Ratiba yako ya kwenda 'Site' ni ipi?

Mimi kabla sijajenga nilinunua Kirikuu ambayo imenisaidia sana kama kupeleka mafundi site, kununua mwenyewe material kama cement nk. Nasimamia ujenzi mwanzo mwisho na wakimaliza jioni nawabeba nawarudisha, hakuna aliyeniibia, zaidi sana mimi nina uelewa wa ufundi hadi ratio za cement nilikuwa nawaelekeza.

Sikuchukua mafundi expensive ila hawa hawa wadogo nilikuwa nawaelekeza navyotaka mimi na sio ushauri wao. Mjengo umeisha na ninaishi himo na familia yangu, kazi nyingi za finishing kama water system, sanitation kama jikoni kuweka marble, kufunga WC (water closet) kupiga gypsm na skimming pamoja na Painting nimefanya mwenyewe!

Nilikuwa nafanya hivi, nikimwita fundi site na nikiona ana gharama kubwa labda kutokana na kazi inahitaji vifaa basi mimi nanunua vifaa hivyo nafanya mwenyewe kazi ikiisha napata faida ya vifaa. MFANO fundi bomba akija anataja gharama yake anaweza kusema kila kupiga thread joint moja ni 500, basi nikanunua Die za bomba pamoja na Vice pamoja na pipe wrench kazi ikiisha vinabaki kuwa vyangu.

Fundi wa mageti nkaona gharama zake ni kubwa anasema kutengeneza geti ni 450,000 basi mimi nanua mashine ya welding ya 280,000 na material za 150,000 nafanya mwenyewe kwa vile naweza kuthubutu, hivyo nimebaki na mashine ya welding na geti nikalishona mwenyewe, hadi sasa nina mashine nyingi za kazi nafanya mwenyewe kurekebisha nyumba pale linapotokea tatizo kwa vile vitendea kazi ninavyo.
Ona muongo mwingine huyu!
 
Mimi kabla sijajenga nilinunua Kirikuu ambayo imenisaidia sana kama kupeleka mafundi site, kununua mwenyewe material kama cement nk. Nasimamia ujenzi mwanzo mwisho na wakimaliza jioni nawabeba nawarudisha, hakuna aliyeniibia, zaidi sana mimi nina uelewa wa ufundi hadi ratio za cement nilikuwa nawaelekeza.

Sikuchukua mafundi expensive ila hawa hawa wadogo nilikuwa nawaelekeza navyotaka mimi na sio ushauri wao. Mjengo umeisha na ninaishi himo na familia yangu, kazi nyingi za finishing kama water system, sanitation kama jikoni kuweka marble, kufunga WC (water closet) kupiga gypsm na skimming pamoja na Painting nimefanya mwenyewe!

Nilikuwa nafanya hivi, nikimwita fundi site na nikiona ana gharama kubwa labda kutokana na kazi inahitaji vifaa basi mimi nanunua vifaa hivyo nafanya mwenyewe kazi ikiisha napata faida ya vifaa. MFANO fundi bomba akija anataja gharama yake anaweza kusema kila kupiga thread joint moja ni 500, basi nikanunua Die za bomba pamoja na Vice pamoja na pipe wrench kazi ikiisha vinabaki kuwa vyangu.

Fundi wa mageti nkaona gharama zake ni kubwa anasema kutengeneza geti ni 450,000 basi mimi nanua mashine ya welding ya 280,000 na material za 150,000 nafanya mwenyewe kwa vile naweza kuthubutu, hivyo nimebaki na mashine ya welding na geti nikalishona mwenyewe, hadi sasa nina mashine nyingi za kazi nafanya mwenyewe kurekebisha nyumba pale linapotokea tatizo kwa vile vitendea kazi ninavyo.
WEWE NI MUONGO.
 
Kwanza tunawapongeza wote mnaoendelea na ujenzi wa makazi. Kumiliki nyumba kuna heshima yake.

Lakini hebu tuambieni, ratiba za kwenda site huwa zikoje?

Mfano wewe unayejenga; site unaenda kila wikiendi kwa ajili ya kusimamia mafundi, au kila unapopata hela ya kujazia jazia vifaa na malipo ya hapa na pale?

Ruhusa kushea picha ya mjengo na mahesabu hasa ya mbao za kupaua kwenye uzi huu ili "kuwatia hasira" na wengine wahamasike!
Shida kwa watu tulio wengi ni kutokuwa na Cashflow ambayo ni Stable, ndio maana tunatumia njia ya kusimamia wenyewe na kutoa fedha wenyewe pale ambapo unalipa material ya ujenzi na labour charge. Kama una stable cashflow unaajiri msimamizi, wewe ni kwenda kuangalia hatua za ujenzi zilizofikiwa kila mwisho wa wiki. Wasimamizi hawa wala hawalipwi fedha nyingi. Ili usiibiwe kwenye material ya ujenzi, unatakiwa kumtafuta Mtaalam wa kukutengezea Schedule of Material. Hivyo, material ya ujenzi yanapoisha unafanya rejea kwenye Schedule of Material na kuagiza mengine.
 
Tupo Ilala Dar es Salaam. Mzigo wa mbao upo kwenye eneo letu la kupaki Buguruni-Chama.

Unaweza kutupigia 0782425190 tuzungumze. Kama upo Dar, delivery ni bure hadi site.

Ukitupigia ukasema umetuona JamiiForums tutakupa upendeleo kwenye huduma na hata bei.

Karibu sana mkuu.
Mmeacha ule mchezo wenu wa kuikata Tape Measure. But just joking!
 
Shida kwa watu tulio wengi ni kutokuwa na Cashflow ambayo ni Stable, ndio maana tunatumia njia ya kusimamia wenyewe na kutoa fedha wenyewe pale ambapo unalipa material ya ujenzina labour charge. Kama una stable cashflow unaajiri msimamizi, wewe ni kwenda kuangalia hatua za ujenzi zilizofikiwa kila mwisho wa wiki. Wasimaizi hawa wala hawalipwi fedha nyingi. Ili usiibiwe kwenye material ya ujenzi, unatakiwa kumtafuta Mtaalam wa kukutengezea Schedule of Materials. Hivyo, material ya ujenzi yanapoisha unafanya rejea kwenye Schedule of Material na kuagiza mengine.
Usijidanganye kwenda site baada ya wiki utakuta madudu mzeya.
Hawa mafundi wetu ni kukaa nao benet tuu yaani ni bumper to bumper.

Tatizo ya mafundi wengi ni kwamba wao wanataka kumaliza kazi wasepe. Hawataki kufikiri. Anza wewe mwenyewe kufikiria changamoto za kila hatua kabla fundi hajaanza kujenga maana wao hawafikiri kabisaa
 
Shida kwa watu tulio wengi ni kutokuwa na Cashflow ambayo ni Stable, ndio maana tunatumia njia ya kusimamia wenyewe na kutoa fedha wenyewe pale ambapo unalipa material ya ujenzi na labour charge. Kama una stable cashflow unaajiri msimamizi, wewe ni kwenda kuangalia hatua za ujenzi zilizofikiwa kila mwisho wa wiki. Wasimamizi hawa wala hawalipwi fedha nyingi. Ili usiibiwe kwenye material ya ujenzi, unatakiwa kumtafuta Mtaalam wa kukutengezea Schedule of Material. Hivyo, material ya ujenzi yanapoisha unafanya rejea kwenye Schedule of Material na kuagiza mengine.

Tatizo ni kwamba unaweza ukanunua material vizuri mfano sehemu kunapotakiwa kuwekwa nondo 3 wataweka moja ili zingine wauze,sehemu ya kuweka kokoto wataweka vipande vidogo vidogo vya tofauti ili kokoto wakauze,utajua hujui
 
Tatizo ni kwamba unaweza ukanunua material vizuri mfano sehemu kunapotakiwa kuwekwa nondo 3 wataweka moja ili zingine wauze,sehemu ya kuweka kokoto wataweka vipande vidogo vidogo vya tofauti ili kokoto wakauze,utajua hujui
Kwa Engineer ambaye ni Professional hivyo vitu havipo Mtani Wangu!
 
Raha ni kuwa benet benet na mafundi, hii inasaidia mnoo, kuna gharama nyingi saana unaweza punguza, nilikuwa site mwenyewe, nilipata baadhi ya vitu kwa bei rahisi zaidi, mfano alikuja mtu ana shida akaniuzia matofali kwa 600, idadi ya yalikuwa matofali zaidi ya 1000.. Halafu yalikuwa pua na mdomo.
Mafundi wakiwa site huwa nafika wakati wowote sina muda maalum kiunoni nikiwa na tape measure yangu nikifika nawapa hai mara baada ya mazungumzo mbili tatu na vuta tape
 
Mafundi wakiwa site huwa nafika wakati wowote sina muda maalum kiunoni nikiwa na tape measure yangu nikifika nawapa hai mara baada ya mazungumzo mbili tatu na vuta tape

Unavuta tape wakati mjengo ushajengwa vuta tape kwenye msingi ndio kila kitu then unakuja kuvuta tape kwenye milango na madirisha baada ya hapo baba jeni bai bai,sasa jichanganye uvute tape mjengo tayari umesimama utajua hujui
 
Unavuta tape wakati mjengo ushajengwa vuta tape kwenye msingi ndio kila kitu then unakuja kuvuta tape kwenye milango na madirisha baada ya hapo baba jeni bai bai,sasa jichanganye uvute tape mjengo tayari umesimama utajua hujui
nazungumzia hatua zote za ujenzi mzee acha kukurupuka kuanzia msingi,boma hadi kupaua kutokana na vipimo vya ramani
 
Back
Top Bottom