Umuhimu au faida ya kutokuwepo upinzani kutaonekana miaka 5 ijayo

Dogo Lao

Member
Nov 2, 2011
94
38
Na ashukuriwe Mungu muumba mbingu na nchi, Ndg. zangu wana JF, Asalamualeykhum.

Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu, kwa rehema zake na wema wake hata tumeweza kuiona siku ya leo. Ndugu zangu, sote tunajua jinsi mchakato wa uchaguzi unavyokuwa mgumu. Siyo kwa wagombea tu, bali hata kwa wanaowaunga mkono. Pamoja na ushindani mkubwa uliojitokeza ktk uchaguzi wa mwaka huu, hatimaye Rais ametangazwa.

Kwani ni siri? Siyo siri, ni dhahiri kuwa CCM imeshinda kwa mujibu wa Tume ya uchaguzi. Yaliyopo nyuma ya ushindi huo siyo kazi yangu kuyasema, ila yaliyoonekana yameonekana, na yaliyosikika kama uvumi yamesikika. Mwisho wa siku tunasema CCM imeshinda kwa kishindo kikuu, upinzani umekosa ridhaa kwa wananchi.

Sasa, miaka 5 ni dhamana ya Chama Cha Mapinduzi. Katika kipindi cha miaka 5 inayokuja ndipo tutajua, Upinzani ulikuwa una umuhimu wake ama haukuwa na umuhimu wowote.

Muda ni mwalimu mzuri.
 
Hakukuwa na ushindani wowote maana kuna walioiipanga tena vzr tuu. Haya matokeo hayaoneshi ushindani labda sijui maana ya ushindani.
 
Tuombe busara,weledi na hofu ya Mungu iwepo kwa viongozi la sivyo kiburi ,dharau na uonevu utatawala na matumizi mabaya ya madaraka yataondoa uwezo wa wananchi na washauri katika kushauri,kusimamia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.
 
Hakuna jipya sana sana serikali itachukia nchi matajiri za western. Itakomaza urafiki na China au Russia. Kuna hatari ya kuwekewa vikwazo kama ilivyokuwa kwa Zimbabwe. Private companies zitakufa maana zitaendelea kutopewa kazi. Mishahara ndo msahau kabisa kuongenzwa. Ajira ndo kabisa. Magufuli hana cha kuogopa tena.Aliogopa na kukerwa na maneno ya wapinzani bungeni. Sasa hawana kinga tena.wakiongea nje atawasweka ndani. Na mtaona ataapishwa faster maana naona leo kina Mbowe wameiitisha maandamano. Ataapishwa ili awashughulikie mapema. Leo ndo nimeamini kuwa Magufuli ni mhutu hawa watu wana roho mbaya sana.
 
Back
Top Bottom