Unafiki na chuki umejaa katika utumbuaji majipu

ya ngoswe muachie ngoswe mwenyewe....ndugu na siku zote ngoma ukiona inalia sana jua kuwa inakaribia kupasuka.
 
Nimejaribu kufuatilia hiki kitu kinaitwa utumbuaji majipu toka umeanza nimeona umejawa na chuki pamoja na unafiki wa hali ya juu.

Nitatoa mifano miwili kuonyesha utumbuaji huu wa majipu ni wa unafiki wa kiwango gani.

Mwaka jana rais alivunja bodi ya wakurugenzi ya TRA kwa kila alichokuja kukisema badae kuwa ilibariki ufunguaji wa Fixed Deposit Account katika mabenki ya kibiashara.

Tunajua kabisa wazo la kufungua Fixed Deposit Account lazima lilitoka katika menejimenti ya TRA na bodi ikalibariki, mkuu wa menejiment ya TRA ni kamishina ambae pia ni katibu wa bodi ya wakurugenzi, mara nyingi kama sio zote katibu wa bodi hupeleka mapendekezo ya menejimenti ya taasisi yake kwenye bodi ili yapewe baraka.

Cha kushangaza, bodi ikavunjwa kwa msingi kua iliruhusu ufunguaji wa Fixed Deposit Account huku muasisi wa hilo wazo kamishina na menejimenti yake wakiachwa wale bata mjini.

Juzi mkurugenzi wa TANESCO amefukuzwa kazi kwa kigezo kua yeye ndie alieanzisha/asisi wazo la kupandisha umeme bei pamoja na menejiment yake ambayo pia imevunjwa, maana yake ni kwamba bodi ilibariki tu mapendekezo ya menejimenti ya TANESCO.

Hapo ndio unafiki na chuki zinapokuja, hapa kwa TANESCO tunaona muasisi wa wazo alifukuzwa kazi na waliobariki(bodi+EWURA) wakiachwa. TRA muasisi wa wazo(kamishina) akaachwa waliobariki wazo la kamishina(bodi) wakafukuzwa kazi.

Hakuna mtiririko ulio wazi wa kutumbua majipu, utumbuaji umejaa unafiki na chuki, unajiuliza au kwa vile bodi ya TRA hakuwa ameiteua yeye na kamishana kamteua yeye, mkurugenzi wa TANESCO hakumteua yeye na bodi ya TANESCO ameiteua yeye?
Inatia hasira mijitu mizima mnaposhinda hapa jf kulalama lalama kama vikinda vya ndege! Hivi hata hujisikii aibu? Chapa kazi acha uki..za.
 
Wakuu naomba mnifungue akili kuhusu hawa wanaotumbuliwa. Najuwa kwamba amewafuta kazi tu. Je wanaweza kurudi kwenye nafasi zao za awali ambazo waliajiriwa? Je vipi mishara yao ni ile ya ukurugenzi?
 
Nimejaribu kufuatilia hiki kitu kinaitwa utumbuaji majipu toka umeanza nimeona umejawa na chuki pamoja na unafiki wa hali ya juu.

Nitatoa mifano miwili kuonyesha utumbuaji huu wa majipu ni wa unafiki wa kiwango gani.

Mwaka jana rais alivunja bodi ya wakurugenzi ya TRA kwa kila alichokuja kukisema badae kuwa ilibariki ufunguaji wa Fixed Deposit Account katika mabenki ya kibiashara.

Tunajua kabisa wazo la kufungua Fixed Deposit Account lazima lilitoka katika menejimenti ya TRA na bodi ikalibariki, mkuu wa menejiment ya TRA ni kamishina ambae pia ni katibu wa bodi ya wakurugenzi, mara nyingi kama sio zote katibu wa bodi hupeleka mapendekezo ya menejimenti ya taasisi yake kwenye bodi ili yapewe baraka.

Cha kushangaza, bodi ikavunjwa kwa msingi kua iliruhusu ufunguaji wa Fixed Deposit Account huku muasisi wa hilo wazo kamishina na menejimenti yake wakiachwa wale bata mjini.

Juzi mkurugenzi wa TANESCO amefukuzwa kazi kwa kigezo kua yeye ndie alieanzisha/asisi wazo la kupandisha umeme bei pamoja na menejiment yake ambayo pia imevunjwa, maana yake ni kwamba bodi ilibariki tu mapendekezo ya menejimenti ya TANESCO.

Hapo ndio unafiki na chuki zinapokuja, hapa kwa TANESCO tunaona muasisi wa wazo alifukuzwa kazi na waliobariki(bodi+EWURA) wakiachwa. TRA muasisi wa wazo(kamishina) akaachwa waliobariki wazo la kamishina(bodi) wakafukuzwa kazi.

Hakuna mtiririko ulio wazi wa kutumbua majipu, utumbuaji umejaa unafiki na chuki, unajiuliza au kwa vile bodi ya TRA hakuwa ameiteua yeye na kamishana kamteua yeye, mkurugenzi wa TANESCO hakumteua yeye na bodi ya TANESCO ameiteua yeye?
Wewe ndio mnafiki na muongo.Huwezi kuwa katika position ya kupata data za kutosha kuliko Magufuli.Waache watu wafanye kazi
 
Yaani unasema wewe ni tumaini kutupandishia bei? Wewe ni hope kuficha pesa za miradi eti kampuni imeona ni faida kuziweka kwenye akaunti ya muda maalumu inayolipa?

Wewe unashauri wakosee TANESCO watumbuliwe EWURA? I dont think the your iq commands rationally.

Unastahili kutumbuliwa moja kwa moja.
boss jamaa kakuambia hujamuelewa mtoa mada rudia usome tena ila bado unaendeleza ligi hata mie naona hujaelewa mada kwa jinsi ulivyojibu
 
Wewe ndio mnafiki na muongo.Huwezi kuwa katika position ya kupata data za kutosha kuliko Magufuli.Waache watu wafanye kazi
Nyie ndio wale watu wasio na akili sawasawa wanaodhani rais ni mungu, ni mjuzi za kila kitu. Endelea kuamini hivyo,sina cha kukusaidia.
 
Wakuu naomba mnifungue akili kuhusu hawa wanaotumbuliwa. Najuwa kwamba amewafuta kazi tu. Je wanaweza kurudi kwenye nafasi zao za awali ambazo waliajiriwa? Je vipi mishara yao ni ile ya ukurugenzi?
Wakurugenzi waku hawarudi kwenye nafasi zao wanaacha kazi kabisa maana wao kazi zao hua ni za mkataba. Wakurugenzi wa idara wengine hua wanaacha kazi kama walitoka nje ya hiyo taasisi, namaaniaha muda mwingine taasisi hutangaza kazi ya ukurugenzi wa idara kwa watu wote,wa ndani ya hiyo taasisi na nje sasa kama atakaeshinda hiyo kazi ni kutoka nje ya taasisi akitumbuliwa huacha kazi lakini kama alitoka ndani basi huonekana kama promotion hubakia na kazi yake ya kudumu. Mshahara hua haushushwi hata kama ukishushwa cheo.
 
Back
Top Bottom