Elections 2010 Unafiki wa TBC na Taarifa za Wagombea

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Jana nilibahatika kusikiza kwa kiasi fulani taarifa ya habari ya saa bili usiku kupitia TBC1. Nilianza na taarifa iliyokuwa ikimgusa Prof. Lipumba. Ilianza kwa mtangazaji wa TBC1 kujikanyaga-kanyaga na baadae akapisha clip ya Lipumba isikike. Wakati Prof. Lipumba akiongea mambo mepesi-mepesi, mawimbi yalikuwa yakisikika vizuri tu. Alipoanza kuponda uozo wa CCM na serikali yake, mara signal ikawa inakatika katika na akawa hasikiki tena, na hamu niliyokuwa nayo ya kusikia ikanitoka kabisa.

Akaja Rais mteule. Dr. Wilbroad Slaa. Hapo TBC1 wakaendelea na propaganda. Safari hii Dr. Slaa alikuwa akisikika, lakini kamera yao ilikuwa ikimulika utitiri wa watoto waliokuwa kwenye kampeni (ili kuihadaa jamii kuwa mikutano ya Dr. Slaa huwa inajaa watoto ambao hata hawana sifa ya kupiga kura). Wizi mtupu!!

TBC acheni unafiki.
 
TBC ndiyo mchezo waoo huo lkn this time wabongo hawadanganyiki. We angalia jinsi weanavyo hariri mikutano ya dk slaa!! hadi aibu!
Nina mashaka sana na Tido Mhando, sijui anapewa nini na JK kinachomfanya aonekane mpuuzi mbele ya watu!
 
nikiwa Dar mbinu kama hiyo waliitumia TV Mlimani, wakitoa taarifa ya uzinduzi wa kampeni za Slaa pale Jangwani , wakaomba radhi kuwa kuna itirafu ktk mfumo wa urushaji picha, kweli habari karibu yoote haikua na picha, iliathiri pia habari zingine.
Ni wajinga tu.
 
Unapoongelea TBC, unamhusisha Tido na CCM, so hapo hakuna cha kusema, ila mwisho wao utafika tu.

Dr Slaa for Prez!!!!!!!!
 
nikiwa Dar mbinu kama hiyo waliitumia TV Mlimani, wakitoa taarifa ya uzinduzi wa kampeni za Slaa pale Jangwani , wakaomba radhi kuwa kuna itirafu ktk mfumo wa urushaji picha, kweli habari karibu yoote haikua na picha, iliathiri pia habari zingine.
Ni wajinga tu.

Mlimani TV kumbe nao wanaREDET habari?
 
Mlimani TV kumbe nao wanaREDET habari?

Mwana redet sana tuu hasa yule jamaa mwenye MAPENGO yule nai.. sijui mwenye damu mbaya...mnafiki sana yule anajidai ajua kila kitu! Sjui nani alimpa kazi utangazaji kweny TV ilhali anamapengo!!
 
TBC1 hawana jipya tangu enzi zeleeee na sasa ni enzi ya tido, nothing has changed 4 sure,
Watangazaji ccm, sielewi taaluma zao sijui ni vihiyo.... wanachubua sura zao ngumu kwenye kamera bure. Sijui tv gani hii; eti ya taifa no si ya taifa hii ni ya ccm.
 
Jana nilibahatika kusikiza kwa kiasi fulani taarifa ya habari ya saa bili usiku kupitia TBC1. Nilianza na taarifa iliyokuwa ikimgusa Prof. Lipumba. Ilianza kwa mtangazaji wa TBC1 kujikanyaga-kanyaga na baadae akapisha clip ya Lipumba isikike. Wakati Prof. Lipumba akiongea mambo mepesi-mepesi, mawimbi yalikuwa yakisikika vizuri tu. Alipoanza kuponda uozo wa CCM na serikali yake, mara signal ikawa inakatika katika na akawa hasikiki tena, na hamu niliyokuwa nayo ya kusikia ikanitoka kabisa.

Akaja Rais mteule. Dr. Wilbroad Slaa. Hapo TBC1 wakaendelea na propaganda. Safari hii Dr. Slaa alikuwa akisikika, lakini kamera yao ilikuwa ikimulika utitiri wa watoto waliokuwa kwenye kampeni (ili kuihadaa jamii kuwa mikutano ya Dr. Slaa huwa inajaa watoto ambao hata hawana sifa ya kupiga kura). Wizi mtupu!!

TBC acheni unafiki.
Aseee hata mimi niliiona yaani sasa hivi sitegemei tena tbc kupata taarifa za uhakika kuhusu vyama vya siasa maana habari za CHADEMA wataonyesha mabaya zaidi(-ve), za CCM wataonyesha mazuri zaidi (+ve) mfano hata kama JK anawatu wachache wataweka kamera zao kiasi kwamba kugundua inakuwa vigumu sana hiyo jana JK alikuwa na watu wachache waliokuwa wamehudhulia lkn kwa njinsi walivyo onyesha ilikuwa vingumu kugundua...
 
ITV ni afadhali kidogo siku hizi, HATA HIVYO KWA SASA tutegemee mabadiliko baada ya mzee mengi kutikiswa na CCM kupitia mafisadi kwa kutaka kubambikizia mtoto wake madawa.Mengi hao CCM si watu babaangu achana nao.Stay independent mseeeeee
 
Back
Top Bottom