LGE2024 Unaenda kupiga kura uchaguzi Serikali za mtaa bila hata kuonyesha uthibitisho kama kweli wewe ndiye mhusika wa jina hilo

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Boi Manda

JF-Expert Member
Oct 26, 2023
388
506
Nilifika asubuhi kituo nilichojiandikisha kupiga kura nikakuta orodha ya majina yamebandikwa nje kwenye kuta nikatafuta jina langu nikaliona

Baada ya hapo nikaingia kupiga kura msimamizi wa uchaguzi akaangalia jina langu kwenye orodha ya daftari lake akalitiki bila hata kupata uthibitisho kama mimi kweli ndiye mwenye jina hilo

Hakuomba kitambulisha cha kura wala NIDA wala kitambulisho chochote cha kazi ili ajiridhishe kama kweli mhusika ndiye mwenyewe

Sasa udhaifu huo unaleta mwanya kwa watu wasio waaminifu kuita watu wao kupiga kura kwa kutumia majina ya watu wengine ambao kwa njia moja au nyingine hawakuweza kufika kituo hapo kupiga kura

Ama baadaye uchaguzi ukiisha wakaangalia majina ambayo hayakutikiwa wakapigia kura wagombea wao wakatiki majina hayo kama yamepiga kura

Ni vizuri ili kuleta uaminifu kwenye chaguzi kama hizi mtu skins jina lake aidha awe na kitambulisho cha mpiga kura au cha NIDA amuonyeshe karani wa kupigisha kura ili kuthibitisha kama kweli mhusika ni yeye.

Comasava TAMISEMI
 
Back
Top Bottom