Unachukuliaje pale unaponyimwa msaada kutoka kwa ndugu au rafiki yako aliye tajiri?

Ukinyimwa msaada na ndugu au rafiki yako ambaye ni tajiri au mtu mwenye uwezo mzuri kidogo kifedha usichukue, usilalamike, usimsimange wala usimseme vibaya kwamba ana roho mbaya au ni mchoyo.

Katika jamii maskini kama zetu watu waliofanikiwa ni wachache na wanaombwa misaada na watu wengi wanaowazunguka sio wewe peke yako, hivyo ni bora kuwa muelewa pale unapokosa msaada unaoutarajia kwa mtu uliyemuomba huo msaada.
Wahenga: Mtegemea cha ndugu hufa masikini.

Hii imesemwa zamani kweusi.
 
Ki binadam najihisi vibaya lakin huwa tunashindwa kufikiria. Nyuma. Kuwa. Hata Alie hela nae huwa anakua nashidaa Zaid hata ya sis. Tunaoombaaaa

Ukiwa na hela unakuwa na shida zipi tena za hela kama una hela ?
 
Umeongea point ya maana sana...

Unakuta binadamu anakuomba msaada ukisema ngoja kwanza anachukia, bila kujua kwamba una msururu wa binadamu wengine wamekuomba msaada pia...
 
Back
Top Bottom