazo yao uwe unawatangazia bure kwenye notes board zako watakupa
Fanya lobbying katika halimashauri hiyo wapige marufuku matangazo kubandikwa ovyo ovyo kwa kuwaelezea hasara zake kama nilivyozitaja hapo juu likiwepo swala la kodi waambie wewe utalipa kodi na VAT.
Hakuna halimashauri itagoma kukupa hii fursa hapo utatengeneza team kwenda maofisi yote na kuomba matangazo na kuacha mawasiliano ya kampuni yako.
Utatoa ajira kwa vijana maana kila kitu kitafanywa na kampuni yako kama Kudezaini, Kusimamia matangazo yenye kutaka kutapeli watu hii itakufanya kuwa karibu sana na Makampuni mengi na Serikali.
Pia hakikisha unakuwa na notes board za kutosha mjini pia uwe mbunifu mfano notes board chini yake unaweza kuweka kituo cha kuuzia magazeti kwenye kila notes board yako na kuwapa bule vijana watumie kuuzia huku wakilinda notes board ya kampuni yako na hii itakusaidia kwenye masoko maana watu wengi usimama kwenye vituo vya magazeti hivyo itakufanya upate wateja wengi wanafika kwenye notes board za kampuni yako na wakati huo kuwashawishi wateja watangaze na wewe.
Utaweka bei ya kawaida ya kuanzia kwa kigezo cha mtu au kampuni inataka kutangaziwa wapi? Kama ni note board moja labda ya posta utajua bei yako iweje kuna mwingine atakwambia anataka kutangaza notes board zote za Dar yaani (promotion announcement) utaweka utaratibu.
Nakaribisha maswali kwa fursa hii labda kama kuna jambo nimesahau kuliandika niulize nitakujibu
Kesho nitakuja na fursa nyingine
Ndio maana watu wengi ushindwa kuziona fursa maana hawapendi kutatua matatizo.
Daktari anatibu mgonjwa na anapata pesa
Mwalimu anapelekewa mwanafunzi hasiyejua kusoma wala kuandika anamtengeneza yeye kuwa Dactari, Mwalimu wake na mwalimu au injinia.
Niende kwenye mada; Tanzania ni kama nchi zingine ambazo zinaendea hivyo Tanzania ina fursa nyingi sana kama ambavyo nchi zote zinazoendelea zilivyojaa fursa.
Kwa kutumia technojia ya habari na mawasiliano kuna fursa kubwa naenda kukupa hapa chini.
Unaanzaje? Zunguka mitaa yote ya Tanzania hasa mijini utakutana na matangazo ya karatasi mtaani huyu anatangaza Shule, huyu anatangaza Chuo, huyu anatangaza ajira, huyu anatangaza tenda, wengine wanajitangaza nyakati za uchaguzi lakini zile Karatasi uwa zinaacha uchafuzi mkubwa wa mazingira hasa kuta mbalimbali za majengo maeneo mbali mbali mijini.
Hii ni fursa kwa sababu zifuatazo
1: Hakuna serikali yeyote duniani inayopenda mazingira yake yachafuliwe
2: Serikali itailinda biashara yako kwa sababu itapanua wigo wa ukusanyaji kodi
3: Makampuni wanatumia gharama kubwa sana kutangaza maana wanachapisha wenyewe matangazo, Wanayasambaza wenyewe na wanayalinda wenyewe yasibanduliwe yalipowekwa utawashawishi kwa kuwafanyia kila kitu.
4: Watu wengi utapeliwa pesa na baadhi ya makampuni hewa ambayo utangaza fursa hewa kwa sababu hakuna monitoring kwa makampuni husika.
Hizi hoja tatu zitakufanya upate pesa wewe kwa kutumia fursa hii ipasavyo.
Jinsi ya kuanza: Kasajili kampuni BRELA ambayo inajihusisha na mambo ya tekinolojia ya mawasiano, Pata Till namba na Reseni ya biashara anza kazi hivi.
Zitumie halimashauri za miji na majiji na uhakikishe unapata eneo la kujenga note board ambayo nitaonyesha picha yake hapo chini, Notes board zako ziwekewe taa ( electrical instillation) yaani wakati wa usiku iwake na waambie halimashauri ya kampuni yako itakapoanzia kwamba unahitaji tenda za matangazo yao uwe unawatangazia bure kwenye notes board zako watakupa
Fanya lobbying katika halimashauri hiyo wapige marufuku matangazo kubandikwa ovyo ovyo kwa kuwaelezea hasara zake kama nilivyozitaja hapo juu likiwepo swala la kodi waambie wewe utalipa kodi na VAT.
Hakuna halimashauri itagoma kukupa hii fursa hapo utatengeneza team kwenda maofisi yote na kuomba matangazo na kuacha mawasiliano ya kampuni yako.
Utatoa ajira kwa vijana maana kila kitu kitafanywa na kampuni yako kama Kudezaini, Kusimamia matangazo yenye kutaka kutapeli watu hii itakufanya kuwa karibu sana na Makampuni mengi na Serikali.
Pia hakikisha unakuwa na notes board za kutosha mjini pia uwe mbunifu mfano notes board chini yake unaweza kuweka kituo cha kuuzia magazeti kwenye kila notes board yako na kuwapa bule vijana watumie kuuzia huku wakilinda notes board ya kampuni yako na hii itakusaidia kwenye masoko maana watu wengi usimama kwenye vituo vya magazeti hivyo itakufanya upate wateja wengi wanafika kwenye notes board za kampuni yako na wakati huo kuwashawishi wateja watangaze na wewe.
Utaweka bei ya kawaida ya kuanzia kwa kigezo cha mtu au kampuni inataka kutangaziwa wapi? Kama ni note board moja labda ya posta utajua bei yako iweje kuna mwingine atakwambia anataka kutangaza notes board zote za Dar yaani (promotion announcement) utaweka utaratibu.
Nakaribisha maswali kwa fursa hii labda kama kuna jambo nimesahau kuliandika niulize nitakujibu
Kesho nitakuja na fursa nyingine