SoC01 Unahitaji kuanzisha biashara? Chukua fursa hii

Stories of Change - 2021 Competition

Nawatania

Senior Member
Jul 13, 2021
148
549
Fursa maana yake ulione tatizo na utafute njia za kulitatua huku ukitengeneza pesa.

Ndio maana watu wengi ushindwa kuziona fursa maana hawapendi kutatua matatizo.

Daktari anatibu mgonjwa na anapata pesa
Mwalimu anapelekewa mwanafunzi hasiyejua kusoma wala kuandika anamtengeneza yeye kuwa Dactari, Mwalimu wake na mwalimu au injinia.

Niende kwenye mada; Tanzania ni kama nchi zingine ambazo zinaendea hivyo Tanzania ina fursa nyingi sana kama ambavyo nchi zote zinazoendelea zilivyojaa fursa.

Kwa kutumia technojia ya habari na mawasiliano kuna fursa kubwa naenda kukupa hapa chini.

Unaanzaje? Zunguka mitaa yote ya Tanzania hasa mijini utakutana na matangazo ya karatasi mtaani huyu anatangaza Shule, huyu anatangaza Chuo, huyu anatangaza ajira, huyu anatangaza tenda, wengine wanajitangaza nyakati za uchaguzi lakini zile Karatasi uwa zinaacha uchafuzi mkubwa wa mazingira hasa kuta mbalimbali za majengo maeneo mbali mbali mijini.

Hii ni fursa kwa sababu zifuatazo

1: Hakuna serikali yeyote duniani inayopenda mazingira yake yachafuliwe

2: Serikali itailinda biashara yako kwa sababu itapanua wigo wa ukusanyaji kodi

3: Makampuni wanatumia gharama kubwa sana kutangaza maana wanachapisha wenyewe matangazo, Wanayasambaza wenyewe na wanayalinda wenyewe yasibanduliwe yalipowekwa utawashawishi kwa kuwafanyia kila kitu.

4: Watu wengi utapeliwa pesa na baadhi ya makampuni hewa ambayo utangaza fursa hewa kwa sababu hakuna monitoring kwa makampuni husika.

Hizi hoja tatu zitakufanya upate pesa wewe kwa kutumia fursa hii ipasavyo.

Jinsi ya kuanza: Kasajili kampuni BRELA ambayo inajihusisha na mambo ya tekinolojia ya mawasiano, Pata Till namba na Reseni ya biashara anza kazi hivi.

Zitumie halimashauri za miji na majiji na uhakikishe unapata eneo la kujenga note board ambayo nitaonyesha picha yake hapo chini, Notes board zako ziwekewe taa ( electrical instillation) yaani wakati wa usiku iwake na waambie halimashauri ya kampuni yako itakapoanzia kwamba unahitaji tenda za matangazo yao uwe unawatangazia bure kwenye notes board zako watakupa

Fanya lobbying katika halimashauri hiyo wapige marufuku matangazo kubandikwa ovyo ovyo kwa kuwaelezea hasara zake kama nilivyozitaja hapo juu likiwepo swala la kodi waambie wewe utalipa kodi na VAT.

Hakuna halimashauri itagoma kukupa hii fursa hapo utatengeneza team kwenda maofisi yote na kuomba matangazo na kuacha mawasiliano ya kampuni yako.

Utatoa ajira kwa vijana maana kila kitu kitafanywa na kampuni yako kama Kudezaini, Kusimamia matangazo yenye kutaka kutapeli watu hii itakufanya kuwa karibu sana na Makampuni mengi na Serikali.

Pia hakikisha unakuwa na notes board za kutosha mjini pia uwe mbunifu mfano notes board chini yake unaweza kuweka kituo cha kuuzia magazeti kwenye kila notes board yako na kuwapa bule vijana watumie kuuzia huku wakilinda notes board ya kampuni yako na hii itakusaidia kwenye masoko maana watu wengi usimama kwenye vituo vya magazeti hivyo itakufanya upate wateja wengi wanafika kwenye notes board za kampuni yako na wakati huo kuwashawishi wateja watangaze na wewe.

Utaweka bei ya kawaida ya kuanzia kwa kigezo cha mtu au kampuni inataka kutangaziwa wapi? Kama ni note board moja labda ya posta utajua bei yako iweje kuna mwingine atakwambia anataka kutangaza notes board zote za Dar yaani (promotion announcement) utaweka utaratibu.

Nakaribisha maswali kwa fursa hii labda kama kuna jambo nimesahau kuliandika niulize nitakujibu

Kesho nitakuja na fursa nyingine
images (21).jpg
images (22).jpg
 
Gharama za mtaji ghafi ni kiasi gani
Kwa kuanza ukiwa na milioni 2.5minimum inatosha unaanza nikupe mchanganua kidogo

Kama hauna fremu maana yake unatakiwa kutafuta frem sio lazima iwe mjini au sehemu inayoonekana no unaweza weka sehemu yeyote chumba hata kikiwa cha 60000×6 ni 360,000

Njoo kwenye usajili wa brela till namba na reseni ya biashara kwa kuanzia utumie 640,000 maana gharama za mizunguko na usumbufu wakati wa kitafuta vibali.

Hiyo million moja anza kudesign mbao za matangazo minimum mbao nzuri ya matangazo ambayo unaweza chukua angalau matangazo 100 kwa wakati mmoja ipigie buget ya laki 3 ila inategemea na mtengenezaji mwingine anaweza kukwambia laki 5

Kwa hiyo ukipata wa laki 3 utaanza na notes board 3 na ukipata wa laki 5 utaanza na notes board 2

Laki tano inayobaki ni kwa kuanza marketing na promotion ya kampuni yako na kwenda field kutafuta biashara katika halimashauri husika.


Lakini kwa milioni 2.5 hii kampuni inasimama na inaanza operations zake.
 
Wazo lako zuri sana na tamu lakini ulipogusia Brela tena na TRA badi muitikio utakuwa mdogo.

Ni bora zingekuwa free kwa sasa zikishakuwa nyingi ndio zisajiliwe na serikali
Pia inawezekana ukaanza bila vibali nimetoa angalizo la kisheria na mambo ya copyright maana ukishaingia kama kampuni monopoly inakuwa ni rahisi badae kutengeneza pesa wakati umetulia kama walivyo posta, tanesco na dawasco.
 
WAZO LA PILI:

Niende moja kwa moja kwenye mada nimesema kila siku nitatoa wazo angalau moja la biashara

Wazo jepesi kabisa ambalo halina mambo mengi ni katika pia tasinia ya Utanashati hasa kwa vijana wa kiume. Ingawa hata vijana wa like viatu vya vinahitaji kufanyiwa polishing.

Ukitembea kwenye miji yetu mingi Tanzania utaona watu bado wanafanya kazi vile vile miaka naenda miaka rudi wenye ubunifu ni wachache wengi wamemezwa na utamaduni hawaendelezi biashara zao kama inavyotakiwa hivyo Mimi nimeiona tena fursa katika biashara ya kung'alisha viatu.

Kungalisha viatu ni nini? Ni kule kuondoka vumbi na uchafu mwingine katika ngozi ya kiatu kiwe cha kiume au cha kike.

Ukipita miji yetu utawakuta vijana wanafanya kazi hii wapo katika mazingira ambayo sio rafiki kwa wateja.

Lakini ukiangalia kwa upana na umakini hii biashara ni moja ya biashara inayolipa kupita maelezo mfano kubrashi kiatu kimoja uchukua kama dakika 5 tu na ni shilling 1000 kwa mijini lakini kazi hii imeonekana sio kazi ya wasomi ni kazi ya watu ambayo hawajaenda shule kabisa kitu ambacho sio kweli kila mtanzania anawezafanya hii kazi uwe na master's, degree, diploma, certificate au hauna cheti chochote unaweza kufanya hii biashara.

Mapungufu ya wale wanaoifanya yachukue kama fursa

Hatua ya kwanza nenda katengeneze viti vya wateja vya kukaa wakati wanasafishiwa viatu nitakuonyesha kwenye picha hapo chini.

Tafuta maeneo ya miji yenye mabosi wengi na wafanyakazi wengi mfano kwa Dar es salaam kuna maeneo mengi ila nakutajia baadhi
Mlima city
Posta ya zamani
Posta mpya
Makumbusho
Muhimbili
Kumara
Stationi
Na maeneo mengine mengi baada ya kutengeneza hicho kiti peleka hayo maeneo tafuta wafanyakazi very smart kila kiti kiwe na wafanyakazi wawili mmoja wa wakike na mwingine wa kiume, wape simina ya angalau wiki moja jinsi ya kufanya kazi na kuwa wakalimu kwa wateja.

Hakikisha kila kiti cha polishing kinakuwa na gazeti moja utakuwa unabadilisha mfano Tanzania watu wengi wanapenda kusoma gazeti gani la siasa na la michezo? Fanya utafiti na hakikisha kila unapofungua asubuhi liwepo.

Pia tafuta mtu mpe tenda ya Ku supply karanga kwenye vituo vyako afunge karanga ndogo ndogo ambazo mteja akija anakula wakati anabrashiwa viatu vyake hii ni kwa sababu ya kupata watu wengi.

Tagert ni watu 30-50 kwa kila kiti chako na ili kukwepa kuibiwa unaweza waambia wale wafanyakazi wako kwamba wakulipe wenyewe kwa siku unawaambia mfano kwa siku moja unahitaji shilingi 12000.
Hapo utaweka shilingi 10000 benki na elf moja utawanunulia gazeti na elf moja utaweka kwenye budget ya karanga kila siku

Chukulia umeanza na vituo 5 maana yake ni 5×10000= 50000×30 ni 1.5 million kwa mwezi

Weka malengo ya kuwa na vituo 200 Tanzania nzima utakuwa ukitengeneza pesa kiasi gani?

Unaanza kupanua biashara zako sasa unaongeza viti na kupanuka ikiwezekana Tanzania nzima utapata wateja wa kutosha na unaliteka soko.

Baada ya hapo unaweza kubadilisha strategies za kufanya biashara yako sasa kulingana na watu wengine utakuwa hauwafikii mfano unaweza kuwa na magari ambayo ndani yake utadesign sehemu ya kubrashi viatu vya wateja kulingana na foleni ya Dar unakuwa na magari yanayoanzia Mbagala kuja mjini mbezi stand ya magufuli kuja mjini na Bunju kuja mjini yakipita maeneo mbali mbali unapandisha watu bure na unaweka sehemu ya kusafishwa viatu kwa wakina mama na baba na kucha kwa wakina Dada ndani ya gari.

Utakusanya pesa za kutosha na kampuni ya namna hii sio lazima uwe na pesa nyingi hapana unaweza kuanza hata na kiti kimoja ila kazi inayotakiwa kufanyika ni kwenye marketing.

Hii ni biashara kubwa na hapa nimeongea 30% ya hiyo idea.

Naomba nikomee hapa kwa Leo nitaongeza pia kesho

images (15).jpeg


images (18).jpeg


images (17).jpeg
 
Ni idea nzuri sana hii mkuu.
Katika utafiti wako ilishawahi kufanywa hapa tz??
Nadhani ina ufanano na wale wa mabango.
Ndio inafanana lakini hii unakuwa unafanya matangazo madogomadogo yaani hata tangazo la msiba unaweka
 
Unadhani mtangazaji atakupa ngapi kwa tangazo lake kwenye notice board ? Na wewe unadhani utatoa ngapi ku-maintain hayo matangazo (ingawa kwa ushauri kwenye supermarkets, mashule na other public areas unaweza kuweka bure...)

Kwa ushauri badala ya kuwaambia watu utawatangazia vipeperushi vyao waambie utawapelekea wateja kiasi kadhaa yaani wakulipe through more business they get, tengeneza booklet ulisambaze bure kwahio watu watakuja kwako kutangaza na wewe utawatangazia (though kwenye huu uchumi wa kati tegemea low turnout ya wateja) yaani huenda mapato yakawa chini kulinganisha na matumizi

By the way kwenye mabango pia mwigulu amepita (ni mwendo wa tozo tu...)
 
Unadhani mtangazaji atakupa ngapi kwa tangazo lake kwenye notice board ? Na wewe unadhani utatoa ngapi ku-maintain hayo matangazo (ingawa kwa ushauri kwenye supermarkets, mashule na other public areas unaweza kuweka bure...)

Kwa ushauri badala ya kuwaambia watu utawatangazia vipeperushi vyao waambie utawapelekea wateja kiasi kadhaa yaani wakulipe through more business they get, tengeneza booklet ulisambaze bure kwahio watu watakuja kwako kutangaza na wewe utawatangazia (though kwenye huu uchumi wa kati tegemea low turnout ya wateja) yaani huenda mapato yakawa chini kulinganisha na matumizi

By the way kwenye mabango pia mwigulu amepita (ni mwendo wa tozo tu...)
Mkuu ndio maana nimekwambia unatakiwa kwenda pole pole kwa kila hatua usiangalie faida kwa nje na haraka angalia utafanya kufanya nini? Na je unataka kutafuta solution ya tatizo?

Jibu ni ndio unatakiwa kuweka utaratibu ambao kwanza utahakikisha kampuni yako inakuwa monopoly kwanza then matangazo yapigwe marufuku kutangazwa ovyo mtaani na halimashauri ukifanikiwa hapo utakuwa maana yake umewini watu wote wanaotangaza mtaani!!

Maana watakuwa hawana sehemu ya kutangaza zaidi ya kwenye mbao zako za matangazo.

Biashara lazima iwepo
 
WAZO LA PILI:

Niende moja kwa moja kwenye mada nimesema kila siku nitatoa wazo angalau moja la biashara

Wazo jepesi kabisa ambalo halina mambo mengi ni katika pia tasinia ya Utanashati hasa kwa vijana wa kiume. Ingawa hata vijana wa like viatu vya vinahitaji kufanyiwa polishing.

Ukitembea kwenye miji yetu mingi Tanzania utaona watu bado wanafanya kazi vile vile miaka naenda miaka rudi wenye ubunifu ni wachache wengi wamemezwa na utamaduni hawaendelezi biashara zao kama inavyotakiwa hivyo Mimi nimeiona tena fursa katika biashara ya kung'alisha viatu.

Kungalisha viatu ni nini? Ni kule kuondoka vumbi na uchafu mwingine katika ngozi ya kiatu kiwe cha kiume au cha kike.

Ukipita miji yetu utawakuta vijana wanafanya kazi hii wapo katika mazingira ambayo sio rafiki kwa wateja.

Lakini ukiangalia kwa upana na umakini hii biashara ni moja ya biashara inayolipa kupita maelezo mfano kubrashi kiatu kimoja uchukua kama dakika 5 tu na ni shilling 1000 kwa mijini lakini kazi hii imeonekana sio kazi ya wasomi ni kazi ya watu ambayo hawajaenda shule kabisa kitu ambacho sio kweli kila mtanzania anawezafanya hii kazi uwe na master's, degree, diploma, certificate au hauna cheti chochote unaweza kufanya hii biashara.

Mapungufu ya wale wanaoifanya yachukue kama fursa

Hatua ya kwanza nenda katengeneze viti vya wateja vya kukaa wakati wanasafishiwa viatu nitakuonyesha kwenye picha hapo chini.

Tafuta maeneo ya miji yenye mabosi wengi na wafanyakazi wengi mfano kwa Dar es salaam kuna maeneo mengi ila nakutajia baadhi
Mlima city
Posta ya zamani
Posta mpya
Makumbusho
Muhimbili
Kumara
Stationi
Na maeneo mengine mengi baada ya kutengeneza hicho kiti peleka hayo maeneo tafuta wafanyakazi very smart kila kiti kiwe na wafanyakazi wawili mmoja wa wakike na mwingine wa kiume, wape simina ya angalau wiki moja jinsi ya kufanya kazi na kuwa wakalimu kwa wateja.

Hakikisha kila kiti cha polishing kinakuwa na gazeti moja utakuwa unabadilisha mfano Tanzania watu wengi wanapenda kusoma gazeti gani la siasa na la michezo? Fanya utafiti na hakikisha kila unapofungua asubuhi liwepo.

Pia tafuta mtu mpe tenda ya Ku supply karanga kwenye vituo vyako afunge karanga ndogo ndogo ambazo mteja akija anakula wakati anabrashiwa viatu vyake hii ni kwa sababu ya kupata watu wengi.

Tagert ni watu 30-50 kwa kila kiti chako na ili kukwepa kuibiwa unaweza waambia wale wafanyakazi wako kwamba wakulipe wenyewe kwa siku unawaambia mfano kwa siku moja unahitaji shilingi 12000.
Hapo utaweka shilingi 10000 benki na elf moja utawanunulia gazeti na elf moja utaweka kwenye budget ya karanga kila siku

Chukulia umeanza na vituo 5 maana yake ni 5×10000= 50000×30 ni 1.5 million kwa mwezi

Weka malengo ya kuwa na vituo 200 Tanzania nzima utakuwa ukitengeneza pesa kiasi gani?

Unaanza kupanua biashara zako sasa unaongeza viti na kupanuka ikiwezekana Tanzania nzima utapata wateja wa kutosha na unaliteka soko.

Baada ya hapo unaweza kubadilisha strategies za kufanya biashara yako sasa kulingana na watu wengine utakuwa hauwafikii mfano unaweza kuwa na magari ambayo ndani yake utadesign sehemu ya kubrashi viatu vya wateja kulingana na foleni ya Dar unakuwa na magari yanayoanzia Mbagala kuja mjini mbezi stand ya magufuli kuja mjini na Bunju kuja mjini yakipita maeneo mbali mbali unapandisha watu bure na unaweka sehemu ya kusafishwa viatu kwa wakina mama na baba na kucha kwa wakina Dada ndani ya gari.

Utakusanya pesa za kutosha na kampuni ya namna hii sio lazima uwe na pesa nyingi hapana unaweza kuanza hata na kiti kimoja ila kazi inayotakiwa kufanyika ni kwenye marketing.

Hii ni biashara kubwa na hapa nimeongea 30% ya hiyo idea.

Naomba nikomee hapa kwa Leo nitaongeza pia kesho

View attachment 1855872

View attachment 1855873

View attachment 1855874
Wazo bora kabisa la biashara hakuna kodi hakuna fremu hakuna chochote yaani kiti chako kimoja unaanza hata mwenyewe.
 
Fursa maana yake ulione tatizo na utafute njia za kulitatua huku ukitengeneza pesa.

Ndio maana watu wengi ushindwa kuziona fursa maana hawapendi kutatua matatizo.

Dactari anatibu mgonjwa na anapata pesa
Mwalimu anapelekewa mwanafunzi hasiyejua kusoma wala kuandika anamtengeneza yeye kuwa Dactari, Mwalimu wake na mwalimu au injinia.

Niende kwenye mada; Tanzania ni kama nchi zingine ambazo zinaendea hivyo Tanzania ina fursa nyingi sana kama ambavyo nchi zote zinazoendelea zilivyojaa fursa.

Kwa kutumia technojia ya habari na mawasiliano kuna fursa kubwa naenda kukupa hapa chini.

Unaanzaje? Zunguka mitaa yote ya Tanzania hasa mijini utakutana na matangazo ya karatasi mtaani huyu anatangaza Shule, huyu anatangaza Chuo, huyu anatangaza ajira, huyu anatangaza tenda, wengine wanajitangaza nyakati za uchaguzi lakini zile Karatasi uwa zinaacha uchafuzi mkubwa wa mazingira hasa kuta mbalimbali za majengo maeneo mbali mbali mijini.

Hii ni fursa kwa sababu zifuatazo
1: Hakuna serikali yeyote duniani inayopenda mazingira yake yachafuliwe

2: Serikali itailinda biashara yako kwa sababu itapanua wigo wa ukusanyaji kodi

3: Makampuni wanatumia gharama kubwa sana kutangaza maana wanachapisha wenyewe matangazo, Wanayasambaza wenyewe na wanayalinda wenyewe yasibanduliwe yalipowekwa utawashawishi kwa kuwafanyia kila kitu.

4: Watu wengi utapeliwa pesa na baadhi ya makampuni hewa ambayo utangaza fursa hewa kwa sababu hakuna monitoring kwa makampuni husika.

Hizi hoja tatu zitakufanya upate pesa wewe kwa kutumia fursa hii ipasavyo.

Jinsi ya kuanza: Kasajili kampuni BRELA ambayo inajihusisha na mambo ya tekinolojia ya mawasiano, Pata Till namba na Reseni ya biashara anza kazi hivi.

Zitumie halimashauri za miji na majiji na uhakikishe unapata eneo la kujenga note board ambayo nitaonyesha picha yake hapo chini, Notes board zako ziwekewe taa ( electrical instillation) yaani wakati wa usiku iwake na waambie halimashauri ya kampuni yako itakapoanzia kwamba unahitaji tenda za matangazo yao uwe unawatangazia bure kwenye notes board zako watakupa

Fanya lobbying katika halimashauri hiyo wapige marufuku matangazo kubandikwa ovyo ovyo kwa kuwaelezea hasara zake kama nilivyozitaja hapo juu likiwepo swala la kodi waambie wewe utalipa kodi na VAT.

Hakuna halimashauri itagoma kukupa hii fursa hapo utatengeneza team kwenda maofisi yote na kuomba matangazo na kuacha mawasiliano ya kampuni yako.

Utatoa ajira kwa vijana maana kila kitu kitafanywa na kampuni yako kama Kudezaini, Kusimamia matangazo yenye kutaka kutapeli watu hii itakufanya kuwa karibu sana na Makampuni mengi na Serikali.

Pia hakikisha unakuwa na notes board za kutosha mjini pia uwe mbunifu mfano notes board chini yake unaweza kuweka kituo cha kuuzia magazeti kwenye kila notes board yako na kuwapa bule vijana watumie kuuzia huku wakilinda notes board ya kampuni yako na hii itakusaidia kwenye masoko maana watu wengi usimama kwenye vituo vya magazeti hivyo itakufanya upate wateja wengi wanafika kwenye notes board za kampuni yako na wakati huo kuwashawishi wateja watangaze na wewe.

Utaweka bei ya kawaida ya kuanzia kwa kigezo cha mtu au kampuni inataka kutangaziwa wapi? Kama ni note board moja labda ya posta utajua bei yako iweje kuna mwingine atakwambia anataka kutangaza notes board zote za Dar yaani (promotion announcement) utaweka utaratibu.

Nakaribisha maswali kwa fursa hii labda kama kuna jambo nimesahau kuliandika niulize nitakujibu

Kesho nitakuja na fursa nyingineView attachment 1854903View attachment 1854904
Unatania wewe ,field hali haiko hivyo,siku hizi matangazo yote ni online,mambo ya notice board sijui billboard yaliisha kitambo
 
Unatania wewe ,field hali haiko hivyo,siku hizi matangazo yote ni online,mambo ya notice board sijui billboard yaliisha kitambo
Kama matangazo yangekuwa hakuna basi tusineona matangazo yanayozakaa mtaani ya kila aina

Madalali, mashule, vyuo, kazi kibao wakina Azzam wanatangaza hayo yote ni matangazo je chukulia mfano halimashauri ikioiga marufuku yatatangazwa wapi? Hii ni fursa ndugu.

Hapa cha kufanya ni kuwa na marketing term iliyo serious na wanaoweza kuwa smart kushawishi makampuni kutangaza nao.

Tanzania tunakwama sehemu moja tu kwenye marketing tukiweza huko tutakuwa na biashara nyingi na maana fursa ni nyingi sana.
 
Kama matangazo yangekuwa hakuna basi tusineona matangazo yanayozakaa mtaani ya kila aina

Madalali, mashule, vyuo, kazi kibao wakina Azzam wanatangaza hayo yote ni matangazo je chukulia mfano halimashauri ikioiga marufuku yatatangazwa wapi? Hii ni fursa ndugu.

Hapa cha kufanya ni kuwa na marketing term iliyo serious na wanaoweza kuwa smart kushawishi makampuni kutangaza nao.

Tanzania tunakwama sehemu moja tu kwenye marketing tukiweza huko tutakuwa na biashara nyingi na maana fursa ni nyingi sana.
Matangazo siku hizi ni digital mkuu,online,tv,radio,social media,mabango na noticeboard hayana dili yanafikia watu wachache thats the risk business usijaribu
 
Matangazo siku hizi ni digital mkuu,online,tv,radio,social media,mabango na noticeboard hayana dili yanafikia watu wachache thats the risk business usijaribu
Nimekuuliza swali kwanini kama ni risk why !!

1: makampuni bado wanatangaza matangazo mtaani ?nijibu

2: kwanini posta mpaka Leo ipo haijafa? Nijibu

3: Kwanini magazeti yapo hayajafa ambayo ni serious? nijibu

4: kwanini ukiweka tangazo mtandaoni ukiwa na follows mfano 100,000 watacoment 10 na like 200? Lakini mtu huyo huyo akiweka picha yake ya utupu atapata comment 10000 na like 80,000 why?

Fanya reseach Nijibu.
 
1,hakuna kampuni ya maana inayotangaza mtaani
2.posta ya enzi za ujima ilikuwa active kukiko sasa kama hujui
3.mauzo ya magazeti yamepungua sana tena sana kulinganisha na miaka kumi nyuma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom