Umri wa kustaafu unawahusu watumishi wa umma pekee au pamoja na viongozi wote wa serikali, mahakama, bunge?

Salvatory Mkami

Senior Member
Apr 17, 2013
146
244
Umri wa kustaafu unawahusu watumishi wa umma pekee au pamoja na viongozi wote wa serikali, Mahakama, Bunge na Wabunge?!

Sheria zetu zinasemaje?!

Kwasababu kituko kitakuwa ni pale ambapo anayetoa taarifa kuhusiana na wale ambao wameghushi vyeti vya kuzaliwa na umri wao ili waendelee kudumu kwenye ajira na yeye mwenyewe akiwa mmoja kati ya wanaotakiwa kustaafu kwa lazima kutokana na umri wake wa kustaafu kuwa umepita kwa miaka kadhaa!

Ifike wakati kama serikali inamaanisha na imeamua katika kweli kulivalia njuga suala la ukomo wa ajira husiana na suala la ukomo wa ajira serikalini kwa maana ya mtumishi, kiongozi kustaafu kwa hiyari au kwa lazima iwe hivyo kwa nafasi zote na sio kwa baadhi ya sekta pekee ilihali sekta nyingine zikifumbiwa macho!

Pia ili kutoa nafasi kwa vijana na fikra mpya katika kuliendeleza taifa kuna haja kubwa ya kuweka ukomo kwa wagombea na wanaoteuliwa kwa nafasi za Ubunge, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu, Wakurugenzi nk. Kwa utaratibu huo tutakuwa tunatekeleza kwa vitendo kile tunachokimaanisha lakini kinyume na hapo ni kama tutakuwa tunaenda mbele hatua tano na kurudi nyuma hatua kumi na kujipongeza!
 
Mbona bashite alikuwa sifuri lakini tukaambiwa mkuu wa mkoa elimu si lazma ni kama vile dereva wa mbunge lazima afike fomu IV lakini mbunge mwenyewe ajue Vowels only afu watu wanasubir viwanda! Usije ambiwa umri hauwagusi politicians kikongwe kama kuchi nae mvi kila kona anathubutu kuzungumzia umri?
 
Ha ha ha! Umenikumbusha issue ya maprofesa. Siku za nyuma walianzisha ka-movement kao eti kutokana na umuhimu wao umri wao wa kustaafu usogezwe hadi 70. Cha ajabu wanapokuwa kwenye masuala yahusuyo maslahi yao hupenda sana haka kamsemo "kazi ya kufundisha ni ngumu na inachosha sana" lakini cha kushangaza hao hao wanaodai kazi ya ni ngumu sana walikuwa wanataka waongezewe kazi hadi miaka 70; what a contradiction! Anyway, sikujisumbua kufuatilia kujua kama waliongezewa au la!
 
  • Thanks
Reactions: a45
...
Ifike wakati kama serikali inamaanisha na imeamua katika kweli kulivalia njuga suala la ukomo wa ajira husiana na suala la ukomo wa ajira serikalini kwa maana ya mtumishi, kiongozi kustaafu kwa hiyari au kwa lazima iwe hivyo kwa nafasi zote na sio kwa baadhi ya sekta pekee ilihali sekta nyingine zikifumbiwa macho!
...
Nasikia makoplo wao ni miaka 45 kwaheri. Maafisa wao wanakula bata hadi 60's na mabingwa wa kujipendekeza kungali mapema wanapiga shavu hadi 70 kupitia "teuzi". Hiki kitu huwa sikielewi.
 
Ha ha ha! Umenikumbusha issue ya maprofesa. Siku za nyuma walianzisha ka-movement kao eti kutokana na umuhimu wao umri wao wa kustaafu usogezwe hadi 70. Cha ajabu wanapokuwa kwenye masuala yahusuyo maslahi yao hupenda sana haka kamsemo "kazi ya kufundisha ni ngumu na inachosha sana" lakini cha kushangaza hao hao wanaodai kazi ya ni ngumu sana walikuwa wanataka waongezewe kazi hadi miaka 70; what a contradiction! Anyway, sikujisumbua kufuatilia kujua kama waliongezewa au la!
Double standard kui avoid aisee ni ngumu sana afu nimecheka sana kuhusu hao maprofesa
 
Ifike wakati Serikali iache double standard zisizo na kichwa wala miguu! Huku sheria zinakubali halafu kule sheria zinakataza. Huku mtanzania huyu anaruhusiwa hiki kule Mtanzania yule haruhusiwi kilekile ilihali ni ndani ya nchi ileile Katiba ileile na raia walewale halafu bado kuna watu hawaoni kwamba Katiba ya nchi haiendani na mahitaji, imepitwa na wakati!
 
Wewe!ishia hapo hapo utaambiwa,acha kazi iishe kwanza,ila kwa sasa pambana kwanza na hali yako.Najuwa mazao...
 
Umri wa kustaafu unawahusu watumishi wa umma pekee au pamoja na viongozi wote wa serikali, Mahakama, Bunge na Wabunge?!

Sheria zetu zinasemaje?!

Kwasababu kituko kitakuwa ni pale ambapo anayetoa taarifa kuhusiana na wale ambao wameghushi vyeti vya kuzaliwa na umri wao ili waendelee kudumu kwenye ajira na yeye mwenyewe akiwa mmoja kati ya wanaotakiwa kustaafu kwa lazima kutokana na umri wake wa kustaafu kuwa umepita kwa miaka kadhaa!

Ifike wakati kama serikali inamaanisha na imeamua katika kweli kulivalia njuga suala la ukomo wa ajira husiana na suala la ukomo wa ajira serikalini kwa maana ya mtumishi, kiongozi kustaafu kwa hiyari au kwa lazima iwe hivyo kwa nafasi zote na sio kwa baadhi ya sekta pekee ilihali sekta nyingine zikifumbiwa macho!

Pia ili kutoa nafasi kwa vijana na fikra mpya katika kuliendeleza taifa kuna haja kubwa ya kuweka ukomo kwa wagombea na wanaoteuliwa kwa nafasi za Ubunge, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu, Wakurugenzi nk. Kwa utaratibu huo tutakuwa tunatekeleza kwa vitendo kile tunachokimaanisha lakini kinyume na hapo ni kama tutakuwa tunaenda mbele hatua tano na kurudi nyuma hatua kumi na kujipongeza!
Katiba mpya inatakiwa kuanisha yote hayo ikiwamo kurejea nguvu anayopewa rais kutuamulia maswala nyeti ktk nchi yetu.
 
Umri wa kustaafu unawahusu watumishi wa umma pekee au pamoja na viongozi wote wa serikali, Mahakama, Bunge na Wabunge?!

Sheria zetu zinasemaje?!

Kwasababu kituko kitakuwa ni pale ambapo anayetoa taarifa kuhusiana na wale ambao wameghushi vyeti vya kuzaliwa na umri wao ili waendelee kudumu kwenye ajira na yeye mwenyewe akiwa mmoja kati ya wanaotakiwa kustaafu kwa lazima kutokana na umri wake wa kustaafu kuwa umepita kwa miaka kadhaa!

Ifike wakati kama serikali inamaanisha na imeamua katika kweli kulivalia njuga suala la ukomo wa ajira husiana na suala la ukomo wa ajira serikalini kwa maana ya mtumishi, kiongozi kustaafu kwa hiyari au kwa lazima iwe hivyo kwa nafasi zote na sio kwa baadhi ya sekta pekee ilihali sekta nyingine zikifumbiwa macho!

Pia ili kutoa nafasi kwa vijana na fikra mpya katika kuliendeleza taifa kuna haja kubwa ya kuweka ukomo kwa wagombea na wanaoteuliwa kwa nafasi za Ubunge, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu, Wakurugenzi nk. Kwa utaratibu huo tutakuwa tunatekeleza kwa vitendo kile tunachokimaanisha lakini kinyume na hapo ni kama tutakuwa tunaenda mbele hatua tano na kurudi nyuma hatua kumi na kujipongeza!
Anazaidi ya miaka 80, shame CCM.
 
Back
Top Bottom