Landson Tz
JF-Expert Member
- May 8, 2011
- 295
- 221
Katika uchumi ardhi ni moja wapo ya rasilimali muhimu. Katika biashara na uwekezaji, ardhi ni kati ya rasilimali muhimu sana. Hivyo, umiliki wa rasilimali hii ni jambo la muhimu sana katika kutumia hii rasilimali muhimu. Juu au ndani ya rasilimali hii, rasilimali zingine huwekwa, za muda mfupi na/au za muda mrefu. Kama mtu/kampuni inataka kuwekeza kwenye majengo (real estate) lazima kuwe na ardhi, ukitaka kuwekeza kwenye kilimo lazima uwe na ardhi, hata ukitaka kujenga nyumba ya kuishi ni lazima uwe na ardhi, ukitaka kufuga lazima uwe na ardhi, mifano iko mingi.
Kuna mitazamo tofauti kuhusu namna bora ya umiliki wa rasili hii.
Namna ya kwanza ni “Kumilikiwa na jamii” (Rais kwa niaba ya raia)
Namna ya pili “Kumilikiwa na mtu bninafsi/ kampuni binafsi
Je! namna ipi ni bora zaidi ili kuchochea uwekezaji?
Kazi za ardhi kama rasilimali;tukijikita kwenye kilimo ardhi ni nyenzo muhimu sana ambapo miundo mbinu yote yakiwemo mazao vinakuwa juu ya ardhi. Kwa lugha nyingine huwezi kuvitenganisha. Kwakuwa baadhi ya miundombinu ya kilimo na mazao haviwezi kutenganishwa na ardhi hivyo mmiliki anapaswa awe mmoja badala ya ardhi ya rais miundombinu na mazao ya mtu binafsi au kampuni binafsi.
Matunda yatokanayo na ardhi; kilimo kinasababisha yapatikane mazao mbalimbali yakiwemo ya chakula. Katika kipindi hiki ambacho sio lazima ulime ili ule, chakula cha kutosha kinahitajika sokoni. Hivyo bila kujali ardhi iliyozalisha ina umiliki gani watu wanahitaji chakula sokoni. Hapo ndo hoja ya umiliki wa jamii inapungua nguvu. Kutokana na hali hiyo, tunahitaji kujua ni njia ipi ya umiliki wa ardhi inaweza kuongeza uzalishaji? Mimi naona njia umiliki wa ardhi wa binafsi unaongeza tija zaidi kuliko umiliki wa jamii.
Katika nchi yetu, tangu uhuru umiliki wa ardhi umekuwa ni wa jamii na kinachoendelea kwenye kilimo kila mmoja anaelewa. Wananchi wanaoshiriki kwenye kilimo wengi wao ni maskini ambao kimsingi hawana namna nyingine ya kujikimu. Na kama wangeweza kuwa namna nyingine basi wengi wao wasingelima. Sekta ya kilimo ndio inayoongoza kwa kufukarisha watu kwani kilimo cha sasa kinahitaji uwekezaji mkubwa unaohitaji mtaji mkubwa ila wameachwa maskini wahangaike nacho bila mafanikio.
Uwekezaji wa kudumu kwenye ardhi unatia moyo wawekezaji (wananchi) kama ardhi inakuwa inamilikiwa na mtu binafsi au kampuni. Ardhi kuwa mikononi mwa Rais kunapunguza marali ya uwekezaji. Rais na wanaomzunguka ni bianadamu na wana mapungufu, hivyo kuna uwezekano wa hujuma. Hujuma hizi zinaweza kuanzia kwa raia wengine na kuishinikiza serikali kufanya unyang’anyi kwa kusingizia maslahi ya umma.
UMILIKI WA ARDHI WA UMMA KUPITIA RAIS NI MSINGI WA UJAMAA – BADO TUMELEWA NA UJAMAA?
Ni katika mfumo wa Ujamaa ambapo ardhi umilikiwa na jamii. Katika mifumo mingine ardhi ni mali kama zilivyo mali nyingie na inapaswa itumike kikaimilifu kuzalisha mali zingine. Kwa mfumo wa Ujamaa serikali ushiriki katika shughuli za uzallishaji kama kilimo laakini mifumo mingine kama uliberali na ubepari serikali haishiriki katika uzalishaji. Kutokana na hali hakuna haja ya serikali yetu baada ya kuachana na Ujamaa kuendelea kung’ang’ani ardhi. Mimi naamini serikali ikimilikisha ardhi kwa raia itaongeza tija na uwekezaji utaongezeka.
Kama tutaendelea na mfumo huu wakati idadi ya watu inaongezeka (inakadiriwa kufikia milioni 100 (2050) kwa kasi ipo siku nchi itaingia kwenye njaa au kuagiza asilimia kubwa ya chakula kutoka nje. Maana waliachiwa kilimo kwa saa ni wale wasio na la kupoteza wanalima wakitaka na mara nyingi sio kwa biashara bali kwa matumizi ya kaya zao.
Kwa sasa miji inaendelea kukua, inahitaji chakula sokoni na si kumiliki ardhi. Tukibadili sera ya ardhi na kuanza kumilikisha kwa raia badala ya kuwakodisha naamini raia wenye nia na mitaji mikubwa wataingi kwenye kilimo na ufugaji hivyo kuleta tija katika sekta ya kilimo na kukuza ajira na kuongeza upatikanaji wa mazao kikiwemo chakula.
Mtazamo wa Landson Tanzania.
Kuna mitazamo tofauti kuhusu namna bora ya umiliki wa rasili hii.
Namna ya kwanza ni “Kumilikiwa na jamii” (Rais kwa niaba ya raia)
Namna ya pili “Kumilikiwa na mtu bninafsi/ kampuni binafsi
Je! namna ipi ni bora zaidi ili kuchochea uwekezaji?
Kazi za ardhi kama rasilimali;tukijikita kwenye kilimo ardhi ni nyenzo muhimu sana ambapo miundo mbinu yote yakiwemo mazao vinakuwa juu ya ardhi. Kwa lugha nyingine huwezi kuvitenganisha. Kwakuwa baadhi ya miundombinu ya kilimo na mazao haviwezi kutenganishwa na ardhi hivyo mmiliki anapaswa awe mmoja badala ya ardhi ya rais miundombinu na mazao ya mtu binafsi au kampuni binafsi.
Matunda yatokanayo na ardhi; kilimo kinasababisha yapatikane mazao mbalimbali yakiwemo ya chakula. Katika kipindi hiki ambacho sio lazima ulime ili ule, chakula cha kutosha kinahitajika sokoni. Hivyo bila kujali ardhi iliyozalisha ina umiliki gani watu wanahitaji chakula sokoni. Hapo ndo hoja ya umiliki wa jamii inapungua nguvu. Kutokana na hali hiyo, tunahitaji kujua ni njia ipi ya umiliki wa ardhi inaweza kuongeza uzalishaji? Mimi naona njia umiliki wa ardhi wa binafsi unaongeza tija zaidi kuliko umiliki wa jamii.
Katika nchi yetu, tangu uhuru umiliki wa ardhi umekuwa ni wa jamii na kinachoendelea kwenye kilimo kila mmoja anaelewa. Wananchi wanaoshiriki kwenye kilimo wengi wao ni maskini ambao kimsingi hawana namna nyingine ya kujikimu. Na kama wangeweza kuwa namna nyingine basi wengi wao wasingelima. Sekta ya kilimo ndio inayoongoza kwa kufukarisha watu kwani kilimo cha sasa kinahitaji uwekezaji mkubwa unaohitaji mtaji mkubwa ila wameachwa maskini wahangaike nacho bila mafanikio.
Uwekezaji wa kudumu kwenye ardhi unatia moyo wawekezaji (wananchi) kama ardhi inakuwa inamilikiwa na mtu binafsi au kampuni. Ardhi kuwa mikononi mwa Rais kunapunguza marali ya uwekezaji. Rais na wanaomzunguka ni bianadamu na wana mapungufu, hivyo kuna uwezekano wa hujuma. Hujuma hizi zinaweza kuanzia kwa raia wengine na kuishinikiza serikali kufanya unyang’anyi kwa kusingizia maslahi ya umma.
UMILIKI WA ARDHI WA UMMA KUPITIA RAIS NI MSINGI WA UJAMAA – BADO TUMELEWA NA UJAMAA?
Ni katika mfumo wa Ujamaa ambapo ardhi umilikiwa na jamii. Katika mifumo mingine ardhi ni mali kama zilivyo mali nyingie na inapaswa itumike kikaimilifu kuzalisha mali zingine. Kwa mfumo wa Ujamaa serikali ushiriki katika shughuli za uzallishaji kama kilimo laakini mifumo mingine kama uliberali na ubepari serikali haishiriki katika uzalishaji. Kutokana na hali hakuna haja ya serikali yetu baada ya kuachana na Ujamaa kuendelea kung’ang’ani ardhi. Mimi naamini serikali ikimilikisha ardhi kwa raia itaongeza tija na uwekezaji utaongezeka.
Kama tutaendelea na mfumo huu wakati idadi ya watu inaongezeka (inakadiriwa kufikia milioni 100 (2050) kwa kasi ipo siku nchi itaingia kwenye njaa au kuagiza asilimia kubwa ya chakula kutoka nje. Maana waliachiwa kilimo kwa saa ni wale wasio na la kupoteza wanalima wakitaka na mara nyingi sio kwa biashara bali kwa matumizi ya kaya zao.
Kwa sasa miji inaendelea kukua, inahitaji chakula sokoni na si kumiliki ardhi. Tukibadili sera ya ardhi na kuanza kumilikisha kwa raia badala ya kuwakodisha naamini raia wenye nia na mitaji mikubwa wataingi kwenye kilimo na ufugaji hivyo kuleta tija katika sekta ya kilimo na kukuza ajira na kuongeza upatikanaji wa mazao kikiwemo chakula.
Mtazamo wa Landson Tanzania.