THE BIG SHOW
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 16,374
- 12,822
- Thread starter
- #101
Vyama vya siasa vina itikadi, malengo na sera tofauti. Kazi yao ni kuwashawishi wananchi juu ya ubora wa mielekeo yao hiyo tofauti katika kuchochea maendeleo na ustawi wa taifa.
Hakuna mantiki kwa vyama hivyo kuungana eti kwa lengo moja tu - kuiondoa CCM madarakani. Vikishaungana vitaeneza itikadi ipi? Malengo gani? Na sera zipi? Vitawaaminisha wananchi vinasimamia nini hasa? Kama kweli CCM ndio chama bora kinachokubalika na Watanzania wengi, tatizo liko wapi?
Tatizo la kubwa la Tanzania sio “mabadiliko ya chama tawala tu”. BALI ni CCM kuwa chama dola kilichohodhi madaraka kidikteta na kuhujumu mfumo mzima wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa. Kwa kutumia vyombo na taasisi za dola, CCM imejihakikishia kukaa madarakani kwa nguvu bila ridhaa ya wananchi.
Kutoliona hilo ni kielelezo cha uongo na unafiki.
Lengo la chama.chochote Cha siasa ni kushika Dola,kwan ww hulitambui hilo??
Sasa kama Nia yao wapinzan ni kushika dola, watawezaje kushika dola ikiwa wamegawanyika??