Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT): Je ni halali kwa chama cha siasa kujimilikisha hili jina?

everybody

JF-Expert Member
Oct 30, 2010
337
103
Hivi ni halali hii jumuiya kuitwa "UWT" kama ni kwa ajili ya wanawake wa CCM tu? Nafikiri kuna umuhimu wa kuibadilisha jina iwe "umoja wa wanawake wa CCM Tanzania" ili UWT litumike pale kutakapokuwa na jumuiya au umoja wa wanawake usiokuwa na linkage to any political party. Nafikiri lengo kuu la kuanzishwa UWT lilikuwa hilo sasa CCM wamehama na jina kama lilivyo wakati UWT ilitakiwa kuwa ya wanawake wote na sio wa CCM tu.
 
Mkuu umeneno na umefikiri vema, mambo hayo yalianziswa kipindi cha chama kimoja I mean before multpartism 1992 in TZ.
siyo haki yao na wala hawasitahili, ila naona kulitengea hili jina ni issue may be wadau wa Law jamvini watatusaidia, huo ni ufisadi
The correct one is umoja wa wanawake CCM
UW-CCM kama Wanavyotumia UV-CCM
Katiba mpya Tunahitaji bado tunafikira za chama kimoja
 
Nakubaliana nawe! Si haki wanawake wasisiemu wachukue jina linalotuwakilisha wanawake wote!

Wajiite UW-CCM kama ilivyoshauriwa hapo juu!

Tunahitaji ushauri; tufanyaje kupigia kelele hili?
To start ngoja nimpigie Ananilea Nkya.
 
Nakubaliana nawe! Si haki wanawake wasisiemu wachukue jina linalotuwakilisha wanawake wote!

Wajiite UW-CCM kama ilivyoshauriwa hapo juu!

Tunahitaji ushauri; tufanyaje kupigia kelele hili?
To start ngoja nimpigie Ananilea Nkya.
YES!
Nkya anafaa vp majibu yake tunakutegemea mkuu, wanasheria JF mnasemaje?
 
Nahisi hawakuwaza kama kutakua na wanawake watakao sio wanachama wa CCM... Ni makosa ya kiutunzi katika kutunga jina na inashangaza kuona watu tulikua hatudoubt
Asante sana everybody kwa kutufungua macho!..
 
Nakwambieni mambo ya Chama kimoja utata mtupu, CCM sio tu wanamiliki UWT, Viwanja vya mipira nk bali wanajiona na ndiyo ilivyo kwamba wanamiliki hadi nchi, serikali na uhuru wa 1961. Hawa watu ni necessity kwanza kuwang'oa ili kurudisha hali nzuri ya hewa, maana nchi inakoelekea ni ushuzi mtupu!
 
Nahisi hawakuwaza kama kutakua na wanawake watakao sio wanachama wa CCM... Ni makosa ya kiutunzi katika kutunga jina na inashangaza kuona watu tulikua hatudoubt
Asante sana everybody kwa kutufungua macho!..

Gamba kuvuka mchezo! Ngoja tutiane adabu kwanza! Tuwabadilishie kibao wao wakalime sie tushike serikali tuwaongoze!
 
YES!
Nkya anafaa vp majibu yake tunakutegemea mkuu, wanasheria JF mnasemaje?

She is driving home; will call her after an hour to discuss more on the issue! Lkn kifupi; naye anaona si haki after vyama vingi, though anasema ni ngumu kuwalazimisha!
 
Hivi ni halali hii jumuiya kuitwa "UWT" kama ni kwa ajili ya wanawake wa CCM tu? Nafikiri kuna umuhimu wa kuibadilisha jina iwe "umoja wa wanawake wa CCM Tanzania" ili UWT litumike pale kutakapokuwa na jumuiya au umoja wa wanawake usiokuwa na linkage to any political party. Nafikiri lengo kuu la kuanzishwa UWT lilikuwa hilo sasa CCM wamehama na jina kama lilivyo wakati UWT ilitakiwa kuwa ya wanawake wote na sio wa CCM tu.

Vyeti fake, chama chenyewe fake (ccm haijasajiliwa), na sasa UWT wanadai wanawakilisha wanawake wote tz? fake fake fake!
 
Si unajua enzi za chama kimoja kila kitu kilifanywa mali ya CCM badala ya kuwa mali ya watanzania ...akina JUWATA,NUTA n.k,nashangaa sana kuona UWT unamilikiwa na CCM ingali wanawake wa Tanzania wamo kwenye vyama vya siasa tofauti

Na labda ndo maana wanawake wanafeli kusimamia ajenda zao maana unapoitwa UWT hushinda na sare za chama na hatimaye hujadili siasa za chama badala ya kujadili mambo yao ya msingi na familia zao,kweli wanatumiwa kotekote.


Akina mama amkeni,acheni kutumika visivyo
 
Hivi ni halali hii jumuiya kuitwa "UWT" kama ni kwa ajili ya wanawake wa CCM tu? Nafikiri kuna umuhimu wa kuibadilisha jina iwe "umoja wa wanawake wa CCM Tanzania" ili UWT litumike pale kutakapokuwa na jumuiya au umoja wa wanawake usiokuwa na linkage to any political party. Nafikiri lengo kuu la kuanzishwa UWT lilikuwa hilo sasa CCM wamehama na jina kama lilivyo wakati UWT ilitakiwa kuwa ya wanawake wote na sio wa CCM tu.

Hpana. Nakataa. Hilo ni jina tu sawa na majina mengine ya vyama kama Tanzania labour party( TLP) yaani ni chama cha wafanyakazi Tanzania lakini sio chama cha wafanya kazi. Kinachoangaliwa sio maana ya jina bali ni malengo ya chama chenye jina hilo.
Jamani kama ni siasa tufanye lakini uko sasa tumezidisha ni zaidi ya siasa.
 
Hpana. Nakataa. Hilo ni jina tu sawa na majina mengine ya vyama kama Tanzania labour party( TLP) yaani ni chama cha wafanyakazi Tanzania lakini sio chama cha wafanya kazi. Kinachoangaliwa sio maana ya jina bali ni malengo ya chama chenye jina hilo.
Jamani kama ni siasa tufanye lakini uko sasa tumezidisha ni zaidi ya siasa.

Hawa watu wanachekesha kweli
 
Hapa sasa wakina mama wafungue macho. Hii ni nafasi yao wote bila kuwa na itikadi yeyote kutokana jina lilivyo. Wanawawake wote ambao ni wabunge wa upinzani washikiane wapeleke mjadala bungeni na hii ngoma ianzie huku umma utasikiliza majibu yatayotolewa. Lengo ni kukiacha hiki chombo kiwe huru zaidi kwa akina mama bila ubaguzi, au itikadi ya siasa.
 
Hpana. Nakataa. Hilo ni jina tu sawa na majina mengine ya vyama kama Tanzania labour party( TLP) yaani ni chama cha wafanyakazi Tanzania lakini sio chama cha wafanya kazi. Kinachoangaliwa sio maana ya jina bali ni malengo ya chama chenye jina hilo.
Jamani kama ni siasa tufanye lakini uko sasa tumezidisha ni zaidi ya siasa.

Sikubaliani na wewe kwenye hili. Huwezi kufananisha UWT na TLP. TLP iliundwa specifically kama sehemu ya vyama vingi. Ila UWT ilikuwa na lengo la kuwaunganisha wanawake wote na ilianzishwa wakati fikra za vyama vingi hazikuwepo. Ilitakiwa ulivyoingia mfumo wa vyama vingi CCM iangalie na kuchuja kipi ni cha wananchi wote na kipi ni kwa ajili ya CCM kama chama. Ingetakiwa waunde umoja mpya ambao ungewahusisha wanawake wa CCM tu na waiache UWT iwe kwa wanawake wote wanaotaka kuunganika bila kuangalia itikadi ya chama.
 
Si unajua enzi za chama kimoja kila kitu kilifanywa mali ya CCM badala ya kuwa mali ya watanzania ...akina JUWATA,NUTA n.k,nashangaa sana kuona UWT unamilikiwa na CCM ingali wanawake wa Tanzania wamo kwenye vyama vya siasa tofauti

Na labda ndo maana wanawake wanafeli kusimamia ajenda zao maana unapoitwa UWT hushinda na sare za chama na hatimaye hujadili siasa za chama badala ya kujadili mambo yao ya msingi na familia zao,kweli wanatumiwa kotekote.


Akina mama amkeni,acheni kutumika visivyo
Hapo kwenye blue, tulishaamka zamani tupo BAWACHA siku hizi, huko UWT wenye kuona mbali tulishawatosa
 
Mkuu umeneno na umefikiri vema, mambo hayo yalianziswa kipindi cha chama kimoja I mean before multpartism 1992 in TZ.
siyo haki yao na wala hawasitahili, ila naona kulitengea hili jina ni issue may be wadau wa Law jamvini watatusaidia, huo ni ufisadi
The correct one is umoja wa wanawake CCM
UW-CCM kama Wanavyotumia UV-CCM
Katiba mpya Tunahitaji bado tunafikira za chama kimoja

Pompo Umenena vyema

Kwanza kwa mujibu wa usajili wa vyama vingi ccm ni batili kama kuwa upc na anc majina ya vya siasa vilivyokuwepo kabla kuanzishwa vyama vingi.

Majengo ya serikali ya kata

Majengo yaliyogharimiwa na serikali

Viwanja vya mpira

Jumuia zilizokuwa za kitaifa kama uwt na otu (Mgogoro wa bawata)

Kuna uhuni ulifanyika wakati wa kuanzisha vyama vingi, na hii ni matokeo tu:smow:
 
Hivi ni halali hii jumuiya kuitwa "UWT" kama ni kwa ajili ya wanawake wa CCM tu? Nafikiri kuna umuhimu wa kuibadilisha jina iwe "umoja wa wanawake wa CCM Tanzania" ili UWT litumike pale kutakapokuwa na jumuiya au umoja wa wanawake usiokuwa na linkage to any political party. Nafikiri lengo kuu la kuanzishwa UWT lilikuwa hilo sasa CCM wamehama na jina kama lilivyo wakati UWT ilitakiwa kuwa ya wanawake wote na sio wa CCM tu.

Mkuu jina hili lilipaswa liwe limekwishabadilishwa mkuu maana lilianzishwa enzi kukiwa na mfumo wa chama kimoja cha siasa ambapo wanawake waliunganishwa chini ya Jumuiya hiyo na ndo maana ya kuwepo UWT,UVCCM,Jumuiya ya Wazazi tanzania na kadhalika. Wanawake wa wakati huo walipaswa au ilikuwa ni lazima wawe wanachama wa jumuiya hii au ina maana kuwa mwanachama wa CCM. na iwapo hukuwa mwanachama wa CCM hukuwa na shirika na jumuiya hii au masuala yanayowahusu wanawake japo walikuwepo ambao hawakuwa wanachama wa CCM wala jumuiya hii
ili kuendana na mfumo wa sasa ambapo kuna vyama vingi na wanawake wanapaswa wawe na chombo huru au wawe huru kujiunga na chama chochote na kuunda mabaraza yao ambayo yatawatetea haki zao. Kwa kuwa wako huru jina kama hili haliunganishi tena wanawake wa tanzania kwa hiyo lilipaswa nalo libadilike na liwe UW-CCM yaani umoja wa wanawake wa CCM

Mnakumbuka miaka ya kati au mwishoni wa 80 kulikuwa na baraza moja lilianzishwa na ambaye ni Waziri wa Ardhi wa sasa ambalo lilikuwa linaitwa BAWATA (Baraza la Wanawake Tanzania) ambalo lilianzishwa kuwaunganisha wanawake wote wa tanzania bila kujali kuwa wako kwenye chama cha siasa au hawapo

Baraza hili ndilo lilikuwa na sura ya utaifa maana halikuhusisha wanaCCM peke yao japo wakati huo CCM ndio ilikuwa madarakani ila liliunganisha wanawake wote bila kujali kama ni wapenzi wa chama tawala au sio japo baadae nalo lilikuja kupigwa marufuku na kufutwa katika utawala wa Mzee Mwinyi na rufaa yake kuja kusikilizwa na kuamuliwa miaka ya karibuni japo nguvu na utashi na madhumuni yake yalishapotea. Lilianza vyema sana ila kutokana na siasa za chama kimoja za wakati huo lilionekana kutaka kukipiku chama tawala na watawala wakaona ni bora walipige marufuku
Ninalotaka kusema hapa ni kuwa kwa CCM hilo jina wanapaswa walibadilishe maana halina sura ya utanzania tena kama lilivyokuwa mwanzoni kuwa ni kiunganishi cha wanawake wote wa tazania na kwa sasa liwe ni la jumuiya ya wanawake wa CCM
 
Hivi ni halali hii jumuiya kuitwa "UWT" kama ni kwa ajili ya wanawake wa CCM tu? Nafikiri kuna umuhimu wa kuibadilisha jina iwe "umoja wa wanawake wa CCM Tanzania" ili UWT litumike pale kutakapokuwa na jumuiya au umoja wa wanawake usiokuwa na linkage to any political party. Nafikiri lengo kuu la kuanzishwa UWT lilikuwa hilo sasa CCM wamehama na jina kama lilivyo wakati UWT ilitakiwa kuwa ya wanawake wote na sio wa CCM tu.

Naunga mkono hoja kwa 200%
 
Back
Top Bottom