Umuhimu wa Maalim Seif kuingia kwenye GNU ni mkubwa iwapo tu Jumuiya ya Kimataifa itashindwa kurejesha uchaguzi mpya Tanzania

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Haya ni maoni yangu binafsi.

Kwanza nianze kusema inaelekea baada ya robo karne ya vyama vingi, sasa kuna mwelekeo mpya duniani.

Haiwezekani mfumo wa vyama vingi hadi Leo Afrika ndio sababu ya mauaji na chuki na kwamba walioleta vyama vingi wameshindwa kuweka nguzo imara ili kila taifa likalazimika kufuata.

Lazima kuna ombwe na hilo ombwe ndio limeleta balaa.

Nirudi kwenye mada.

Maalim hakuna ubishi kwamba ni gwiji wa siasa na mweledi, anayekubalika na asiyeyumba.

Huyu mzee kamuanika kila mnafiki wakiwemo CCM, mabeberu na vitimbakwiri wa CCM wakiwemo masheikh, maaskofu na taasisi mbali mbali.

Licha ya kuporwa ushindi Mara kadhaa alikubali maridhiano zaidi ya Mara 3 hadi kufikia kuyaingiza kwenye katiba ya Zanzibar. Hapa inaonekana CCM ndio imeifanya iwe peak ya kisiasa ya vyama vingi Zanzibar.

Baada ya CCM kuona kuwa wamekataliwa Zanzibar walikubali hadaa hii ambayo iliwagharimu vile vile.

Mwaka 2015 ulikwa ndio wa majaribio ya ghilba na kilichotokea ndio kimewalazimisha Leo kuchukuwa mwelekeo wa kufuta vyama vingi.

Ama kwa kuzidiwa au kwa mission za tokea awali sasa CCM imelazimika kufuta upinzani uliouumba kwa robo karne.

Kwa upande wa Maalim Seif kama asemavyo mwenyewe yeye na Zanzibar na wazanzibari. Mara zote amekuwa akitanguliza maslahi ya umma ndio akalazimika kukubali hadi maridhiano limradi jamii iwe pamoja.

CCM wameshindwa Mara nyingi na wameonesha unafiki wao kuhusu demokrasia ya vyama vingi bara na Zanzibar.

Yaliyotokea 2015 ilikuwa ni zamu ya kuwaaibisha wazungu na demokrasia yao. Huyu nguli amewafundisha wazungu maana ya political science na ile digrii yake ya houner pale UDSM.
Wazungu kimya na mfumo wao wamekubali demokrasia kuchezewa na kunajisiwa.

Uchafuzi wa 2020 umezidi kuwavua nguo na sioni dalili za kupatiwa suluhu.

Kama hivyo ndivyo basi nashauri Maalim Seif aufikirie upya msimamo wa kushiriki offer ( ya kinafiki) ya Dr Hussein Mwinyi kwa sababu zifuatazo.

1. Kwa kuwa 2015 hakuna kilichotokea kuhusu kuwajibishwa waliovuruga basi atumie fursa finyu iliyopo aridhie na kukubaliana baadhi ya mambo ili viongozi wenziwe wapate japo huruma ya teuzi chache kwenye nafasi 10 za Rais, wengine kwenye sifa za kuajiriwa waajiriwe serikalini ambayo yeye ni sehemu yake kwa maslahi ya Wazanzibari wote ilimradi dunia imeshindwa kusimamia haki.

2. Kukilea chama chake na upinzani kwa ujumla ikiwa tu dunia itashindwa kuja na suluhisho LA kurejewa uchaguzi.

3. Awasilishe mapendekezo ya kufidiwa mauaji yaliyofanywa na CCM na kujumuishwa wapinzani kwenye nafasi muhimu serikalini ili kuponya madonda.

4. Kuwemo serikalini kutampa fursa ya kushauri na kuitetea Zanzibar pale inapotaka kuangamizwa ingawa tayari amekatwa mikono na miguu kwa kunyimwa wabunge na wawakilishi kwenye ngome zake.

5. Atapata fursa za kujua kinachopangwa na kupata kujipanga mbadala kwenye kipindi hiki cha dhoruba ya udikteta uchwara hadi hapo hali itakapotulia.

6. Nje ya uingiliaji wa kimataifa, CCM haina cha kupoteza Zanzibar. Walishatamukiwa na kususia na sasa wameshachukuwa kwa mizengwe majimbo yote ya ngome za Maalim Seif. Hii ni kuwa wataendelea na mipango yao na ni jamii ya Zanzibar ndio itaumia na kutengwa, kunyanyaswa na kunyimwa fursa za ajira na ushirikishwaji. Kwa kuangalia mbele in bora tu kushiriki walau kupunguza makali ya hujuma.

7. CCM wanamuhitaji Maalim Seif kwa kiasi lakini inaonekana wamejipanga hata akikataa ndio maana wamechukuwa majimbo kwa ghilba kubwa ili wafanikishe azma yao. Bora aingie na japo watu wachache akaimarishe network nje na ndani kuliko kukosa yote ilimradi tu dunia imeitupa mkono demokrasia ya vyama vingi.

8. Kwa kuwa inaonesha dola imechukuwa mwelekeo huo, pengine ndio msimamo wa deep state zote, pengine mda wa vyama vingi umefika mwisho Afrika bora waingie na kujenga hoja ndani kuliko kutengwa nje na kutosikilizwa na mataifa na ndani.

9. Kuna kila dalili vyama kufutwa na kunyanganywa jukwaa LA kusemea. Hii inavihusu vyama vyote makini na huu in mtego. Ngamueni mtego na mkubali kwa lengo LA kuhami hata kama ni kubahatisha. Tangulizeni wengine ndani wengine wabaki nje. Maalim kuwa ndani hasa Zanzibar na wazanzibari ni muhimu sasa kuliko kuwa nje.


Masharti ya mtazamo huu in iwapo hakuna msimamo wa kurudiwa uchaguzi kutoka jumuiya ya kimataifa

Kwa sasa ni hayo tu

Kishada
 
Basi na watoto wanaofeli mtihani wa kidato cha nne nao magomee matokeo ili kupata maridhiano. A looser should be forced to accept his loss
 
Uchanguzi umekwisha, ulikuwa huru na wa haki, mshindi amepatikana ki haki na ki halali na ameapishwa, there is no one can do anything now ni kusubiria uchaguzi mwingine ni 2025!.
P
 
Akishiriki kwenye serikali ukifika wakati wa kampeni atakuwa anasema kwanini achaguliwe yeye maana atakuwa anatetea mafanikio ya CCM maana chama kinachotawala pamoja na kumshirikisha. Sasa mtu amepata kura chini ya 20% kuna haja gani ya kumshirikisha hao asilimia 80% waliokuchagua hawatoshi kutoa ridhaa kwa Rais na chama chao kutawala
 
Akishiriki kwenye serikali ukifika wakati wa kampeni atakuwa anasema kwanini achaguliwe yeye maana atakuwa anatetea mafanikio ya CCM maana chama kinachotawala pamoja na kumshirikisha. Sasa mtu amepata kura chini ya 20% kuna haja gani ya kumshirikisha hao asilimia 80% waliokuchagua hawatoshi kutoa ridhaa kwa Rais na chama chao kutawala
Pitia tena makala nukta kwa nukta uelewe mantiki kwanza.

Maalim Seif ana Umma, CCM INA dola.

Madhara yanayokuja sasa ni makubwa.

Upinzani unahitajika ndani na nje japo kama huko ndani nako utakuwa umebanwa.
Ya 2015 yasirudiwe hats kama halo in mbaya vipi.

Kuna kila dalili vyama makini kufutwa
 
Mkuu P.
Kwenye uchaguzi huu tafadhali kwa heshima yako hapa JF ondowa neno huru na haki.

Baki na uchaguzi umekwisha tu.

Pata mda fuatilia ya Zanzibar utanielewa.


Uchanguzi umekwisha, ulikuwa huru na wa haki, mshindi amepatikana ki haki na ki halali na ameapishwa, there is no one can do anything now ni kusubiria uchaguzi mwingine ni 2025!.
 
Mazingira ya Zanzibar in tofauti na bara.

Bila uingiliaji was kimataifa Kyle in kugumu. Wazanzibari wametumia mbinu zote za kidemokrasia na kidiplomasia bado kabisa.

Mazingira ya Kule yamejengwa kwa mfumo wa mtawala kulinda koloni lake.
Juzi na Jana makarandika, vifaru na wanajeshi wameanza kurudishwa bara.

Meli zimeanza kushusha.nNi kama vile CCM inarudi vitani nchi jirani.

Askari wetu wameshafanya kila aina ya ukatili Unguja na Pemba na sasa wanarudi bara.

Kwa kuangalia mambo kama haya na mengine yaliyojificha, kuna kulazimishwa CCM kutawala hata ngome za upinzani.

Na mwelekeo in ile ule inayoitwa Zanzibar mpya.

Hapa in ukitaka uingie hutaki baki lkn yaliyokusudiwa yatendeke.

Nauona umuhimu wa Maalim kuwemo ndani huku nje akiwa na umma na azungumze hadharani asiyoyakubali yenye hadhi ya kitaifa.

Bila mataifa kuingilia kati huu mkwamo, haya hip fursa dhaifu itakosekana.
 
Jumuiya ya Kimataifa haitofanya chochote na Uchaguzi huu hautarudiwa. The earlier we come to terms with this, the better for our mental health!

Vyama 10 vya upinzani tayari vimejitokeza na ‘kuubariki’ uchaguzi huu. Dr. Mwinyi kaapishwa leo, Dr. Magufuli anaapishwa Jumatano, wananchi wamegoma kutokea kwenye maandamano na wapo busy kuhamasishana kupitia social media ambayo hata access yake ni mashaka

Kwa hali hii unategemea Beberu afanye nini?
 
Uchanguzi umekwisha, ulikuwa huru na wa haki, mshindi amepatikana
Hizi sarcastic languages ni wachache sana wanaweza kukuelewa now that munkari upo juu
Offcourse uchaguzi haukuwa huru wala wa haki. Wewe andika kitu direct tu.

Hapo kwenye “nobody can do anything now” upo sahihi
 
Hahaha sasa akiingia huko serikali ya mseto itasaidia nini?!

Kukubali kuingia kwenye mseto ni kukubaliana na wizi na kuwadanganya wananchi, ni ujinga na urafi wa vyeo vya kijinga.
 
Tunapanda mbegu mbaya sana nchini,na viongozi wetu wa leo hawalioni hili kwa ajili ya kesho.

Sioni sababu kwa nini Maalim Seif akubaliane na wazandiki CCM.

Yale yalikuwa ni mapinduzi ndani ya nchi huru siyo uchaguzi ule.
 
Mkuu P.
Kwenye uchaguzi huu tafadhali kwa heshima yako hapa JF ondowa neno huru na haki.

Baki na uchaguzi umekwisha tu.

Pata mda fuatilia ya Zanzibar utanielewa.
Labda wewe atakua amekuelewa. Watu wamejitahidi sana kumuelewesha lakini anaonekana maji ya bendera ya kijani aliyokunywa yamefika hadi kwenye ubongo na kuleta madhara. Pamoja na kura yake moja kwenye kura za maoni pale Kawe, amekua haelewi kabisa. Ngoja tuone baada ya ushauri wako labda tutaona mabadiliko kwenye comments zake.
 
Uchanguzi umekwisha, ulikuwa huru na wa haki, mshindi amepatikana ki haki na ki halali na ameapishwa, there is no one can do anything now ni kusubiria uchaguzi mwingine ni 2025!.
P
It's like someone stepping on your toes, and when you want to let him and the world know that he stepped on your toes, he is silencing you so you can't even talk!
 
Back
Top Bottom