Umwamba barabarani wa maafisa wa Serikali mlioko Dodoma, unatumaliza kwa ajali

Zygot

JF-Expert Member
Apr 14, 2016
2,238
2,864
Mara baada ya maafisa waandamizi kuhamia Dodoma kumekuwa na mtindo mpya wa uendeshaji magari barabarani. Kila gari ya serikali itokayo Dodoma kwenda nje ya mkoa huwasha taa na kukimbia kwa mwendo kasi zaidi ya alama za barabarani.

Huu ni umwamba wa kijinga kwa kisingizio cha haraka au dhalula. Haiwezekani kila gari ya serikali iwe na dhalula na uhitaji wa mwendo kasi kiasi hicho. Matokeo yake ni hizi ajali ambazo zingeweza kuepukika.

Isingekuwa tatizo kama ajali ni zenu tu lakini ukweli ni hata waendeshaji wengine munawaingiza ktk ajali za kizembe kama hizi.

Hakuna sababu ya kutofuata sheria na alama za barabarani kwa kisingizio cha haraka au dhalula. Fuateni sheria na kuacha kuchekelea mwendo kasi. Polisi munashindwa kuwatia adabu watu hawa kwa uzembe wenu pia!
 
Ndo madhara ya kulazimisha watu wahamie dodoma bila maandalizi....wewe unategemea nini mtu anaishi Dar lkni kituo cha kazi ni dodoma kwahiyo hamna namna akichelewa atatumbuliwa bure, familia yake na mkopo nani atavimudu akikosa ajira kwa ujinga wa kufuata sheria za barabarani....hamna jinsi mkuu.
 
Ajali za magari madogo ya Serikali ina sura nyingi.
Tukumbuke kwanza, madereva wazoefu walienguliwa kwa kukosa vyeti vya Form IV.

Madereva vijana wengi wana uzoefu tu wa kuendesha mijini, hasa wale waliohamia Dodoma toka Dar.

Wengi wa madereva vijana hawaelewi kuwa huko porini barabarani, mfalme ni malori.

Malori yanaenda mwendo wa kawaida na hayana papara.
Vile vile malori yakishika mwendo na yana mzigo tani 20 hadi 40, hayana breki za karibu.
Kupunguza mwendo ni kwa kupangua gia.
Hivyo lori haliwezi kukukwepa, haliwezi kupiga breki kusimama ghafla.

Kwa mtaji huu madereva vijana wengi watapotea na abiria wao wakicheza na malori yenye mwendo na yaliyosheheni mzigo.
 
Huwaga wanakimbia Sana Hawa wafanyakazi wa serikalini walipigwa tochi manyoni mbele wakapata ajali na kufariki woote,RIP hawakusimama
IMG_20181022_080552.jpg
IMG_20181022_080546.jpg
IMG-20181021-WA0041.jpg
IMG-20181022-WA0004.jpg
IMG-20181021-WA0039.jpg
 
Inaelekea wewe ni polisi Trafiki.
Utetezi wako hautoshelezi.
Huna simu ili iwekwe road block mbele?
Mikono ya kazi yako ina damu!
Usiwe na hasira na Traffic police. Nini uelewa wa dereva? Kuwa na namba za ST isiwe ni umaarufu wa kukiuka sheria. Hiyo inayoonyeshwa ni somo kwa wote! Ukikimbia mkono wa sheria ukakutana na ajali na kifo, nini umwamba wako? Tunakutana nao barabarani na wanalazimisha uwapishe, eti tu kwa sababu kawasha taa kuonyesha ana haraka, mara unawakuta morogoro wnakula supu! wakiondoka upuuzi ule ule!

Binadamu anayependa umaarufu eti hakamatwi, tunapita tu, wanatuogopa, sisi muhimu, sisi waheshimiwa, n.k. haiwasaidii zaidi ya hatari kwao na kwa wengine. Maisha ya umaarufu ni mafupi sana! Barabara ya Dodoma - Dar imekuwa ni ya kuwasha taa tuuuu na overtake za kishenzi tu.
 
Sasa ukutane na hawa wana WA Dora. Au ving'ora juu utashangaa hii miendo ya kifo inawapeleka kuzimu.nilikutana na msafara WA mmoja WA marais wetu mpendwa Mimi na Volkswagen kangu T126AAD tena kwenye kona niliamini kwa mwendo ule lazima tufanye uchaguzi maana speed zao ilikuwa wanazunguka around makaburi yao.nadhani walifika salama.nashauri sheria ikate huku na huku.
 
Inaelekea wewe ni polisi Trafiki.
Utetezi wako hautoshelezi.
Huna simu ili iwekwe road block mbele?
Mikono ya kazi yako ina damu!
chakwanza mimi sio polisi,na chapili hizi picha zilitolewa mitandaoni na polisi baada ya hii ajali kusudi madereva wazembe wajifunze kitu,na cha tatu jukumu la kusimamia sheria hasa za barabarani si la polisi pekee bali nilakila mtu hata hao waliopata ajali walitakiwa wajijali wao kwanza kwa kufuata alama za barabarani na kuwa na mwendo ambao hauta hatarisha maisha yao,damu zao zipo juu ya vichwa vyao wenyewe hasa dereva ambaye alikuwa anakimbia bila kufuata alama za barabarani,usitegemee traffiki wakusaidie na namna ya kuendesha gari kama huwezi kufuata sheria za barabarani kwa manufaa yako na yawengine usiendeshe gari
 
Mara baada ya maafisa waandamizi kuhamia Dodoma kumekuwa na mtindo mpya wa uendeshaji magari barabarani. Kila gari ya serikali itokayo Dodoma kwenda nje ya mkoa huwasha taa na kukimbia kwa mwendo kasi zaidi ya alama za barabarani.

Huu ni umwamba wa kijinga kwa kisingizio cha haraka au dhalula. Haiwezekani kila gari ya serikali iwe na dhalula na uhitaji wa mwendo kasi kiasi hicho. Matokeo yake ni hizi ajali ambazo zingeweza kuepukika.

Isingekuwa tatizo kama ajali ni zenu tu lakini ukweli ni hata waendeshaji wengine munawaingiza ktk ajali za kizembe kama hizi.

Hakuna sababu ya kutofuata sheria na alama za barabarani kwa kisingizio cha haraka au dhalula. Fuateni sheria na kuacha kuchekelea mwendo kasi. Polisi munashindwa kuwatia adabu watu hawa kwa uzembe wenu pia!
Shida ni kuwa Madereva wengi wazoefu wameondolewa na vyeti feki ndio maana waliopo ambao ni vijana wanamaliza watu na kukimbia hovyo wakidhani ni ushujaa.
 
Hawa jamaa wanakimbia mwendo Wa hovyo sana na watakufa mpaka wakome Leo nilikuwa naenda iringa walikuwa wanatupita kama tumesimama
Spidi na vituko hivi vimeanza kipindi hiki baada ya kuhamia Dodoma, maana kuvunja sheria za barabara kwa kisingizio cha uafisa wako, kilikwama kipindi kile mke wa waziri mwenye maringo alipotiwa kibano. Nawaangalia watumishi hawa wa serikali kama kikundi cha watu wanaojiamini wao wako juu kwa ufahamu. Nahisi ni ile syndrome ya kuhama Dar wanaamini bado Dodoma ni mkoani, kumbe wote wamehamia Dodoma. Ujuaji mwingi bila sababu!

Ukiangalia watumishi hao wa wizara ya kilimo walikuwa wengi ktk gari moja na ni watu wazima, wote above 30. ilikuwaje asipatikane hata mmoja mwenye uelewa wa kutoa onyo kwa wenzake na kusikilizwa. Ni kama walikuwa wanamchochea dereva wao asisimame. Wana haraka! Wana kazi muhimu, nk. wako wapi sasa! Nahisi pia ktk hii tumbua tumbua, kuna watu wamepewa madaraka premature. Ukiona mtu anapewa ukurugenzi na anajivuna kwa hilo kama yule aliyewahi kumtolea bastola traffic police pale Morogoro, hiyo ni ishara ya ubora duni wa akili. Ukiwa Mkurugenzi, Mbunge, Waziri, public figure, boss fulani, inatakiwa uwe smart! Ujue risk za kila jambo, hata maneno unayotumia yawe standardized. Leo hii ni bureeeee!
 
Wapumzike kwa amani ila hata abiria wanachangia kutokea ajali tusilaumu madereva pekee. Wakati dereva anakimbiza gari walimkemea? Mimi upumbavu wa kuonyesha umwamba kukimbiza gari siuvumiliagi. Kwanza gari ikiwa speed napata panic attack. Tuanze kukataa mwendo kasi sisi kabla ya kupeleka lawama kwa madereva
 
Shida ni kuwa Madereva wengi wazoefu wameondolewa na vyeti feki ndio maana waliopo ambao ni vijana wanamaliza watu na kukimbia hovyo wakidhani ni ushujaa.
Naungana na mtoa hoja mmoja hapo juu.
Mwamba wa barabarani huko mbugani ni malori.
Yana mwendo mdogo, yana mizigo mizito, dereva wa V8 waheshimuni hao barabarani, ukimpiga mitkas, hasimami wala hakupishi.

Wafwa!
 
Wapumzike kwa amani ila hata abiria wanachangia kutokea ajali tusilaumu madereva pekee. Wakati dereva anakimbiza gari walimkemea? Mimi upumbavu wa kuonyesha umwamba kukimbiza gari siuvumiliagi. Kwanza gari ikiwa speed napata panic attack. Tuanze kukataa mwendo kasi sisi kabla ya kupeleka lawama kwa madereva
Najiuliza; Hapo kuna dereva wa darasa la saba aliyeajiliwa kabla ya katazo au kuna form 4 fulani aliyebahatika kuajiliwa. Pembeni kuna afisa msomi wa kiwango cha University mwenye uelewa kiwango cha kuiendeleza nchi. Eti hawa kuna kipindi wana mawazo ya aina moja kwamba tukimbize gari. Polisi wakitusimamisha wee nenda tu! Overtake! Halafu wakifika salama dereva huyu anapongezwa kwa kuaminika. Lazima dereva ajisikie sifa kwa kupongezwa na msomi wa wizarani. Sasa wasipofika kama hii iliyotokea, eti tunasema madereva wabaya. Hapana! Dereva anamkoga bosi, naye anakogeka na kutoa pongezi!
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom