MakinikiA
JF-Expert Member
- Jun 7, 2017
- 5,011
- 6,542
Hii ilikuwa 16 Novemba 2016 baada ya kushinda uchaguzi
Rais mteule Donald Trump amesema hatapokea mshahara wa rais wa $400,000 (£319,500) kila mwaka
Rais mteule wa Marekani Donald Trump amesema hataki kulipwa mshahara wa rais wa $400,000 atakapochukua hatamu Januari mwakani. Badala yake atakuwa akilipwa $1 pekee kila mwaka.
Alifichua mpango wake huo wakati wa mahojiano na Lesley Stahl kipindi cha 60 Minutes cha CBS News.
Ingawa hakujua rais huwa analipwa pesa ngapi, Bw Trump alisema alidhani anahitaji kuchukua tu $1.
Baada ya Bi Stahl kumjulisha kwamba mshahara wa rais ni $400,000, alisema: "Hapana, sitaupokea mshahara huo. Sizichukui kamwe."