Umoja wa mataifa umesema umewaita nyumbani walinda amani 46 kutoka Ghana waliotuhumiwa kufanya unyanyasaji wa kingono wakati wa shughuli zao nchini Sudan Kusini.
Msemaji wa umoja wa mataifa amesema kulikua na taarifa za walinda amani wa Ghana kutuhumiwa kununua wanawake kwa ajili ya kufanya ngono.
Amesema umoja wa mataifa hautafumbia macho tabia kama hizo nchini Sudan na kwingineko.
Chanzo: BBC Swahili