Unafiki at work; Kutoka Facebook

Mphamvu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
10,702
3,288
Unafki mwingine bwana...
Limtu tuko nalo hapa hapa mtaani
kwetu. Kipindi kile kafa Mzee
Mwakilembe ilikuwa kimya kimya,
lahaula fil-aiti, tukakutana kwenye
kuaga maiti, kipindi fulani akatutoka kijana mwenzetu Tito, nikamgumia msibani wakati nampa sinia la ubwabwa (nilikuwa mwandazi), haya kipindi kile akafariki jirani yangu Sophia... namtext ananiambia atachelewa kuzika anaenda Magomeni kuna kibeseni shoga yao amejifungua.
Picha halijaisha hapo, akafariki alwatan Mzee Shaaban Irembe, kimya kimya tulionana kwenye kisomo msikiti mkubwa... Alivyodondoka Tina si nikajua atanipa taarifa kwa kuwa wamesoma wote, ebwana tulionana Mwembejini tukigombania usafiri wa
kurudi.
Leo kafa Sharo Milionea (hata sijui kama walishaonana na huyu kiumbe) usiku nimelala ananipigia simu, sauti anaisikia kabisa ya usingizi, afu aniuliza "Eti Sharo amefariki kweli?", jamani usiku
huu mie tajuaje? Halafu misiba yote
Mikocheni hukuguswa mpaka hii ya mastaa?
Kipindi kile cha Marehemu Kanumba ulifanya hivi hivi, nikakukaushia... Ona sasa umeniharibia usingizi wangu, na
utaulipa nakuambia!
 
Mphamvu rafiki, umeenda kufanya nini huko fb? Kule kuna utoto mpaka utavimbiwa bhana! Stay here @ JF meen!
 
Mphamvu rafiki, umeenda kufanya nini huko fb? Kule kuna utoto mpaka utavimbiwa bhana! Stay here @ JF meen!

Facebook kuna raha yake, only if ukitumia wisely.
Unaonaga zile updates zangu kule Jukwaa la Michezo, huezi amini kuwa over 70 percent huwa zinaoriginate facebook...
 
Facebook kuna raha yake, only if ukitumia wisely.
Unaonaga zile updates zangu kule Jukwaa la Michezo, huezi amini kuwa over 70 percent huwa zinaoriginate facebook...

Kama una maslahi binafsi fb siingilii Mphamvu.
 
Last edited by a moderator:
kijana ndivyo ilivyo hata kule mbagala ndoa kibao zilivunjika siku ya kanumba alipokufa kila mtu anamjua..

usiogope mkuu ndio maana NN akasaini Miafrika Ndivyo Tulivyo..

am out!
 
Unafki mwingine bwana...
Limtu tuko nalo hapa hapa mtaani
kwetu. Kipindi kile kafa Mzee
Mwakilembe ilikuwa kimya kimya,
lahaula fil-aiti, tukakutana kwenye
kuaga maiti, kipindi fulani akatutoka kijana mwenzetu Tito, nikamgumia msibani wakati nampa sinia la ubwabwa (nilikuwa mwandazi), haya kipindi kile akafariki jirani yangu Sophia... namtext ananiambia atachelewa kuzika anaenda Magomeni kuna kibeseni shoga yao amejifungua.
Picha halijaisha hapo, akafariki alwatan Mzee Shaaban Irembe, kimya kimya tulionana kwenye kisomo msikiti mkubwa... Alivyodondoka Tina si nikajua atanipa taarifa kwa kuwa wamesoma wote, ebwana tulionana Mwembejini tukigombania usafiri wa
kurudi.
Leo kafa Sharo Milionea (hata sijui kama walishaonana na huyu kiumbe) usiku nimelala ananipigia simu, sauti anaisikia kabisa ya usingizi, afu aniuliza "Eti Sharo amefariki kweli?", jamani usiku
huu mie tajuaje? Halafu misiba yote
Mikocheni hukuguswa mpaka hii ya mastaa?
Kipindi kile cha Marehemu Kanumba ulifanya hivi hivi, nikakukaushia... Ona sasa umeniharibia usingizi wangu, na
utaulipa nakuambia!


Halafu ukimuuliza huyo sharo jina lake kamili ni nani?
Hamjuo.
Ukimuuliza je huyo sharo ashawahi kukununulia hata Vita Malt?
Atabaki anapepesa macho tu...
 
kijana ndivyo ilivyo hata kule mbagala ndoa kibao zilivunjika siku ya kanumba alipokufa kila mtu anamjua..

usiogope mkuu ndio maana NN akasaini Miafrika Ndivyo Tulivyo..

am out!

Maisha ya kuigiza ndo hulka yetu...
 
Halafu ukimuuliza huyo sharo jina lake kamili ni nani?
Hamjuo.
Ukimuuliza je huyo sharo ashawahi kukununulia hata Vita Malt?
Atabaki anapepesa macho tu...

Si ndo pale sasa!
Afu utakuta huku uswahilini kwetu ndo wako wa kumwaga, siku ya mazishi ya Kanumba walikusanyana mpaka Kinondoni, na wengine nasikia wakaua watoto migongoni.
Kama wana uchungu wapande Raha Leo waende Muheza...
 
siku aliyokufa Kambarage, kuna watu nao walikufa sababu ikiwa ni mshtuko...
 
Back
Top Bottom