SoC01 Umuhimu wa kuwa na Dira ya Maendeleo ya Taifa inayotekelezeka kwa wakati na kwa kuzingatia rasilimali zilizopo

Stories of Change - 2021 Competition

Abrianna

JF-Expert Member
Mar 30, 2021
4,697
15,379
Utangulizi
Dira kwa maana fupi ni muelekeo. Dira ya Maendeleo ya Tanzania (Tanzania Development Vision (TDV) 2025 ilianzishwa mwaka 1994 na kuzinduliwa rasmi mwaka 1999 ambapo utekelezaji wake ulianza mwaka 2000 lengo kuu likiwa kuongoza harakati za maendeleo ya uchumi na jamii zitakazoiwezesha Tanzania kufikia uchumi wa kati na kuondokana na umaskini uliokithiri ifikapo mwaka 2025. 'www.tanzania.go.tz' (tovuti kuu ya serikali)

Melengo makuu matano yalioainishwa katika Dira ya Maendeleo 2025 ni pamoja na kuboresha hali ya maisha ya kila Mtanzania, kuwepo kwa mazingira ya amani usalama na umoja,kujenga utawala bora,kujenga jamii iliyoelimika na kujenga uchumi imara unaokabiliana na ushindani. (Nukuu kutoka Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025).

Katika andiko hili, nitaangazia malengo makuu matano kama yalivyoainishwa katika Dira ya Maendeleo 2025. Andiko langu litaangazia pia utekelezaji wa malengo haya na uhalisia wa maisha ya Mtanzania.

Katika uhalisia, Maendeleo ya Nchi yetu kwa asilimia kubwa yamekua yakitegemea Ilani ya chama tawala pamoja vipaumbele vya Rais aliye madarakani. Mfano halisi ni ununuzi wa ndege na ujenzi wa madaraja ambao uliingiza nchi katika madeni makubwa na umaskini. Ni wazi kwamba Dira ya Maendeleo ni kijarida tu ambacho kimetengenezwa kutimiza wajibu lakini hakina nafasi kubwa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Serikali imeunda mipango mingi kwa ajili ya utekelezaji wa maendeleo kama vile mpango wa maendeleo wa miaka mitanpo (Five Year Development Plan), MKUKUTA, Mpango wa Big Results Now (Matokeo Makubwa Sasa), Mpango wa maboresho ya utumishi wa Umma,pamoja na Maleongo ya Maendeleo ya Millenia chini ya nchi za Umoja wa Mataifa.

Katika mipango tajwa, yote ina malengo yanayolandana kwa maana ya kutokomeza umaskini kwa kuboresha huduma za afya, elimu, nishati, kilimo, maji, biashara, mahusiano ya kimataifa, ajira, kuboresha utumishi wa umma, kuweka usawa wa kijinsia pamoja na mengine mengi.

Hebu tuangazie miaka kumi nyuma tulinganishe na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na hali halisi ya Watanzania mpaka leo hii.

Hali ya maisha ya Mtanzania imezidi kuwa duni pamoja na kwamba nchi yetu ipo katika uchumi wa kati wa chini, Mtanzania wa kawaida anashindwa kumudu gharama ndogo za mlo wa siku ilhali tunatangaziwa uchumi wetu umekua kwa asilimia 7% ( NBS 2019/2020).

Katika kujenga utawala bora, hali imezidi kuwa tete, ni wazi kwamba utawala wa sheria umekua jambo gumu katika nchi yetu hali inayopelekea kutokuwajibika kwa pamoja na ubadhirifu wa mali za umma (Rejea ripoti ya CAG 2020).

Katika Dira ya Mendeleo 2025, serikali imeonyesha nia ya kujenga jamii iliyoelimika na inayojifunza kila siku kulingana na mazingira na nyakati tulizopo, tukirudi kwenye uhalisia, kiwango cha ubora wa elimu zetu hakikidhi viwango vitakavyowawezesha wasomi wetu kuingia katika ushindani ndani na nje ya Tanzania, shule zetu nyingi hazina waalimu wa kutosha wala vifaa vya kufundishia, matamko ya kisiasa kwa upande mwingine yamekua yakiathiri mifumo ya elimu.

Kwa mfano mnamo mwezi Desemba 2020, Rais JPM aliagiza somo la historia ya Tanzania lianze kufundishwa katika shue za msingi mpaka sekondari, Wizara ya elimu iliandaa machapisho kwa ajili ya somo husika lakini baada ya Rais Samia kuingia madarakani somo hilo lilisitishwa rasmi.

Kwa upande mwingine serikali ilichangia kupotosha jamii badala ya kuelimisha. Nitoe mfano mdogo wa janga la Covid 19. Serikali ilisimama kidete kuuaminisha umma kwamba janga hili ni vita ya mabeberu dhidi yetu badala ya kutumia wataalamu wa afya kutoa elimu kuhusu namna bora ya kujikinga ili kuepuka maambukizi. Serikali ilienda mbali zaidi na kuhamasisha tiba mbadala na njia za asili ambazo zilitumika katika vituo vya afya pia.

Kauli ya serikali pamoja na viongozi wakuu wa nchi imeleta mkanganyiko pamoja na hisia tofauti juu ya janga hili na kusababisha watu kuishi pasipo kuchukua tahadhari hata baada ya serikali kubadili msimamo na kuamua kufuata njia za kitaalamu. Ukijaribu kuongea na watanzania kumi, tisa kati yao wanaogopa chanjo na kuamini kwamba mabeberu wanataka kutumaliza.
1626861526209.png
1626861576665.png

(picha kutoka mtandaoni)

Katika uboreshaji wa utumishi wa umma, vilio vimekua vingi, utekelezaji wa dhima hii umesahaulika kwa miaka zaidi ya mitano iliyopita, vilio vingi vya wafanyakazi kuhusu nyongeza za mishahara pamoja na kupanda madaraja, makato makubwa, na mishahara duni ambayo haikidhi maisha ya kila siku.

Mambo ya muhimu yaliyotajwa katika utekelezaji wa malengo ya milenia ni pamoja na kukuza mahusiano ya kimataifa, kutokomeza umaskini wa kipato na njaa. Kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, Tanzania imepuuza kwa kiasi kikubwa sana mahusiano ya kimataifa kutokana na misimamo ya kiongozi aliyekua madarakani. Vipato vya wananchi vimeshuka kutokana na tozo kubwa katika bidhaa na huduma, mfumuko wa bei umeathiri pembejeo za kilimo na bidhaa mbalimbali, uonevu kwa wafanyabiashara,ubambikaji wa kesi na kodi uliosababisha biashara nyingi kufungwa. Tunao mfano halisi wa sasa katika tozo ya miamala ambayo imeleta taharuki kubwa kwa wananchi masikini ambao hata kula yao ni ya tabu.

Mapendekezo
• Serikali ianzishe taasisi maalumu kwaajili ya kuandaa na kusimamia Dira ya Maendeleo ya Taifa. Chombo hicho kiwe na kazi ya kuandaa, kusimamia pamoja na kuishauri serikali iliyopo madarakani bila kujali chama.Taasisi hii ihakikishe sera sera na mipango ya taasisi mbalimbali za serikali pamoja na wizara zina uelekeo mmoja na zinashirikiana ka ukaribu. Kwa mfano suala la kuzalisha wahitimu wenye weledi ni lazima liendane na uboreshaji mfumo wa elimu, kwa hiyo ni lazima wizara ya kazi na wizara ya elimu zishirikiane kubaini mapungufu yanayoonekana kwa wahitimu wanaoajiriwa ili waweze kubaini njia bora ya kuboresha.

Taasisi hii ipewe mamlaka ya kusimamia serikali kama ilivyo bunge na mahakama na kwamba ilani ya chama cha kiongozi aliyeko madarakani ilenge kutafuta au kuonyesha njia sahihi za kuipeleka nchi kule ambako dira inaonyesha, hii itasaidia kutekeleza miradi iliyoachwa au iliyoanzishwa na kiongozi aliemaliza muda wake, mfano wakati Rais JPM naingia madarakani alisitisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kwa madai kwamba mikataba ilikua mibovu na iliyojaa unyonyaji, siku chache baada ya Rais Samia kuingia madarakani mapitio ya ujenzi wa bandari yameanza, hii ni kwa sababu hakuna mfumo wa kusimamia viapaumbele vya maendeleo ya Taifa badala yake kila kiongozi anajiamulia kile anachopenda.

• Ipatikane katiba imara ambayo itasaidia kudhibiti na kusimamia viongozi walioko madarakani na hata baada ya kustaafu kama ilivyo kwa nchi nyingine kama Marekani na Afrika ya Kusini. Hii itahakikisha viongozi wote wanafanya kazi kwa kuheshimu haki za binadamu na sheria na taratibu zilizopo bila kuathiri malengo ya Taifa kwa ujumla. Katiba imara pia itasaidia kuweka uwajibikaji na usawa kati ya watumishi/viongozi, kuondoa ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.

• Serikali ijikite zaidi katika kuvumbua vyanzo vipya vya mapato badala ya kujikita katika kuongeza kodi katika huduma mbalimbali za kijamii ili kupunguza mzigo mkubwa wa kodi kwa wananchi na badala yake wananchi wapate unafuu wa maisha. Mfano sekta ya utalii na madini zinaweza kuwa vyanzo vizuri vya mapato kama tukiweka usimamizi mzuri na mifumo ya kuaminika ili kuepusha mianya ya ubadhirifu. Pia serikali ijikite katika kuboresha mfumo wa elimu ili kuruhusu vijana wengi kujiajiri katika nyanja mbalimbali badala ya kutegemea ajira kutoka serikalini.

• Bajeti za maendeleo zilizoidhinishwa na bunge zisitumike kinyume na lengo ili tuweze kutekeleza mipango iliyopangwa katika mwaka wa fedha wa serikali. Huko nyuma tulishuhudia pesa zikipelekwa katika matumizi ambayo hayakuidhinishwa na bunge hali iliyochangia kukwamishwa kwa miradi mingi ya maendeleo iliyoidhinishwa na bunge. Bajeti inayoidhinishwa pia iende sambamba na Dira ya Maendeleo ya Taifa.

• Serikali iunde mfumo shirikishi utakaosaidia wananchi kushiriki katika kuonyesha vipaumbele vya maendeleo pamoja na utekelezaji. Hii itasaidia wananchi kuwa wasimamizi wa moja kwa moja wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

• Serikali iwatumie wataalamu wa masuala ya uchumi walioko nchini badala ya kutumia wanasiasa pekee katika kuandaa bajeti na matumizi ya serikali, pia serikali ijenge utamaduni wa kuwatumia wataalamu waliobobea katika fani mbalimbali nchini katika kuandaa na kusimamia sera mbali mbali kwaajili ya kukuza uchumi na kuleta maendeleo ya Taifa pamoja na kuheshimu mawazo na maelekezo ya wataalamu katika sekta mbalimbali hata pale yanapotokea majanga yanayohitaji ufumbuzi wa kitaalamu. Kwa kufanya hivi, tutapunguza au kudhibiti matamko ya kisiasa katika mambo nyeti yanayohitaji ufumbuzi wa kitaalamu kama vile Afya, Elimu na Uchumi.

Hitimisho
Natoa wito kwa viongozi/wenye mamlaka, na watunga sera wa nchi, maamuzi yoyote wanayofanya yanaathiri au kufaidisha jamii nzima, wao ni sehemu ya jamii na hivyo wataathirika au kufaidika na maamuzi hayo kwa namna moja au nyingine. Ni vyema kufanya uchambuzi yakinifu kabla ya kufanya maamuzi ili kuepuka athari zozote zitakazoisababishwa na maamuzi yao ikiwa ni pamoja na kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.

Asanteni Sana​
 
Utangulizi
Dira kwa maana fupi ni muelekeo. Dira ya Maendeleo ya Tanzania (Tanzania Development Vision (TDV) 2025 ilianzishwa mwaka 1994 na kuzinduliwa rasmi mwaka 1999 ambapo utekelezaji wake ulianza mwaka 2000 lengo kuu likiwa kuongoza harakati za maendeleo ya uchumi na jamii zitakazoiwezesha Tanzania kufikia uchumi wa kati na kuondokana na umaskini uliokithiri ifikapo mwaka 2025. 'www.tanzania.go.tz' (tovuti kuu ya serikali)

Melengo makuu matano yalioainishwa katika Dira ya Maendeleo 2025 ni pamoja na kuboresha hali ya maisha ya kila Mtanzania, kuwepo kwa mazingira ya amani usalama na umoja,kujenga utawala bora,kujenga jamii iliyoelimika na kujenga uchumi imara unaokabiliana na ushindani. (Nukuu kutoka Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025).

Katika andiko hili, nitaangazia malengo makuu matano kama yalivyoainishwa katika Dira ya Maendeleo 2025. Andiko langu litaangazia pia utekelezaji wa malengo haya na uhalisia wa maisha ya Mtanzania.

Katika uhalisia, Maendeleo ya Nchi yetu kwa asilimia kubwa yamekua yakitegemea Ilani ya chama tawala pamoja vipaumbele vya Rais aliye madarakani. Mfano halisi ni ununuzi wa ndege na ujenzi wa madaraja ambao uliingiza nchi katika madeni makubwa na umaskini. Ni wazi kwamba Dira ya Maendeleo ni kijarida tu ambacho kimetengenezwa kutimiza wajibu lakini hakina nafasi kubwa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Serikali imeunda mipango mingi kwa ajili ya utekelezaji wa maendeleo kama vile mpango wa maendeleo wa miaka mitanpo (Five Year Development Plan), MKUKUTA, Mpango wa Big Results Now (Matokeo Makubwa Sasa), Mpango wa maboresho ya utumishi wa Umma,pamoja na Maleongo ya Maendeleo ya Millenia chini ya nchi za Umoja wa Mataifa.

Katika mipango tajwa, yote ina malengo yanayolandana kwa maana ya kutokomeza umaskini kwa kuboresha huduma za afya, elimu, nishati, kilimo, maji, biashara, mahusiano ya kimataifa, ajira, kuboresha utumishi wa umma, kuweka usawa wa kijinsia pamoja na mengine mengi.

Hebu tuangazie miaka kumi nyuma tulinganishe na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na hali halisi ya Watanzania mpaka leo hii.

Hali ya maisha ya Mtanzania imezidi kuwa duni pamoja na kwamba nchi yetu ipo katika uchumi wa kati wa chini, Mtanzania wa kawaida anashindwa kumudu gharama ndogo za mlo wa siku ilhali tunatangaziwa uchumi wetu umekua kwa asilimia 7% ( NBS 2019/2020).

Katika kujenga utawala bora, hali imezidi kuwa tete, ni wazi kwamba utawala wa sheria umekua jambo gumu katika nchi yetu hali inayopelekea kutokuwajibika kwa pamoja na ubadhirifu wa mali za umma (Rejea ripoti ya CAG 2020).

Katika Dira ya Mendeleo 2025, serikali imeonyesha nia ya kujenga jamii iliyoelimika na inayojifunza kila siku kulingana na mazingira na nyakati tulizopo, tukirudi kwenye uhalisia, kiwango cha ubora wa elimu zetu hakikidhi viwango vitakavyowawezesha wasomi wetu kuingia katika ushindani ndani na nje ya Tanzania, shule zetu nyingi hazina waalimu wa kutosha wala vifaa vya kufundishia, matamko ya kisiasa kwa upande mwingine yamekua yakiathiri mifumo ya elimu.

Kwa mfano mnamo mwezi Desemba 2020, Rais JPM aliagiza somo la historia ya Tanzania lianze kufundishwa katika shue za msingi mpaka sekondari, Wizara ya elimu iliandaa machapisho kwa ajili ya somo husika lakini baada ya Rais Samia kuingia madarakani somo hilo lilisitishwa rasmi.

Kwa upande mwingine serikali ilichangia kupotosha jamii badala ya kuelimisha. Nitoe mfano mdogo wa janga la Covid 19. Serikali ilisimama kidete kuuaminisha umma kwamba janga hili ni vita ya mabeberu dhidi yetu badala ya kutumia wataalamu wa afya kutoa elimu kuhusu namna bora ya kujikinga ili kuepuka maambukizi. Serikali ilienda mbali zaidi na kuhamasisha tiba mbadala na njia za asili ambazo zilitumika katika vituo vya afya pia.

Kauli ya serikali pamoja na viongozi wakuu wa nchi imeleta mkanganyiko pamoja na hisia tofauti juu ya janga hili na kusababisha watu kuishi pasipo kuchukua tahadhari hata baada ya serikali kubadili msimamo na kuamua kufuata njia za kitaalamu. Ukijaribu kuongea na watanzania kumi, tisa kati yao wanaogopa chanjo na kuamini kwamba mabeberu wanataka kutumaliza.
View attachment 1862120View attachment 1862121
(picha kutoka mtandaoni)

Katika uboreshaji wa utumishi wa umma, vilio vimekua vingi, utekelezaji wa dhima hii umesahaulika kwa miaka zaidi ya mitano iliyopita, vilio vingi vya wafanyakazi kuhusu nyongeza za mishahara pamoja na kupanda madaraja, makato makubwa, na mishahara duni ambayo haikidhi maisha ya kila siku.

Mambo ya muhimu yaliyotajwa katika utekelezaji wa malengo ya milenia ni pamoja na kukuza mahusiano ya kimataifa, kutokomeza umaskini wa kipato na njaa. Kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, Tanzania imepuuza kwa kiasi kikubwa sana mahusiano ya kimataifa kutokana na misimamo ya kiongozi aliyekua madarakani. Vipato vya wananchi vimeshuka kutokana na tozo kubwa katika bidhaa na huduma, mfumuko wa bei umeathiri pembejeo za kilimo na bidhaa mbalimbali, uonevu kwa wafanyabiashara,ubambikaji wa kesi na kodi uliosababisha biashara nyingi kufungwa. Tunao mfano halisi wa sasa katika tozo ya miamala ambayo imeleta taharuki kubwa kwa wananchi masikini ambao hata kula yao ni ya tabu.

Mapendekezo
• Serikali ianzishe taasisi maalumu kwaajili ya kuandaa na kusimamia Dira ya Maendeleo ya Taifa. Chombo hicho kiwe na kazi ya kuandaa, kusimamia pamoja na kuishauri serikali iliyopo madarakani bila kujali chama.Taasisi hii ihakikishe sera sera na mipango ya taasisi mbalimbali za serikali pamoja na wizara zina uelekeo mmoja na zinashirikiana ka ukaribu. Kwa mfano suala la kuzalisha wahitimu wenye weledi ni lazima liendane na uboreshaji mfumo wa elimu, kwa hiyo ni lazima wizara ya kazi na wizara ya elimu zishirikiane kubaini mapungufu yanayoonekana kwa wahitimu wanaoajiriwa ili waweze kubaini njia bora ya kuboresha.

Taasisi hii ipewe mamlaka ya kusimamia serikali kama ilivyo bunge na mahakama na kwamba ilani ya chama cha kiongozi aliyeko madarakani ilenge kutafuta au kuonyesha njia sahihi za kuipeleka nchi kule ambako dira inaonyesha, hii itasaidia kutekeleza miradi iliyoachwa au iliyoanzishwa na kiongozi aliemaliza muda wake, mfano wakati Rais JPM naingia madarakani alisitisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kwa madai kwamba mikataba ilikua mibovu na iliyojaa unyonyaji, siku chache baada ya Rais Samia kuingia madarakani mapitio ya ujenzi wa bandari yameanza, hii ni kwa sababu hakuna mfumo wa kusimamia viapaumbele vya maendeleo ya Taifa badala yake kila kiongozi anajiamulia kile anachopenda.

• Ipatikane katiba imara ambayo itasaidia kudhibiti na kusimamia viongozi walioko madarakani na hata baada ya kustaafu kama ilivyo kwa nchi nyingine kama Marekani na Afrika ya Kusini. Hii itahakikisha viongozi wote wanafanya kazi kwa kuheshimu haki za binadamu na sheria na taratibu zilizopo bila kuathiri malengo ya Taifa kwa ujumla. Katiba imara pia itasaidia kuweka uwajibikaji na usawa kati ya watumishi/viongozi, kuondoa ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.

• Serikali ijikite zaidi katika kuvumbua vyanzo vipya vya mapato badala ya kujikita katika kuongeza kodi katika huduma mbalimbali za kijamii ili kupunguza mzigo mkubwa wa kodi kwa wananchi na badala yake wananchi wapate unafuu wa maisha. Mfano sekta ya utalii na madini zinaweza kuwa vyanzo vizuri vya mapato kama tukiweka usimamizi mzuri na mifumo ya kuaminika ili kuepusha mianya ya ubadhirifu. Pia serikali ijikite katika kuboresha mfumo wa elimu ili kuruhusu vijana wengi kujiajiri katika nyanja mbalimbali badala ya kutegemea ajira kutoka serikalini.

• Bajeti za maendeleo zilizoidhinishwa na bunge zisitumike kinyume na lengo ili tuweze kutekeleza mipango iliyopangwa katika mwaka wa fedha wa serikali. Huko nyuma tulishuhudia pesa zikipelekwa katika matumizi ambayo hayakuidhinishwa na bunge hali iliyochangia kukwamishwa kwa miradi mingi ya maendeleo iliyoidhinishwa na bunge. Bajeti inayoidhinishwa pia iende sambamba na Dira ya Maendeleo ya Taifa.

• Serikali iunde mfumo shirikishi utakaosaidia wananchi kushiriki katika kuonyesha vipaumbele vya maendeleo pamoja na utekelezaji. Hii itasaidia wananchi kuwa wasimamizi wa moja kwa moja wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

• Serikali iwatumie wataalamu wa masuala ya uchumi walioko nchini badala ya kutumia wanasiasa pekee katika kuandaa bajeti na matumizi ya serikali, pia serikali ijenge utamaduni wa kuwatumia wataalamu waliobobea katika fani mbalimbali nchini katika kuandaa na kusimamia sera mbali mbali kwaajili ya kukuza uchumi na kuleta maendeleo ya Taifa pamoja na kuheshimu mawazo na maelekezo ya wataalamu katika sekta mbalimbali hata pale yanapotokea majanga yanayohitaji ufumbuzi wa kitaalamu. Kwa kufanya hivi, tutapunguza au kudhibiti matamko ya kisiasa katika mambo nyeti yanayohitaji ufumbuzi wa kitaalamu kama vile Afya, Elimu na Uchumi.

Hitimisho
Natoa wito kwa viongozi/wenye mamlaka, na watunga sera wa nchi, maamuzi yoyote wanayofanya yanaathiri au kufaidisha jamii nzima, wao ni sehemu ya jamii na hivyo wataathirika au kufaidika na maamuzi hayo kwa namna moja au nyingine. Ni vyema kufanya uchambuzi yakinifu kabla ya kufanya maamuzi ili kuepuka athari zozote zitakazoisababishwa na maamuzi yao ikiwa ni pamoja na kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.

Asanteni Sana​
Mkuu bandiko zuri japo ukiliweka kwenye uhalisia halina jipya Sana, hujatoka nje ya utendeji ila umejielekeza kwenye siasa, mkuu unafikri dira ya nchi inatumgwa, unawekwa au ni ilani?

Je kwa mfano was bandali ya bagamoyo unasema ilisitishwa halafu ikafufuliwa na hyu was Sasa, je unahisi ilikuwa na tija?


Mkuu umasikini wa mtanzania unakwenda sawa na lasilimali zilizopo?? Yaan tz Ni masikini kwa kipato, elimu, uchumi au nchi?? Je dira hapo inayachakata vipi hayo??

Mkuu hebu tuambie ukiacha siasa njia za kujikinga na c-19 alizo apply JPM zinamanafaa au hazikuwa na manufaaa, ukitumia mifano walao 2 eleza kwa uchache nchi ipi ilifanikiwa Sana kwa kuaply fact za c-19??

Mkono wangu haujakupa kura maana nataka utoke kwenye siasa uje kwenye uhalisia mkuu, unakitu kizur naomba majibu plz
 
Kama bunge letu lingekuwa linatimiza majukumu yake kiweledi na wala si ushabiki wa kisiasa/kivyama, hakika tusingehitaji hiyo taasisi ya kusimamia dira ya Taifa.

Lakini kutokana na udhaifu wa muhimili wa bunge, nakubaliana kabisa tunahitaji taasisi independent (huru) kusimamia dira, vipaumbele, na tunu za kitaifa. Kiongozi wake awe na protection kama ilivyo kwa CAG na judge mkuu ili afanye kazi zake kwa Uhuru pasipo kuingiliwa na majukumu yake na serikali.

Taasisi hii iwe na wabobezi katika nyanja za sheria, uchumi & ujasusi
 
Safi kabisa. Kwenye mapendekezo umeshauri paundwe kamati, nafikiri yote uliyashauri kwa kamati itayoundwa yanastahili kufanywa na Bunge. Nafikiri tunatakiwa kuwa na Bunge imara na huru ambalo litatakiwa kuisimamaia serikali sio kuisifia na kuitetea.
Ni kweli kabisa, sio bunge imara tu bali bunge huru, bunge letu la sasa sio huru, hawawakilishi mawazo ya wananchi bali wanatetea serikali, hawawezi kuwajibisha serikali bali kuisifia na kuitetea, ili tuwe na bunge huru tunahitaji tume huru ya uchaguzi
 
Umechambua vizuri sana kwa kutumia data halisi, hivyo basi Suluhisho la yote ni kupata katiba mpya ambayo itatenganisha chama flani na serikali,kwa sababu mambo yanayo hitaji kutekelezwa kitaifa hua yanatekelezwa kichama na kwa masilahi mapana ya chama kuliko Taifa.

Chini ya katiba ya iliyopo na sheria zilizopo ambazo zingine tumeachiwa na mkoloni,zilitungwa enzi za chama kimoja pia zimetungwa na kupitishwa kwa hati ya dharula na bunge ambalo limejaa wabunge wa chama kimoja kwa kauli moja ili kulinda maslahi ya chama ni ngumu kufika huko tunapo pataka.
Well said mkuu, nakubaliana na wewe 100%
 
Dira ya maendeleo ya Taifa itafanya kazi vizuri endapo Luna mipango na mikakati mizuri ya kuitekeleza.
Mpango mkakati lazima uanishe rasilimali zilozopo kuanzia watu,na vifaa .
Je kama Taifa tuna dira ya Taifa Taifa ambayo wanasiasa wetu wanatambua vipaumbile vya wamanchi.
Leo unaleta ndege kuchochea uchumi halafu shirika halina wataalam wa kuliendesha,hakuna biashara katika kipindi hiki cha janga la corona mwishowe ndege zinakuja kutengeneza hasara

Dira ya Taifa lazima iguse wananchi moja kwa moja.
Mfano kuangiza masuala ya kilimo ambapo wananchi wengi (70%) wanategemea kipato chao huko.
Kilimo ni pamoja na (uvuvi,ufugaji na misitu).

Miundombinu safi
Usafiri (reli na barabara)
Afya (dawa na wataalamu)
Elimu

Suala kubwa ambalo linakwamisha utekelezaji wa dira ya Taifa ni commitment kutoka kwa wanasiasa
Rushwa na ubadhirifu wa mali za umma .
Kukosa wataalamu (wabobezi)
Kubwa ambalo linakuja kwa kasi na linakwamisha dira ya Taifa Mabadiliko ya tabia ya nchi na ongezeko la watu.
Nchi yetu inahitaji watu lakini kasi ya ongezeko hilo hatujajipanga kwendana na standard ya huduma zinalotolewa.

Mfano darasa moja =45
Barabara moja magari =2000 per year
Hosptal moja wagonjwa =50 per day
Daktari mmoj wagonjw =6 per day
Polisi mmoja alinde watu =1500
Lakini leo ni overwhelming (oversize) kwa kila kitu.

Tunalo la kujifunza kwa wenzetu kutoa elimu bora ya kutosha kwa vijana wetu tena ya ufundi -techinical skills ili badae akiamua achukue soft skills tu .
La sivyo tutapiga marktime sana.
Umeeleza mambo ya msingi sana, tunahitaji rasilimali zinazoweza kusaidia utekelezaji wa dira, pia tunapaswa kuangalia vipaumbele vya wananchi, suala la ndege hata mimi linanishangaza na bado zimeletwa zingine achilia mbali hasara kubwa iliyopatikana

Viwango vya huduma zinazotolewa kwenye taasisi za serikali ni duni na hazikidhi, mahospitali yameelemewa, madawa hakuna, walimu hawatoshi na bado maslahi ya atumishi ni duni

Changamoto ni nyingi na serikali haiangalii kuziboresha
 
Tatizo la kwanza nchi hii ni ujinga uliokithiri miongoni mwa wananchi walio wengi! Tatizo la pili ni mifumo iliyokufa ndani ya ccm. Tatizo la tatu ni ukosefu wa vyama vya siasa vinavyojitambua!
Tunachokiona ni siasa tu kwenye malengo, maamuzi, mipango na hizo dira! Na ndo maana ni za muda mfupi mfupi zikilenga kutukuza watawala!
Naungana na wewe kwenye uanzishwaji wa mamlaka au tume itakayokasimiwa majukumu ya kuandaa malengo, mikakati na dira za taifa za muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu.
Kama ilivyo tume ya uchaguzi na tume nyinginezo basi iwepo tume ya dira na malengo ya kitaaluma kabisa na isiingiliwe na mifumo yetu ya kisiasa.
Ukosefu wa malengo, mikakati na dira za kitaifa za kueleweka kumesababisha kila awamu iingiapo madarakani inataka ifanye inavyotaka!
Hii si sawa!!
Asante sana mkuu kwa maoni yako, nakubaliana na wewe kabisa
 
Utangulizi
Dira kwa maana fupi ni muelekeo. Dira ya Maendeleo ya Tanzania (Tanzania Development Vision (TDV) 2025 ilianzishwa mwaka 1994 na kuzinduliwa rasmi mwaka 1999 ambapo utekelezaji wake ulianza mwaka 2000 lengo kuu likiwa kuongoza harakati za maendeleo ya uchumi na jamii zitakazoiwezesha Tanzania kufikia uchumi wa kati na kuondokana na umaskini uliokithiri ifikapo mwaka 2025. 'www.tanzania.go.tz' (tovuti kuu ya serikali)

Melengo makuu matano yalioainishwa katika Dira ya Maendeleo 2025 ni pamoja na kuboresha hali ya maisha ya kila Mtanzania, kuwepo kwa mazingira ya amani usalama na umoja,kujenga utawala bora,kujenga jamii iliyoelimika na kujenga uchumi imara unaokabiliana na ushindani. (Nukuu kutoka Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025).

Katika andiko hili, nitaangazia malengo makuu matano kama yalivyoainishwa katika Dira ya Maendeleo 2025. Andiko langu litaangazia pia utekelezaji wa malengo haya na uhalisia wa maisha ya Mtanzania.

Katika uhalisia, Maendeleo ya Nchi yetu kwa asilimia kubwa yamekua yakitegemea Ilani ya chama tawala pamoja vipaumbele vya Rais aliye madarakani. Mfano halisi ni ununuzi wa ndege na ujenzi wa madaraja ambao uliingiza nchi katika madeni makubwa na umaskini. Ni wazi kwamba Dira ya Maendeleo ni kijarida tu ambacho kimetengenezwa kutimiza wajibu lakini hakina nafasi kubwa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Serikali imeunda mipango mingi kwa ajili ya utekelezaji wa maendeleo kama vile mpango wa maendeleo wa miaka mitanpo (Five Year Development Plan), MKUKUTA, Mpango wa Big Results Now (Matokeo Makubwa Sasa), Mpango wa maboresho ya utumishi wa Umma,pamoja na Maleongo ya Maendeleo ya Millenia chini ya nchi za Umoja wa Mataifa.

Katika mipango tajwa, yote ina malengo yanayolandana kwa maana ya kutokomeza umaskini kwa kuboresha huduma za afya, elimu, nishati, kilimo, maji, biashara, mahusiano ya kimataifa, ajira, kuboresha utumishi wa umma, kuweka usawa wa kijinsia pamoja na mengine mengi.

Hebu tuangazie miaka kumi nyuma tulinganishe na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na hali halisi ya Watanzania mpaka leo hii.

Hali ya maisha ya Mtanzania imezidi kuwa duni pamoja na kwamba nchi yetu ipo katika uchumi wa kati wa chini, Mtanzania wa kawaida anashindwa kumudu gharama ndogo za mlo wa siku ilhali tunatangaziwa uchumi wetu umekua kwa asilimia 7% ( NBS 2019/2020).

Katika kujenga utawala bora, hali imezidi kuwa tete, ni wazi kwamba utawala wa sheria umekua jambo gumu katika nchi yetu hali inayopelekea kutokuwajibika kwa pamoja na ubadhirifu wa mali za umma (Rejea ripoti ya CAG 2020).

Katika Dira ya Mendeleo 2025, serikali imeonyesha nia ya kujenga jamii iliyoelimika na inayojifunza kila siku kulingana na mazingira na nyakati tulizopo, tukirudi kwenye uhalisia, kiwango cha ubora wa elimu zetu hakikidhi viwango vitakavyowawezesha wasomi wetu kuingia katika ushindani ndani na nje ya Tanzania, shule zetu nyingi hazina waalimu wa kutosha wala vifaa vya kufundishia, matamko ya kisiasa kwa upande mwingine yamekua yakiathiri mifumo ya elimu.

Kwa mfano mnamo mwezi Desemba 2020, Rais JPM aliagiza somo la historia ya Tanzania lianze kufundishwa katika shue za msingi mpaka sekondari, Wizara ya elimu iliandaa machapisho kwa ajili ya somo husika lakini baada ya Rais Samia kuingia madarakani somo hilo lilisitishwa rasmi.

Kwa upande mwingine serikali ilichangia kupotosha jamii badala ya kuelimisha. Nitoe mfano mdogo wa janga la Covid 19. Serikali ilisimama kidete kuuaminisha umma kwamba janga hili ni vita ya mabeberu dhidi yetu badala ya kutumia wataalamu wa afya kutoa elimu kuhusu namna bora ya kujikinga ili kuepuka maambukizi. Serikali ilienda mbali zaidi na kuhamasisha tiba mbadala na njia za asili ambazo zilitumika katika vituo vya afya pia.

Kauli ya serikali pamoja na viongozi wakuu wa nchi imeleta mkanganyiko pamoja na hisia tofauti juu ya janga hili na kusababisha watu kuishi pasipo kuchukua tahadhari hata baada ya serikali kubadili msimamo na kuamua kufuata njia za kitaalamu. Ukijaribu kuongea na watanzania kumi, tisa kati yao wanaogopa chanjo na kuamini kwamba mabeberu wanataka kutumaliza.
View attachment 1862120View attachment 1862121
(picha kutoka mtandaoni)

Katika uboreshaji wa utumishi wa umma, vilio vimekua vingi, utekelezaji wa dhima hii umesahaulika kwa miaka zaidi ya mitano iliyopita, vilio vingi vya wafanyakazi kuhusu nyongeza za mishahara pamoja na kupanda madaraja, makato makubwa, na mishahara duni ambayo haikidhi maisha ya kila siku.

Mambo ya muhimu yaliyotajwa katika utekelezaji wa malengo ya milenia ni pamoja na kukuza mahusiano ya kimataifa, kutokomeza umaskini wa kipato na njaa. Kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, Tanzania imepuuza kwa kiasi kikubwa sana mahusiano ya kimataifa kutokana na misimamo ya kiongozi aliyekua madarakani. Vipato vya wananchi vimeshuka kutokana na tozo kubwa katika bidhaa na huduma, mfumuko wa bei umeathiri pembejeo za kilimo na bidhaa mbalimbali, uonevu kwa wafanyabiashara,ubambikaji wa kesi na kodi uliosababisha biashara nyingi kufungwa. Tunao mfano halisi wa sasa katika tozo ya miamala ambayo imeleta taharuki kubwa kwa wananchi masikini ambao hata kula yao ni ya tabu.

Mapendekezo
• Serikali ianzishe taasisi maalumu kwaajili ya kuandaa na kusimamia Dira ya Maendeleo ya Taifa. Chombo hicho kiwe na kazi ya kuandaa, kusimamia pamoja na kuishauri serikali iliyopo madarakani bila kujali chama.Taasisi hii ihakikishe sera sera na mipango ya taasisi mbalimbali za serikali pamoja na wizara zina uelekeo mmoja na zinashirikiana ka ukaribu. Kwa mfano suala la kuzalisha wahitimu wenye weledi ni lazima liendane na uboreshaji mfumo wa elimu, kwa hiyo ni lazima wizara ya kazi na wizara ya elimu zishirikiane kubaini mapungufu yanayoonekana kwa wahitimu wanaoajiriwa ili waweze kubaini njia bora ya kuboresha.

Taasisi hii ipewe mamlaka ya kusimamia serikali kama ilivyo bunge na mahakama na kwamba ilani ya chama cha kiongozi aliyeko madarakani ilenge kutafuta au kuonyesha njia sahihi za kuipeleka nchi kule ambako dira inaonyesha, hii itasaidia kutekeleza miradi iliyoachwa au iliyoanzishwa na kiongozi aliemaliza muda wake, mfano wakati Rais JPM naingia madarakani alisitisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kwa madai kwamba mikataba ilikua mibovu na iliyojaa unyonyaji, siku chache baada ya Rais Samia kuingia madarakani mapitio ya ujenzi wa bandari yameanza, hii ni kwa sababu hakuna mfumo wa kusimamia viapaumbele vya maendeleo ya Taifa badala yake kila kiongozi anajiamulia kile anachopenda.

• Ipatikane katiba imara ambayo itasaidia kudhibiti na kusimamia viongozi walioko madarakani na hata baada ya kustaafu kama ilivyo kwa nchi nyingine kama Marekani na Afrika ya Kusini. Hii itahakikisha viongozi wote wanafanya kazi kwa kuheshimu haki za binadamu na sheria na taratibu zilizopo bila kuathiri malengo ya Taifa kwa ujumla. Katiba imara pia itasaidia kuweka uwajibikaji na usawa kati ya watumishi/viongozi, kuondoa ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.

• Serikali ijikite zaidi katika kuvumbua vyanzo vipya vya mapato badala ya kujikita katika kuongeza kodi katika huduma mbalimbali za kijamii ili kupunguza mzigo mkubwa wa kodi kwa wananchi na badala yake wananchi wapate unafuu wa maisha. Mfano sekta ya utalii na madini zinaweza kuwa vyanzo vizuri vya mapato kama tukiweka usimamizi mzuri na mifumo ya kuaminika ili kuepusha mianya ya ubadhirifu. Pia serikali ijikite katika kuboresha mfumo wa elimu ili kuruhusu vijana wengi kujiajiri katika nyanja mbalimbali badala ya kutegemea ajira kutoka serikalini.

• Bajeti za maendeleo zilizoidhinishwa na bunge zisitumike kinyume na lengo ili tuweze kutekeleza mipango iliyopangwa katika mwaka wa fedha wa serikali. Huko nyuma tulishuhudia pesa zikipelekwa katika matumizi ambayo hayakuidhinishwa na bunge hali iliyochangia kukwamishwa kwa miradi mingi ya maendeleo iliyoidhinishwa na bunge. Bajeti inayoidhinishwa pia iende sambamba na Dira ya Maendeleo ya Taifa.

• Serikali iunde mfumo shirikishi utakaosaidia wananchi kushiriki katika kuonyesha vipaumbele vya maendeleo pamoja na utekelezaji. Hii itasaidia wananchi kuwa wasimamizi wa moja kwa moja wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

• Serikali iwatumie wataalamu wa masuala ya uchumi walioko nchini badala ya kutumia wanasiasa pekee katika kuandaa bajeti na matumizi ya serikali, pia serikali ijenge utamaduni wa kuwatumia wataalamu waliobobea katika fani mbalimbali nchini katika kuandaa na kusimamia sera mbali mbali kwaajili ya kukuza uchumi na kuleta maendeleo ya Taifa pamoja na kuheshimu mawazo na maelekezo ya wataalamu katika sekta mbalimbali hata pale yanapotokea majanga yanayohitaji ufumbuzi wa kitaalamu. Kwa kufanya hivi, tutapunguza au kudhibiti matamko ya kisiasa katika mambo nyeti yanayohitaji ufumbuzi wa kitaalamu kama vile Afya, Elimu na Uchumi.

Hitimisho
Natoa wito kwa viongozi/wenye mamlaka, na watunga sera wa nchi, maamuzi yoyote wanayofanya yanaathiri au kufaidisha jamii nzima, wao ni sehemu ya jamii na hivyo wataathirika au kufaidika na maamuzi hayo kwa namna moja au nyingine. Ni vyema kufanya uchambuzi yakinifu kabla ya kufanya maamuzi ili kuepuka athari zozote zitakazoisababishwa na maamuzi yao ikiwa ni pamoja na kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.

Asanteni Sana​
Absolutely Good
 
Asante sana mkuu kwa andiko lako. Ni vigumu sana kufikia maendeleo kama ilivyoonyeshwa ktk Dira ya maendeleo kwa nchi yetu maana Katiba na sheria zetu hazimlazimishi wala kumuwajibisha Rais na serikali yake kufuata na kutekekeza vipaumbele kama inavyoonyeshwa kwenye Dira ya maendeleo.

Vv
Tunahitaji katiba ya wananchi inayoweza kuwasimamia na kuwawajibisha viongozi
 
Mkuu bandiko zuri japo ukiliweka kwenye uhalisia halina jipya Sana, hujatoka nje ya utendeji ila umejielekeza kwenye siasa, mkuu unafikri dira ya nchi inatumgwa, unawekwa au ni ilani?

Je kwa mfano was bandali ya bagamoyo unasema ilisitishwa halafu ikafufuliwa na hyu was Sasa, je unahisi ilikuwa na tija?


Mkuu umasikini wa mtanzania unakwenda sawa na lasilimali zilizopo?? Yaan tz Ni masikini kwa kipato, elimu, uchumi au nchi?? Je dira hapo inayachakata vipi hayo??

Mkuu hebu tuambie ukiacha siasa njia za kujikinga na c-19 alizo apply JPM zinamanafaa au hazikuwa na manufaaa, ukitumia mifano walao 2 eleza kwa uchache nchi ipi ilifanikiwa Sana kwa kuaply fact za c-19??

Mkono wangu haujakupa kura maana nataka utoke kwenye siasa uje kwenye uhalisia mkuu, unakitu kizur naomba majibu plz
Boniface, asante sana kwa maoni yako na mwaswali yako

Nianze na suala la bandari, kusema kwamba haina tija, inamaanisha walioazisha huo mradi ni wapuuzi kwa maana ya kwamba hawakuangalia manufaa, tukisema ina tija basi waliositisha huo mradi nao walikua ni wapuuzi kwa sababu hawakuangalia hasara za kusitisha mradi, na mwisho hawa waliofudua mradi kwa mara nyingine tena maana yake ni kwamba serikali haina misimamo kwenye maamuzi yake, ndio maana nasema tunahitaji dira inayotekelezeka bila kujali awamu za uongozi, kama dira yetu alianisha mradi wa bagamoyo, basi mamlaka za usimamizi wa dira zingehakikisha mradi unatekelezwa hata anapoingia Rais mwingine madarakani bado angeendeleza pale palipobaki.

Tukija kwenye suala la rasilimali, Kama umesoma andiko langu vizuri nimesema kwamba serikali ibuni vyanzo vya uhakika vya mapato vitakavyotuwezesha kutekeleza mipango yetu ya maendeleo given that tuna rasilimali nyingi lakini hazina usimamizi matokeo yake wachache ndio wanaofaidi huku wengi tukiumia, nimetoa mfano wa sekta ya madini, kukiwa na usimamizi thabiti unaozuia upotevu wa mali basi tunaweza kuendesha nchi kwa rasilimali za madini na gesi bila kuwaumiza wananchi na tozo

tukija kwenye suala la C19, bado nimesema wananchi hawaelewi msimamo wa serikali ni upi, wataalamu wetu wameshindwa kuishauri serikali au taaluma zao ziliingiliwa na siasa, tuliaminishwa kwamba tupo kwenye vita ya kiuchumi na sasa tunaaminishwa kwamba chanjo ni salama.
 
Mkuu denooJ, asante sana kwa maoni yako, katika pendekezo langu nimeeleza kwamba ni lazima tupate katiba imara itakayosaidia kuwawajibisha viongozi hata baada ya kuachia madaraka, kwa maana hiyo tunategemea vile vipengele vinanvyowalinda watawala viondolewe ili watawala wawajibike kwa kila wanachokifanya wanapopewa nafasi, katiba imara pia itasaidia kusimamia dira yetu ya maendeleo pamoja na utekelezaji wake katika ngazi zote.

Kama nilivyosema hapo juu kwamba tunahitaji chombo kinachopewa mamlaka kikatiba ili kusimamia dira ya maendeleo pasipo kuathiriwa au kuingiliwa na siasa, kwa maana hiyo kila Rais anapoingia madarakani bila kujali itikadi yake ya chama au matakwa yake atalazimika kutekeleza dira ya maendeleo ya Taifa, na hii itawezekana tu kama mamlaka ya Rais yatapunguzwa.
Nisikusifie sana, but naona umejiongeza kwa kuandika topic ambayo iko hot currently, wengi walioandika za kwao ni nzuri pia, but vitu kama tatizo la ajira na mengineyo yamekuwa yakiimbwa muda mrefu ni kama yamewachosha wasomaji na wengi wameshakata tamaa, but hii issue uliyoweka inaendana na our current state of political affairs.

Magufuli ameondoka akaja Samia, jinsi anavyoendesha mambo serikalini kila mtu sasa hivi anajiuliza huyu mama yuko sawa or not, kuna kama "some sort of discussion" inayoendelea mtaani about hiki ulichoandika, ndio maana unaona unapata wachangiaji wengi kwenye uzi wako, simply because umewapa uwanja wakutoa maoni yao kwenye issue inayo trend.

The rest wish you all the best.
 
Boniface, asante sana kwa maoni yako na mwaswali yako

Nianze na suala la bandari, kusema kwamba haina tija, inamaanisha walioazisha huo mradi ni wapuuzi kwa maana ya kwamba hawakuangalia manufaa, tukisema ina tija basi waliositisha huo mradi nao walikua ni wapuuzi kwa sababu hawakuangalia hasara za kusitisha mradi, na mwisho hawa waliofudua mradi kwa mara nyingine tena maana yake ni kwamba serikali haina misimamo kwenye maamuzi yake, ndio maana nasema tunahitaji dira inayotekelezeka bila kujali awamu za uongozi, kama dira yetu alianisha mradi wa bagamoyo, basi mamlaka za usimamizi wa dira zingehakikisha mradi unatekelezwa hata anapoingia Rais mwingine madarakani bado angeendeleza pale palipobaki.

Tukija kwenye suala la rasilimali, Kama umesoma andiko langu vizuri nimesema kwamba serikali ibuni vyanzo vya uhakika vya mapato vitakavyotuwezesha kutekeleza mipango yetu ya maendeleo given that tuna rasilimali nyingi lakini hazina usimamizi matokeo yake wachache ndio wanaofaidi huku wengi tukiumia, nimetoa mfano wa sekta ya madini, kukiwa na usimamizi thabiti unaozuia upotevu wa mali basi tunaweza kuendesha nchi kwa rasilimali za madini na gesi bila kuwaumiza wananchi na tozo

tukija kwenye suala la C19, bado nimesema wananchi hawaelewi msimamo wa serikali ni upi, wataalamu wetu wameshindwa kuishauri serikali au taaluma zao ziliingiliwa na siasa, tuliaminishwa kwamba tupo kwenye vita ya kiuchumi na sasa tunaaminishwa kwamba chanjo ni salama.
Huu mfano wa bandari na mingine ya muonekano huo kama madini, gas, etc ningependa pawepo na chombo maalum kitakachojitegemea kitakachojihusisha na ufuatiliaji wa hiyo mikataba waone kama itakuwa na manufaa kwa nchi ndio isainiwe.

- Hiki kiundwe kisheria (Katiba Mpya) na kiwe independent ikibidi kisiundwe na wanasiasa kabisa. Wawepo watu wa profession kama law, wahasibu, etc.

Ukisema dira pekee hapa haitoshi coz hiyo dira itatekelezwa na wanasiasa na ndio watatudumaza kama kawaida kwa mambo yao yasiyo na vision, from Kilimo Kwanza, leo tuko Big Results Now (BRN) ambazo zote sioni umuhimu wake mpaka leo.

Nasema chombo kinachojitegemea kwasababu kama Rais atatoka kwenye chama cha siasa ndio mambo ya 10% huibukia huko, anakalishwa chini na watu wa chama chake/kundi lake, then wanapanga namna ya kulipiga taifa kwa manufaa yao.

Kwenye issue ya Covid- 19 hapo, stick na Katiba Mpya tu; naamini Katiba Mpya itamaliza yote, kama Katiba pendekezwa itaainisha majukumu ya kila kiongozi, utekelezaji wake, na mipaka ya kutekeleza majukumu yake.

Atawafanya viongozi wengine serikalini wafanye kazi zao kwa uhuru bila hofu ya kutumbuliwa au kumchukiza bosi aliewapa mkate.

Hili likifanyika hapatakuwepo tena na viongozi kufuata mkumbo wa kukubaliana na kila anachosema bosi wao (Rais) hata kama msimamo wake haukubaliwi na wengine, mambo kama ya nyungu kupigiwa debe na madaktari wa sayansi hayawezi kuwepo tena kwasababu watakuwa wanalindwa kisheria kwenye majukumu yao, na sio kwa mapenzi ya mteule kama ilivyo sasa.
 
Nisikusifie sana, but naona umejiongeza kwa kuandika topic ambayo iko hot currently, wengi walioandika za kwao ni nzuri pia, but vitu kama tatizo la ajira na mengineyo yamekuwa yakiimbwa muda mrefu ni kama yamewachosha wasomaji na wengi wameshakata tamaa, but hii issue uliyoweka inaendana na our current state of political affairs.

Magufuli ameondoka akaja Samia, jinsi anavyoendesha mambo serikalini kila mtu sasa hivi anajiuliza huyu mama yuko sawa or not, kuna kama "some sort of discussion" inayoendelea mtaani about hiki ulichoandika, ndio maana unaona unapata wachangiaji wengi kwenye uzi wako, simply because umewapa uwanja wakutoa maoni yao kwenye issue inayo trend.

The rest wish you all the best.
Asante sana denooJ Kwa compliment yako,asante pia kwa kuuelewa uzi wangu, naamini nimewagusa wengi lakini pia binafsi nimejifunza mengi kutoka kwa wachangiaji
 
Huu mfano wa bandari na mingine ya muonekano huo kama madini, gas, etc ningependa pawepo na chombo maalum kitakachojitegemea kitakachojihusisha na ufuatiliaji wa hiyo mikataba waone kama itakuwa na manufaa kwa nchi ndio isainiwe.

- Hiki kiundwe kisheria (Katiba Mpya) na kiwe independent ikibidi kisiundwe na wanasiasa kabisa. Wawepo watu wa profession kama law, wahasibu, etc.

Ukisema dira pekee hapa haitoshi coz hiyo dira itatekelezwa na wanasiasa na ndio watatudumaza kama kawaida kwa mambo yao yasiyo na vision, from Kilimo Kwanza, leo tuko Big Results Now (BRN) ambazo zote sioni umuhimu wake mpaka leo.

Nasema chombo kinachojitegemea kwasababu kama Rais atatoka kwenye chama cha siasa ndio mambo ya 10% huibukia huko, anakalishwa chini na watu wa chama chake/kundi lake, then wanapanga namna ya kulipiga taifa kwa manufaa yao.

Kwenye issue ya Covid- 19 hapo, stick na Katiba Mpya tu; naamini Katiba Mpya itamaliza yote, kama Katiba pendekezwa itaainisha majukumu ya kila kiongozi, utekelezaji wake, na mipaka ya kutekeleza majukumu yake.

Atawafanya viongozi wengine serikalini wafanye kazi zao kwa uhuru bila hofu ya kutumbuliwa au kumchukiza bosi aliewapa mkate.

Hili likifanyika hapatakuwepo tena na viongozi kufuata mkumbo wa kukubaliana na kila anachosema bosi wao (Rais) hata kama msimamo wake haukubaliwi na wengine, mambo kama ya nyungu kupigiwa debe na madaktari wa sayansi hayawezi kuwepo tena kwasababu watakuwa wanalindwa kisheria kwenye majukumu yao, na sio kwa mapenzi ya mteule kama ilivyo sasa.
Umesema vyema, katiba ni muhimu sana, tume huru na taasisi huru sizizoingiliwa na wanasiasa, mamlaka ya Rais yapunguzwe ili kuhmruhusu uhuru wa watendaji pamoja na taasisi zitakazosimamia dira pamoja na miradi mingine ya maendeleo

Rais aongozwe na sio aamue tu kufanya anavyojisikia, pia nafasi za wakurugenzi au makatibu wakuu ziwe nafasi za ushindani na sio za uteuzi, nadhani hili kwa kiasi kikubwa linakwamisha utendaji na usimamizi ma miradi katika ofisi na taasisi za umma
 
Tatizo lingine kubwa ni self traits za watanzania Je ni kweli tunahitaji maendeleo? How capable are we as citizens, nasem vitu vinavyoturudisha nyuma vingine hata maendeleo hayaji ni utashi wetu wa kufanya kazi, tu watu wa kukata tamaa kabla hatujatenda meaning wavivu, Hatusumbui sana akili yetu kufikiria majawabu ya changamoto zetu, very irresponsible mfano ule mfumo wa mwanzo wa kutoza kodi ya majengo wananchi walikuwa wanapuuzia kulipa labda sababu TRA wamestimate kodi kubwa basi mwananchi anafungi vitumbua ile tax note na halipi.

Wananchi wanahitaji elimu na uhamasishaji mkubwa toka watoto kupenda kazi, kuongeza thamani kwenye kila wanalolitenda. Etc
 
Tatizo lingine kubwa ni self traits za watanzania Je ni kweli tunahitaji maendeleo? How capable are we as citizens, nasem vitu vinavyoturudisha nyuma vingine hata maendeleo hayaji ni utashi wetu wa kufanya kazi, tu watu wa kukata tamaa kabla hatujatenda meaning wavivu, Hatusumbui sana akili yetu kufikiria majawabu ya changamoto zetu, very irresponsible mfano ule mfumo wa mwanzo wa kutoza kodi ya majengo wananchi walikuwa wanapuuzia kulipa labda sababu TRA wamestimate kodi kubwa basi mwananchi anafungi vitumbua ile tax note na halipi.

Wananchi wanahitaji elimu na uhamasishaji mkubwa toka watoto kupenda kazi, kuongeza thamani kwenye kila wanalolitenda. Etc
Mkuu kwa hili naungana na wewe kwa kiasi kikubwa, Watanzania sisi ni wavivu sana, hatupendi kuumiza vichwa kufikiri nje ya boksi,tunapenda sana kulalamika kuliko kazi,ni kweli serikali inafanya mambo mengi yasiyo na maana kwa maendeleo ya Nchi,lakini sisi wenyewe kwanza tumekosa uzalendo kwa kiasi kikubwa ni wavivu wa kupindikia,ndio maana Rais Magufuli pamoja na mambo yake mengine mengi alikuwa anasisitiza sana tupige kazi kwa bidii.
 
Back
Top Bottom