Umuhimu wa Kutoa elimu kwa lugha ya kwanza (Kiswahili)

Jehanamu Hii

Member
Dec 16, 2016
41
31
KUTOA ELIMU KWA LUGHA YA KWANZA AU LUGHA INAYOELEWEKA KUNAMPA MTOTO FURSA YA KUUNGANISHA ELIMU NA MAISHA YA KAWAIDA. KIINGEREZA KWA TANZANIA NI UKUTA UNAOZUIA MUUNGANISHO HUO.

PIA, KUNAMPA MZAZI FURSA YA KUCHANGIA KATIKA UELIMISHAJI. HADITHI ZA KITOTO HUWAELIMISHA MTOTO TOKA WANAPOKUWA WADOGO. HADITHI HIZO ZIMEBEBA ELIMU YAKIWEMO MAMBO YANAYOHUSU SAYANSI, HISTORIA NA BURUDANI. VITU HIVI HUPASWA KUENDELEZWA MASHULENI ILI KULETA UUNGANISHO WA KILE MTOTO ALICHOPATA KATIKA HADITHI NA ELIMU YA SHULE YA MSINGI, SEKONDARI HADI CHUO KIKUU.

WAZAZI WENGI WANAZUNGUMZA KISWAHILI. ELIMU INATOLEWA KIINGEREZA, HUONI KAMA UNAMNYIMA MZAZI HAKI NA JUKUMU LA KUFUATILIA ELIMU YA MWANAYE? MATOKEO YAKE NI KWAMBA JUKUMU LA ELIMU LIMEACHWA KWA WALIMU PEKE YAKE. NA WAZAZI WANAFIKIRI WAJIBU WAO NI KUWA NA PESA NYINGI YA KUMPELEKA MTOTO KATIKA SHULE BINAFSI ILI AKAPATE ELIMU BORA AMBAYO INAAMIKA ELIMU BORA NI ILE INAYOTOLEWA KWA KIINGEREREZA.

KUNA UMUHIMU WA WATU KUELIMISHWA NINI MAANA YA ELIMU NA TOFAUTI ILIYOPO BAINA YA ELIMU BORA NA LUGHA YA KIINGEREZA. ELIMU BORA INAWEZA KUWA KWA LUGHA YOYOTE.

KUNA UWEZEKANO WA KUJIFUNZA KIINGEREZA BILA KUFANYA LUGHA YA KUTOLEA ELIMU.

KUNA UWEZEKANO WA KUONGEA KISWAHILI BILA KUCHANGANYA NA KIINGEREZA. KUCHANGANYA SI UJANJA, NI UPUNGUFU WA USTADI KATIKA LUGHA. MTU STADI KATIKA LUGHA NI YULE ANAYEWEZA KUZUNGUMZA LUGHA MOJA KWA UFASAHA WAKE.

 
Nakubali. Nchi kama Uswidi, Uholanzi, Ujerumani watoto wote husoma kwa lugha ya kitaifa hadi chuo kikuu; Kiingereza wanasoma kama lugha ya kigeni hata hivyo watu wengi wanaelewa Kiingereza vema kushinda wanafunzi wa Tanzania wanaojaribu kusoma kwa Kiingereza kama lugha ya mafundisho. Na matokeo ni afadhali kwa masomo yote.
 
Nakubali. Nchi kama Uswidi, Uholanzi, Ujerumani watoto wote husoma kwa lugha ya kitaifa hadi chuo kikuu; Kiingereza wanasoma kama lugha ya kigeni hata hivyo watu wengi wanaelewa Kiingereza vema kushinda wanafunzi wa Tanzania wanaojaribu kusoma kwa Kiingereza kama lugha ya mafundisho. Na matokeo ni afadhali kwa masomo yote.
Je sisi tukisoma kiswahili hicho kingereza tutakielewa kama unavyosema hapa kuhusu wenzetu? Tuko nyuma kielimu na kimaendeleo lakini tukitumia kiswahili mashuleni tutarudi nyuma mara mia zaidi ya pale tulipo! Kuna sababu nyingi na nafkiri badala ya kufanya hivyo inabidi kingereza kifundishwe kuanzia primary mpaka chuo hii itakuwa ni bora zaidi kwetu na baada ya miaka kama kumi mabadiliko ya kimaendeleo na kuelimika kwa watu kutakuwepo watu wanakuwa kizani kwa kukosa kukijua kingereza tu
 
Je sisi tukisoma kiswahili hicho kingereza tutakielewa kama unavyosema hapa kuhusu wenzetu? Tuko nyuma kielimu na kimaendeleo lakini tukitumia kiswahili mashuleni tutarudi nyuma mara mia zaidi ya pale tulipo! Kuna sababu nyingi na nafkiri badala ya kufanya hivyo inabidi kingereza kifundishwe kuanzia primary mpaka chuo hii itakuwa ni bora zaidi kwetu na baada ya miaka kama kumi mabadiliko ya kimaendeleo na kuelimika kwa watu kutakuwepo watu wanakuwa kizani kwa kukosa kukijua kingereza tu

Soma hii, itakusaidia:

Hivi watanzania wanafikiria nini kujifunza maudhui ya Kiswahili kwa kutumia Kiingereza? Ni kama Mchina kuamua kijifunza maudhui ya Kichina kwa kutumia Kiswahili, sio uchizi huo? Au mwingireza kujifunza maudhui yake ya hukooo ulaya kwa kutumia Kichina, si uchizi huo? Na Mswahili wa bongo kutumia Kiingereza kujifunza uraia!!!!!

Nina maswali machache kwenu mnaoamini Kiingereza ni elimu, na si lugha kama zilivyo lugha zingine!

  1. China wanatumia Kiingereza kujifunza? Hawana elimu au watu walioelimika?
  2. Japani wanatumia Kiingereza kufundisha maswala ya kijapani? Hawana elimu au hakuna walioelimika?
  3. Ufaransa wanatumia Kichina? Hawana elimu au watu walioelimika?
  4. Korea wanatumia Kiswahili? Hawana elimu au watu waliolimika?
Nchi zote hizo nilizozitaja hapo juu zinatumia lugha zao wenyewe kujielimisha. Lakini nchi hizo zinawazungumzaji wazuri wa Kiingereza kuliko Tanzania.

Ukweli ni kwamba....

Nchi tajwa hapo juu wanajifunza Kiingereza kwa chini ya miaka mitatu nawanakizungumza kwa ufasaha zaidi ya Mtanzania aliyesoma Kiingereza, sekondari hadi chuo kwa miaka zaidi ya kumi!! Umewahi kujiuliza ni kwanini? Kwa ufupi sana nitajaribu kukujibu:

KUNA TOFAUTI KATI KUBWA KATI YA LUGHA YA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZA LUGHA FULANI

Kuna tofauti kubwa kati ya lugha ya kufundishia na kujifunza lugha ya kigeni. Watu wanafikiria kutumia Kiingereza kujifunza vitu kama kilimo cha mbogamboga cha Tanzania ndiyo kujifunza Kiingereza na ndiyo kuelimika. Kumbe Kiingereza kinatakiwa kifundishwe kwa ubora wake, pamoja na mambo yahayohusiana na Kiingereza. Namaanisha ni ujinga kujifunza sheria ya Tanzania ama somo la urai linalohusiana na Tanzania kwa lugha ya Kiingereza wakati kwanza, katiba ya Kiingereza imeandikwa kwa Kiswahili, siasa (masuala ya uraia kama vile kampeni) zinafanyika kwa Kiswahili--leo unataka utumie Kiingereza kujifunzia maudhui hayo ya Kiswahili! Kwa nchi zilizoendelea lugha ya kigeni hufunzwa na wazawa (natives) wa lugha hiyo au waliyojifunza lugha hiyo kama vile Kiingereza na kuchangamana na wazawa wa lugha, pamoja na kufundisha maudhui yanayohusiana na lugha.

Huoni kama ni upungufu wa akili kama leo Mchina atatumia Kiswahili kujifunza nyimbo za Kichina? Huo ndio huohuo upunguani ambao Mchina hakukubali kutumia Kiingereza kujifunza mapishi ya vyakula vya Kichina. Geuza kwa watanzania, ni upunguani kujifunza mambo ya watanzania, na maisha ya waswahili kwa Kiingereza badala ya kutumia Kiswahili! Kumbuka Kiingereza si lugha yetu, inawenyewe, kubali ukatae, inawenyewe wanaozungumza kwa ufasaha wake, na kiingereza vilevile kina utamaduni! Kama vile Kichina kilivyo na utamaduni!

Maudhui ya Kiingereza yanajumuisha utamaduni wake. Na hapa kwa vile wanasema tunajifunza Kiingereza cha Uingereza (jambo amabalo pia sikubaliani nalo) lugha ya watu wa Uingereza wana utamaduni wao.Huo ndiyo tungetakiwa kujifunza ili kuweza kuwasiliana na watu hao. Hatuna haja ya kujifunza Kiingereza ili tuweze kuwasiliana sisi kwa sisi, yaani watanzania wenyewe, kwani sisi kwa sisi tunamawasiliano tayari. Mawasiliano yetu yapo kwa lugha Kiswahili na lugha zingine za nyumbani kama vile Kichaga, Kipare, Kimasai, Kisukuma n.k Mambo yanayohusiana na lugha ya Kiingereza na ambayo yangeleta maana ya kujifunza Kiingereza, ni vitu kama teknolojia ya watu wa Uingereza, Marekani na sehemu zingine ambazo maudhui yao yanapatikana kwa lugha ya Kiingereza. Mazoezi ambayo wanafunzi wangefanya darasani ambayo yangeleta maana ya kujifunza Kiingereza ni kama vile kutafuta tiketi ya ndege (kwa kawaida zipo kwa lugha ya Kiingereza), katiba ya marekani (ipo kwa Kiingereza), n.k. Hivyo ndivyo wenzetu wanavyojifunza lugha za watu, kikiwemo Kiswahili.

Nakumbusha tena, lengo la kujifunza lugha ya kigeni ni kuweza kuwasiliana na mgeni, siyo kuweza kuwasiliana sisi kwa sisi, sisi tayari tuna lugha na hatuna haja ya kutumia lugha za watu kujielimisha kwa mambo yanayotuhusu. Si akili kuchukua lugha ya mgeni kujielimisha kuhusu mambo yanayotuhusu!!!! Ni kama vile tuseme tutumie lugha ya Kiingereza kuwasiliana hapa JF.

Sidhani kama utanielewa sana lakini nitashukuru kama utaelewa kidogo, elimu bora haimaanishi Kiingereza. Elimu bora ni maudhui. Na ili maudhui hayo yawafikie walengwa, ni laima itolewe kwa lugha inayoeleweka.

Kutumia Kiingereza kunawapa watu majukumu mawili, kujifunza lugha kwanza, halafu kuanza kutafsiri maudhui katika Kiswahili ili kupata ujumbe. Hiyo ni biashara kubwa sana unaipa ubongo, na wachache ndiyo hufanikiwa kufanya biashara hiyo. Wengi wanaishia kukariri na kufaulu mtihani basi.

Kuna uwezekano wa kujifunza lugha ya Kiingereza bila kutoa elimu ya Tanzania inayowahusu watanzania kwa kutumia lugha wanasiyoielewa ya Kiingereza. Lugha inayoeleweka ni Kiswahili, itumike kuelimisha watu.

Faida za kutumia Kiswahili
  1. Ni lugha inayoeleweka hivyo kila mtu atapata fursa ya kupata elimu kwa urahisi zaidi kwani hakutakuwa na haja ya kutafsiri ujumbe kwenda Kiswahili ili kuuelewa.
  2. Mzazi atachangia katika kumuelimisha mtoto. Katika jamii nyingi zilizoendelea, wazazi huanza kuwaelimisha watoto wao wakiwa wachanga kabisa kwa kuwasomea hadithi. Kwa nchi kama Marekani, watoto husomewa hadithi nyingi sana za Kiingereza--lugha wanayoizungumza, vivyo hivyo nchini china, watoto husomewa hadithi nyingi sana za Kichina --lugha wanayoizungumza, Ujerumani vilevile stori za watoto zipo Kijerumani. Hadithi hizi wazazi huwasomea watoto kabla ya kulala, au wawapo katika mapumziko. Hadithi hizi zimejaa elimu. Mbali na kuwa zingine ni stori za maisha tu na kufurahisa, nyingi huwa na masuala yanayohusu tanzu mbalimbali za elimu kama vile sayansi, hesabu, historia, uraia n.k. Mtoto anapoanza kusoma shuleni, elimu ile inakuwa imeunganishwa na hadithi alizozisoma, au waalimu hufundishwa kuunganisha hadithi hizo na masomo ya shuleni. Matokeo yake ni kwamba mzazi anakuwa ameshamjengea mtoto msingi wa elim na kupenda kusoma na msingi huo huendelezwa na walimu. Kwa Tanzania ni vigumu msingi huo kujengwa, kwani hata mzazi angemwanzishia mawanawe kusoma hadithi za Kiswahili (maana wazazi wengi wanaelewa na kusema vizuri Kiswahili zaidi ya Kiingereza--ni vigumu kumsomea mtoto hadithi kwa lugha asiyoijua--hakutakuwa na matunda bora) elimu inakuja kumtenganisha na ule msingi wa alioupata kwa wazazi. Na kifupi tu ni kwamba hata wazazi wenyewe hawaoni haja ya kujenga msingi utakaobomolewa hivyo wamewaacha watoto katika mikono ya walimu kwa kusubiri mtoto akue ampeleke 'English Medium". Hilo ni kosa! Si ujanja ni kosa.
  3. Wazazi wengi wasiyojua Kiingereza watakuwa na uwezo wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao kwani alama zitaandikwa kwa Kiswahili. Wazazi wengi hawawezi kabisa kutoa maoni yao kwa watoto wao kwa kutoelewa hata ripoti inayotumwa kwa mzazi ambayo ipo kwa Kiingereza au matokeo ambayo yamefafanuliwa kwa Kiingereza.
  4. Maudhui yatasadifu lugha. Kama nilivyotangulia kusema, haina maana ya yoyote kujifunza mambo ya wabongo kwa lugha ya kigeni wakati tuna lugha tayari!
Sasa itakuwaje kwa Kiingereza, lugha ambayo ni muhimu kuijua katika dunia ya sasa?

Kama nilivyotangulia kusema, huna haja ya kupata elimu kwa lugha ya Kiingereza ili kukijua Kiingereza. Wachina wanaojifunza Kiingereza kwa muda mfupi na kukizungumza vizuri zaidi yetu hawajakitumia katika elimu, wamejifunza chenyewe kama chenyewe. Hilo ndilo tunalotakiwa tulifanye.

Hatua zifuatazo zichukuliwe:
  1. Kiingereza kifundishwe na watu wazawa wa lugha hiyo, au watu waliofunzwa vizuri na kufikia kukizungumza katika ubora wake. Mara nyingi watu hawa pia lazima wawe wamepata nafasi ya kukizungumza na wazawa mashuleni kwao au kwa kusafiri na kuishi na wazawa wanaotumia lugha ya Kiingereza. Hii itasaidia mtu kusoma Kiingereza sahihi kwa muda mfupi. Kwa sasa Kiingereza ambacho si sahihi kinafundishwa kwa muda mrefu sekondari, vyuoni na mtaani.
  2. Maudhui yalenge nia na madhumuni ya kusoma Kiingereza. Nchini Tanzania, sababu inayotajwa watu kujifunza Kiingereza ni kuweza kuwasiliana na watu wa nje. Kama hiyo ndiyo sababu, basi maudhui yanayotolewa yawe ya nje. Kwa mfano, kama dhumuni ni kufanya mipango ya biashara na watu wa Marekani au Uingereza, mada ambayo inatakiwa iwe kwenye kitabu cha kufundishia Ni kama vile 'MAZUNGUMZO YA KIBIASHARA". Mifano mbalimbali ya mazungumzo ya kibiashara yachukuliwe kutoka kwa watu wa Marekani au Uingereza wakifanya makubaliano ya kibiashara. Misamiati kama "Dollar, Euro," n.k lazima itaonekana kwenye mifano hiyo. Mifano hii inaweza kupatikana mtandaoni kwa urahisi au katika vitabu vinavyotumiwa kufundishia Kiingereza Marekani ama Ulaya.
Jambo lingine:

Umewahi kujiuliza kwanini wazungu wengi wakizungumza wanasimulia hadithi zao za utoto? Yaani si jambo la kushangaza kumsikia mzungu akisema 'When I was a child....'

Ngoja nikupe siri. Katika elimu kuna kitu kinaitwa 'Connection' (Uunganishaji). Unamfundisha mtoto kuunganisha jambo lolote analojifunza darasani na maisha yake ya kawaida. Kwa mfano, unapomfundisha mtoto sheria ya Newton, na kumtaka aikariri lazima umsaidie kuunganisha sheria hiyo na maisha ya kawaida. Mfano mzuri ni kwamba ni huwa nikiwafundisha wanafunzi wangu wa nje za nchi jambo, huniuliza 'Kwa nini ninatakiwa kujua jambo hili?" Hilo ndilo swahili linaloleta 'uunganisho' katika elimu, ama mada, au dhana inayofundishwa. Mwalimu anaposhindwa kujibu swali hilo inaonesha haelewi jambo analolifundisha kwa undani wake. Na si kosa, anaweza kuomba msaada kwa wanafunzi au walimu wenzake.

Elimu ya Tanzania haina UUNGANISHO, imeachana kuanzia suala la lugha mpaka maudhui.
 
Soma hii, itakusaidia:

Hivi watanzania wanafikiria nini kujifunza maudhui ya Kiswahili kwa kutumia Kiingereza? Ni kama Mchina kuamua kijifunza maudhui ya Kichina kwa kutumia Kiswahili, sio uchizi huo? Au mwingireza kujifunza maudhui yake ya hukooo ulaya kwa kutumia Kichina, si uchizi huo? Na Mswahili wa bongo kutumia Kiingereza kujifunza uraia!!!!!

Nina maswali machache kwenu mnaoamini Kiingereza ni elimu, na si lugha kama zilivyo lugha zingine!

  1. China wanatumia Kiingereza kujifunza? Hawana elimu au watu walioelimika?
  2. Japani wanatumia Kiingereza kufundisha maswala ya kijapani? Hawana elimu au hakuna walioelimika?
  3. Ufaransa wanatumia Kichina? Hawana elimu au watu walioelimika?
  4. Korea wanatumia Kiswahili? Hawana elimu au watu waliolimika?
Nchi zote hizo nilizozitaja hapo juu zinatumia lugha zao wenyewe kujielimisha. Lakini nchi hizo zinawazungumzaji wazuri wa Kiingereza kuliko Tanzania.

Ukweli ni kwamba....

Nchi tajwa hapo juu wanajifunza Kiingereza kwa chini ya miaka mitatu nawanakizungumza kwa ufasaha zaidi ya Mtanzania aliyesoma Kiingereza, sekondari hadi chuo kwa miaka zaidi ya kumi!! Umewahi kujiuliza ni kwanini? Kwa ufupi sana nitajaribu kukujibu:

KUNA TOFAUTI KATI KUBWA KATI YA LUGHA YA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZA LUGHA FULANI

Kuna tofauti kubwa kati ya lugha ya kufundishia na kujifunza lugha ya kigeni. Watu wanafikiria kutumia Kiingereza kujifunza vitu kama kilimo cha mbogamboga cha Tanzania ndiyo kujifunza Kiingereza na ndiyo kuelimika. Kumbe Kiingereza kinatakiwa kifundishwe kwa ubora wake, pamoja na mambo yahayohusiana na Kiingereza. Namaanisha ni ujinga kujifunza sheria ya Tanzania ama somo la urai linalohusiana na Tanzania kwa lugha ya Kiingereza wakati kwanza, katiba ya Kiingereza imeandikwa kwa Kiswahili, siasa (masuala ya uraia kama vile kampeni) zinafanyika kwa Kiswahili--leo unataka utumie Kiingereza kujifunzia maudhui hayo ya Kiswahili! Kwa nchi zilizoendelea lugha ya kigeni hufunzwa na wazawa (natives) wa lugha hiyo au waliyojifunza lugha hiyo kama vile Kiingereza na kuchangamana na wazawa wa lugha, pamoja na kufundisha maudhui yanayohusiana na lugha.

Huoni kama ni upungufu wa akili kama leo Mchina atatumia Kiswahili kujifunza nyimbo za Kichina? Huo ndio huohuo upunguani ambao Mchina hakukubali kutumia Kiingereza kujifunza mapishi ya vyakula vya Kichina. Geuza kwa watanzania, ni upunguani kujifunza mambo ya watanzania, na maisha ya waswahili kwa Kiingereza badala ya kutumia Kiswahili! Kumbuka Kiingereza si lugha yetu, inawenyewe, kubali ukatae, inawenyewe wanaozungumza kwa ufasaha wake, na kiingereza vilevile kina utamaduni! Kama vile Kichina kilivyo na utamaduni!

Maudhui ya Kiingereza yanajumuisha utamaduni wake. Na hapa kwa vile wanasema tunajifunza Kiingereza cha Uingereza (jambo amabalo pia sikubaliani nalo) lugha ya watu wa Uingereza wana utamaduni wao.Huo ndiyo tungetakiwa kujifunza ili kuweza kuwasiliana na watu hao. Hatuna haja ya kujifunza Kiingereza ili tuweze kuwasiliana sisi kwa sisi, yaani watanzania wenyewe, kwani sisi kwa sisi tunamawasiliano tayari. Mawasiliano yetu yapo kwa lugha Kiswahili na lugha zingine za nyumbani kama vile Kichaga, Kipare, Kimasai, Kisukuma n.k Mambo yanayohusiana na lugha ya Kiingereza na ambayo yangeleta maana ya kujifunza Kiingereza, ni vitu kama teknolojia ya watu wa Uingereza, Marekani na sehemu zingine ambazo maudhui yao yanapatikana kwa lugha ya Kiingereza. Mazoezi ambayo wanafunzi wangefanya darasani ambayo yangeleta maana ya kujifunza Kiingereza ni kama vile kutafuta tiketi ya ndege (kwa kawaida zipo kwa lugha ya Kiingereza), katiba ya marekani (ipo kwa Kiingereza), n.k. Hivyo ndivyo wenzetu wanavyojifunza lugha za watu, kikiwemo Kiswahili.

Nakumbusha tena, lengo la kujifunza lugha ya kigeni ni kuweza kuwasiliana na mgeni, siyo kuweza kuwasiliana sisi kwa sisi, sisi tayari tuna lugha na hatuna haja ya kutumia lugha za watu kujielimisha kwa mambo yanayotuhusu. Si akili kuchukua lugha ya mgeni kujielimisha kuhusu mambo yanayotuhusu!!!! Ni kama vile tuseme tutumie lugha ya Kiingereza kuwasiliana hapa JF.

Sidhani kama utanielewa sana lakini nitashukuru kama utaelewa kidogo, elimu bora haimaanishi Kiingereza. Elimu bora ni maudhui. Na ili maudhui hayo yawafikie walengwa, ni laima itolewe kwa lugha inayoeleweka.

Kutumia Kiingereza kunawapa watu majukumu mawili, kujifunza lugha kwanza, halafu kuanza kutafsiri maudhui katika Kiswahili ili kupata ujumbe. Hiyo ni biashara kubwa sana unaipa ubongo, na wachache ndiyo hufanikiwa kufanya biashara hiyo. Wengi wanaishia kukariri na kufaulu mtihani basi.

Kuna uwezekano wa kujifunza lugha ya Kiingereza bila kutoa elimu ya Tanzania inayowahusu watanzania kwa kutumia lugha wanasiyoielewa ya Kiingereza. Lugha inayoeleweka ni Kiswahili, itumike kuelimisha watu.

Faida za kutumia Kiswahili
  1. Ni lugha inayoeleweka hivyo kila mtu atapata fursa ya kupata elimu kwa urahisi zaidi kwani hakutakuwa na haja ya kutafsiri ujumbe kwenda Kiswahili ili kuuelewa.
  2. Mzazi atachangia katika kumuelimisha mtoto. Katika jamii nyingi zilizoendelea, wazazi huanza kuwaelimisha watoto wao wakiwa wachanga kabisa kwa kuwasomea hadithi. Kwa nchi kama Marekani, watoto husomewa hadithi nyingi sana za Kiingereza--lugha wanayoizungumza, vivyo hivyo nchini china, watoto husomewa hadithi nyingi sana za Kichina --lugha wanayoizungumza, Ujerumani vilevile stori za watoto zipo Kijerumani. Hadithi hizi wazazi huwasomea watoto kabla ya kulala, au wawapo katika mapumziko. Hadithi hizi zimejaa elimu. Mbali na kuwa zingine ni stori za maisha tu na kufurahisa, nyingi huwa na masuala yanayohusu tanzu mbalimbali za elimu kama vile sayansi, hesabu, historia, uraia n.k. Mtoto anapoanza kusoma shuleni, elimu ile inakuwa imeunganishwa na hadithi alizozisoma, au waalimu hufundishwa kuunganisha hadithi hizo na masomo ya shuleni. Matokeo yake ni kwamba mzazi anakuwa ameshamjengea mtoto msingi wa elim na kupenda kusoma na msingi huo huendelezwa na walimu. Kwa Tanzania ni vigumu msingi huo kujengwa, kwani hata mzazi angemwanzishia mawanawe kusoma hadithi za Kiswahili (maana wazazi wengi wanaelewa na kusema vizuri Kiswahili zaidi ya Kiingereza--ni vigumu kumsomea mtoto hadithi kwa lugha asiyoijua--hakutakuwa na matunda bora) elimu inakuja kumtenganisha na ule msingi wa alioupata kwa wazazi. Na kifupi tu ni kwamba hata wazazi wenyewe hawaoni haja ya kujenga msingi utakaobomolewa hivyo wamewaacha watoto katika mikono ya walimu kwa kusubiri mtoto akue ampeleke 'English Medium". Hilo ni kosa! Si ujanja ni kosa.
  3. Wazazi wengi wasiyojua Kiingereza watakuwa na uwezo wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao kwani alama zitaandikwa kwa Kiswahili. Wazazi wengi hawawezi kabisa kutoa maoni yao kwa watoto wao kwa kutoelewa hata ripoti inayotumwa kwa mzazi ambayo ipo kwa Kiingereza au matokeo ambayo yamefafanuliwa kwa Kiingereza.
  4. Maudhui yatasadifu lugha. Kama nilivyotangulia kusema, haina maana ya yoyote kujifunza mambo ya wabongo kwa lugha ya kigeni wakati tuna lugha tayari!
Sasa itakuwaje kwa Kiingereza, lugha ambayo ni muhimu kuijua katika dunia ya sasa?

Kama nilivyotangulia kusema, huna haja ya kupata elimu kwa lugha ya Kiingereza ili kukijua Kiingereza. Wachina wanaojifunza Kiingereza kwa muda mfupi na kukizungumza vizuri zaidi yetu hawajakitumia katika elimu, wamejifunza chenyewe kama chenyewe. Hilo ndilo tunalotakiwa tulifanye.

Hatua zifuatazo zichukuliwe:
  1. Kiingereza kifundishwe na watu wazawa wa lugha hiyo, au watu waliofunzwa vizuri na kufikia kukizungumza katika ubora wake. Mara nyingi watu hawa pia lazima wawe wamepata nafasi ya kukizungumza na wazawa mashuleni kwao au kwa kusafiri na kuishi na wazawa wanaotumia lugha ya Kiingereza. Hii itasaidia mtu kusoma Kiingereza sahihi kwa muda mfupi. Kwa sasa Kiingereza ambacho si sahihi kinafundishwa kwa muda mrefu sekondari, vyuoni na mtaani.
  2. Maudhui yalenge nia na madhumuni ya kusoma Kiingereza. Nchini Tanzania, sababu inayotajwa watu kujifunza Kiingereza ni kuweza kuwasiliana na watu wa nje. Kama hiyo ndiyo sababu, basi maudhui yanayotolewa yawe ya nje. Kwa mfano, kama dhumuni ni kufanya mipango ya biashara na watu wa Marekani au Uingereza, mada ambayo inatakiwa iwe kwenye kitabu cha kufundishia Ni kama vile 'MAZUNGUMZO YA KIBIASHARA". Mifano mbalimbali ya mazungumzo ya kibiashara yachukuliwe kutoka kwa watu wa Marekani au Uingereza wakifanya makubaliano ya kibiashara. Misamiati kama "Dollar, Euro," n.k lazima itaonekana kwenye mifano hiyo. Mifano hii inaweza kupatikana mtandaoni kwa urahisi au katika vitabu vinavyotumiwa kufundishia Kiingereza Marekani ama Ulaya.
Jambo lingine:

Umewahi kujiuliza kwanini wazungu wengi wakizungumza wanasimulia hadithi zao za utoto? Yaani si jambo la kushangaza kumsikia mzungu akisema 'When I was a child....'

Ngoja nikupe siri. Katika elimu kuna kitu kinaitwa 'Connection' (Uunganishaji). Unamfundisha mtoto kuunganisha jambo lolote analojifunza darasani na maisha yake ya kawaida. Kwa mfano, unapomfundisha mtoto sheria ya Newton, na kumtaka aikariri lazima umsaidie kuunganisha sheria hiyo na maisha ya kawaida. Mfano mzuri ni kwamba ni huwa nikiwafundisha wanafunzi wangu wa nje za nchi jambo, huniuliza 'Kwa nini ninatakiwa kujua jambo hili?" Hilo ndilo swahili linaloleta 'uunganisho' katika elimu, ama mada, au dhana inayofundishwa. Mwalimu anaposhindwa kujibu swali hilo inaonesha haelewi jambo analolifundisha kwa undani wake. Na si kosa, anaweza kuomba msaada kwa wanafunzi au walimu wenzake.

Elimu ya Tanzania haina UUNGANISHO, imeachana kuanzia suala la lugha mpaka maudhui.

KUMBUKA KUWA KIINGEREZA NI LUGHA, SI ELIMU. ELIMU ITOLEWE KAMA ELIMU NA LUGHA IFUNDISHWE KAMA LUGHA. HIVYO NDIVYO NCHI ZA WENYE KUJITAMBUA ZINAVYOFANYA. THAMANI YA ELIMU NI MAUDHUI, SI KUJUA KUSEMA YES, NO. KAMA UNA MAUDHUI MAZURI KWA LUGHA YAKO DUNIA YOTE ITAKUTAFUTA NA KUTAFSIRI. SI KUBABAISHA KWA KUTUMIA LUGHA YA WATU.
 
Nakubali. Nchi kama Uswidi, Uholanzi, Ujerumani watoto wote husoma kwa lugha ya kitaifa hadi chuo kikuu; Kiingereza wanasoma kama lugha ya kigeni hata hivyo watu wengi wanaelewa Kiingereza vema kushinda wanafunzi wa Tanzania wanaojaribu kusoma kwa Kiingereza kama lugha ya mafundisho. Na matokeo ni afadhali kwa masomo yote.
Maendeleo hayaigwi.. Maendeleo yanatengenezwa.... Ukifanya kitu kwa kusema ndivyo kinavyotakiwa ni kosa... Ila kusema nafanya kitu kiwe vile ninavyotaka ndio ustadi ulipo.
Maendeleo bora ya nchi ni yale yatakayo beba ama kubebwa na tamaduni za nchi husika.
Lugha ya Kiswahili ni moja ya nyenzo ya Tamaduni zetu pamoja na nguzo ya uzalendo na nchi yetu.
Kiswahili sio sababu ya kuturudisha nyuma kama nchi, sababu itabaki kua kwetu kwa kuona vya kigeni ni bora kuliko vya kwetu.
Lugha ni kiunganishi cha jamii zetu... Makabila zaidi ya 120 yameungwa na Kiswahili iweje leo tukitupe kwa kisingizio cha hatuta endelea..!?
 
Soma hii, itakusaidia:

Hivi watanzania wanafikiria nini kujifunza maudhui ya Kiswahili kwa kutumia Kiingereza? Ni kama Mchina kuamua kijifunza maudhui ya Kichina kwa kutumia Kiswahili, sio uchizi huo? Au mwingireza kujifunza maudhui yake ya hukooo ulaya kwa kutumia Kichina, si uchizi huo? Na Mswahili wa bongo kutumia Kiingereza kujifunza uraia!!!!!

Nina maswali machache kwenu mnaoamini Kiingereza ni elimu, na si lugha kama zilivyo lugha zingine!

  1. China wanatumia Kiingereza kujifunza? Hawana elimu au watu walioelimika?
  2. Japani wanatumia Kiingereza kufundisha maswala ya kijapani? Hawana elimu au hakuna walioelimika?
  3. Ufaransa wanatumia Kichina? Hawana elimu au watu walioelimika?
  4. Korea wanatumia Kiswahili? Hawana elimu au watu waliolimika?
Nchi zote hizo nilizozitaja hapo juu zinatumia lugha zao wenyewe kujielimisha. Lakini nchi hizo zinawazungumzaji wazuri wa Kiingereza kuliko Tanzania.

Ukweli ni kwamba....

Nchi tajwa hapo juu wanajifunza Kiingereza kwa chini ya miaka mitatu nawanakizungumza kwa ufasaha zaidi ya Mtanzania aliyesoma Kiingereza, sekondari hadi chuo kwa miaka zaidi ya kumi!! Umewahi kujiuliza ni kwanini? Kwa ufupi sana nitajaribu kukujibu:

KUNA TOFAUTI KATI KUBWA KATI YA LUGHA YA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZA LUGHA FULANI

Kuna tofauti kubwa kati ya lugha ya kufundishia na kujifunza lugha ya kigeni. Watu wanafikiria kutumia Kiingereza kujifunza vitu kama kilimo cha mbogamboga cha Tanzania ndiyo kujifunza Kiingereza na ndiyo kuelimika. Kumbe Kiingereza kinatakiwa kifundishwe kwa ubora wake, pamoja na mambo yahayohusiana na Kiingereza. Namaanisha ni ujinga kujifunza sheria ya Tanzania ama somo la urai linalohusiana na Tanzania kwa lugha ya Kiingereza wakati kwanza, katiba ya Kiingereza imeandikwa kwa Kiswahili, siasa (masuala ya uraia kama vile kampeni) zinafanyika kwa Kiswahili--leo unataka utumie Kiingereza kujifunzia maudhui hayo ya Kiswahili! Kwa nchi zilizoendelea lugha ya kigeni hufunzwa na wazawa (natives) wa lugha hiyo au waliyojifunza lugha hiyo kama vile Kiingereza na kuchangamana na wazawa wa lugha, pamoja na kufundisha maudhui yanayohusiana na lugha.

Huoni kama ni upungufu wa akili kama leo Mchina atatumia Kiswahili kujifunza nyimbo za Kichina? Huo ndio huohuo upunguani ambao Mchina hakukubali kutumia Kiingereza kujifunza mapishi ya vyakula vya Kichina. Geuza kwa watanzania, ni upunguani kujifunza mambo ya watanzania, na maisha ya waswahili kwa Kiingereza badala ya kutumia Kiswahili! Kumbuka Kiingereza si lugha yetu, inawenyewe, kubali ukatae, inawenyewe wanaozungumza kwa ufasaha wake, na kiingereza vilevile kina utamaduni! Kama vile Kichina kilivyo na utamaduni!

Maudhui ya Kiingereza yanajumuisha utamaduni wake. Na hapa kwa vile wanasema tunajifunza Kiingereza cha Uingereza (jambo amabalo pia sikubaliani nalo) lugha ya watu wa Uingereza wana utamaduni wao.Huo ndiyo tungetakiwa kujifunza ili kuweza kuwasiliana na watu hao. Hatuna haja ya kujifunza Kiingereza ili tuweze kuwasiliana sisi kwa sisi, yaani watanzania wenyewe, kwani sisi kwa sisi tunamawasiliano tayari. Mawasiliano yetu yapo kwa lugha Kiswahili na lugha zingine za nyumbani kama vile Kichaga, Kipare, Kimasai, Kisukuma n.k Mambo yanayohusiana na lugha ya Kiingereza na ambayo yangeleta maana ya kujifunza Kiingereza, ni vitu kama teknolojia ya watu wa Uingereza, Marekani na sehemu zingine ambazo maudhui yao yanapatikana kwa lugha ya Kiingereza. Mazoezi ambayo wanafunzi wangefanya darasani ambayo yangeleta maana ya kujifunza Kiingereza ni kama vile kutafuta tiketi ya ndege (kwa kawaida zipo kwa lugha ya Kiingereza), katiba ya marekani (ipo kwa Kiingereza), n.k. Hivyo ndivyo wenzetu wanavyojifunza lugha za watu, kikiwemo Kiswahili.

Nakumbusha tena, lengo la kujifunza lugha ya kigeni ni kuweza kuwasiliana na mgeni, siyo kuweza kuwasiliana sisi kwa sisi, sisi tayari tuna lugha na hatuna haja ya kutumia lugha za watu kujielimisha kwa mambo yanayotuhusu. Si akili kuchukua lugha ya mgeni kujielimisha kuhusu mambo yanayotuhusu!!!! Ni kama vile tuseme tutumie lugha ya Kiingereza kuwasiliana hapa JF.

Sidhani kama utanielewa sana lakini nitashukuru kama utaelewa kidogo, elimu bora haimaanishi Kiingereza. Elimu bora ni maudhui. Na ili maudhui hayo yawafikie walengwa, ni laima itolewe kwa lugha inayoeleweka.

Kutumia Kiingereza kunawapa watu majukumu mawili, kujifunza lugha kwanza, halafu kuanza kutafsiri maudhui katika Kiswahili ili kupata ujumbe. Hiyo ni biashara kubwa sana unaipa ubongo, na wachache ndiyo hufanikiwa kufanya biashara hiyo. Wengi wanaishia kukariri na kufaulu mtihani basi.

Kuna uwezekano wa kujifunza lugha ya Kiingereza bila kutoa elimu ya Tanzania inayowahusu watanzania kwa kutumia lugha wanasiyoielewa ya Kiingereza. Lugha inayoeleweka ni Kiswahili, itumike kuelimisha watu.

Faida za kutumia Kiswahili
  1. Ni lugha inayoeleweka hivyo kila mtu atapata fursa ya kupata elimu kwa urahisi zaidi kwani hakutakuwa na haja ya kutafsiri ujumbe kwenda Kiswahili ili kuuelewa.
  2. Mzazi atachangia katika kumuelimisha mtoto. Katika jamii nyingi zilizoendelea, wazazi huanza kuwaelimisha watoto wao wakiwa wachanga kabisa kwa kuwasomea hadithi. Kwa nchi kama Marekani, watoto husomewa hadithi nyingi sana za Kiingereza--lugha wanayoizungumza, vivyo hivyo nchini china, watoto husomewa hadithi nyingi sana za Kichina --lugha wanayoizungumza, Ujerumani vilevile stori za watoto zipo Kijerumani. Hadithi hizi wazazi huwasomea watoto kabla ya kulala, au wawapo katika mapumziko. Hadithi hizi zimejaa elimu. Mbali na kuwa zingine ni stori za maisha tu na kufurahisa, nyingi huwa na masuala yanayohusu tanzu mbalimbali za elimu kama vile sayansi, hesabu, historia, uraia n.k. Mtoto anapoanza kusoma shuleni, elimu ile inakuwa imeunganishwa na hadithi alizozisoma, au waalimu hufundishwa kuunganisha hadithi hizo na masomo ya shuleni. Matokeo yake ni kwamba mzazi anakuwa ameshamjengea mtoto msingi wa elim na kupenda kusoma na msingi huo huendelezwa na walimu. Kwa Tanzania ni vigumu msingi huo kujengwa, kwani hata mzazi angemwanzishia mawanawe kusoma hadithi za Kiswahili (maana wazazi wengi wanaelewa na kusema vizuri Kiswahili zaidi ya Kiingereza--ni vigumu kumsomea mtoto hadithi kwa lugha asiyoijua--hakutakuwa na matunda bora) elimu inakuja kumtenganisha na ule msingi wa alioupata kwa wazazi. Na kifupi tu ni kwamba hata wazazi wenyewe hawaoni haja ya kujenga msingi utakaobomolewa hivyo wamewaacha watoto katika mikono ya walimu kwa kusubiri mtoto akue ampeleke 'English Medium". Hilo ni kosa! Si ujanja ni kosa.
  3. Wazazi wengi wasiyojua Kiingereza watakuwa na uwezo wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao kwani alama zitaandikwa kwa Kiswahili. Wazazi wengi hawawezi kabisa kutoa maoni yao kwa watoto wao kwa kutoelewa hata ripoti inayotumwa kwa mzazi ambayo ipo kwa Kiingereza au matokeo ambayo yamefafanuliwa kwa Kiingereza.
  4. Maudhui yatasadifu lugha. Kama nilivyotangulia kusema, haina maana ya yoyote kujifunza mambo ya wabongo kwa lugha ya kigeni wakati tuna lugha tayari!
Sasa itakuwaje kwa Kiingereza, lugha ambayo ni muhimu kuijua katika dunia ya sasa?

Kama nilivyotangulia kusema, huna haja ya kupata elimu kwa lugha ya Kiingereza ili kukijua Kiingereza. Wachina wanaojifunza Kiingereza kwa muda mfupi na kukizungumza vizuri zaidi yetu hawajakitumia katika elimu, wamejifunza chenyewe kama chenyewe. Hilo ndilo tunalotakiwa tulifanye.

Hatua zifuatazo zichukuliwe:
  1. Kiingereza kifundishwe na watu wazawa wa lugha hiyo, au watu waliofunzwa vizuri na kufikia kukizungumza katika ubora wake. Mara nyingi watu hawa pia lazima wawe wamepata nafasi ya kukizungumza na wazawa mashuleni kwao au kwa kusafiri na kuishi na wazawa wanaotumia lugha ya Kiingereza. Hii itasaidia mtu kusoma Kiingereza sahihi kwa muda mfupi. Kwa sasa Kiingereza ambacho si sahihi kinafundishwa kwa muda mrefu sekondari, vyuoni na mtaani.
  2. Maudhui yalenge nia na madhumuni ya kusoma Kiingereza. Nchini Tanzania, sababu inayotajwa watu kujifunza Kiingereza ni kuweza kuwasiliana na watu wa nje. Kama hiyo ndiyo sababu, basi maudhui yanayotolewa yawe ya nje. Kwa mfano, kama dhumuni ni kufanya mipango ya biashara na watu wa Marekani au Uingereza, mada ambayo inatakiwa iwe kwenye kitabu cha kufundishia Ni kama vile 'MAZUNGUMZO YA KIBIASHARA". Mifano mbalimbali ya mazungumzo ya kibiashara yachukuliwe kutoka kwa watu wa Marekani au Uingereza wakifanya makubaliano ya kibiashara. Misamiati kama "Dollar, Euro," n.k lazima itaonekana kwenye mifano hiyo. Mifano hii inaweza kupatikana mtandaoni kwa urahisi au katika vitabu vinavyotumiwa kufundishia Kiingereza Marekani ama Ulaya.
Jambo lingine:

Umewahi kujiuliza kwanini wazungu wengi wakizungumza wanasimulia hadithi zao za utoto? Yaani si jambo la kushangaza kumsikia mzungu akisema 'When I was a child....'

Ngoja nikupe siri. Katika elimu kuna kitu kinaitwa 'Connection' (Uunganishaji). Unamfundisha mtoto kuunganisha jambo lolote analojifunza darasani na maisha yake ya kawaida. Kwa mfano, unapomfundisha mtoto sheria ya Newton, na kumtaka aikariri lazima umsaidie kuunganisha sheria hiyo na maisha ya kawaida. Mfano mzuri ni kwamba ni huwa nikiwafundisha wanafunzi wangu wa nje za nchi jambo, huniuliza 'Kwa nini ninatakiwa kujua jambo hili?" Hilo ndilo swahili linaloleta 'uunganisho' katika elimu, ama mada, au dhana inayofundishwa. Mwalimu anaposhindwa kujibu swali hilo inaonesha haelewi jambo analolifundisha kwa undani wake. Na si kosa, anaweza kuomba msaada kwa wanafunzi au walimu wenzake.

Elimu ya Tanzania haina UUNGANISHO, imeachana kuanzia suala la lugha mpaka maudhui.
Nadhani nitachukua muda... Mpaka kukutana na Makala kuhusu Kiswahili yenye maana zaidi kushinda hii kaka.... Labda nitakayo andika mimi.... HONGERA SANA KAKA... NIMEKUELEWA SAANAAA
 
Soma hii, itakusaidia:

Hivi watanzania wanafikiria nini kujifunza maudhui ya Kiswahili kwa kutumia Kiingereza? Ni kama Mchina kuamua kijifunza maudhui ya Kichina kwa kutumia Kiswahili, sio uchizi huo? Au mwingireza kujifunza maudhui yake ya hukooo ulaya kwa kutumia Kichina, si uchizi huo? Na Mswahili wa bongo kutumia Kiingereza kujifunza uraia!!!!!

Nina maswali machache kwenu mnaoamini Kiingereza ni elimu, na si lugha kama zilivyo lugha zingine!

  1. China wanatumia Kiingereza kujifunza? Hawana elimu au watu walioelimika?
  2. Japani wanatumia Kiingereza kufundisha maswala ya kijapani? Hawana elimu au hakuna walioelimika?
  3. Ufaransa wanatumia Kichina? Hawana elimu au watu walioelimika?
  4. Korea wanatumia Kiswahili? Hawana elimu au watu waliolimika?
Nchi zote hizo nilizozitaja hapo juu zinatumia lugha zao wenyewe kujielimisha. Lakini nchi hizo zinawazungumzaji wazuri wa Kiingereza kuliko Tanzania.

Ukweli ni kwamba....

Nchi tajwa hapo juu wanajifunza Kiingereza kwa chini ya miaka mitatu nawanakizungumza kwa ufasaha zaidi ya Mtanzania aliyesoma Kiingereza, sekondari hadi chuo kwa miaka zaidi ya kumi!! Umewahi kujiuliza ni kwanini? Kwa ufupi sana nitajaribu kukujibu:

KUNA TOFAUTI KATI KUBWA KATI YA LUGHA YA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZA LUGHA FULANI

Kuna tofauti kubwa kati ya lugha ya kufundishia na kujifunza lugha ya kigeni. Watu wanafikiria kutumia Kiingereza kujifunza vitu kama kilimo cha mbogamboga cha Tanzania ndiyo kujifunza Kiingereza na ndiyo kuelimika. Kumbe Kiingereza kinatakiwa kifundishwe kwa ubora wake, pamoja na mambo yahayohusiana na Kiingereza. Namaanisha ni ujinga kujifunza sheria ya Tanzania ama somo la urai linalohusiana na Tanzania kwa lugha ya Kiingereza wakati kwanza, katiba ya Kiingereza imeandikwa kwa Kiswahili, siasa (masuala ya uraia kama vile kampeni) zinafanyika kwa Kiswahili--leo unataka utumie Kiingereza kujifunzia maudhui hayo ya Kiswahili! Kwa nchi zilizoendelea lugha ya kigeni hufunzwa na wazawa (natives) wa lugha hiyo au waliyojifunza lugha hiyo kama vile Kiingereza na kuchangamana na wazawa wa lugha, pamoja na kufundisha maudhui yanayohusiana na lugha.

Huoni kama ni upungufu wa akili kama leo Mchina atatumia Kiswahili kujifunza nyimbo za Kichina? Huo ndio huohuo upunguani ambao Mchina hakukubali kutumia Kiingereza kujifunza mapishi ya vyakula vya Kichina. Geuza kwa watanzania, ni upunguani kujifunza mambo ya watanzania, na maisha ya waswahili kwa Kiingereza badala ya kutumia Kiswahili! Kumbuka Kiingereza si lugha yetu, inawenyewe, kubali ukatae, inawenyewe wanaozungumza kwa ufasaha wake, na kiingereza vilevile kina utamaduni! Kama vile Kichina kilivyo na utamaduni!

Maudhui ya Kiingereza yanajumuisha utamaduni wake. Na hapa kwa vile wanasema tunajifunza Kiingereza cha Uingereza (jambo amabalo pia sikubaliani nalo) lugha ya watu wa Uingereza wana utamaduni wao.Huo ndiyo tungetakiwa kujifunza ili kuweza kuwasiliana na watu hao. Hatuna haja ya kujifunza Kiingereza ili tuweze kuwasiliana sisi kwa sisi, yaani watanzania wenyewe, kwani sisi kwa sisi tunamawasiliano tayari. Mawasiliano yetu yapo kwa lugha Kiswahili na lugha zingine za nyumbani kama vile Kichaga, Kipare, Kimasai, Kisukuma n.k Mambo yanayohusiana na lugha ya Kiingereza na ambayo yangeleta maana ya kujifunza Kiingereza, ni vitu kama teknolojia ya watu wa Uingereza, Marekani na sehemu zingine ambazo maudhui yao yanapatikana kwa lugha ya Kiingereza. Mazoezi ambayo wanafunzi wangefanya darasani ambayo yangeleta maana ya kujifunza Kiingereza ni kama vile kutafuta tiketi ya ndege (kwa kawaida zipo kwa lugha ya Kiingereza), katiba ya marekani (ipo kwa Kiingereza), n.k. Hivyo ndivyo wenzetu wanavyojifunza lugha za watu, kikiwemo Kiswahili.

Nakumbusha tena, lengo la kujifunza lugha ya kigeni ni kuweza kuwasiliana na mgeni, siyo kuweza kuwasiliana sisi kwa sisi, sisi tayari tuna lugha na hatuna haja ya kutumia lugha za watu kujielimisha kwa mambo yanayotuhusu. Si akili kuchukua lugha ya mgeni kujielimisha kuhusu mambo yanayotuhusu!!!! Ni kama vile tuseme tutumie lugha ya Kiingereza kuwasiliana hapa JF.

Sidhani kama utanielewa sana lakini nitashukuru kama utaelewa kidogo, elimu bora haimaanishi Kiingereza. Elimu bora ni maudhui. Na ili maudhui hayo yawafikie walengwa, ni laima itolewe kwa lugha inayoeleweka.

Kutumia Kiingereza kunawapa watu majukumu mawili, kujifunza lugha kwanza, halafu kuanza kutafsiri maudhui katika Kiswahili ili kupata ujumbe. Hiyo ni biashara kubwa sana unaipa ubongo, na wachache ndiyo hufanikiwa kufanya biashara hiyo. Wengi wanaishia kukariri na kufaulu mtihani basi.

Kuna uwezekano wa kujifunza lugha ya Kiingereza bila kutoa elimu ya Tanzania inayowahusu watanzania kwa kutumia lugha wanasiyoielewa ya Kiingereza. Lugha inayoeleweka ni Kiswahili, itumike kuelimisha watu.

Faida za kutumia Kiswahili
  1. Ni lugha inayoeleweka hivyo kila mtu atapata fursa ya kupata elimu kwa urahisi zaidi kwani hakutakuwa na haja ya kutafsiri ujumbe kwenda Kiswahili ili kuuelewa.
  2. Mzazi atachangia katika kumuelimisha mtoto. Katika jamii nyingi zilizoendelea, wazazi huanza kuwaelimisha watoto wao wakiwa wachanga kabisa kwa kuwasomea hadithi. Kwa nchi kama Marekani, watoto husomewa hadithi nyingi sana za Kiingereza--lugha wanayoizungumza, vivyo hivyo nchini china, watoto husomewa hadithi nyingi sana za Kichina --lugha wanayoizungumza, Ujerumani vilevile stori za watoto zipo Kijerumani. Hadithi hizi wazazi huwasomea watoto kabla ya kulala, au wawapo katika mapumziko. Hadithi hizi zimejaa elimu. Mbali na kuwa zingine ni stori za maisha tu na kufurahisa, nyingi huwa na masuala yanayohusu tanzu mbalimbali za elimu kama vile sayansi, hesabu, historia, uraia n.k. Mtoto anapoanza kusoma shuleni, elimu ile inakuwa imeunganishwa na hadithi alizozisoma, au waalimu hufundishwa kuunganisha hadithi hizo na masomo ya shuleni. Matokeo yake ni kwamba mzazi anakuwa ameshamjengea mtoto msingi wa elim na kupenda kusoma na msingi huo huendelezwa na walimu. Kwa Tanzania ni vigumu msingi huo kujengwa, kwani hata mzazi angemwanzishia mawanawe kusoma hadithi za Kiswahili (maana wazazi wengi wanaelewa na kusema vizuri Kiswahili zaidi ya Kiingereza--ni vigumu kumsomea mtoto hadithi kwa lugha asiyoijua--hakutakuwa na matunda bora) elimu inakuja kumtenganisha na ule msingi wa alioupata kwa wazazi. Na kifupi tu ni kwamba hata wazazi wenyewe hawaoni haja ya kujenga msingi utakaobomolewa hivyo wamewaacha watoto katika mikono ya walimu kwa kusubiri mtoto akue ampeleke 'English Medium". Hilo ni kosa! Si ujanja ni kosa.
  3. Wazazi wengi wasiyojua Kiingereza watakuwa na uwezo wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao kwani alama zitaandikwa kwa Kiswahili. Wazazi wengi hawawezi kabisa kutoa maoni yao kwa watoto wao kwa kutoelewa hata ripoti inayotumwa kwa mzazi ambayo ipo kwa Kiingereza au matokeo ambayo yamefafanuliwa kwa Kiingereza.
  4. Maudhui yatasadifu lugha. Kama nilivyotangulia kusema, haina maana ya yoyote kujifunza mambo ya wabongo kwa lugha ya kigeni wakati tuna lugha tayari!
Sasa itakuwaje kwa Kiingereza, lugha ambayo ni muhimu kuijua katika dunia ya sasa?

Kama nilivyotangulia kusema, huna haja ya kupata elimu kwa lugha ya Kiingereza ili kukijua Kiingereza. Wachina wanaojifunza Kiingereza kwa muda mfupi na kukizungumza vizuri zaidi yetu hawajakitumia katika elimu, wamejifunza chenyewe kama chenyewe. Hilo ndilo tunalotakiwa tulifanye.

Hatua zifuatazo zichukuliwe:
  1. Kiingereza kifundishwe na watu wazawa wa lugha hiyo, au watu waliofunzwa vizuri na kufikia kukizungumza katika ubora wake. Mara nyingi watu hawa pia lazima wawe wamepata nafasi ya kukizungumza na wazawa mashuleni kwao au kwa kusafiri na kuishi na wazawa wanaotumia lugha ya Kiingereza. Hii itasaidia mtu kusoma Kiingereza sahihi kwa muda mfupi. Kwa sasa Kiingereza ambacho si sahihi kinafundishwa kwa muda mrefu sekondari, vyuoni na mtaani.
  2. Maudhui yalenge nia na madhumuni ya kusoma Kiingereza. Nchini Tanzania, sababu inayotajwa watu kujifunza Kiingereza ni kuweza kuwasiliana na watu wa nje. Kama hiyo ndiyo sababu, basi maudhui yanayotolewa yawe ya nje. Kwa mfano, kama dhumuni ni kufanya mipango ya biashara na watu wa Marekani au Uingereza, mada ambayo inatakiwa iwe kwenye kitabu cha kufundishia Ni kama vile 'MAZUNGUMZO YA KIBIASHARA". Mifano mbalimbali ya mazungumzo ya kibiashara yachukuliwe kutoka kwa watu wa Marekani au Uingereza wakifanya makubaliano ya kibiashara. Misamiati kama "Dollar, Euro," n.k lazima itaonekana kwenye mifano hiyo. Mifano hii inaweza kupatikana mtandaoni kwa urahisi au katika vitabu vinavyotumiwa kufundishia Kiingereza Marekani ama Ulaya.
Jambo lingine:

Umewahi kujiuliza kwanini wazungu wengi wakizungumza wanasimulia hadithi zao za utoto? Yaani si jambo la kushangaza kumsikia mzungu akisema 'When I was a child....'

Ngoja nikupe siri. Katika elimu kuna kitu kinaitwa 'Connection' (Uunganishaji). Unamfundisha mtoto kuunganisha jambo lolote analojifunza darasani na maisha yake ya kawaida. Kwa mfano, unapomfundisha mtoto sheria ya Newton, na kumtaka aikariri lazima umsaidie kuunganisha sheria hiyo na maisha ya kawaida. Mfano mzuri ni kwamba ni huwa nikiwafundisha wanafunzi wangu wa nje za nchi jambo, huniuliza 'Kwa nini ninatakiwa kujua jambo hili?" Hilo ndilo swahili linaloleta 'uunganisho' katika elimu, ama mada, au dhana inayofundishwa. Mwalimu anaposhindwa kujibu swali hilo inaonesha haelewi jambo analolifundisha kwa undani wake. Na si kosa, anaweza kuomba msaada kwa wanafunzi au walimu wenzake.

Elimu ya Tanzania haina UUNGANISHO, imeachana kuanzia suala la lugha mpaka maudhui.
Uko sahihi sana mkuu! Ila tuiongelee tanzania tunapotaka kutumia kiswahili kama lugha ya kufundishia, je kuna mpango gani kukihusu kingereza?

Kwa sababu kwa sasa kingereza sio tu lugha ya muingereza bali ni lugha ya kimataifa,najifunza kingereza sio niende kuwasiliana na muingereza hapana kwa sababu ni lugha ya biashara naweza kukutana na mjapani au mchina na tukafanya biashara tunaweza kutumia kingereza na tukaelewana lakini vipi kama sijui hii lugha? Hata nia tu yakukutana na hawa watu nitakuwa sina.

Ivyo ulivyosema ni sawa kwa aina ya nchi za wenzetu lakini kwa tanzania kufundisha kiswahili tutakuwa tumepoteza sana,
Elimu ni kama itarudi nyuma kwa sababu hata mpango wa hicho kingereza hautakuwepo

Lakini cha kukumbuka sisi tanzania ni maskini tujifunze kiswahili tu tutakuwa nyuma sana tutashindwa kujichanganya na watu wa mataifa,watu wengi wanapata ajira kwa kujua tu kuongea kingereza vizuri

Wasauth waligoma kufundishwa kwa lugha yao kwa sababu kupitia hiyo huwezi kupata ajira ni lazima ujue kingereza
 
Bado kiswahi ni lugha changa haijakamilika kwa uyo itakuwa ngumu tu kwenye iyo mitaala
 
Unaposema Lugha changa unamaanisha nini...!?
Na unaposema haijakamilika... Unazungumzia ukamilifu upi...!?
Kwa mfano somo kama physics, chemistry au biology yatakuwa na maneno mengi ambayo hayapatikani kwa kiswahili chake na maneno mengine ya kiswahili yatawasumbua wanafunzi kwa sababu hawajapata kuyasikia popote pale
 
Kwa maandalizi yapi kimtaala?
Uliwahi kuwaza pia soko la ajira baada ya kujifunzia hii lugha unayoisema?
Wenzetu wamefika walipo kwa kuwa wanajitosheleza ila sisi kwa mfumo wetu wa maisha wa kuunga unga kulazimishwa kusoma kitu ambacho hakitakusaidia maishani ni kurithishana umasikini..wee msomeshe mwanao kwa mfumo unaotaka! Elimu ni huria!
 
Kwa mfano somo kama physics, chemistry au biology yatakuwa na maneno mengi ambayo hayapatikani kwa kiswahili chake na maneno mengine ya kiswahili yatawasumbua wanafunzi kwa sababu hawajapata kuyasikia popote pale
Kwani kabla ya kuanza kusoma hayo maneno ya sayansi... Uliwahi kuyaona wapi...!? Na unataka kusema hayaku kusumbua kipindi unaanza kujifunza...!?

Hio sio sababu... Haina mashiko kabisa. Maneno yapo changamoto ipo kwa watumiaji na utayari wetu wa kutambua kua Kiswahili ni kipana na kinakidhi mahitaji ya kila idara.
 
Kwa maandalizi yapi kimtaala?
Uliwahi kuwaza pia soko la ajira baada ya kujifunzia hii lugha unayoisema?
Wenzetu wamefika walipo kwa kuwa wanajitosheleza ila sisi kwa mfumo wetu wa maisha wa kuunga unga kulazimishwa kusoma kitu ambacho hakitakusaidia maishani ni kurithishana umasikini..wee msomeshe mwanao kwa mfumo unaotaka! Elimu ni huria!
Unapokua tayari kufanya mabadiliko ni lazima ujiandae kufanya hayo mabadiliko na kubadilika pia...!
Mitaala inaandaliwa...
Tunasoma kingereza ni soko lipi Ajira ambalo tunafaidika nalo kupitia hio lugha tuliyojifunzia...!?
 
Unapokua tayari kufanya mabadiliko ni lazima ujiandae kufanya hayo mabadiliko na kubadilika pia...!
Mitaala inaandaliwa...
Tunasoma kingereza ni soko lipi Ajira ambalo tunafaidika nalo kupitia hio lugha tuliyojifunzia...!?

Iliwezekana Ujerumani mtu kusoma kuanzia shule ya awali hadi ngazi ya ubobezi kwa kuwa tu walikuwa na miundombinu rafiki na uhakika wa kufanyia kazi kile walichojifunzia nyumbani!
Ni vitabu vingapi vya kiada na ziada mmeandaa kwa lugha ya kiswahili na ni namna gani mmeweka motisha kwa walimu na maslahi ili kazi ya ualimu wasifanye wale waliokosa kazi nyingine? Na kwa utafiti wako unahisi soko la ajira kwa mfumo huu wa serikali isiyoendeshwa kitaasisi utakuwaje?
Tuache kupotosha ukweli,kiswahili kibaki Lugha ya kutongozea na kuandika barua za posa tu,ila lugha za kigeni zitumike kutafutia mbinu za kujikwamua kwa kujumuika na walimwengu kwenye majukwaa ya kimataifa!
 
Kwa nini Kiingereza kilichaguliwa kuwa lugha ya kufundishia? Je, wale wanafunzi wa mwanzo toka enzi ya mkoloni wazazi wao walikuwa wanajua Kiingereza (ingawaje walikuwa wana kaa bweni lakini walikuwa wanaenda likizo na mpaka siku hizi kuna bweni). Je, kwa nini kipindi kile cha marehemu Jackson Makweta kama sikosei serikali ilitangaza kubadili lugha ya kufundishia kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili lakini mpaka leo kitu hicho hakijawahi kutekelezwa. Haya sera ya elimu ya juzi imesema tu na kiswahili kitatumika kufundishia basi tusubiri tuone.

Kama kweli wazazi wanataka watoto wao waelimike basi ni lazima wajifunze lugha ya Kiingereza na watoto watie bidii kujifunza lugha hiyo ili waelimike. Je, wanafunzi wanaofaulu wakati wamefundishwa kwa Kiingereza wanatumia mbinu gani? Au maelezo yake yakoje? Maana yake wewe umetupa maelezo ya wanaofeli tu.
 
Kwa nini Kiingereza kilichaguliwa kuwa lugha ya kufundishia? Je, wale wanafunzi wa mwanzo toka enzi ya mkoloni wazazi wao walikuwa wanajua Kiingereza (ingawaje walikuwa wana kaa bweni lakini walikuwa wanaenda likizo na mpaka siku hizi kuna bweni). Je, kwa nini kipindi kile cha marehemu Jackson Makweta kama sikosei serikali ilitangaza kubadili lugha ya kufundishia kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili lakini mpaka leo kitu hicho hakijawahi kutekelezwa. Haya sera ya elimu ya juzi imesema tu na kiswahili kitatumika kufundishia basi tusubiri tuone.

Kama kweli wazazi wanataka watoto wao waelimike basi ni lazima wajifunze lugha ya Kiingereza na watoto watie bidii kujifunza lugha hiyo ili waelimike. Je, wanafunzi wanaofaulu wakati wamefundishwa kwa Kiingereza wanatumia mbinu gani? Au maelezo yake yakoje? Maana yake wewe umetupa maelezo ya wanaofeli tu.
Jamani kujua kuzungumza kingereza haina maana ndio umeelimika jamani.

Tatizo lilopo katika kuratibu na kutekeleza mipango ya kukipa nguvu kiswahili kufundishia ni sisi wenyewe... Ni dhana potofu kusema kudhani kingereza ndio kigezo cha kuelimika.
 
Iliwezekana Ujerumani mtu kusoma kuanzia shule ya awali hadi ngazi ya ubobezi kwa kuwa tu walikuwa na miundombinu rafiki na uhakika wa kufanyia kazi kile walichojifunzia nyumbani!
Ni vitabu vingapi vya kiada na ziada mmeandaa kwa lugha ya kiswahili na ni namna gani mmeweka motisha kwa walimu na maslahi ili kazi ya ualimu wasifanye wale waliokosa kazi nyingine? Na kwa utafiti wako unahisi soko la ajira kwa mfumo huu wa serikali isiyoendeshwa kitaasisi utakuwaje?
Tuache kupotosha ukweli,kiswahili kibaki Lugha ya kutongozea na kuandika barua za posa tu,ila lugha za kigeni zitumike kutafutia mbinu za kujikwamua kwa kujumuika na walimwengu kwenye majukwaa ya kimataifa!
Aisee.... Umeamua kabisa kuzuia ubongo wako kufikiria mazuri ya Kutumia Lugha yetu ya Kiswahili (sio dhihaka)

Maandili ya kufanya kitu lazima yawe na upana wake utakao weza kweli kukidhi mahitaji ya mpango husika.

Tutakapo amua kweli kutumia kiswahili maana yake tutajiandaa wa kila nyanja.. Kuandaa vitabu, mitaala na mazingira bora ya wanafunzi kutumia hiko kiswahili. Hii ni mipango.. Wataalamu tunao tatizo ni uvivu wetu na ufinyu wa kukubali mabadiliko.

Tunatumia kingereza lakini bado watoto wanafika kidato cha nne wengine hawawezi kusoma vitabu, wala kuandika hicho kingereza... Em jaribu kufikiria tukitumia lugha ambayo mtu ana ustadi nayo.

Soko la Ajira linatengenezwa na kuandaliwa kwani hata leo tunatumia hicho kingereza lakini bado kuna tatizo la soko hilo la ajira.

Kuhusu mawasiliano na wageni kutoka mataifa hayo.. Ni mipango tu katika sera zetu za elimu na nchi... Tutakapo kua na mikakati madhubuti ya kimaendeleo watakao vutiwa na sisi ni lazima watasoma lugha yetu.
Vivo hivyo pia kwenye elimu... Kingereza kibaki kua somo na kifundishwe na wataalamu kweli walio somea lugha hio sio kwamba kisifundishwe kabisa.

Kiswahili kinakua katika nchi za kigeni kuliko kwetu... Vyuo vingi vinakifundisha...

Tunasingizia kwamba lugha yetu haijakamilika sijui ni changa sijui haina misamiatu...

HAPANA: Ni uvivu wetu wa kukubali mabadiliko ambayo hatutaki kuamini kama kweli tunaweza kufanikiwa kwasababu hutujiamini wala kithamini vilivyo vya kwetu.
 
Jamani kujua kuzungumza kingereza haina maana ndio umeelimika jamani.

Tatizo lilopo katika kuratibu na kutekeleza mipango ya kukipa nguvu kiswahili kufundishia ni sisi wenyewe... Ni dhana potofu kusema kudhani kingereza ndio kigezo cha kuelimika.

Mbona somo la Kiswahili kwenye continuous assessments na matokeo ya mwisho wanafunzi na wahitimu wote hawapati A wakati wanazungumza Kiswahili halafu kati yao wanafaulu vizuri Kiingereza kama somo.
 
Nakubali. Nchi kama Uswidi, Uholanzi, Ujerumani watoto wote husoma kwa lugha ya kitaifa hadi chuo kikuu; Kiingereza wanasoma kama lugha ya kigeni hata hivyo watu wengi wanaelewa Kiingereza vema kushinda wanafunzi wa Tanzania wanaojaribu kusoma kwa Kiingereza kama lugha ya mafundisho. Na matokeo ni afadhali kwa masomo yote.
Usiifananishe German na nchi za kishenzi....
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom