Wadau wa Umoja House salaam!
Nimeona nisilifumbie macho suala hili maana linaharibu uzuri wa Mjengo mzima na kitendekacho humo ndani.
Awali ya yote napenda kuzipongeza balozi za Uingereza, Uholanzi na Ujerumani kwa kujipanga vizuri na kushirikiana kuweka jengo zuri, safi na la kisasa ili kufanyia shughuli za kibalozi na pia ushirikiano wa kimaendelea unaosaidia nchi yetu kusukuma gurudumu la maendeleo.
Aidha niwapongeze pia kwa kutoa ajira lukuki kwa watanzania wenzetu pale kuanzia ulinzi hadi visa na usimamizi wa miradi ya maendeleo kupitia taasis kama DFID n.k.
Kero yangu inahusiana sana na walinzi walioajiriwa kulinda pale getini.Hawa ni kero kubwa na kwa kiasi kikubwa wanazidhalilisha balozi husika.Ukiingia tu eneo la karibu kuanzia parking ambazo kwanza siyo za UMOJA HOUSE unakumbana na hawa Ultimate Security- wataanza kukutishia maisha kisa parking ili uwape kitu kidogo!
Ukiingia eneo sasa la mjengo ndio balaa.Wakijua umefuata visa utaipata fresh.Wataanza kukuzungusha kuwa muda bado.. mara hujajaza fomu husika, mara huwezi kupata visa..mradi wakupandishe presha tu.Ukifanikiwa kuingia na kufanya shughuli zako, ukitoka lazima wakutoe upepo na kisingizio chao eti hawana kitu kabisa na kuwa watakusaidia ili mambo yako yawe fresh! LOL MAKUBWA! Kuna ushirika gani kati ya walinzi hawa na wafanyakazi wa ubalozi kwenye kutoa viza?KWANI BALOZI HAMLIPI VIZURI ILI WALINZI HAWA WAWEZE KUMUDU MAISHA?
Kero nyingine hasa inaelekezwa kwa ubalozi wa Uingereza. Kabla ya kulalamika, nawapongeza sana kwa mfumo wao mpya wa ku apply kupitia mtandao ( online) maana hili limewezesha kuondokana na zile foleni za kulala pale nje ya ubalozi ili kukesha uwahi nafasi kesho yake.Hili lilikuwa linatudhalilisha sana watanzania hivyo tunashukuru kuturudishia utu wetu.
Hata hivyo, utaratibu wao wa kutokuwa na mahojiano ya ana-kwa ana au kwa wafanyakazi wao kutokuwa na msaada kwa waombaji ili angalau kuwaonyesha wapi kuna upungufu katika application ili mapungufu hayo yarekebishwe kabla ya karatasi za maombi na passport kwenda Nairobi ni kitu ambacho hakiwapi maksi ubalozi.
Haiyumkini kwa jinsi watanzania walivyo, bado wanahitaji human touch katika mambo mengi. Inashangaza na kusikitisha pale passport yako inapopelekwa Nairobi baada ya kulipa malaki ya fedha, inakaa huko karibu mwezi halafu unakuja kuambiwa kuwa maombi yako hayakukamilika - kwamba hukuweka barua ya mwajiri wako, au hukuambatanisha hati mbalimbali etc! Hivi kama maafisa viza pale wangemwambia muombaji alete hati hizo , si ingewezekana kurekebisha na kuokoa pesa za mhusika?
Jamani Ubalozi wa Uingereza mjirekebishe kwenye hili kwa maana mnapochukua 450,000/ au 150,000/- za muombaji( kutegemeana na muda anaoomba) huku mkijua kabisa angeweza kurekebisha hati zake akapewa viza, hamuoni mnawaibia watanzania? Kwanini nyie mkija kwetu tunawapa viza zenu pale eapot na hatuwahangaishi kama mnavyotufanyia? Kwamba watanzania ni maskini hivyo hamuwahitaji kule kwenu, kumbukeni siyo kila mtanzania anataka kuzamia uingereza! Wengine wana maisha yao mazuri sana Tanzania, huko kwenu wanaenda kibiashara kama na nyie watu wenu wanavyokuja hapa kwetu hivyo acheni dharau!
Nawapongeza sana Ubalozi wa Ujerumani hasa wafanya kazi wa viza maana wao kwa kweli hawako kama kikwazo kama wenzao ubalozi wa Uingereza bali wapo pale kama wawezeshaji na hiki ndicho kinachotakiwa na inashangza iweje majirani walio karibu vile kiofisi na hata ki nchi kuwa na utendaji tofauti vile.
HONGERA UJERUMANI.... muendelee hivyohivyio maana hii ndio haswa ushirikiano wa kimataifa ambapo nchi zote tunaheshimiana.
HILI SIO JUNGU BALI NI UJUMBE MAHUSUSI..JIREKEBISHENI MAANA NAJUA HUWA MNAINGIA HUMU JF.
Nimeona nisilifumbie macho suala hili maana linaharibu uzuri wa Mjengo mzima na kitendekacho humo ndani.
Awali ya yote napenda kuzipongeza balozi za Uingereza, Uholanzi na Ujerumani kwa kujipanga vizuri na kushirikiana kuweka jengo zuri, safi na la kisasa ili kufanyia shughuli za kibalozi na pia ushirikiano wa kimaendelea unaosaidia nchi yetu kusukuma gurudumu la maendeleo.
Aidha niwapongeze pia kwa kutoa ajira lukuki kwa watanzania wenzetu pale kuanzia ulinzi hadi visa na usimamizi wa miradi ya maendeleo kupitia taasis kama DFID n.k.
Kero yangu inahusiana sana na walinzi walioajiriwa kulinda pale getini.Hawa ni kero kubwa na kwa kiasi kikubwa wanazidhalilisha balozi husika.Ukiingia tu eneo la karibu kuanzia parking ambazo kwanza siyo za UMOJA HOUSE unakumbana na hawa Ultimate Security- wataanza kukutishia maisha kisa parking ili uwape kitu kidogo!
Ukiingia eneo sasa la mjengo ndio balaa.Wakijua umefuata visa utaipata fresh.Wataanza kukuzungusha kuwa muda bado.. mara hujajaza fomu husika, mara huwezi kupata visa..mradi wakupandishe presha tu.Ukifanikiwa kuingia na kufanya shughuli zako, ukitoka lazima wakutoe upepo na kisingizio chao eti hawana kitu kabisa na kuwa watakusaidia ili mambo yako yawe fresh! LOL MAKUBWA! Kuna ushirika gani kati ya walinzi hawa na wafanyakazi wa ubalozi kwenye kutoa viza?KWANI BALOZI HAMLIPI VIZURI ILI WALINZI HAWA WAWEZE KUMUDU MAISHA?
Kero nyingine hasa inaelekezwa kwa ubalozi wa Uingereza. Kabla ya kulalamika, nawapongeza sana kwa mfumo wao mpya wa ku apply kupitia mtandao ( online) maana hili limewezesha kuondokana na zile foleni za kulala pale nje ya ubalozi ili kukesha uwahi nafasi kesho yake.Hili lilikuwa linatudhalilisha sana watanzania hivyo tunashukuru kuturudishia utu wetu.
Hata hivyo, utaratibu wao wa kutokuwa na mahojiano ya ana-kwa ana au kwa wafanyakazi wao kutokuwa na msaada kwa waombaji ili angalau kuwaonyesha wapi kuna upungufu katika application ili mapungufu hayo yarekebishwe kabla ya karatasi za maombi na passport kwenda Nairobi ni kitu ambacho hakiwapi maksi ubalozi.
Haiyumkini kwa jinsi watanzania walivyo, bado wanahitaji human touch katika mambo mengi. Inashangaza na kusikitisha pale passport yako inapopelekwa Nairobi baada ya kulipa malaki ya fedha, inakaa huko karibu mwezi halafu unakuja kuambiwa kuwa maombi yako hayakukamilika - kwamba hukuweka barua ya mwajiri wako, au hukuambatanisha hati mbalimbali etc! Hivi kama maafisa viza pale wangemwambia muombaji alete hati hizo , si ingewezekana kurekebisha na kuokoa pesa za mhusika?
Jamani Ubalozi wa Uingereza mjirekebishe kwenye hili kwa maana mnapochukua 450,000/ au 150,000/- za muombaji( kutegemeana na muda anaoomba) huku mkijua kabisa angeweza kurekebisha hati zake akapewa viza, hamuoni mnawaibia watanzania? Kwanini nyie mkija kwetu tunawapa viza zenu pale eapot na hatuwahangaishi kama mnavyotufanyia? Kwamba watanzania ni maskini hivyo hamuwahitaji kule kwenu, kumbukeni siyo kila mtanzania anataka kuzamia uingereza! Wengine wana maisha yao mazuri sana Tanzania, huko kwenu wanaenda kibiashara kama na nyie watu wenu wanavyokuja hapa kwetu hivyo acheni dharau!
Nawapongeza sana Ubalozi wa Ujerumani hasa wafanya kazi wa viza maana wao kwa kweli hawako kama kikwazo kama wenzao ubalozi wa Uingereza bali wapo pale kama wawezeshaji na hiki ndicho kinachotakiwa na inashangza iweje majirani walio karibu vile kiofisi na hata ki nchi kuwa na utendaji tofauti vile.
HONGERA UJERUMANI.... muendelee hivyohivyio maana hii ndio haswa ushirikiano wa kimataifa ambapo nchi zote tunaheshimiana.
HILI SIO JUNGU BALI NI UJUMBE MAHUSUSI..JIREKEBISHENI MAANA NAJUA HUWA MNAINGIA HUMU JF.