Umewahi kuzushiwa kashfa mbovu/ kuchukiwa katika jamii kutokana na mafanikio fulani?

screpa

JF-Expert Member
Sep 10, 2015
10,791
15,693
Hii tabia sijui tuseme ni ya waafrika au nini, tuna roho ya kwanini pale mtu fulani kwenye jamii anapoonekana wa tofauti, yaani kapiga hatua fulani kuliko wengine, tunatamani wote tuwe sawa, anapotokea fulani anakuzidi ndipo chuki zinaanza.

Mi nakumbukuka mamaangu (mfanyabiashara) waliwahi mzushia kashfa ya uchawi/ushirikina mtaani kisa ana duka ambalo linauza sana, majirani walisambaza uzushi eti analeta waganga kila siku na watu waliamini.

hawakutaka kufikiria kwamba pengine anauza sana kuliko wengine kutokana location aliyopo (njia panda) na ana vitu vingi vinavyoshawishi wateja, wao akili yao iliwapeleka kwenye uchawi tu, lakini nashukuru Mungu huo uzushi haumkumrudisha nyuma aliendelea kuchapa kazi na wakaacha wenyewe kusema.

Je, umewahi kukumbana na uzushi (kashfa) za namna hii kwenye jamii/ masomo/ biashara/ makazini kutokana na kupiga hatua fulani?

Na je uliweza vipi kukabiliana nao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii tabia sijui tuseme ni ya waafrika au nini, tuna roho ya kwanini pale mtu fulani kwenye jamii anapoonekana wa tofauti, yaani kapiga hatua fulani kuliko wengine, tunatamani wote tuwe sawa, anapotokea fulani anakuzidi ndipo chuki zinaanza.

Ndio, na CCM baada ya kuhutubia mkutano wa Chadema!

Nilikabiliana nao kwa kuonyesha siogopi kuwekwa ndani kwa kosa la kuwaamba wanaendesha nchi kinyume cha maumbile!
 
Kuna wazushi wengine ni balaa...

wanakuzulia jambo linaloweza kukuua....au kukuacha na athar za maisha!

Binadamu ni moja kati ya viumbe wabaya mno!

Kona wanayokuweka..
utalipia uhuru wako...na maisha yako mpaka unakufa!




Sent using Jamii Forums mobile app

Nalipia gharama ya uongo mbaya tena wa fedheha niliyonenewa. Nobody understands me isipokua Mungu tu. Ila yule aliyeninenea uongo alipata malipo yake stahiki kabisa toka kwa Mungu. Maumivu na mateso aliyopitia ni makali mno mpaka huruma ilinijia tena


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiyaendekeza maneno yao ya kizushi na kuyasikiliza na ukataka kujiosha kama vyombo, ujue kuna siku utaamua usile chakula ili vyombo, viendelee kuwa safi. Matokeo yake vidonda vya tumbo na kufilisika juu, wataanza kusema tulijua hatofika mbali!
 
Siku ukianza kuitwa mchawi ndo utakapoamini kwamba uchawi haupo...

Mimi nshazushiwa mpka ujambazi, kuna kipindi watoto walikuwa wanapotea sana na mm nilikuwa na mazoea jion naenda nje ya mji napark gari eneo natulia zangu.. Kuna mzee akanifata ndo akaanza kunichana hizo habar, yan nilishangaa sana..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom