Umiliki wa ardhi Tanzania: Lease VS Free hold system

Ng'azagala

JF-Expert Member
Jun 7, 2008
1,286
221
Wana forums

kwa manufaa ya nchi yetu ningependa tujadili suala hili la umiliki wa ardhi kati ya system mbili Lease hold ambayo inatumika sasa na nyingine ni Free hold. nimeona makundi mbalimbali yakijadili haya masuala hasa NGO ya HAKIARIDHI na wamekuwa wakisisitiza kwamba Tanzania ihamie kwenye Free Hold System iachane na Lease hold. ni vizuri tukajadili kwa upana hasa tukiangalia hali ya uchumi wa mtu binafsi, na uzuri na ubaya wa kila system katika nchi yetu.

kwa kifupi Tanzania tunatumia lease kwa maana mwananchi anakodishiwa ardhi kwa miaka kadhaa kisha anaweza kuomba kuongeza muda wa umiliki lakini wakati wote ardhi inakuwa chini ya mamlaka ya serikali (President)

Free hold ni umiliki usio na mipaka wa mwananchi binafsi, na kwa sababu ardhi ni pesa! mara nyingi wenye pesa ndiyo watamiliki ardhi bila mipaka. Hii ilitumika wakati wa ukoloni na bado inatumika sana nchi za kibepari na hata nchi nyingi za afrika kama Zimbabwe, Kenya nk. Ukifuatilia historia ya Tanzania utaratibu wa Free hold ulikuwepo wakati wa ukoloni na ulipigwa marufuku na Mwl Nyerere baada ya Uhuru kwani tayari wazungu walikuwa wamenunua sehemu kubwa ya Tanzania.

nawasilisha
 
Kuwa na free hold ni hatari kwa taifa mana wenye hela tu ndo watamiliki sie wengne tutakuwa masquarterz! Nyerere alikuwa na akili sana ktk hl!
 
Free hold system siyo mfumo mzuri wa kumiliki ardhi kwa Tanzania na kwamaslahi ya Wananchi. Ukiangalia nchi nyingi zenye migogoro ya ardhi na wananchi wenye umaskini wa kupindukia ni zile zenye mfumo huu wa umiliki wa ardhi. Ardhi huwa mikononi mwa watu wachache matajiri na wengine hugeuzwa watumwa tu.
NGO ni vyombo vinavyofadhiliwa na mataifa ya magharibi ili kupenyeza na kusimamia agenda zao kwa manufaa yao na kamwe si kwa wananchi wa nchi husika.
Kundi kubwa la wananchi masikini wa Kenya, Zimbabwe, Africa Kusini nk ni zao la mfumo huu hivyo ni mfumo wa kuuogopa sana.

Leo hii mtanzania yoyote anaweza kuwa na ardhi popote nchini na akaitumia kwa shughuli mbalimbali za uzalishaji kitu ambacho ni vigumu kwa nchi nilizotaja hapo juu.
 
mkuu Tanzania tuna "right of occupancy" which is just a right limmited in using and possesing intrest over the land!hii ina inatofauti kidogo na leasehold!! ardhi yote ya tanzania ni ya umma(watu wote) but leasehold inaoperate kwenye private land ownership maana kunakua na landlords na ternants!
Kuhusu mfumo upi ni mzuri kwetu sisi mimi nadhani "haki miliki" inafaa kwasababu tukiruhusu freehold tutaharalisha land grabing eventually only a ssmall percente of the population watakua na ardhi either wengine watakua wapangaji au watumwa kabisaa
 
Back
Top Bottom