Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,000
- 9,861
Jeshi la Polisi ipo kwa lengo la kuwahakikishia wananchi usalama wao na mali zao kudumisha amani na utulivu katika jamii
Pia jeshi la polisi lipo ili kubaini na kupambana na uhalifu. Jeshi la Polisi lipo ili kuhakikisha kila mtu anafuata sheria kila hatua
Kwa Tanzania kuna Jeshi moja la Polisi ambalo lina vikosi, idara na vitengo mbalimbali kama vile vikosi kikosi cha kutuliza ghasia, kikosi cha usalama barabarani, idara ya upelelezi nk
Kulingana na sheria ya Jeshi la Polisi kuna askari polisi wasaidizi ambao wana uwezo wa kipolisi wa kupekua na kukamata. Wakikamata mtu wanawajibika kumkabidhi kwa polisi au kituo cha polisi
Sasa kuna wahuni watakuja kupinga halafu wakidhulumiwa au kupata majanga wanakimbilia polisi,
Nakumbuka westgate kuna watu walijificha nyuma ya polisi ili kuokoa uhai wao.
Sasa wewe unayekuja kuponda jiulize, ikitokea mmevamiwa na wahalifu wenye silaha huwa mnawaza nini cha kwanza, chukulia matukio kama ya kuvamiwa benki au kuibiwa hela na vibaka
MAMLAKA YA POLISI
Jeshi la polisi lina mamlaka mbalimbali yaliyowekwa kisheria na linapaswa kutumia mamlaka kulingana na taratibu zilizoainishwa katika sheria husika
Polisi wanaweza kukamata, kufanya upekuzi, kushikilia, kumpeleleza mtuhumiwa, kumhoji shahidi na kufanya mahojiano na mtuhumiwa
Pia Kutawanya waandamanaji wenye nia ovu na kuhakikisha usalama katika jamii. Hawafanyi wapendavyo bali hufuata sheria
Matumizi yoyote ya mabaya ya mamlaka au uzembe katika kazi unapelekea utovu wa nidhamu na uhalifu, afisa wa polisi anayetenda hayo anapaswa kuchukuliwa hatua
Pia jeshi la polisi lipo ili kubaini na kupambana na uhalifu. Jeshi la Polisi lipo ili kuhakikisha kila mtu anafuata sheria kila hatua
Kwa Tanzania kuna Jeshi moja la Polisi ambalo lina vikosi, idara na vitengo mbalimbali kama vile vikosi kikosi cha kutuliza ghasia, kikosi cha usalama barabarani, idara ya upelelezi nk
Kulingana na sheria ya Jeshi la Polisi kuna askari polisi wasaidizi ambao wana uwezo wa kipolisi wa kupekua na kukamata. Wakikamata mtu wanawajibika kumkabidhi kwa polisi au kituo cha polisi
Sasa kuna wahuni watakuja kupinga halafu wakidhulumiwa au kupata majanga wanakimbilia polisi,
Nakumbuka westgate kuna watu walijificha nyuma ya polisi ili kuokoa uhai wao.
Sasa wewe unayekuja kuponda jiulize, ikitokea mmevamiwa na wahalifu wenye silaha huwa mnawaza nini cha kwanza, chukulia matukio kama ya kuvamiwa benki au kuibiwa hela na vibaka
MAMLAKA YA POLISI
Jeshi la polisi lina mamlaka mbalimbali yaliyowekwa kisheria na linapaswa kutumia mamlaka kulingana na taratibu zilizoainishwa katika sheria husika
Polisi wanaweza kukamata, kufanya upekuzi, kushikilia, kumpeleleza mtuhumiwa, kumhoji shahidi na kufanya mahojiano na mtuhumiwa
Pia Kutawanya waandamanaji wenye nia ovu na kuhakikisha usalama katika jamii. Hawafanyi wapendavyo bali hufuata sheria
Matumizi yoyote ya mabaya ya mamlaka au uzembe katika kazi unapelekea utovu wa nidhamu na uhalifu, afisa wa polisi anayetenda hayo anapaswa kuchukuliwa hatua