Umoja wa madhehebu ya Kikristo Dodoma kuandaa siku kumpongeza na kumuombea Rais Magufuli

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,251
Magufuli.jpg

UMOJA wa madhehebu ya Kikristo mkoani Dodoma umesema utaandaa siku maalum ya kumpongeza na kumuombea Rais John Magufuli kutokana na kazi anazofanya zinazoleta tumaini jipya kwa wananchi wa kawaida.

Mwenyekiti wa umoja huo, Dk Damas Mukasa alisema hayo juzi kwenye makao makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo wanachama, wazee wa mkoa wa Dodoma na viongozi wa chama ngazi ya mkoa na wilaya ya Dodoma Mjini walipojitokeza kumpongeza Rais Magufuli kutokana uamuzi mgumu anaochukua wa kulinda rasilimali za nchi.

Dk Mukasa alisema kazi anazofanya Rais Magufuli zinaleta msisimko kwa wananchi wa kawaida hasa kwa kubaini ufisadi mkubwa kwenye raslimali za nchi. “Anaondoa mafisadi anahakikisha rasilimali za nchi hazinufaishi watu wachache, ameondoa watu wasiostahili serikalini, tumeona kwa macho yetu na kushuhudia alivyoiondoa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA),” alisema.

Alisema hata mwanzoni mwa wiki hii, Rais Magufuli alipotoa ripoti kuhusu ufisadi mkubwa unaofanyika kwenye madini wananchi wameshangilia. “Wakristo wa Dodoma wamefurahishwa sana na uamuzi huo tutaandaa ibada maalumu ya kumpongeza Rais Magufuli kwa uamuzi mgumu anaochukua wa kulinda maslahi ya nchi kwa manufaa ya taifa,” alisema.

Kwa upande wake kada wa CCM, Emmanuel Kamara alisema ripoti ya pili kuhusu madini rais Magufuli ameipokea kwa weledi na upeo mkubwa. “Rais alichogundua waliotuangusha ni ni watanzania wenzetu tena ni wasomi ni viongozi wetu na tena na cha kusikitisha zaidi walifanya kama makusudi katika kutekeleza jambo hilo,” alisema.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CCM, mkoa wa Dodoma Balozi Job Lusinde alisema sasa ni wakati wa kuunga mkono juhudi za Rais ili nchi ikae kwenye mstari. Katibu wa baraza la wazee mkoa wa Dodoma, Mohamed Makbel alisema watanzania wana kila sababu ya kumshukuru Mungu kutokana na madudu yanayoibuliwa ambayo yalifanya taifa lipate hasara kubwa kutokana na tamaa za watu wachache.

Chanzo: HabariLeo
 
UMOJA wa madhehebu ya Kikristo mkoani Dodoma umesema utaandaa siku maalum ya kumpongeza na kumuombea Rais John Magufuli kutokana na kazi anazofanya zinazoleta tumaini jipya kwa wananchi wa kawaida.

Mwenyekiti wa umoja huo, Dk Damas Mukasa alisema hayo juzi kwenye makao makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo wanachama, wazee wa mkoa wa Dodoma na viongozi wa chama ngazi ya mkoa na wilaya ya Dodoma Mjini walipojitokeza kumpongeza Rais Magufuli kutokana uamuzi mgumu anaochukua wa kulinda rasilimali za nchi.

Dk Mukasa alisema kazi anazofanya Rais Magufuli zinaleta msisimko kwa wananchi wa kawaida hasa kwa kubaini ufisadi mkubwa kwenye raslimali za nchi. “Anaondoa mafisadi anahakikisha rasilimali za nchi hazinufaishi watu wachache, ameondoa watu wasiostahili serikalini, tumeona kwa macho yetu na kushuhudia alivyoiondoa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA),” alisema.

Alisema hata mwanzoni mwa wiki hii, Rais Magufuli alipotoa ripoti kuhusu ufisadi mkubwa unaofanyika kwenye madini wananchi wameshangilia. “Wakristo wa Dodoma wamefurahishwa sana na uamuzi huo tutaandaa ibada maalumu ya kumpongeza Rais Magufuli kwa uamuzi mgumu anaochukua wa kulinda maslahi ya nchi kwa manufaa ya taifa,” alisema.

Kwa upande wake kada wa CCM, Emmanuel Kamara alisema ripoti ya pili kuhusu madini rais Magufuli ameipokea kwa weledi na upeo mkubwa. “Rais alichogundua waliotuangusha ni ni watanzania wenzetu tena ni wasomi ni viongozi wetu na tena na cha kusikitisha zaidi walifanya kama makusudi katika kutekeleza jambo hilo,” alisema.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CCM, mkoa wa Dodoma Balozi Job Lusinde alisema sasa ni wakati wa kuunga mkono juhudi za Rais ili nchi ikae kwenye mstari. Katibu wa baraza la wazee mkoa wa Dodoma, Mohamed Makbel alisema watanzania wana kila sababu ya kumshukuru Mungu kutokana na madudu yanayoibuliwa ambayo yalifanya taifa lipate hasara kubwa kutokana na tamaa za watu wachache.

Chanzo: HabariLeo
Msiyiiiiii hakunaga watu wanafiki kama viongozi wa dini apa nchini. Nikupongeza tu mbona amjawahi ata shauli. Kibiti, ikwiriri watu wanakufa mpo kimya, mikataba mibovu mpo kimya, ukosefu wa ajira kwa vijana kimya bunge live mpo kimya, kuna mambo mengi ya kuishauli serikali mnakaa kupanga mda kufanya upuuzi ninyi ni viongozi wa matumbo na maslai viongozi wa dini hua awaogopi kesema ukweli ata kama niserikali mkafie mbele. Njaa zinawasumbua
 
Msiyiiiiii hakunaga watu wanafiki kama viongozi wa dini apa nchini. Nikupongeza tu mbona amjawahi ata shauli. Kibiti, ikwiriri watu wanakufa mpo kimya, mikataba mibovu mpo kimya, ukosefu wa ajira kwa vijana kimya bunge live mpo kimya, kuna mambo mengi ya kuishauli serikali mnakaa kupanga mda kufanya upuuzi ninyi ni viongozi wa matumbo na maslai viongozi wa dini hua awaogopi kesema ukweli ata kama niserikali mkafie mbele. Njaa zinawasumbua
Na Lowasa nae kapongeza sijui tumueteje, ila sisi tumefunzwa adabu na wazee wetu haturuhusiwi kutukana wazee, ukitukana wazee ni laana. Kwa hiyo naomba unisaidie mzee Luwasa nae tumuiteje? ntakuja baadae
 
Wampongeze tu ila wasiandam
UMOJA wa madhehebu ya Kikristo mkoani Dodoma umesema utaandaa siku maalum ya kumpongeza na kumuombea Rais John Magufuli kutokana na kazi anazofanya zinazoleta tumaini jipya kwa wananchi wa kawaida.

Mwenyekiti wa umoja huo, Dk Damas Mukasa alisema hayo juzi kwenye makao makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo wanachama, wazee wa mkoa wa Dodoma na viongozi wa chama ngazi ya mkoa na wilaya ya Dodoma Mjini walipojitokeza kumpongeza Rais Magufuli kutokana uamuzi mgumu anaochukua wa kulinda rasilimali za nchi.

Dk Mukasa alisema kazi anazofanya Rais Magufuli zinaleta msisimko kwa wananchi wa kawaida hasa kwa kubaini ufisadi mkubwa kwenye raslimali za nchi. “Anaondoa mafisadi anahakikisha rasilimali za nchi hazinufaishi watu wachache, ameondoa watu wasiostahili serikalini, tumeona kwa macho yetu na kushuhudia alivyoiondoa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA),” alisema.

Alisema hata mwanzoni mwa wiki hii, Rais Magufuli alipotoa ripoti kuhusu ufisadi mkubwa unaofanyika kwenye madini wananchi wameshangilia. “Wakristo wa Dodoma wamefurahishwa sana na uamuzi huo tutaandaa ibada maalumu ya kumpongeza Rais Magufuli kwa uamuzi mgumu anaochukua wa kulinda maslahi ya nchi kwa manufaa ya taifa,” alisema.

Kwa upande wake kada wa CCM, Emmanuel Kamara alisema ripoti ya pili kuhusu madini rais Magufuli ameipokea kwa weledi na upeo mkubwa. “Rais alichogundua waliotuangusha ni ni watanzania wenzetu tena ni wasomi ni viongozi wetu na tena na cha kusikitisha zaidi walifanya kama makusudi katika kutekeleza jambo hilo,” alisema.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CCM, mkoa wa Dodoma Balozi Job Lusinde alisema sasa ni wakati wa kuunga mkono juhudi za Rais ili nchi ikae kwenye mstari. Katibu wa baraza la wazee mkoa wa Dodoma, Mohamed Makbel alisema watanzania wana kila sababu ya kumshukuru Mungu kutokana na madudu yanayoibuliwa ambayo yalifanya taifa lipate hasara kubwa kutokana na tamaa za watu wachache.

Chanzo: HabariLeo
Mpongezeni tu mkitumia ukumbi mtakaochagua ila msiandamane kwa kuwa maandamano yamepigwa marufuku!
 
Na Lowasa nae kapongeza sijui tumueteje, ila sisi tumefunzwa adabu na wazee wetu haturuhusiwi kutukana wazee, ukitukana wazee ni laana. Kwa hiyo naomba unisaidie mzee Luwasa nae tumuiteje? ntakuja baadae
Alichofanya jpm sio kipya labda machoni kwako na pia kulingana na uelewa wako. Tume zimekua zikiundwa na kila raisi juu madini lkn mwisho amma kitu. Na nmakuelezs issue iyo ya acacia ndio kwishiney. Nakawa watalipa ata 1/3 ya pesa anoyoitaka jpm naacha siasa.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom