Umoja wa Wakuu wa Shule Manispaa watangaza Mgogoro na DC wa Tabora Mjini Mh. Eric Komanya Kitwala

MwanaMagongo

Member
Aug 15, 2011
74
43
DC KOMANYA WA TABORA MJINI KAMWE HATUTOKUPA USHIRIKIANO ZAIDI YA KUISHI NAWE KINAFIKI

KAMA UMOJA WA WAKUU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI TUMEDHAMIRIA YAFUATAYO

1: Kutokukupa ushirikiano wa aina yoyote ule ktk harakati zako za kutafuta kiki.

2: Kutokualika ktk shughuli zozote za kielimu zitakazojitokeza ktk maeneo yetu ya kazi

3: Kumtangaza adui mkuu wa shule yeyote atakayejipendekeza kwako na kumwondoa ktk ushirika wetu.

4: Kuhakikisha tunatumia mbinu mbadala kuufikidha uovu wako kwa wananchi wanaotuzunguka kwa jinsi unavyokiuka taratibu na haki za kiutumishi.

5: Kuhakikisha tunatoa hadharani video zote za lugha za kejeli na dhihaka unazotutolea na unazowatolea wakubwa zetu akiwemo Mkurugenzi wetu tunayemheshimu sana.
6: Kuhakikisha tunahudhuria vikao vyako lakini hatutoi ushirikiano wala michango ya mawazo.

SABABU KUU ZA UAMUZI HUU NI ZIFUATAZO

1: Tumechoka na dhihaka zako za kutuita vikaza na kutukashfu mbele za walimu na wananchi.
2: Tumechoshwa na tabia yako ya kufika ktk maeneo ya kazi kwa ajili ya kupiga picha ili kuuhadaa umma kuwa unawajibika ilihali unatuachia matatizo kwa wananchi.
3: Tumechoshwa na utapeli unaoufanya dhidi ya michango yetu na ile ya wadau wa elimu tuliyoitoa cash na materials ambapo uliunda kamati fake usiyoipa majukumu na isiyotoa mrejesho wa mapato na matumizi ya fedha za umma.
4: Tumechoshwa na tabia zako za kututuhumu kuwa wezi na wabadhirifu bila kuwepo na ushahidi wala kufikishwa mahakamani.

5: Tumechoshwa na mwenendo wa genge/ kikundi unachokipa rushwa ili kitumike kuzima malalamiko na kero zetu dhidi yako na hivyo kuidanganya serikali dhidi ya unyama wako.
6: Tumechoshwa na mwenendo wako wa kuingilia masuala ya baraza la mitihani wakati ukijua ya kuwa wewe sio miongoni mwa wajumbe wa kamati ya mitihani lakini Cha kushangaza unaita walimu kuwatishia,kuwaita vilaza na kujisifia kinyume kabisa na mwongozo wa baraza la mitihani la taifa.
7: Tumechoshwa na vikao vyako vya dharula visivyozingatia umbali wa maeneo yetu ya kazi lakini pamoja na kujitahidi kuhudhuria umekuwa ukitutimua kwa madai ya kuchelewa sambamba na kututolea lugha chafu.
8: Tumechoshwa na majigambo yako yasiyo na tija kiutendaji.

FAHAMU YAFUATAYO
TABORA MJINI Iliwahi kuwa na DC anaitwa CHANG'A (MUNGU AMREHEMU) hakuwa na elimu kubwa lakini ndiye mwasisi wa Andiko dhidi ya uboreshaji wa miundombinu unayoiona leo na kujigamba kwayo.

PIA tambua palikuwepo na Mhe SULEIMAN KUMCHAYA- Tabora haijawahi kuwa na historia ya majungu Kama unavyoeneza Jambo hili.

Sambamba na hilo mtangulizi wako mama yetu mpendwa Mhe QEEN MLOZI aliiongoza tabora na hakuwahi kubainisha umajungu unaouseme wewe.

DC KOMANYA WEWE NI DC WA HOVYO KUPATA KUTOKEA KTK HISTORIA YA TABORA MJINI

KILA MPENDA HAKI NA A-SHARE UJUMBE HUU.
NI SISI WAHANGA WA DHIHAKA WAKUU WA SHULE- TABORA MJINI
 
DC ukiamua kubadilika ni wewe na pia ukiamua kukomaa ni wewe, Kama hawa wanaokulalamkia wako sawa badilika
 
Kama kweli hili ni tamko la walimu, linatofauti gani na la wale vijana wa UDSM walioiagiza Serikali ndani ya saa 72. Yajayo yanafurahisha...
 
Kwamba walimu wanafikisha malalamiko ya DC kwa wananchi badala ya Rais ambaye ni mteuaji? Ndio nasikia leo
 
Kama kweli hili ni tamko la walimu, linatofauti gani na la wale vijana wa UDSM walioiagiza Serikali ndani ya saa 72. Yajayo yanafurahisha...
Wewe Pimbi uwe unatumia akili huyo Komanya ni Pimbi wa kutupa anasumbua watu wewe unamtetea, ni empty head, tabulalasa, premature imbecile, kipindi nimetembelea Tabora nilikuta kazusha ujinga wa kuanzisha mipaka mipya ya shule na kuingiza makazi ya watu ,alizua taharuki mpaka alipokuja waziri mkuu na kumtuma Lukuvi ndio kumaliza tatizo,huyo ni limbukeni wa kutupa,alienda standi ya zamani kwa wenye Tabora wanywa kahawa awazuie kunywa kahawa mida ya kazi walimgandisha kwenye gari akakoma ,naona sasa anahangaika na watumishi tu.Akileta za kuleta nendeni kipiri,kabwe radi shilingi 1500 mtwangeni mbona mnamchelewesha.Kwakuwa una akili ndogo kwani rais kaajiliwa na nani?katiba18 (I).
 
Mkuu wa Wilaya, Komanya anaweza akawa na madhaifu yake lakini ninachokiona kwa sasa ni kama kuna juhudi fulani hivi za kumchafua!

Hili bandiko linaonyesha juhudi hizo za kumchafua lakini tatizo kwa wanaomchafua ni kutojua kuwa hii serikali ya sasa haifanyii kazi majungu na fitina!
Inabidi wewe uende tabora ukautafute ukweli
Alafu utulete humu jf..... Fanya hivyo kamanda

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom