UN yatoa tamko sakata la Loliondo, yataka Tanzania kuondoa maafisa wa Polisi Ngorongoro

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Feb 13, 2017
320
899
Umoja wa mataifa (UN) umeitaka Tanzania kuondoa maafisa wake wa usalama Loliondo ili kukomesha ukiukwaji wa haki za binadamu na unyanyasaji unaodaiwa kufanyika katika eneo hilo ili kuruhusu waandishi wa habari, wanasheria, waangalizi wa haki za binadamu na asasi za kiraia kuingia Loliondo, kuzungumza na Wamasai walioathirika na kuripoti hali hiyo bila vitisho.

Kupitia taarifa ,Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wenyeji ama watu wa asili limeeleza kusikitishwa kwake na juhudi zinazoendelea za kuwaondoa zaidi ya Wamasai 70,000 wa tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro, Tanzania kutoka eneo la kilomita za mraba 1,500, ambazo ni ardhi ya vijiji iliyosajiliwa kisheria.

Jukwaa hilo limesema kwamba mnamo Juni 8, lilipata taarifa kuwa polisi wa Tanzania kwa kutumia nguvu, ikiwa ni pamoja na kutumia silaha kiholela, waliwaondoa kwa nguvu Wamasai katika ardhi zao na kusababisha makumi ya watu kujeruhiwa huku baadhi ya watu wakikimbilia msituni. Pia iliripotiwa matukio mbalimbali ya kukamatwa kwa viongozi wa jamii hiyo, wakiwemo Madiwani wa Vijiji na Wenyeviti. Umoja wa mataifa unataja vitendo hivi kuwa ni ukiukwaji wa wazi wa haki za binadamu na za Wamasai wa Loliondo.

Tanzania imesema nini hadi sasa?​

Serikali ya Tanzania tayari imekwisha jibu shutuma mbali mbali ambazo zimekuwa zikitolewa huku wakitaka raia na wanaharakati kuto changanya uondokaji wa watu kwa hiari katika hifadhi ya ngorongoro na uwekwaji wa mipaka katika eneo la Loliondo ambapo ndipo mvutano unapodaiwa kutokea.

Siku moja baada ya kuibuka taarifa za vurugu Loliondo, wakati akilihutubia Bunge mjini Dodoma, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema hakuna mapigano katika eneo hilo .

Majaliwa alisema Serikali inaweka alama za mipaka ya eneo la hifadhi ya Loliondo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 1,500 kutoka sehemu iliyotengwa kwa ajili ya shughuli za kibinadamu.

"Kilichotokea hasa ni magari ya Serikali kupita katika baadhi ya vijiji vya Loliondo yakienda kuweka minara.

Ndipo baadhi ya wakazi ambao hawakufahamu hatua hiyo wakakusanyika ili kujadili suala hilo," alisema Bw Majaliwa ambaye alikuwa akitoa taarifa ya serikali baada ya kusambazwa kwa video hizo.

"Wakati wa mkutano wao, baadhi ya watu waliandamana wakidhani kwamba watafukuzwa'.

Alitoa hakikisho kuwa hakuna mtu atakayefukuzwa Loliondo .

Pia Simon Sirro, Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania siku ya Jumatatu alionya na kusema, "Zoezi hili la kuweka alama za mipaka linaloendelea Loliondo ni zoezi la kisheria linalopaswa kuheshimiwa na watu wote, wanaochochea jamii zinazoishi katika eneo hili waache kufanya hivyo.

Tutahakikisha amani inakuwepo na tutawashughulikia wale wanaojaribu kwenda kinyume na sheria. Uwekaji mipaka wa eneo hilo ulikuwa kwa maslahi ya nchi na tutahakikisha kuwa kuna amani katika mchakato huo.'

Majeruhi walikimbilia Kenya?​

Serikali ya Tanzania ilipuuzilia mbali ripoti za Mbunge wa Ngorongoro Emmanuel Ole Shangai kwamba baadhi ya raia wake walikimbia nje ya nchi kutafuta matibabu.

Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa alisema "Serikali ya Tanzania haina taarifa za wanaodai kutibiwa Kenya, tunashughulika na watu walio ndani ya mipaka yetu pekee. Wanaodai kupata matibabu kwa majirani zetu wajue tuna kila kitu na hawana sababu za kwenda nje ya nchi.
 
Aisee.
JamiiForums1510998594_512x265.jpg
 
UN na haki za BINADAMU wapi na wapi?
Wangeanzia Palestina wakaja Yemen kabla ya kufika Pemba na Tanzania kwa ujumla
 
Mbona mnapokea ARV na misaada kibao kutoka kwao na hamlalamiki?
Mbona ninyi ccm mliharibu chaguzi za 2019 na 2020 wazungu walikaa kimya na mliona ni sawa?

Sent from my TECNO-N8 using JamiiForums mobile app
Mimi sio ccm uwe na adabu,halafu hakuna kitu UN au Beberu anakitoa bure. Uliza kwanini tunalazimishwa kununua ARV's Kutoka kwao halafu wanasema ni misaada?
 
Umoja wa mataifa (UN) umeitaka Tanzania kuondoa maafisa wake wa usalama Loliondo ili kukomesha ukiukwaji wa haki za binadamu na unyanyasaji unaodaiwa kufanyika katika eneo hilo ili kuruhusu waandishi wa habari, wanasheria, waangalizi wa haki za binadamu na asasi za kiraia kuingia Loliondo, kuzungumza na Wamasai walioathirika na kuripoti hali hiyo bila vitisho.

Kupitia taarifa ,Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wenyeji ama watu wa asili limeeleza kusikitishwa kwake na juhudi zinazoendelea za kuwaondoa zaidi ya Wamasai 70,000 wa tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro, Tanzania kutoka eneo la kilomita za mraba 1,500, ambazo ni ardhi ya vijiji iliyosajiliwa kisheria.

TH

Jukwaa hilo limesema kwamba mnamo Juni 8, lilipata taarifa kuwa polisi wa Tanzania kwa kutumia nguvu, ikiwa ni pamoja na kutumia silaha kiholela, waliwaondoa kwa nguvu Wamasai katika ardhi zao na kusababisha makumi ya watu kujeruhiwa huku baadhi ya watu wakikimbilia msituni.

Pia iliripotiwa matukio mbalimbali ya kukamatwa kwa viongozi wa jamii hiyo, wakiwemo Madiwani wa Vijiji na Wenyeviti. Umoja wa mataifa unataja vitendo hivi kuwa ni ukiukwaji wa wazi wa haki za binadamu na za Wamasai wa Loliondo.

Tanzania imesema nini hadi sasa?

Serikali ya Tanzania tayari imekwisha jibu shutuma mbali mbali ambazo zimekuwa zikitolewa huku wakitaka raia na wanaharakati kuto changanya uondokaji wa watu kwa hiari katika hifadhi ya ngorongoro na uwekwaji wa mipaka katika eneo la Loliondo ambapo ndipo mvutano unapodaiwa kutokea.

Msemaji wa serikali Gerson Msigwa akizungumza na BBC amesema serikali haijaenda kuwaondoa Wamasai Loliondo au Ngorongoro ila wananchi wamepewa fursa ya kujiondoa kwa uhiari ili kupisha utunzaji wa mazingira

'Hakuna askari,serikali ama kiongozi serikali aliyetumwa kumuondoa mwananchi ama Masai kwenye makazi yake'

Bw.Msigwa amesema katika eneo la Ngorongoro,serikali imekuwa ikizungumza na wananchi ili waweze kupisha utunzaji wa mazingira katika eneo hilo na wanaojiandikisha kwa hiari ndio wanaohamishwa.

Siku moja baada ya kuibuka taarifa za vurugu Loliondo, wakati akilihutubia Bunge mjini Dodoma, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema hakuna mapigano katika eneo hilo.

Majaliwa alisema Serikali inaweka alama za mipaka ya eneo la hifadhi ya Loliondo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 1,500 kutoka sehemu iliyotengwa kwa ajili ya shughuli za kibinadamu.

"Kilichotokea hasa ni magari ya Serikali kupita katika baadhi ya vijiji vya Loliondo yakienda kuweka minara. Ndipo baadhi ya wakazi ambao hawakufahamu hatua hiyo wakakusanyika ili kujadili suala hilo," alisema Bw Majaliwa ambaye alikuwa akitoa taarifa ya serikali baada ya kusambazwa kwa video hizo.

"Wakati wa mkutano wao, baadhi ya watu waliandamana wakidhani kwamba watafukuzwa'.
Alitoa hakikisho kuwa hakuna mtu atakayefukuzwa Loliondo .

Pia Simon Sirro, Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania siku ya Jumatatu alionya na kusema, "Zoezi hili la kuweka alama za mipaka linaloendelea Loliondo ni zoezi la kisheria linalopaswa kuheshimiwa na watu wote, wanaochochea jamii zinazoishi katika eneo hili waache kufanya hivyo.

Tutahakikisha amani inakuwepo na tutawashughulikia wale wanaojaribu kwenda kinyume na sheria. Uwekaji mipaka wa eneo hilo ulikuwa kwa maslahi ya nchi na tutahakikisha kuwa kuna amani katika mchakato huo.'

Majeruhi walikimbilia Kenya?

Serikali ya Tanzania ilipuuzilia mbali ripoti za Mbunge wa Ngorongoro Emmanuel Ole Shangai kwamba baadhi ya raia wake walikimbia nje ya nchi kutafuta matibabu.

Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa alisema "Serikali ya Tanzania haina taarifa za wanaodai kukimbilia Kenya, tunashughulika na watu walio ndani ya mipaka yetu pekee. Wanaodai kupata matibabu kwa majirani zetu wajue tuna kila kitu na hawana sababu za kwenda nje ya nchi.

Source:
BBC Swahili
 

1655361281868.png

Wataalamu wa Masuala ya Haki za Binadamu Umoja wa Mataifa (UN) wametoa wito kwa Serikali ya Tanzania kusitisha mipango ya kuwahamisha Watu waishio Loliondo na eneo la Hifadhi la Ngorongoro Wameshauri Serikali kuanza mazungumzo ili kutambua changamoto zilizopo na kuzitatua.
 
Hao UN walipinga ujenzi wa bwawa la umeme kwamba ni kuharibu mazingira lakini sasa hivi wanapinga kuwahamisha wamasai ili kulinda mazingira!

Mtu mweusi amka
 
upuuzi mtupu.

zoezi lina endelea kama lilivyo pangwa,

sisi wakazi wa Loliondo wala hatuna tatizo na zoezi hili bali kuna watu wanatuwekea maneno mdomoni kwa malengo yao maovu.
Serikali isiyumbishwe na hao wadangaji.
 
Hilo linalofanyika ngorongoro...si kwa maslahi yq taifa..ni kwa maslahi ya waarabu na hao viongozi...kwa nini hilo jambo halikufanyika tokea awamu zilizopita au hiyo ngorongoro na hao wamasai hawakuwepo..
Tokea Samia aanze safari za uarabuni ndio hilo swala likaibuka..?
 
upuuzi mtupu.

zoezi lina endelea kama lilivyo pangwa,

sisi wakazi wa Loliondo wala hatuna tatizo na zoezi hili bali kuna watu wanatuwekea maneno mdomoni kwa malengo yao maovu.
Serikali isiyumbishwe na hao wadangaji.
Dah nchi ngumu Sana hii
 
Hao UN walipinga ujenzi wa bwawa la umeme kwamba ni kuharibu mazingira lakini sasa hivi wanapinga kuwahamisha wamasai ili kulinda mazingira!

Mtu mweusi amka
Mazungumzo ya kutatua changamoto kwanza kabla ya kuaanza kuwahamisha, siyo kwamba wasihamishwe.

Mfano taarifa ilitolewa na Serikali kwamba wamekaa vikao na mikutano na wakazi husika na wote kuafiki kuhama. Kumbe ikaja kuonekana kwalichukua watu wachache (maasai bandia) wakaweka kamkutano tu.
 
Umoja wa mataifa (UN) umeitaka Tanzania kuondoa maafisa wake wa usalama Loliondo ili kukomesha ukiukwaji wa haki za binadamu na unyanyasaji unaodaiwa kufanyika katika eneo hilo ili kuruhusu waandishi wa habari, wanasheria, waangalizi wa haki za binadamu na asasi za kiraia kuingia Loliondo, kuzungumza na Wamasai walioathirika na kuripoti hali hiyo bila vitisho.

Kupitia taarifa ,Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wenyeji ama watu wa asili limeeleza kusikitishwa kwake na juhudi zinazoendelea za kuwaondoa zaidi ya Wamasai 70,000 wa tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro, Tanzania kutoka eneo la kilomita za mraba 1,500, ambazo ni ardhi ya vijiji iliyosajiliwa kisheria.

Jukwaa hilo limesema kwamba mnamo Juni 8, lilipata taarifa kuwa polisi wa Tanzania kwa kutumia nguvu, ikiwa ni pamoja na kutumia silaha kiholela, waliwaondoa kwa nguvu Wamasai katika ardhi zao na kusababisha makumi ya watu kujeruhiwa huku baadhi ya watu wakikimbilia msituni. Pia iliripotiwa matukio mbalimbali ya kukamatwa kwa viongozi wa jamii hiyo, wakiwemo Madiwani wa Vijiji na Wenyeviti. Umoja wa mataifa unataja vitendo hivi kuwa ni ukiukwaji wa wazi wa haki za binadamu na za Wamasai wa Loliondo.

Tanzania imesema nini hadi sasa?​

Serikali ya Tanzania tayari imekwisha jibu shutuma mbali mbali ambazo zimekuwa zikitolewa huku wakitaka raia na wanaharakati kuto changanya uondokaji wa watu kwa hiari katika hifadhi ya ngorongoro na uwekwaji wa mipaka katika eneo la Loliondo ambapo ndipo mvutano unapodaiwa kutokea.

Siku moja baada ya kuibuka taarifa za vurugu Loliondo, wakati akilihutubia Bunge mjini Dodoma, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema hakuna mapigano katika eneo hilo .

Majaliwa alisema Serikali inaweka alama za mipaka ya eneo la hifadhi ya Loliondo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 1,500 kutoka sehemu iliyotengwa kwa ajili ya shughuli za kibinadamu.

"Kilichotokea hasa ni magari ya Serikali kupita katika baadhi ya vijiji vya Loliondo yakienda kuweka minara.

Ndipo baadhi ya wakazi ambao hawakufahamu hatua hiyo wakakusanyika ili kujadili suala hilo," alisema Bw Majaliwa ambaye alikuwa akitoa taarifa ya serikali baada ya kusambazwa kwa video hizo.

"Wakati wa mkutano wao, baadhi ya watu waliandamana wakidhani kwamba watafukuzwa'.

Alitoa hakikisho kuwa hakuna mtu atakayefukuzwa Loliondo .

Pia Simon Sirro, Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania siku ya Jumatatu alionya na kusema, "Zoezi hili la kuweka alama za mipaka linaloendelea Loliondo ni zoezi la kisheria linalopaswa kuheshimiwa na watu wote, wanaochochea jamii zinazoishi katika eneo hili waache kufanya hivyo.

Tutahakikisha amani inakuwepo na tutawashughulikia wale wanaojaribu kwenda kinyume na sheria. Uwekaji mipaka wa eneo hilo ulikuwa kwa maslahi ya nchi na tutahakikisha kuwa kuna amani katika mchakato huo.'

Majeruhi walikimbilia Kenya?​

Serikali ya Tanzania ilipuuzilia mbali ripoti za Mbunge wa Ngorongoro Emmanuel Ole Shangai kwamba baadhi ya raia wake walikimbia nje ya nchi kutafuta matibabu.

Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa alisema "Serikali ya Tanzania haina taarifa za wanaodai kutibiwa Kenya, tunashughulika na watu walio ndani ya mipaka yetu pekee. Wanaodai kupata matibabu kwa majirani zetu wajue tuna kila kitu na hawana sababu za kwenda nje ya nchi.
Tuwakumbuke majirani na Ndugu zetu Kenya ktk Uchaguzi wao Mungu awapitishe salama,

Kwa maana wagombea wote wawili wanawindwa na Shetani. Amen
 
Serikali iweke mpaka kuzuia wakenya kujipenyeza tena na makundi yao ya ng'ombe na kujifanya wao ni masai wa Tanzania, wahakikishe hili swala limekaa kwenye msitari.....
 
Umoja wa mataifa (UN) umeitaka Tanzania kuondoa maafisa wake wa usalama Loliondo ili kukomesha ukiukwaji wa haki za binadamu na unyanyasaji unaodaiwa kufanyika katika eneo hilo ili kuruhusu waandishi wa habari, wanasheria, waangalizi wa haki za binadamu na asasi za kiraia kuingia Loliondo, kuzungumza na Wamasai walioathirika na kuripoti hali hiyo bila vitisho.

Kupitia taarifa ,Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wenyeji ama watu wa asili limeeleza kusikitishwa kwake na juhudi zinazoendelea za kuwaondoa zaidi ya Wamasai 70,000 wa tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro, Tanzania kutoka eneo la kilomita za mraba 1,500, ambazo ni ardhi ya vijiji iliyosajiliwa kisheria.

Jukwaa hilo limesema kwamba mnamo Juni 8, lilipata taarifa kuwa polisi wa Tanzania kwa kutumia nguvu, ikiwa ni pamoja na kutumia silaha kiholela, waliwaondoa kwa nguvu Wamasai katika ardhi zao na kusababisha makumi ya watu kujeruhiwa huku baadhi ya watu wakikimbilia msituni. Pia iliripotiwa matukio mbalimbali ya kukamatwa kwa viongozi wa jamii hiyo, wakiwemo Madiwani wa Vijiji na Wenyeviti. Umoja wa mataifa unataja vitendo hivi kuwa ni ukiukwaji wa wazi wa haki za binadamu na za Wamasai wa Loliondo.

Tanzania imesema nini hadi sasa?​

Serikali ya Tanzania tayari imekwisha jibu shutuma mbali mbali ambazo zimekuwa zikitolewa huku wakitaka raia na wanaharakati kuto changanya uondokaji wa watu kwa hiari katika hifadhi ya ngorongoro na uwekwaji wa mipaka katika eneo la Loliondo ambapo ndipo mvutano unapodaiwa kutokea.

Siku moja baada ya kuibuka taarifa za vurugu Loliondo, wakati akilihutubia Bunge mjini Dodoma, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema hakuna mapigano katika eneo hilo .

Majaliwa alisema Serikali inaweka alama za mipaka ya eneo la hifadhi ya Loliondo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 1,500 kutoka sehemu iliyotengwa kwa ajili ya shughuli za kibinadamu.

"Kilichotokea hasa ni magari ya Serikali kupita katika baadhi ya vijiji vya Loliondo yakienda kuweka minara.

Ndipo baadhi ya wakazi ambao hawakufahamu hatua hiyo wakakusanyika ili kujadili suala hilo," alisema Bw Majaliwa ambaye alikuwa akitoa taarifa ya serikali baada ya kusambazwa kwa video hizo.

"Wakati wa mkutano wao, baadhi ya watu waliandamana wakidhani kwamba watafukuzwa'.

Alitoa hakikisho kuwa hakuna mtu atakayefukuzwa Loliondo .

Pia Simon Sirro, Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania siku ya Jumatatu alionya na kusema, "Zoezi hili la kuweka alama za mipaka linaloendelea Loliondo ni zoezi la kisheria linalopaswa kuheshimiwa na watu wote, wanaochochea jamii zinazoishi katika eneo hili waache kufanya hivyo.

Tutahakikisha amani inakuwepo na tutawashughulikia wale wanaojaribu kwenda kinyume na sheria. Uwekaji mipaka wa eneo hilo ulikuwa kwa maslahi ya nchi na tutahakikisha kuwa kuna amani katika mchakato huo.'

Majeruhi walikimbilia Kenya?​

Serikali ya Tanzania ilipuuzilia mbali ripoti za Mbunge wa Ngorongoro Emmanuel Ole Shangai kwamba baadhi ya raia wake walikimbia nje ya nchi kutafuta matibabu.

Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa alisema "Serikali ya Tanzania haina taarifa za wanaodai kutibiwa Kenya, tunashughulika na watu walio ndani ya mipaka yetu pekee. Wanaodai kupata matibabu kwa majirani zetu wajue tuna kila kitu na hawana sababu za kwenda nje ya nchi.
tanzania ni sovereigh state hatuwezi kuamliwa mambo yetu na wazungu,mbona wao yanawashinda.waende russia wakamsaidie ukraine.
 
Back
Top Bottom