Elections 2010 Umuhimu wa Kikwete kwenye Historia ya Tanzania baada ya Nyerere

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,546
19,407
Nyerere anakumbukwa kwa mengi katika historia ya Tanzania, lakini kubwa linalomtofautisha na maraisi wenzie ni kuwa aliondoka madarakani wakati angeliweza kuendelea, ukimwacha Abdul Wakil wa Zanzibar. Baada ya hapo maraisi wote waliomfuatia Nyerere wamekuwa wanaondoka madarakani kwa mujibu wa katiba baada ya kutawala kwa miaka kumi, na kuna waliojaribu kuongezea muda huo.

Nadhani Kikwete anaweza kuja kukumbukwa sana kama rais wa kwanza Tanzania kuachia madaraka hayo kwa hiari baada ya kutopata kura za kutosha; yaani hakupenda kutumia madaraka hayo vibaya kujiongezea muda wa kutawala kama alivyofanya Kibaki na Mugabe.
 
Nyerere anakumbukwa kwa mengi katika historia ya Tanzania, lakini kubwa linalomtofautisha na maraisi wenzie ni kuwa aliondoka madarakani wakati angeliweza kuendelea, ukaiachilia Abdul Wakil wa Zanzibar. Baada ya hapo maraisi wote waliomfuatia wamekuwa wanaondoka madarakani kwa mujibu wa katiba baada ya kutawala kwa miaka kumi, na kuna waliojaribu kuongezea muda huo.

Nadhani Kikwete anaweza kuja kukumbukuwa sana kama rais wa kwanza Tanzania kuachia madaraka hayo kwa hiari baada ya kutopata kura za kutosha; yaani hakupenda kutumia madaraka hayo vibaya kujiongezea muda wa kutawala kama alivyofanya Kibaki na Mugabe.

Gud one!
 
Ndoto za Ali Nacha. :becky: :becky: :becky:

Mara nyingi ndoto kama hizi husababishwa na kuvimbiwa na ugali wa muhogo kwa matembele. :becky: :becky: :becky:
 
Ndoto za Ali Nacha. :becky: :becky: :becky:

Mara nyingi ndoto kama hizi husababishwa na kuvimbiwa na ugali wa muhogo kwa matembele. :becky: :becky: :becky:

Kwa hiyo unamaanisha kikwete hawezi kuachia madaraka kwa hiari asipopata kura za kutosha? basi kama hataachia kwa hiari ataachishwa kwa nguvu
 
Si mpaka hizo kura zisitoshe? :tonguez:
Kudadeki, Mkuu ushabiki wako usio na reasoning unafurahisha! Bila shaka unajua mbinu mtakazotumia ili kura za Dk. Slaa zisitoshe kwa sababu mna record ya kufanya hivyo. Pia hata kama Dk. Slaa atampita kwa kura nyingi mgombea wenu kwenye baadhi ya maeneo bado hamtaridhika mtataka mzipunguze! Halafu mnatamba kwamba mmeimarisha/mnaimarisha demokrasia nchini. Shame on you! Kitu kinachonifurahisha katika uchaguzi huu ni kuona idadi imeongezeka ya wananchi wenye uelewa wa kisiasa.
 
Back
Top Bottom