Unachopaswa kujua kuhusu Ushoga

Babu wa Kambo

JF-Expert Member
May 2, 2016
559
807
KUHUSU USHOGA
----------------------------
Historia: Kwa ufupi tu, mapenzi yaJinsia moja hasa jinsia ya kiume yamekuwa yakipigwa vita miaka nenda miaka rudi katika maeneo mbalimbali duniani. Tamaduni, sheria na dini zimekuwa zikipingana na ushoga kwa sababu sio jambo la asili. Mnamo karne ya 12, kanisa katoliki lilipiga marufuku waumini wake kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja (ushoga). Kabla ya hapo, ushoga haukuwa kitu cha kujadili, ulipuuzwa. Lakini marufuku za kidini na kisheria zilianza kuwekwa pale ushoga ulipoanza kuota mizizi katika jamii.

Wataalamu wa tiba mbalimbali, madaktari na wanasaikolojia wamekuwa wakishindana kufanya tafiti juu ya ushoga; sababu, chanzo na tiba. Baadhi ya wataalamu wameona kuwa ushoga sio jambo la asili, huku wengine kama Dr. Sigmund Freud wakiona kuwa ushoga ni jambo la asili na hakuna sababu ya kutafuta tiba wala kuwatungia sheria za kuwakataza watu kushiriki mapenzi ya jinsia moja. Hata hivyo kwa kipindi kirefu ushoga uliwekwa kwenye kundi la maradhi ya akili (psychological disorders).

Ilipofika mwaka 1973, taasisi ya magonjwa ya akili ya Marekani (American Psychiatrist Association) iliondoa ushoga kwenye kundi la maradhi ya akili, hii ilifuatiwa pia na ushirika wa saikolojia wa hukohuko marekani (American Psychology Association) ulipouondoa ushoga kwenye kundi la matatizo ya kisaikolojia mwaka 1975. Kwa hiyo katika marekani, ushoga ukatolewa kwenye maradhi ya akili, na vilevile kwenye matatizo ya kisaikolojia. Uamuzi huu haukufanywa kwa sababu za kitafiti kama taaluma za kitabibu zinavyoelekeza bali kwa ushawishi wa kilaghai (lobying) na mashinikizo kutoka makundi ya mashoga huko marekani.

Mnamo mwaka 1990, shirika la afya duniani, WHO nalo likafuata mkondo wa kuondoa ushoga kwenye kundi la maradhi ya akili.

Saikolojia
Hakuna hitimisho rasmi la kutosha kueleza kama mapenzi ya jinsia moja ni matokeo ya maradhi ya akili au ni jambo la asili. Ingawa tafiti fulani zinaonesha kuwa watu wengi wanaojihusisha na tabia hii wame'ipata' baada ya kuzaliwa (acquired) na sio ya kuzaliwa nayo.

Elimu ya viumbe hai (biologia) haitoi ushahidi wa binadamu kuwa sahihi katika mapenzi ya jinsia moja. Vilevile, elimu ya maumbile ya binadamu (Human Anatomy) haitoi ushirikiano katika muingiliano wa kimapenzi baina ya wanadamu wa jinsia moja. Lakini jambo la hakika ni kwamba watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja wapo na wanafurahia tendo hilo. Hapo ndipo penye kufikiri.

Mwanasaikolojia Dr. Sigmund Freud anajaribu kuelezea namna mabadiliko ya akili-ngono (psychosexual) yanavyotokea kwa binadamu. Katika kile kinachoitwa 'Oedipus Complex, Freud anasema,
Akili-ngono (psychosexual) ya mtoto hukua kwa kupitia hatua tano, hatua hizo ni 1. Oral (mdomo) 2. Anal (mkundu) 3.Phallic (Uume) 4. The latent satage (hatua ya mpito) 5. Genetalia (sehemu zote za siri). Ni katika hatua ya tatu (phallic stage) ambapo mtoto huanza kujitambua kimaumbile na kujitofautisha na watu wa jinsia tofauti. Hatua hii hutokea kati ya umri wa miaka 3-6.

Katika hatua hii, binadamu huyu mtoto huanza kuwaona watu wa jinsia tofauti Kama watu tofauti na yeye. Vivo hivyo huweza kutamani kingono watu wa jinsia tofauti, wa umri wote. Kwa hivyo kwa watoto wa kiume huweza kuwatamani mama zao ambao huambatana nao kwa karibu kuliko mtu yeyote, na mtoto wa kike kutamani baba zao. Karibu mara zote, hatua hii hupita, na mara chache huweza kuendelea hadi wakati wa kubalehe. Lakini pia, katika hatua hii ya Tatu ya ukuaji wa akili ngono, mtoto huweza kujitamani mwenyewe. Na hapo ndio kunaweza kuambatana na kutamani watu wa jinsia yake. Bado elimu zaidi inahitajika kujifunza zaidi mambo haya yenye utata.

Dunia na ushoga.
Katika kitabu chake cha Conspirators Hierarchy, mwana intelijensia Dr. John Coleman anaeleza kwa kifupi tu namna serikali za marekani na uingereza zinavyofanyakazi kwa mashinikizo ya makundi ya siri, yakiwemo makundi ya mashoga. (Homosexuals). Makundi hayo ya (homosexuals) wamejiingiza katika makundi maengine ya siri kama vile, Order of st John of Jerusalem, Bachofen, Royal Institute for International Affairs (RIILA), Illuminati, Bilderbelgers, Trialterals, Freemasonry, Round Table, Cini foundation, Club of Rome, The Fabianist (waanglikana), Council of Foreign Relations (CFR), Zionist, Hellfire clubs, The Venetian Black Nobility, The Mont Pelerin Society, Bolshevism-Rosicrucianism, Rothchildren of Europe. Nk.

Yapo makundi mengi yenye nguvu ya fedha na intelijensia. Nimependa kunakili orodha hiyo ili ifahamike kuwa sio kitu rahisi tunapozugumzia ushawishi wa makundi haya katika serikali kubwa za dunia. Tunaweza pia kuwaongeza Jesuits Fathers (wakatoliki) ambao hawakutajwa na Dr. Coleman. Ni makundi ambayo serikali za dunia ya tatu hazifui dafu kupambana nayo.

Mara nyingi sisi watu wadogo tunanufaika na/au kuathirika pale makundi haya yanapokinzana au yanapoafikiana katika kazi zao, ndio pale unapoona sasa kanisa la Anglican linakubali ushoga, na katika kuliingilia kanisa katoliki tunaona papa Benedict anajiuzulu na anaingia papa Francis na kuweka rekodi ya kuwa 'Mjesuits' wa kwanza kushika wadhifa wa upapa. Ni mapambano tu.

Sasa; ushoga ulianza kwanza kukubalika (acceptable), maana yake katika mataifa hayo ushoga ulikubalika na kuwa sehemu ya maisha ya kawaida. Pili ukatungiwa sheria (legal), maana yake hutakiwi kuwapinga, la! Utahukumiwa. Lakini si hivyo tu, sasa hivi unatangazwa na kuhamasishwa kupitia vyombo mbali mbali vya magharibi. Mbinu kadhaa zinatumika kuhamasisha ushoga, Moja! Kupitia filamu na muziki, mbili kupitia vitabu vya nchi za magharibi na kuzuia vitabu vya nchi za Asia ya Kati (Arabia, Armaic) au 'semitic books'. Tatu kupitia dini (anglican church) kwa udhanio wa uratibu wa "The Fabianists".

Nne kupitia wataalamu wa tiba (madaktari na wanasaikolojia), tano kutumia intelijensia ya habari, sita kutumia tasisi za misaada (sir Elton John ni moja Kati ya wafadhili wakubwa wa tafiti za afya Tanzania) na kadhalika kadhalika.

Swali bado linabaki kuwa, kwanini haikutosha kuruhusu ushoga badala yake unatangazwa na kuhamasishwa! Tuendelee kujifunza

Bado kuna mengi ya kuandika , jinsi serikali za nchi nyingine zinavyopambana na ushoga wa magharibi, kwa mfano Urusi na Uchina zinavyodhibiti filamu, miziki, video na mitandao ya kijamii ya magharabi, mathalani tamthilia maarufu ya 'Game of thrones, lazima ichujwe name kundoa 'scenes' zote zinazohusu ushoga kabla ya kurushwa kwenye televisheni za China.

Tamthilia hiyo pia imepigwa marufuku kuoneshwa katika kambi za jeshi la uturuki (TSK). Orodha ya filamu na tamthilia zinazohamasisha ushoga ni nyingi. Intelijensia za magharibi zimetamalaki katika kutumia teknohama kueneza itikadi zao, na 'mambo yao' .Wakati mwengine huenezwa propaganda kuwa watu wa zamani wenye ushawishi walikuwa mashoga, mfano mwanasayansi Sir Isaac Newton, na Leonardo da Vinci. Lengo ni kutaka kuhalalaisha ushoga kwenye akili za watu.
Hatuwezi kumaliza kuandika.

Nitoe rai tu kwa watanzania, huku tukiendelea kujiuliza swali lilelile; kwa nini haikutosha kuruhusu ushoga na badala yake unatangazwa in kuhamasishwa?
Majibu ya swali hili yanaweza Kuwa magumu kuliko swali lenyewe, na bahati mbaya tayari tumeshaingiliwa. Katika mikoa ya kanda za juu kusini, Njombe, iringa nk, kumekuwa na ugawaji wa vilainishi kwa wanaume wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja, zoezi linaloambatana na upimaji wa VVU. Lakini kwa bahati mbaya zoezi hilo linafanywa kwa namna ya kuhamasisha ushoga.

Kuna habari ya mtoto wa kiume aliyeingiliwa kinyume na watu wazima huko Njombe. Kisha akapewa vilainishi (lubricants) au jelly, na yeye akawakusanya wenzake wa kiume ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi kisha wakafanyiana na kugawana vilainishi!

Lengo la vilainishi laweza kuwa kurahisisha huo mchezo na kupunguza uwezekano wa kuambukizana maradhi, lakini zaidi, vilainishi vinaacha hamu ya kurudiarudia tendo hili ambalo kwa imani za wengi ni kharamu. Kwa nini kuhamasisha ushoga?

Wazazi na Walezi chukueni tahadhari, Serikali tuondoleeni hii aibu.....
 
Majibu ya swali hili yanaweza Kuwa magumu kuliko swali lenyewe, na bahati mbaya tayari tumeshaingiliwa. Katika mikoa ya kanda za juu kusini, Njombe, iringa nk, kumekuwa na ugawaji wa vilainishi kwa wanaume wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja, zoezi linaloambatana na upimaji wa VVU. Lakini kwa bahati mbaya zoezi hilo linafanywa kwa namna ya kuhamasisha ushoga.
Kuna habari ya mtoto wa kiume aliyeingiliwa kinyume na watu wazima huko Njombe. Kisha akapewa vilainishi (lubricants) au jelly, na yeye akawakusanya wenzake wa kiume ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi kisha wakafanyiana na kugawana vilainishi!
Mpwa natamani sana saana MUNGU amuongoze Makonda asome au afiukishiwe ujumbe huu kisha anitafute privately niongee nae kwa kirefu, watu wengi sana wanapiga kelele tu pamoja na yeye Makonda aidha kwa kujua au kwa kutokuja kuwa tumeshaingiliwa na imeshakaa pabaya, ulichokisema kuhusu huko ni ukweli mtupu kabisa.

Kwa bahati mbaya sana sana hatutaweza kutumia hasira kama Makonda bali busara na Neema ya MUNGU peke yake ituongoze otherwise tatizo ni kubwa kuliko tunavyodhani, naongea kwa facts.
 
KUHUSU USHOGA
----------------------------
Historia: Kwa ufupi tu, mapenzi yaJinsia moja hasa jinsia ya kiume yamekuwa yakipigwa vita miaka nenda miaka rudi katika maeneo mbalimbali duniani. Tamaduni, sheria na dini zimekuwa zikipingana na ushoga kwa sababu sio jambo la asili. Mnamo karne ya 12, kanisa katoliki lilipiga marufuku waumini wake kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja (ushoga). Kabla ya hapo, ushoga haukuwa kitu cha kujadili, ulipuuzwa. Lakini marufuku za kidini na kisheria zilianza kuwekwa pale ushoga ulipoanza kuota mizizi katika jamii.
Wataalamu wa tiba mbalimbali, madaktari na wanasaikolojia wamekuwa wakishindana kufanya tafiti juu ya ushoga; sababu, chanzo na tiba. Baadhi ya wataalamu wameona kuwa ushoga sio jambo la asili, huku wengine kama Dr. Sigmund Freud wakiona kuwa ushoga ni jambo la asili na hakuna sababu ya kutafuta tiba wala kuwatungia sheria za kuwakataza watu kushiriki mapenzi ya jinsia moja. Hata hivyo kwa kipindi kirefu ushoga uliwekwa kwenye kundi la maradhi ya akili (psychological disorders).

Ilipofika mwaka 1973, taasisi ya magonjwa ya akili ya Marekani (American Psychiatrist Association) iliondoa ushoga kwenye kundi la maradhi ya akili, hii ilifuatiwa pia na ushirika wa saikolojia wa hukohuko marekani (American Psychology Association) ulipouondoa ushoga kwenye kundi la matatizo ya kisaikolojia mwaka 1975. Kwa hiyo katika marekani, ushoga ukatolewa kwenye maradhi ya akili, na vilevile kwenye matatizo ya kisaikolojia. Uamuzi huu haukufanywa kwa sababu za kitafiti kama taaluma za kitabibu zinavyoelekeza bali kwa ushawishi wa kilaghai (lobying) na mashinikizo kutoka makundi ya mashoga huko marekani.

Mnamo mwaka 1990, shirika la afya duniani, WHO nalo likafuata mkondo wa kuondoa ushoga kwenye kundi la maradhi ya akili.

Saikolojia
Hakuna hitimisho rasmi la kutosha kueleza kama mapenzi ya jinsia moja ni matokeo ya maradhi ya akili au ni jambo la asili. Ingawa tafiti fulani zinaonesha kuwa watu wengi wanaojihusisha na tabia hii wame'ipata' baada ya kuzaliwa (acquired) na sio ya kuzaliwa nayo.

Elimu ya viumbe hai (biologia) haitoi ushahidi wa binadamu kuwa sahihi katika mapenzi ya jinsia moja. Vilevile, elimu ya maumbile ya binadamu (Human Anatomy) haitoi ushirikiano katika muingiliano wa kimapenzi baina ya wanadamu wa jinsia moja. Lakini jambo la hakika ni kwamba watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja wapo na wanafurahia tendo hilo. Hapo ndipo penye kufikiri.

Mwanasaikolojia Dr. Sigmund Freud anajaribu kuelezea namna mabadiliko ya akili-ngono (psychosexual) yanavyotokea kwa binadamu. Katika kile kinachoitwa 'Oedipus Complex, Freud anasema,
Akili-ngono (psychosexual) ya mtoto hukua kwa kupitia hatua tano, hatua hizo ni 1. Oral (mdomo) 2. Anal (mkundu) 3.Phallic (Uume) 4. The latent satage (hatua ya mpito) 5. Genetalia (sehemu zote za siri). Ni katika hatua ya tatu (phallic stage) ambapo mtoto huanza kujitambua kimaumbile na kujitofautisha na watu wa jinsia tofauti. Hatua hii hutokea kati ya umri wa miaka 3-6.
Katika hatua hii, binadamu huyu mtoto huanza kuwaona watu wa jinsia tofauti Kama watu tofauti na yeye. Vivo hivyo huweza kutamani kingono watu wa jinsia tofauti, wa umri wote. Kwa hivyo kwa watoto wa kiume huweza kuwatamani mama zao ambao huambatana nao kwa karibu kuliko mtu yeyote, na mtoto wa kike kutamani baba zao. Karibu mara zote, hatua hii hupita, na mara chache huweza kuendelea hadi wakati wa kubalehe. Lakini pia, katika hatua hii ya Tatu ya ukuaji wa akili ngono, mtoto huweza kujitamani mwenyewe. Na hapo ndio kunaweza kuambatana na kutamani watu wa jinsia yake. Bado elimu zaidi inahitajika kujifunza zaidi mambo haya yenye utata.

Dunia na ushoga.
Katika kitabu chake cha Conspirators Hierarchy, mwana intelijensia Dr. John Coleman anaeleza kwa kifupi tu namna serikali za marekani na uingereza zinavyofanyakazi kwa mashinikizo ya makundi ya siri, yakiwemo makundi ya mashoga. (Homosexuals). Makundi hayo ya (homosexuals) wamejiingiza katika makundi maengine ya siri kama vile, Order of st John of Jerusalem, Bachofen, Royal Institute for International Affairs (RIILA), Illuminati, Bilderbelgers, Trialterals, Freemasonry, Round Table, Cini foundation, Club of Rome, The Fabianist (waanglikana), Council of Foreign Relations (CFR), Zionist, Hellfire clubs, The Venetian Black Nobility, The Mont Pelerin Society, Bolshevism-Rosicrucianism, Rothchildren of Europe. Nk.

Yapo makundi mengi yenye nguvu ya fedha na intelijensia. Nimependa kunakili orodha hiyo ili ifahamike kuwa sio kitu rahisi tunapozugumzia ushawishi wa makundi haya katika serikali kubwa za dunia. Tunaweza pia kuwaongeza Jesuits Fathers (wakatoliki) ambao hawakutajwa na Dr. Coleman. Ni makundi ambayo serikali za dunia ya tatu hazifui dafu kupambana nayo. Mara nyingi sisi watu wadogo tunanufaika na/au kuathirika pale makundi haya yanapokinzana au yanapoafikiana katika kazi zao, ndio pale unapoona sasa kanisa la Anglican linakubali ushoga, na katika kuliingilia kanisa katoliki tunaona papa Benedict anajiuzulu na anaingia papa Francis na kuweka rekodi ya kuwa 'Mjesuits' wa kwanza kushika wadhifa wa upapa. Ni mapambano tu.

Sasa; ushoga ulianza kwanza kukubalika (acceptable), maana yake katika mataifa hayo ushoga ulikubalika na kuwa sehemu ya maisha ya kawaida. Pili ukatungiwa sheria (legal), maana yake hutakiwi kuwapinga, la! Utahukumiwa. Lakini si hivyo tu, sasa hivi unatangazwa na kuhamasishwa kupitia vyombo mbali mbali vya magharibi. Mbinu kadhaa zinatumika kuhamasisha ushoga, Moja! Kupitia filamu na muziki, mbili kupitia vitabu vya nchi za magharibi na kuzuia vitabu vya nchi za Asia ya Kati (Arabia, Armaic) au 'semitic books'. Tatu kupitia dini (anglican church) kwa udhanio wa uratibu wa "The Fabianists". Nne kupitia wataalamu wa tiba (madaktari na wanasaikolojia), tano kutumia intelijensia ya habari, sita kutumia tasisi za misaada (sir Elton John ni moja Kati ya wafadhili wakubwa wa tafiti za afya Tanzania) na kadhalika kadhalika.
Swali bado linabaki kuwa, kwanini haikutosha kuruhusu ushoga badala yake unatangazwa na kuhamasishwa! Tuendelee kujifunza

Bado kuna mengi ya kuandika , jinsi serikali za nchi nyingine zinavyopambana na ushoga wa magharibi, kwa mfano Urusi na Uchina zinavyodhibiti filamu, miziki, video na mitandao ya kijamii ya magharabi, mathalani tamthilia maarufu ya 'Game of thrones, lazima ichujwe name kundoa 'scenes' zote zinazohusu ushoga kabla ya kurushwa kwenye televisheni za China. Tamthilia hiyo pia imepigwa marufuku kuoneshwa katika kambi za jeshi la uturuki (TSK). Orodha ya filamu na tamthilia zinazohamasisha ushoga ni nyingi. Intelijensia za magharibi zimetamalaki katika kutumia teknohama kueneza itikadi zao, na 'mambo yao' .Wakati mwengine huenezwa propaganda kuwa watu wa zamani wenye ushawishi walikuwa mashoga, mfano mwanasayansi Sir Isaac Newton, na Leonardo da Vinci. Lengo ni kutaka kuhalalaisha ushoga kwenye akili za watu.
Hatuwezi kumaliza kuandika.

Nitoe rai tu kwa watanzania, huku tukiendelea kujiuliza swali lilelile; kwa nini haikutosha kuruhusu ushoga na badala yake unatangazwa in kuhamasishwa?
Majibu ya swali hili yanaweza Kuwa magumu kuliko swali lenyewe, na bahati mbaya tayari tumeshaingiliwa. Katika mikoa ya kanda za juu kusini, Njombe, iringa nk, kumekuwa na ugawaji wa vilainishi kwa wanaume wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja, zoezi linaloambatana na upimaji wa VVU. Lakini kwa bahati mbaya zoezi hilo linafanywa kwa namna ya kuhamasisha ushoga.
Kuna habari ya mtoto wa kiume aliyeingiliwa kinyume na watu wazima huko Njombe. Kisha akapewa vilainishi (lubricants) au jelly, na yeye akawakusanya wenzake wa kiume ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi kisha wakafanyiana na kugawana vilainishi!

Lengo la vilainishi laweza kuwa kurahisisha huo mchezo na kupunguza uwezekano wa kuambukizana maradhi, lakini zaidi, vilainishi vinaacha hamu ya kurudiarudia tendo hili ambalo kwa imani za wengi ni kharamu. Kwa nini kuhamasisha ushoga?

Wazazi na Walezi chukueni tahadhari, Serikali tuondoleeni hii aibu.....

Mkuu umeleza vzr sana kwa kukusaidia kupata jibu kwanini ushoga umekuwa ukipromotiwa kwa kiasi kikubwa kama ulivyoeleza
Kasome kitu kinachoitwa "global depopulation policy"
Pia tafuta kitabu ki achoitwa KILLING US SOFT cha kelvin Galilae
 
Simulizi za mababu wakati babu zetu walipokua wanachukuliwa utumwani kulikuwa na wenye nguvu na hawakupenda kitendo kile, waliwapa shida sana wamiliki wao baada ya kununuliwa. Hii ilipelekea kuwafunga kwa minyororo na kuwalawiti mbele ya wengine ili (a way of humiliating them) kuwapunguza nguvu psychologically.
 
Nyendo za kishoga zinatia mawaa hata kuzisikia. Ni huzuni kuona mtu fulani katopea katika mambo hayo. Ni vema basi jamii yetu ijifunze na kujiridhisha namna bora za kuokoa kizazi chetu.

Ni ajabu sana kwa baadhi ya members humu JF kuwa na hulka ya kumshambulia awaye yote anayetaka kutoa andiko la kujielimisha kuhusu tabia hizi zinazokirihisha nafsi za waungwana. Tujadili kwa kujenga hoja imara.
 
Uzi umetulia sana...

Ila sidhani kama watu wanaufahamu na tamthilia "pendwa" zinazorushwa kwenye vituo vyetu vya Tv ambazo nyingi zina scene za ushoga zimewekwa kwa makusudi ili kusoftmind zetu ili ionekane hilo ni jambo la kawaida hata ukiliona mtaani kwako usishangae.
 
Uchafu tu, afadhali ushoga wa wanawake kwa wanawake hawaingiliani kwenye haja kubwa
 
Ahsante kwa habari. Naweza kusema kuwa ushoga unatangazwa kwa nguvu sana ni hii inatokana na kuendelea kukua kwa population duniani.
Ukifikira matatizo mengi tuliyonayo duniani kama vita,maradhi,food shortage zote zinaashiria kiwa kuna ongezeko kubwa la watu. Ndio maana watu wanazusha vita na maradhi kupunguza watu.

Kwahio watu wakijamiana kama wanawake kwa wanawake hali kathalika na wanaume then kuna punguza uwezekano wa kuzaliana baina ya mwaname na mwanamke.

Tatizo ni resources vs population.

Serikali ya Tanzania inapokea misaada bila kujali,kuchunguza hv vitu mfano madawa,pembejeo,hata mbolea na hata vyakula.

Wazungu wameelekeza nguvu zao kibwa sana kuharibu udongo wa africa na kuwaua waafrica in massive huku wanaua wenzao taratibu pia.

Dunia imekwisha hii
 
By beholding, we become changed. Maneno haya wanayatumia vizuri sana. Wewe jiulize, ukiachana na wanaume wanaofanyiziana kwenye sehemu ya haja kubwa, wanaume wanaowaingilia kinyume na maumbile mabinti na wamama, wengi huwa ni waliotazama sana video za ngono.

Japo pia, mtu anaweza kubadilika kupitia kusikia kwa wenzake, kama ambavyo imeanza kuingizwa taratibu kupitia shoga na kupitia bwana Makonda. Maana Makonda anaweeza kuwa anafanya jambo sahihi kabisa, lakini matamshi yake yanaweza kuwa kichocheo cha mtu flani kujaribu ajue kuna nini katika hicho kinachopigiwa kelele.
 
Sasa unasema Anglican church inaunga mkono ushoga mbona juzi mtoto wa Desmond tutu aliyekua mchungaji alimuoa mwanamke mwenzake kanisa likamfukuza na kumvua uchungaji inakuwaje hapo?
 
Any publicity is good publicity. Nguvu nyingi inatumika kupambana na hili janga wakati in reality sio janga kubwa kama watu wadhaniavyo matokeo yake ushoga utazidi kuchanja mbuga kiulaini.
 
Ushoga ni moja kati ya agenda za new world order inaangukia kwenye section ya population control pamoja na abortion na family plan na facebook wamezindua mpya kwa wafanya kazi wao kutoa mbegu zao zinawekwa preserved then watachagua muda muafaka watakapotaka kupata mtoto na Japan wameshaichukua hiyo technology.
 
isidingo ni tamthilia ambayo imekuwa inapendwa na watu wengi lakini nyuma ya pazia wanapromoti mapenzi ya jinsia moja na kuwafanya wahusika wanaofanya hivyo waonekane mashujaa, tamthiliya za kifilipino nazo nyingi zimekuwa zikipromoti mapenzi ya jinsia moja kiasi cha kubadili mtazamo wa wengi na kuona kitendo hicho kama cha kawaida mbaya zaidi kinaangaliwa na watoto ambao hawajafikia miaka 18
 
Back
Top Bottom