Unafungua daftari la michango ya rambirambi unakuta mtu wa kwanza kaandika 1,200,000/=

Good afternoon jamiiforums

Umeenda kwenye msiba wa baba yake rafiki yako sasa umefungua daftari la rambirambi unataka kuandika mchango wako wa 10,000/= mara ghafla unakutana na jina la mtu wa kwanza (sijui ni boss wa marehemu) amechangia 1,200,000/= unafanyaje? Yamenikuta sana haya miaka ya 2011 - 2017.

Unaweza ukajikuta unarudisha daftari la michango na kumuuliza mwenyeji wako "Frank, eti washroom ndio wapi?"

Mara nyingi nilipokuwa ninakutana na hali kama hii nilikuwa ninaamua kutokuandika kabisa katika daftari kisha ninaenda kwenye magenge ya hapo jirani na kununua nyanya, vitunguu na unga wa ugali kilo kadhaa au mikate ya waombolezaji kunywea chai asubuhi.

Nilikuwa ninaona aibu sana kuandika mchango mdogo wakati majina matatu ya juu wa kwanza ni 1,200,000, wa pili 900,000 na wa tatu 700,000/= alafu wa nne ndio niwe mimi na 15,000/= yangu? Hapana aisee bora nikampe mfiwa pesa mkononi.

Kuna mzee mmoja alikuwa ni dereva katika kampuni moja niliyokuwa ninafanyia kazi nilikuwa ninamuitaga mzee Juma.

Mzee nilimsimulia namna ambayo nimekuwa nikikutana na hali kama hii akacheka sana akniambia, babu hayo majina ya mwanzo ya waliochangia pesa kubwa huwa yanawekwa kwa makusudi ili kuhamasisha hawa wa chini wachangie nyingi pia kwa aibu.

Najua JF imejaa wamama na wababa wenye umri mkubwa (above 45) ambao wamepitia sana hali ya kubeba changamoto hizi za misiba majumbani mwao na wanaweza kutuambia kama ni kweli yale majina ya mwanzo yanatumiaka kama hamasa ama la. Ninaomba kuelimishwa.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Sasa yanarudi mkuu, enzi za fanya kazi ndio upate pesa zimeenda na mwenye hiyo falsafa, sasa ni ongea maneno matamu ingiza mamilioni kilaini
 
Waswahili husema ya kwamba, "uso umeumbwa na haya"
Basi wewe kwenye maisha huenda unapata tabu sana. Siku zote mchango siyo mashindano. Unaweza kutoa sh. elfu kumi ikawa umejitoa zaidi ya mtu aliyetoa sh. milioni mbili. Kwenye maisha ukishanza kuishi maisha ya ku-fake uko juu kuliko kipato chako utaumia. Kwa wale wakristo wanajua maandiko haya kutoka kwenye biblia: Kisha Yesu akaketi karibu na sehemu ya kutolea sadaka Hekaluni akawaangalia watu walivyokuwa wakiweka sadaka zao kwenye chombo cha sadaka. Matajiri wengi waliweka humo kiasi kikubwa cha fedha. Lakini mjane mmoja fukara, alikuja akaweka sarafu mbili zenye thamani ya senti kumi.
Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia, “Ninawaambia hakika, huyu mjane ametoa zaidi kuliko wote! Wengine wote wametoa kutokana na ziada ya mali zao; lakini huyu mama ingawa ni fukara, ameweka kila kitu alichokuwa nacho, hata na kile alicho hitaji kwa ajili ya riziki yake.
 
Siku zote mchango siyo mashindano. Unaweza kutoa sh. elfu kumi ikawa umejitoa zaidi ya mtu aliyetoa sh. milioni mbili. Kwenye maisha ukishanza kuishi maisha ya ku-fake uko juu kuliko kipato chako utaumia.
Ni bora kumpa mkononi mfiwa pesa ndogo kuliko kuandika kwenye daftari
 
Niliona aibu nikaamua kumpa jamaa pesa mkononi
Kukubali maisha yako ni kitu muhimu sana, unayakubali halafu unakata mshipa wa noma.

Hususan kama umeshajaribu kuyabadili ukashindwa

Na wewe una utu ambao haupimwi kwa hela, mtu anaweza kutoa hela nyingi lakini akawa hana mawazo mazuri, hela ikawa haijasaidia.

Au huyo mwenye hela akawa yuko busy sana hawezi kusaidia kazi fulani, sisi wengine ambao hatuna hela sana ndio tukapiga kazi.

Yote maisha tu, unyonge mwingine utajipa mwenyewe bila sababu.

Mwaka 1998 nishawahi kutoa Sh 10,000 kwenye msiba nikajiona mnyonge sana kwamba natoa kidogo.

Baadaye ikaonekana hiyo 10,000 ndiyo ilikuwa kati ya watemi, kuna watu walitoa mpaka 500.

Lakini unaweza kuambiwa kuna mama katoa 500 halafu kafanya kazi kubwa sana ya kupika msibani.

Nyerere alitufundisha, "Utu wa mtu ni kazi, pesa ni matokeo".

Mzalendo nafikiri unayajua haya mambo, basi tu.
 
Kukubali maisha yako ni kitu muhimu sana, unayakubali halafu unakata mshipa wa noma.

Hususan kama umeshajaribu kuyabadili ukashindwa

Na wewe una utu ambao haupimwi kwa hela, mtu anaweza kutoa hela nyingi lakini akawa hana mawazo mazuri, hela ikawa haijasaidia.

Au huyo mwenye hela akawa yuko busy sana hawezi kusaidia kazi fulani, sisi wengine ambao hatuna hela sana ndio tukapiga kazi.

Yote maisha tu, unyonge mwingine utajipa mwenyewe bila sababu.

Mwaka 1998 nishawahi kutoa Sh 10,000 kwenye msiba nikajiona mnyonge sana kwamba natoa kidogo.

Baadaye ikaonekana hiyo 10,000 ndiyo ilikuwa kati ya watemi, kuna watu walitoa mpaka 500.

Lakini unaweza kuambiwa kuna mama katoa 500 halafu kafanya kazi kubwa sana ya kupika msibani.

Nyerere alitufundisha, "Utu wa mtu ni kazi, pesa ni matokeo".

Mzalendo nafikiri unayajua haya mambo, basi tu.
Asante mkuu, umefafanua vema sana. Thanks.
 
Kisha Yesu akaketi karibu na sehemu ya kutolea sadaka Hekaluni akawaangalia watu walivyokuwa wakiweka sadaka zao kwenye chombo cha sadaka. Matajiri wengi waliweka humo kiasi kikubwa cha fedha. Lakini mjane mmoja fukara, alikuja akaweka sarafu mbili zenye thamani ya senti kumi.
Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia, “Ninawaambia hakika, huyu mjane ametoa zaidi kuliko wote! Wengine wote wametoa kutokana na ziada ya mali zao; lakini huyu mama ingawa ni fukara, ameweka kila kitu alichokuwa nacho, hata na kile alicho hitaji kwa ajili ya riziki yake.
Asante mtumishi wa Mungu
 
Back
Top Bottom