Unafanya nini kabla ya kulala ili kupata usingizi mzuri?

Mr. Purpose

JF-Expert Member
Nov 12, 2016
1,439
2,690
Habari wakuu!

Ili kuishi maisha ya furaha na kuwa na afya njema kulala usingizi mzuri ni sehemu muhimu ambayo huweza kuimarisha afya ya akili na mwili pia.

Leo naomba tujadili, wewe ili upate usingizi mzuri, unafanya nini kabla ya kulala?

Nikianza Mimi Mr. Purpose binafsi, ili nipate usingizi mzuri ni lazima nifanye moja ya vitu vifuatavyo au vyote kwa pamoja:-

1. Mazoezi ya viungo.

Jioni nikifanya jogging au mazoezi yoyote ya viungo huwa akili inatulia hivyo kupata usingizi mzuri bila tatizo.

2. Kuoga maji ya baridi kabla ya kulala.

3. Kufanya meditation jioni kabla ya kulala.

Hii huwa na mchango mkubwa sana na huwa hata nikiamka asubuhi mambo yangu huwa yanaenda vizuri sana.

4. Kusoma kitabu au makala yoyote.

5. Tendo la ndoa.

Hii nayo huwa ni sehemu ya kupata usingizi mzuri hasa pale ambapo limefanyika kwa umakini na umaridadi wa kutosha huwa nalala vizuri sana.

NB: kumbuka tendo la ndoa ni dawa na inasaidia kutibu magonjwa kadhaa, ntaleta uzi kulielezea kwa kina.

Sasa mdau, turudi kwako, wewe unafanya nini ili kupata usingizi mnono na kuamka ukiwa mchangamfu kiakili nakimwili pia?

Karibu tujadili.
 
Habari wakuu!

Ili kuishi maisha ya furaha na kuwa na afya njema kulala usingizi mzuri ni sehemu muhimu ambayo huweza kuimarisha afya ya akili na mwili pia.

Leo naomba tujadili, wewe ili upate usingizi mzuri, unafanya nini kabla ya kulala?

Nikianza Mimi Mr. Purpose binafsi, ili nipate usingizi mzuri ni lazima nifanye moja ya vitu vifuatavyo au vyote kwa pamoja:-

1. Mazoezi ya viungo.

Jioni nikifanya jogging au mazoezi yoyote ya viungo huwa akili inatulia hivyo kupata usingizi mzuri bila tatizo.

2. Kuoga maji ya baridi kabla ya kulala.

3. Kufanya meditation jioni kabla ya kulala.

Hii huwa na mchango mkubwa sana na huwa hata nikiamka asubuhi mambo yangu huwa yanaenda vizuri sana.

4. Kusoma kitabu au makala yoyote.

5. Tendo la ndoa.

Hii nayo huwa ni sehemu ya kupata usingizi mzuri hasa pale ambapo limefanyika kwa umakini na umaridadi wa kutosha huwa nalala vizuri sana.

NB: kumbuka tendo la ndoa ni dawa na inasaidia kutibu magonjwa kadhaa, ntaleta uzi kulielezea kwa kina.

Sasa mdau, turudi kwako, wewe unafanya nini ili kupata usingizi mnono na kuamka ukiwa mchangamfu kiakili nakimwili pia?

Karibu tujadili.
Umezunguka sana mbuyu.ila Uzi wako mzima ulilenga hyo no 5.
Kwa jinsi ulivyoitolea maelezo lukuki.
 
nikiwa na uhakika wa kula usingizi nalala
Kuna kupata usingizi mnono, ule ambao ukiamka asubuhi akili ipo sawa na mwili uko fiti na unajihisi mchangamfu sana mkuu. Maana kulala kila mmoja analala, tatizo ni unajisikiaje unapoamka?

Kama uhakika wa msosi tu unakupa hiyo aina ya usingizi basi hongera sana mkuu, maana kuna watu wana uhakika wa vyote ila huo usingizi hawaupati, mtu anaingia kitandani kwasababu ni usiku hana namna lazima alazimishe usingizi.
 
Nikaoge maji baridi yasio na chembe ya chumvi kisha niwashe feni namba 2 tu! Hapo lazma pakuche provided nimepiga cha usiku sina njaa. Ni JF mpaka natopea usingizini
Hongera sana mkuu. Suala la usingizi wengi hulitazamia kawaida ila lina athari sana katika maisha yetu ya kila siku.

Shukuru Mungu ukiweza tambua njia bora ya wewe kuupata usingizi, maana hata siku mambo yakiwa magumu basi unajua namna bora ya kutuliza akili na mwili.
 
Hata sijui mkuu
Kuna baadhi ya siku unaamka mchangamfu wa akili na mwili na unajisikia furaha tu kwasababu ya usingizi ulioupata na pia kuna baadhi ya siku unaamka bila kuona utofauti wowote.

Hebu jaribu kufanya jaribio hali hizo mbili zinapokutokea ujaribu kujiuliza kwanini leo nimeamka mchangamfu kiakili na kimwili pia mwenye furaha tofauti na siku zingine? Fanya hivyo kwa hali ya pili pia , nina imani utaweza gundua baadhi ya vitu.

Either kuna mambo ukifanya unapata usingizi mzuri au kinyume chake.
 
Kuna baadhi ya siku unaamka mchangamfu wa akili na mwili na unajisikia furaha tu kwasababu ya usingizi ulioupata na pia kuna baadhi ya siku unaamka bila kuona utofauti wowote.

Hebu jaribu kufanya jaribio hali hizo mbili zinapokutokea ujaribu kujiuliza kwanini leo nimeamka mchangamfu kiakili na kimwili pia mwenye furaha tofauti na siku zingine? Fanya hivyo kwa hali ya pili pia , nina imani utaweza gundua baadhi ya vitu.

Either kuna mambo ukifanya unapata usingizi mzuri au kinyume chake.
Kinachoniamsha vizuri au vibaya ni boss, inategemea jana yake tuliachanaje
 
Umezunguka sana mbuyu.ila Uzi wako mzima ulilenga hyo no 5.
Kwa jinsi ulivyoitolea maelezo lukuki.
Nikifanya mojawapo ya hayo katika list hiyo au vyote kwa pamoja mkuu.

Target siyo namba tano.

Niseme tu kuna watu hawajawahi kupata ule usingizi mnono, yaani ule usingizi halisi mkuu, kuna baadhi wanalala kwasababu ni usiku anasubiri pakuche, ila kuna watu wanalala kupumzika.

Kuna tofauti ya kiafya ya akili na mwili kati ya hao wawili.

Tuendelee kujifunza kupitia comments za wadau.
 
Sijalala siku 2,hapa kichwa kiko waruwaru tu.
Nagonga kali ila bado jicho nyanya linadai tu,sijui nifanyeje
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom