#COVID19 Umoja wa Afrika umeshindwa kutengeneza chanjo ya COVID-19?

baba anjela

JF-Expert Member
Mar 17, 2013
430
310
Kuna tatizo kubwa Afrika, Yaani hata kwa kuunganisha Nguvu zetu kwa pamoja kuja na chanjo moja imeshindikana, tunabaki kuwapa pongezi kubwa wazungu kwa kutuletea chanjo.

maisha ya mwafrika yapo mikononi mwa mzungu. Sasa tuna Uhuru gani? Uhuru wa kupandisha bendera na kushusha basi. Uhuru wa kuchagua raisi basi.

Jambo kubwa linalo tutafuna afrika ni disunity.( kukosekana kwa umoja). Jambo ambalo wazungu wanalitumia kama mlango wakuendelea kututafuna. Bado mataifa yetu ni machanga,kusimama kila taifa peke yake ni ngumu kusonga mbele.

Tuna kila sababu ya kupata umoja wa Afrika wenye maono ya kulikomboa bara la Afrika. Na si huu umoja uliobebwa na kivuli cha mzungu. Tutaendelea kuwapigia magoti wazungu mpaka lini?

Linapokuja jambo la afya ,usalama ,uchumi.. Afrika lazima tuwapigie magoti wazungu, sasa Uhuru wetu ni UPI??... Vita na magonjwa havitokuja kwisha africa,ili wazungu waendelee kutafuna Mali zetu. Leo mama Africa anagombaniwa na kila mwanaume. Hana uwezo wakujisimamia.

Baba Africa uko wapi?
 
Shida je utaalam huo wanao?

Hizo elimu walizosomea za utabubu zinaweza kuwawezesha kutengeneza chanjo ya magonjwa mbalambali?
 
wako busy kuhakikisha kuwa wao na vyama vyao wanaendelea kubaki madarakani hata kwa kumwaga damu. hayo mengine waachieni wazungu
 
Ni wazo jema, lakini ili kutekeleza hili ni pale tutakapovunja minyororo ya fikra na kuwa tayari. Kwani hata huko mbele kwa wenzetu wanaotengeneza dawa au chanjo au vifaa tiba si serikali bali ni makampuni makubwa yaliyowekeza kwenye mifumo hiyo ya utengenezaji wa dawa, chanjo na vifaa tiba.

Haya mambo yanauhitaji wa very sophisticated technology, huge investment, commitment non interfered environment and very systematic.

Utayari ulenge:
1: Utashi wa kisiasa/kuunganisha mfumo husika kwa kumaanisha.

2: Kiuchumi/utaratibu wa kuwezesha chombo kitakachohusika kwenye haya yote.

3: Kitechnolojia/kuwa tayari kuunganisha teknolojia tuliyonayo na ku-import pale inapobidi.

4: Kuunganisha utaalamu/ kuwaunganisha wataalamu watakaohitajika ili kufanikisha suala husika na kuongeza wengine toka nje pale itakapohitajika.

Hivyo, tutahitaji au tunahitaji utayari wa kweli.
 
Umoja wa Africa hautengenezi chanjo

Wanasayansi na maabara z Africa zinatengeneza

Too much politicking is terrible for your Heath
 
Kuna tatizo kubwa Afrika, Yaani hata kwa kuunganisha Nguvu zetu kwa pamoja kuja na chanjo moja imeshindikana, tunabaki kuwapa pongezi kubwa wazungu kwa kutuletea chanjo.
Uganda wamegundua tiba, siyo chanjo, tiba. Lakini inasemekana wameificha ili kumlinda mgunduzi hasi'athiriwe' na watengeneza chanjo. Kwa hiyo....! Tumeshindwa kama Afrika kumlida aliyetaka kutambua mgonjwa wa uviko kwa kutumia 'paka akitoka.....utawala', sembuse kuwaza jambo hili zito!
 
Back
Top Bottom