Unadhani Mwanga ndio kitu chenye spidi ya juu kushinda kila kitu? Vipi kuhusu hili jambo?

(Unahisi kipi kina spidi zaidi, Mwanga au Fikra


  • Total voters
    50
  • Poll closed .
Mfano mdogo huu hapa

Unaweza ukaniambia

2,424,697,415,356 x 7,786,326,964,664= sawasawa ni ngapi?

Sidhani hata kama umesoma hizo namba, zisome kwanza.

Je fikra zako zitaweza kuchakata hiyo taarifa chini au ndani ya sekunde 1 Bila ya msaada wowote?

Teenager
Usitake kuchanganya mambo kirahisi namna hii. Huyu bwana yeye anaongelea "travel speed" ya fikra wakati wewe unaanza kuingiza mambo mengine ya "processing speed". Hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. Farasi ana speed nzuri ya kukimbia, wakati kompyuta haina speed ya kukimbia, isipokuwa yenyewe ina "processing speed" kubwa possibly kuliko viumbe vyote vyenye uhai vilivyopo hapa duniani
 
Speed ni umbali unaopimwa kwa muda..distance per time,fikra haina specific measurable distance ili tupime speed yake
Hapo ulipo wewe wakati unapata tuseme mawazo ya kuwaza sehemu yoyote ile ambayo unaijua, ila kwa sasa iko mbali na wewe, je kwenye fikra zako hupaoni, yaani huko ambako kwa sasa haupo ila uliwahi kuwepo? Je, ukitaka kusafiri tuseme kwenda safari ya mbali kidogo, huwa huhitaji usafiri au hupandi basi? Au huwa inatokea tu ukishawaza kuwa unataka kwenda mahali fulani tayari unajikuta uko pale pasipo kusafiri? Umbali tunaoungelea hapa unatokana na sehemu mbili, moja ikiwa ni pale ulipo sasa hivi na ya pili ni kule unakopawaza, ambapo hauko kule kwa muda huu na ukihitaji kwenda huko inabidi utumie usafiri kama siyo kutembea kwa miguu
 
Kwenye somo la fizikia ya kidato cha kwanza, tuliambiwa kwamba laws of physics tunazozisoma zinaweza zisiaplai kwenye skeli ya sub-atomic na kwenye gargantuan scales za kwenye space huko.
Quantum (Physics) Mechanics is a branch of Physics where the laws of classical physics fail. Equation ya energy-speed relationship (E=mc^2) ya Einstein iko kwenye Quantum Physics. Au labda mimi nimeshaanza kusahau?
 
Huwezi kumuona kwa speed itakayozidi speed ya mwanga, kwa sababu utahitaji mwanga kumuona.

Na hivyo mawazo yako, hayawezi kuzidi speed ya mwanga.

Pia, mawazo yako yanategemea reactions za electrochemical processes kichwani mwako,ambazo nazo zipo limited na speed ya mwanga, kwa hiyo huwezi kuwaza kwa speed ya zaidi ya speed ya mwanga.

Actually biological organs kama ubongo zina slow down speed ya mawazo kwa sehemu kubwa sana.
Tatizo mnachanganya vitu viwili, travel speed na processor speed. Sasa hivi mimi hapa nilipo sekunde moja iliyopita, nilikuwa ninaiwaza nearest galaxy Canis Major Dwarf ambayo iko umbali wa 25,000 light years. Nimetumia sekunde moja tu kuwaza umbile ambalo mwanga unaweza kufika huko baada ya miaka elfu 25. Msichanganye processor speed na travel speed. Aliyeanzisha mada anaongelea hiki cha pili, yaani travel speed
 
Yaani hapa ili uwe na kasi ya mwanga inabidi uwe na infinity energy! Mwanga una kasi hiyo kwa sababu unaundwa na 'photons' ambazo ni particles pekee zenye 'zero' resting mass! Yaani hazina uzito kabisa!
Ewaaa Ufalme wa mbinguni hauko Mbali nawewe
 
Mimi nadhani kilicho na chonzo Ni mwanga, kwa sababu mwanga una mwanzo na umenzishwa na kitu.

Kitu sisicho kua na chanzo Ni kiza.

Kwa maana hio giza lipo kabla ya mwanga na ndio kusema giza ndio lenye mwendo kazi zaidi ya mwanga

Pia giza ndio asili ya ulimwengu, mwanga umekuja umelikuta giza, mwanga hukifukuza giza pindi huo mwanga ukiwepo.

Huo mwanga ukitoweka giza hurudia mahali pake kwa speed ile ya mwanga kutoweka .

Giza Ni kama maji yaliopo ndani ya ndoo, pindi uwekapo labda jiwe Yale maji hutoka na kuliachia jiwe nafasi kadiri ya ukubwa wake Hilo jiwe.

Kwa kua mwanga umekuja umelikuta giza hutumia nguvu nyingi kupata nafasi ndani ya giza na giza halitaki ubishi hulipa nafasi mwanga kwa sababu lenyewe giza linajua ndio asili ya kila kilichopo.

Kwa hio unaposema mwanga ndio wenye na kutembea kwa mwendo zaidi tusisahau giza.


Lakini bado fikra hazina uwezo wa kutembea sawa au kuzidi mwanga, kwa sababu fikra zimefungwa katika mwanga, fikra hazina uwezo wowote nje wa mwanga, so kilichotangulia kimetangulia tu. Kadhalika mwanga haufui dafu kwa giza kwa vile giza lipo kabla ya mwanga.
Umeeleza kwa upeo mkubwa sana, ila bado sikubaliani na wew juu ya uwepo giza, samahani lakini kutokuwepo kwa kitu(mwanga) hakumaanishi uwepo wa kitu(giza)
 
yani ukimuona tu na shati jeupe MOJA KWA MOJA utajua getto-mate C amevaa shati la manjano
Kuona - Mwanga umeingia kwenye macho
Kutambua Shati - Ubongo umepokea taarifa kutoka kwenye macho na kufanya utambuzi

Swali la msingi....

Taarifa zinatoka vipi kutoka kwenye sensor kwenda kwenye ubongo? Vipi speed yake?
 
Hapana.. Kitu chenye speed zaidi ni Gravity mkuu.
Gravity ina speed kuliko mwanga..ndio maana mwanga hua haukatizi kwenye black holes/wormhole. Mwanga ukifika kwenye black holes hua unamezwa maana pale kuna gravity kubwa

Time is just a speed, So ukiwa na speed kubwa unaweza kuBend muda. So scientist wengi wanajaribu kutengeneza wormhole zenye garvity kubwa kama zilizopo kwenye spaces.

Regarding Your example naamini nervous system ndio kitu chenye speed zaidi. (Stimulus----->>>Response)

Mchakato wake upo chini ya nano second, imagine sauti inavyopita kwenye vipengele vyote ndani ya sikio la nje hadi la ndani kisha kwenda kwenye ubongo kutafsiriwa na kurudisha majibu kua ulichosikia kinamaanisha kitu fulani. Its matter of nano second
Mwanga 360m/s , sauti ni less than

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uko sahihi kabisa fikra zina spidi zaidi kuliko kitu kingine chochote kile. Kinachotakiwa ni mwanadamu kuwa na uwezo wa kujitowesha kimwili (total annihilation) bila kufa, kwenye point A aliyopo muda huu, na baada ya hapo ndiyo anasafiri kwa kutumia spidi ya fikra halafu anaenda kuunda upya mwili wake kwenye point B ambako alikuwa ametarajia kuwepo. Kwa mtindo huu mtu anaweza akatoka Afrika akaenda Marekani na Ulaya na kurudi tena Afrika katika muda mfupi zaidi kuliko ule unaoweza kutumiwa na mwanga
Ngoja nikuulize haka kaswali kadogo.

Nikikuonyesha picha ya New York city huku wewe ukiwa Tanzania na wewe ukaimagine uko New York city, je hiyo itamaanisha wewe umetravel kwenda New York city na kurudi Tanzania?

Na je hiyo inamaanisha fikra zako zina speed zaidi ya light speed?

Unajaribu kumpinga huku ukiwa unamusupport tena kwa wakati huo huo. The fact kwamba mwanga una speed ambayo ni constant wakati fikra zina infinite speed, is a proof kwamba fikra zina speed kuliko mwanga. Zaidi ni kuwa starting point ya speed ya fikra ni pale alipo mtu mwenye fikra hiyo, na destination ni kule mbali anakokuwaza, let's kwenye neighbouring galacxy yetu. Naomba usome pia hoja yangu hapo post #81
Kama fikra zingekuwa na speed ambayo ni infinity.
basi ingekuwa possible kuwa na infinity speed kwenye situation yoyote ile, kitu ambacho hakiwezekani kwa fikra means speed ya fikra ni finite just not constant.
Kutokuwa constant hakufanyi kitu fulani kuwa infinity.

That's why niliandika kitendo cha mwanga kuwa na speed constant under any circumstances basi mwanga ndio wenye speed kuliko fikra.

Ila kitendo cha fikra kuwa na speed ambayo inadepends ipo kwenye situation gani basi definitely speed ya fikra ni finite na sio constant vilevile.

Teenager
Usitake kuchanganya mambo kirahisi namna hii. Huyu bwana yeye anaongelea "travel speed" ya fikra wakati wewe unaanza kuingiza mambo mengine ya "processing speed". Hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. Farasi ana speed nzuri ya kukimbia, wakati kompyuta haina speed ya kukimbia, isipokuwa yenyewe ina "processing speed" kubwa possibly kuliko viumbe vyote vyenye uhai vilivyopo hapa duniani
Mfano wa mleta mada ni wa kuona shati na kugundua hili shati ni la fulani, obviously hapo imejumuishwa processing speed hivyo mimi siko mbali sana na mleta mada.

Considering kitu kinachotakiwa ni how fast fikra zinafanyakazi comparing na speed of light ndani ya muda fulani.

Well obviously fikra haziwezi kuwa na speed ya kukimbia kama farasi lakini bado speed ya fikra tunaweza kuimeasure physically na kuicompare na light speed.
au hii comparison yote ingekuwa nonsense.

Kizuri hapa hatuongelei vitu vyenye asili ya matter kama mfano wako wa farasi bali tunaongelea vitu viwili ambavyo definitely ni comparable yaani light speed na processing speed sababu vina uwiano mkubwa.

Hivyo ni sahihi mimi kutumia hiyo njia kufanya hiyo comparison.

Technically unaposema travel inakuwa inamaanisha kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa vipimo vya umbali fulani.
means mpaka hapo "travel" ni something physically ambapo kinawezekana only in 3D-space.

Na maana nyingine ya Speed ni rate inayoonyesha how fast or slow something moves, operates or functions.

Means mpaka hapo hakuna "travel speed ya fikra" na kamwe hautoweza kumeasure hiyo speed sababu it's not something physically.
Kitu ambacho kinafanya hoja yangu kuwa sahihi.

Kama "Travel Speed ya fikra" inaexist then niambie how ina function, operates or moves. na how unaweza kumeasure hiyo speed?
 
Hii napingana nayo.

Ili upate speed ya kitu lazima utahitaji starting point na destination.
Kitu ambacho kwa mwanga kinawezekana ila kwa fikra ni ngumu kidogo.
Hivyo ili tuweze kumeasure thought speed itabidi tutumie speed ya fikra kuchakata taarifa mpaka pale utakapopata jibu.

Mwanga always uko na speed constant isiyobadilika.

Lakini fikra haziwezi kuwa na speed constant na sidhani kama kuna uwezekano wa kufikia light speed.

ili kujaribu kuprove hilo kwamba speed ya fikra sio constant.
Na sometimes inaweza kuwa slow zaidi ya bando la Airtel au gari lisilo na engine.

Mfano mdogo huu hapa

Unaweza ukaniambia

2,424,697,415,356 x 7,786,326,964,664= sawasawa ni ngapi?

Sidhani hata kama umesoma hizo namba, zisome kwanza.

Je fikra zako zitaweza kuchakata hiyo taarifa chini au ndani ya sekunde 1 Bila ya msaada wowote?

Bila shaka hakuna binadamu duniani anaweza kuchakata hiyo taarifa chini au ndani ya sekunde 1 kwa mara ya kwanza na ukapata jibu bila msaada wowote.

Lakini wakati huohuo ukisema 1+1= ngapi?
Bila shaka asilimia kubwa ya watu wote duniani wanaweza kujua jibu ya hiyo taarifa chini au ndani ya seconds.
Baada ya kuona tu hiyo taarifa tayari fikra zako zimeshachakata hiyo taarifa ndani ya some milliseconds.

Hivyo mpaka hapo tayari speed ya fikra sio constant.

Kuna mengi hapo katikati ila kitendo cha light kuwa na speed constant isiyobadilika under any circumstances tayari speed of light ni almost untouchable at everything.

So in my opinion speed of light wins.

Kingine ni kwamba
technically black hole haimezi mwanga.
Bali massive gravity ya blackhole inabend space.
Na mwanga unafuatisha na kuexist kwenye space hivyo black hole ikibend space then mwanga nao utabend in ili kufuata au kuendana na hiyo space curvature.

Anayeweza kuniprove wrong, kunikosoa au kunichallenge Aje.

Umetisha baba, nimependa namna ulivyotoa mfano halisi.
Labda nami niongezee kwamba hizi nadharia mbili ni mtambuka. Tuseme hivi..
1.) tupime spidi ya mwanga tangu unapotoka katika chanzo chake hadi kutua katika uso wa kitu kingine,
VS
2.) spidi ya fikra tangu inapoona kitu na kung’amua kuwa ni kitu gani (iwe imekifahamu au kutokifahamu bali imekiona na kujua kuwa hiki ni kitu)
Changamoto hapo ni uwezekano wa kimojawapo kupimika na kingine kutopimika. Mfano: spidi pindi mwanga ulipotua ktk uso wa kitu na fikra kung’amua kuwa huu ni mwanga ni kitu ambacho kupima ni vigumu.
 
... nini maana ya spidi? Fikra inakuwaje na spidi? Huwezi kuzungumzia spidi bila kuzungumzia umbali; fikra inasafiri kutoka wapi kwenda wapi (source to destination)?

Hapana spidi sio lazima iwe na umbali. Fikiria kuhusu gurudumu linalozungushwa na injini bila kutembea au motor, je huwezi pima spidi yake?
 
Kwa namna gani giza si kitu?

Kwa namna gani kwamba giza halina speed?
Mi kwa mtazamo wangu ni kwamba giza ni mwanga pia the problem is it cant be registered by our sensory operators and if it does it cant be significantly interpreted so it filtered away, the same can not happen to some other animals, for they can see better in the darkness so to them darkness is light , if it is light to them probably it has got speed of its own who knows, this world was created fare for all inhabitants if we make our own human generalization to cover all dwellers we bound to destroy it , kuhusu kip chenye speed kubwa kati ya mwanga na nerve impulse , mi nadhan kwa sababu speed of light can scientifically be proven let it be cause we are talking in scientific perspective, on nerve impulse speed it depends with on the intensity of the impulse registered on the receptors, sometimes type of receptors also determine the speed at which the nerve impulse can travel to trigger certain response, mi napendekeza speed of electricity although hata nerve impulse ni electricity ila mimi naongelea huu wa tanesco wakuu yaan ile switch unawasha mpaka unahisi switch ndo imechelewa kuwasha ,
 
Hapana spidi sio lazima iwe na umbali. Fikiria kuhusu gurudumu linalozungushwa na injini bila kutembea au motor, je huwezi pima spidi yake?
... swali zuri. Tatizo umejikita zaidi kwenye linear motion pengine ukasahau kuna angular motion. Maelezo ni marefu kidogo ila rejea topic inayoitwa "angular motion" angular displacement, angular velocity, radian, angular acceleration, n.k.

Labda nikuulize swali; kwa mfano mdudu akiwa kwenye point fulani kwenye tairi la gari linalozunguka bila gari kutembea ukimtazama atakuwa pale pale? Hutamwona akitoka Point A to Point B? Kama ndivyo, huo ndio umbali.
 
....
2.) spidi ya fikra tangu inapoona kitu na kung’amua kuwa ni kitu gani (iwe imekifahamu au kutokifahamu bali imekiona na kujua kuwa hiki ni kitu)
Changamoto hapo ni uwezekano wa kimojawapo kupimika na kingine kutopimika. Mfano: spidi pindi mwanga ulipotua ktk uso wa kitu na fikra kung’amua kuwa huu ni mwanga ni kitu ambacho kupima ni vigumu.
... labda utoe mfano mwingine kwa mlango mwingine wa fahamu ila kwa mlango wa fahamu uliotumia KUONA, huwezi kuzungumzia kuona bila kuzungumzia mwanga; yaani hadi huko "kung'amua"kwa kuona unakozungumzia wewe kutokee ni matokeo ya mwanga hayo!
 
... swali zuri. Tatizo umejikita zaidi kwenye linear motion pengine ukasahau kuna angular motion. Maelezo ni marefu kidogo ila rejea topic inayoitwa "angular motion" angular displacement, angular velocity, radian, angular acceleration, n.k.

Labda nikuulize swali; kwa mfano mdudu akiwa kwenye point fulani kwenye tairi la gari linalozunguka bila gari kutembea ukimtazama atakuwa pale pale? Hutamwona akitoka Point A to Point B? Kama ndivyo, huo ndio umbali.

Pamoja sana nakuelewa..
 
... labda utoe mfano mwingine kwa mlango mwingine wa fahamu ila kwa mlango wa fahamu uliotumia KUONA, huwezi kuzungumzia kuona bila kuzungumzia mwanga; yaani hadi huko "kung'amua"kwa kuona unakozungumzia wewe kutokee ni matokeo ya mwanga hayo!

Namaanisha uwezo wa macho kuona na kupeleka hiyo taarifa kwa ubongo ikachakatwa na kung’amua ilichokiona ni mwanga, je spidi yake ilikuwa kubwa/ndogo ukiilinganisha na ile ya mwanga kutoka from “source” to “destination”?
Mantiki yangu ndio ipo hapo katika kufikirisha kitu chenye spidi kubwa zaidi ya kingine kati ya mwanga na fikra
 
Back
Top Bottom