Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,758
- 71,136
Huu mwenendo hautusaidii Watanzania. Na umeletwa na CCM kwa sababu zao za kutaka fikra ziwe kwenye uchaguzi tuu.
Inakuwaje kila jambo jema linalofanywa na Serikali hii ya CCM sifa anapewa Rais na hasa mambo haya yalianzia kwa Magufuli na sasa yameota mizizi.
Lakini Serikali hiyo hiyo inaposhindwa jambo mfano hili janga la Umeme sasa hivi husikii akitajwa Rais Samia wala Serikali ya CCM bali January Makamba.
Au mambo ya Wamachinga, ukosefu wa maji Dar, kushindwa kwenye michezo, ukosefu wa ajira nk Rais hahusishwi kabisa bali yeye wanasubiri avae gwanda la Jeshi basi maccm yote yanalundikana kumsifu tuu.
Huu unafiki utatufikisha wapi? Jee hawajui kuwa kuficha donda ni kulifanya liwe donda ndugu?
Inakuwaje kila jambo jema linalofanywa na Serikali hii ya CCM sifa anapewa Rais na hasa mambo haya yalianzia kwa Magufuli na sasa yameota mizizi.
Lakini Serikali hiyo hiyo inaposhindwa jambo mfano hili janga la Umeme sasa hivi husikii akitajwa Rais Samia wala Serikali ya CCM bali January Makamba.
Au mambo ya Wamachinga, ukosefu wa maji Dar, kushindwa kwenye michezo, ukosefu wa ajira nk Rais hahusishwi kabisa bali yeye wanasubiri avae gwanda la Jeshi basi maccm yote yanalundikana kumsifu tuu.
Huu unafiki utatufikisha wapi? Jee hawajui kuwa kuficha donda ni kulifanya liwe donda ndugu?