kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,991
- 17,890
Katibu Mkuu wa Umoja wa maraufa amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unatoa himaya na uungaji mkono kwa makundi ya kigaidi likiwemo la Jabhat al-Nusra linaloendesha harakati zake huko nchini Syria.
Antonio Guterres amesema kuwa, imekuja katika ripoti maalumu ya kikosi cha kusimamia amani cha Umoja wa Mataifa katika eneo linalokaliwa kwa mabavu la miinuko ya Golan ya Syria kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel kuna wakati umekuwa ukituma misaada na hata kuwa na uratibu wa moja kwa moja na makundi ya kigaidi ya nchini Syria.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo ni kuwa, hadi sasa kikosi hicho cha Umoja wa Mataifa kimesajili kesi 16 za mawasiliano baina ya utawala wa Kizayuni wa Israel na makundi ya kigaidi.
Wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akieleza hayo, kuna nyaraka za wazi zinazoonyesha kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel umekuwa ukiyasaidia makundi ya kigaidi nchini Syria yanayofanya mauaji dhidi ya raia wasio na hatia kwa kisingizio cha kutaka kuindoa madarakani serikali ya Rais Bashar al-Assad.
Baadhi ya ripoti zinaonyesha kuwa, hata magaidi wanaojeruhiwa katika mapigano yao na wanajeshi wa Syria wamekuwa wakipatiwa matibabu huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel).
Licha ya hayo na hata kuweko ripoti za Umoja wa Mataifa zinazothibitisha wazi juu ya misaada ya Israel kwa makundi ya kigaidi, umoja huo umekuwa ukitosheka tu na kutoa ripoti za kukemea kitendo hicho; kwani hadi sasa haujachukua hatua za maana dhidi ya utawala huo ghasibu.
Parstoday
Antonio Guterres amesema kuwa, imekuja katika ripoti maalumu ya kikosi cha kusimamia amani cha Umoja wa Mataifa katika eneo linalokaliwa kwa mabavu la miinuko ya Golan ya Syria kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel kuna wakati umekuwa ukituma misaada na hata kuwa na uratibu wa moja kwa moja na makundi ya kigaidi ya nchini Syria.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo ni kuwa, hadi sasa kikosi hicho cha Umoja wa Mataifa kimesajili kesi 16 za mawasiliano baina ya utawala wa Kizayuni wa Israel na makundi ya kigaidi.
Wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akieleza hayo, kuna nyaraka za wazi zinazoonyesha kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel umekuwa ukiyasaidia makundi ya kigaidi nchini Syria yanayofanya mauaji dhidi ya raia wasio na hatia kwa kisingizio cha kutaka kuindoa madarakani serikali ya Rais Bashar al-Assad.
Baadhi ya ripoti zinaonyesha kuwa, hata magaidi wanaojeruhiwa katika mapigano yao na wanajeshi wa Syria wamekuwa wakipatiwa matibabu huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel).
Licha ya hayo na hata kuweko ripoti za Umoja wa Mataifa zinazothibitisha wazi juu ya misaada ya Israel kwa makundi ya kigaidi, umoja huo umekuwa ukitosheka tu na kutoa ripoti za kukemea kitendo hicho; kwani hadi sasa haujachukua hatua za maana dhidi ya utawala huo ghasibu.
Parstoday