Umewahi kusoma kitabu, The Richest Man In Babylon? Ulijifunza nini? Kinasaidia?

"Siku moja nilitoka nje ya jiji tena, nilishangaa nilipokuta umati mkubwa wa watu umekusanyika. Nilipomuuliza mtu mmoja kuna nini alinijibu, 'hujasikia? Kuna mtumwa amemuua mlinzi hivyo amekamatwa na atachapwa hadi afe kwa uhalifu wake. Hata mfalme mwenyewe atakuwepo hapa leo!'

"Watu walikuwa wengi sana wakiwa wamezunguka nguzo ya kumfunga mtuhumiwa anayechapwa. Niliogopa kusogea karibu nisije mwaga sinia langu la keki. Nilipanda juu ya ukuta uliokuwa unajengwa na kuangalia kutoka juu. Siku hiyo ndiyo nilipata bahati ya kumuona Nebkadneza akiwa amepanda gari la kuendeshwa kwa farasi, gari la dhahabu. Sijawahi ona mtu aliyekuwa kapambwa ghali kiasi kile. Kwenye nguo zake kulikuwa dhahabu ikining'inia na nguo za hariri.

"Sikuweza kuona anayechapwa lakini niliweza kusikia kilio chake. Niliwaza inakuwaje mfalme wetu mwema anaruhusu ukatili kama ule na cha kushangaza alikuwa anacheka na kutaniana na watu wengine mashuhuri. Hapo nilifahamu kuwa alikuwa ni katili sana na pia nikaelewa ni kwanini wale watu hufanyishwa kazi ya kujenga ukuta kama wanyama.

"Baada ya mfungwa yule kufa, mwili wake ulitundikwa kwenye nguzo kichwa chini miguu juu ili kila mtu aone. Watu walipopungua nilisogea kuona mwili ule. Kwenye kifua chake niliona tatuu ya nyoka aliyejikunja. Alikuwa ni Haramia!

"Siku niliyokutana tena na Arad Gula alikuwa amebadilika sana. Alikuwa mchangamfu na alinisalimia. 'Tazama mtumwa aliyekuwa unamjua sasa ni mtu huru. Tayari biashara yangu inakua na mke wangu ana furaha. Yeye ni mtu huru pia, mpwa wa bwana wangu. Amenishauri tuhamie mji ambao hakuna mtu anayejua kuwa nimewahi kuwa mtumwa. Anataka watoto wetu wasikue na aibu kuwa baba yao alikuwa mtumwa. Kazi imekuwa msaidizi wangu mkubwa, imenirudishia kujiamini na kuongeza uwezo wangu wa kufanya biashara.'

Nilifurahi kuwa ushauri wangu ulikuwa umemsaidia.

"Siku moja jioni Swasti alinifuata akiwa mwenye wasiwasi sana: 'Bwana wetu ana tatizo, nina wasiwasi juu yake. Miezi kadhaa iliyopita alipoteza pesa nyingi kwenye mchezo wa kamari. Mkulima ambaye humletea nafaka na asali hajamlipa. Pia alikopa pesa sehemu na hajalipa. Watu hao wana hasira juu yake na wameanza kumtishia.'''

"Kwa nini tunajihangaisha na matatizo yake. Sisi si walezi wake,' nilisema bila kufikiri.

'''Kijana mpumbavu! Huelewi chochote. Amekuweka wewe kama dhamana kwa mkopesha pesa. Chini ya sheria, mkopeshaji anaweza kukuchukua na kukuuza. Mimi sielewi cha kufanya, Nana-Naid ni bwana mzuri, hata sielewi kwanini amejiingiza kwenye matata haya?'

"Swasti alikuwa sahihi kabisa kuwa na wasiwasi. Asubuhi moja nilipokuwa naoka mikate mkopesha pesa alifika akiwa na mtu mwingine aliyeitwa Sasi. Yule mtu aliniangalia na kusema kuwa nitafaa.

"Yule mkopesha pesa hakusubiri bwana wangu arudi bali alimwambia Swasti amjulishe kuwa amenichukua. Nilichukuliwa nikiwa na nguo nilizovaa tu na pochi yangu ya pesa kwenye mkanda.

"Nilichukuliwa kama vile mti unaong'olewa toka msituni na kimbunga na kutupwa baharini. Matumaini yangu yalipotea. Kwa mara nyingine kamari na bia ziliniletea matatizo.

"Sasi alikuwa ni mkatili na mtu asiye na mzaha. Alipokuwa ananiongoza kupita jijini nilimueleza kuhusu kazi nzuri niliizomfanyia Nana-Naid na nikamwambia kuwa natumaini kumfanyia kazi nzuri pia. Majibu yake yalikuwa ya kukatisha tamaa kabisa. Alijibu:

"'Sipendi hii kazi na bosi wangu haipendi kata kidogo. Mfalme amemuagiza anitume nikajenge sehemu ya mfereji. Ameniambia ninunue watumwa wengi na wafanye kazi kwa bidii ili iishe haraka. Boh! Mtu anawezaje kumaliza haraka kazi kubwa namna ile?"

"Piga picha ya jangwa lisilo na miti bali vichaka vidogovidogo vya hapa na pale. Jua linawaka hadi maji kwenye mapipa yanakuwa ya moto na hayanyweki. Tena piga picha msururu wa watu wakishuka chini unakochimbwa mfereji na kutoka wamebeba vikapu vizito vya udongo toka asubuhi hadi usiku unapoingia. Vuta picha chakula kimewekwa ndani ya karai refu na tumejipanga tukila kama nguruwe. Kulikuwa hakuna hema wala kitanda cha nyasi. Hayo ndiyo maisha niliyoishi. Pochi yangu ya fedha niliichimbia sehemu nilipoweka alama lakini sikuwa na matumaini iwapo nitakuja kuichimbua.

"Mwanzoni nilifanya kazi kwa bidii lakini kadri miezi ilivyozidi kwenda nilianza kukata tamaa.
Nilipatwa na homa kutokana na joto kali na nikapoteza hamu ya kula. Usiku nilikuwa nikijigeuza geuza tu kwa kukosa usingizi.

"Katika taabu ile nilikumbuka maneno ya Zabado, 'kutojivunja mgongo kwa kutegea kazi'. Hapo nikakumbuka hali niliyomuona nayo kwa mara ya mwisho. Nikaona kuwa mbinu yake haisaidii kitu.

"Nikamkumbuka Haramia na ujeuri wake. Nikawaza iwapo nipambane na kuua. Lakini kumbukumbu ya mwili wake uliojaa damu ikaniambia kuwa mbinu yake haisaidii kitu.

"Mwishowe nikakumbuka mara ya mwisho niliyoonana na Megiddo. Mikono yake ilikuwa imekomaa kwa kufanya kazi kwa bidii lakini uso wake ulikuwa ni wenye furaha sana. Mbinu yake ndiyo ilikuwa bora zaidi.
Mkuu! Kuna roho nyingi sana unaziponya kwa kupitia kazi yako njema!! Hakika Mungu atakulipa mara dufu!! maana hakuna aliyemtumikia Mungu akabaki mikono mitupu!! hakuna aliyemtumikia Mungu akapata aibu! Mungu aukumbuke na uzao wako!!
 
Kimenifunza vingi sana hiki kitabu,Hongera mkuu kwa kazi ngumu uliyoifanya

Binafsi,hivi ni vitu nilivyojifunza katika sura zote hizo

1.Usiwe mtumwa wa pesa,ifanye pesa iwe mtumwa wako
-Asilimia 80 ya watu tumekua watumwa wa pesa bila kutambua,pesa inatutumikisha kila siku,inabidi kila siku tufanye kazi kuipata pesa ili watoto wale,chakula kipatikane,bundle liwepo,Tanesco,tuwahonge watoto wakali etc
Tunajikuta tupo kwenye duara(loop) la kuitumikia pesa kwa kufanya kazi ili tuwezo kutimiza mambo ya lazima pamoja na matamanio yetu mengine

Na siku ikipita bila kufanya kazi,pesa inatuadhibu kwa kutotimiza matumizi yetu(mambo ya lazima na matamanio yetu)

Kitabu kinatufunza kuondoa hii "mindset" ya kimasikini na kuifanya pesa iwe mtumwa wetu

Badala ya sisi kufanya kazi na kupata pesa itakayokidhii mahitaji yetu,basi itufanyie kazi ya kukidhii mahitaji yetu

Hapa kinatupa siri kuwa,masikini tunaamini sisi ndiyo tuna jukumu la kufanya kazi kwa bidii ili maisha yaende wakati "matajiri" pesa ndiyo inajukumu la kufanya kazi kwa bidii ili maisha yaendee

MATAJIRI HAWAFANYI KAZI,UKITAKA KUWA TAJIRI ACHA KUFANYA KAZI,AJIRI PESA IKUFANYIE KAZI

2.Funzo la pili nililojifunza hapa,ni jinsi ya kuajiri pesa
-Pesa sio ile tunayoipata baada ya kufanya kazi(iwe faida kwenye biashara au mshahara wa mwisho wa mwezi)
-Pesa ni kile tunachokitunza kwa kuweka akiba
-Kama unaingiza Tsh 10,000 kwa siku basi hakikisha unaweka akiba ya 1,000,yaani 1/10 ya kipato chako cha kila siku

Kama unategemea mshahara,labda wa Tsh 300,000 kwa mwezi,kwa siku unaingiza kiasi cha Tsh 300,000(mshahara wako)/30(idadi ya siku katika mwezi) ambayo ni sawa na Tsh 10,000 kwa siku
Hapa hakikisha matumizi yako kwa siku hayazidi Tsh 9000
Hapa utakua unaweza kuokoa Tsh 1,000 kila siku katika mshahara wako na kujikuta una akiba ya Tsh 30,000 kila mwezi(1000 * 30(idadi ya siku katika mwezi)

Fanya hivyo kwa kipindi cha mda maalum(napendekeza ndani ya kipindi cha mwaka mmoja au zaidi)

Kwa mwenye kipato cha 10,000 kwa siku,ndani ya mwaka mmoja atakua na akiba ya Tsh (10,000/10 * 366(idadi ya siku katika mwaka)
Sawa na Tsh 366,000 kwa mwaka

Kwa mwenye mshahara wa Tsh 300,000 mpaka mwisho wa mwezi atakua na Akiba ya Tsh 366,000 pia
(Hapo tumeona jinsi gani ya kuweka akiba kwa mfanyabiashara au mfanyakazi)
10% ya pato lako ni kiwango cha chini zaidi ya pato lako,unaweza kuiongeza kwa kupunguza matumizi yasio ya lazima (matamanio)

Kwa mfano kama mahitaji yako ya kila siku ni Tsh 9,000 na kipato chako kwa siku ni Tsh 10,000 hapa akiba yako kwa siku (10% ya pato lako) ni Tsh 1,000.unaweza kuiongeza kuiongeza kwa kuondoa matamanio kwenye matumizi yako ya kila siku

Hii ni kanuni rahisi,
Mahitaji ya kila siku = matumizi ya lazima kwa siku + matamanio ya siku

Hakikisha, matamanio ya siku = 0
Hapa unaweza jikuta unatumia Tsh 7,000 badala ya Tsh 9,000 na akiba yako ikawa Tsh 2,000 (20% ya pato lako) badala ya Tsh 1,000(10% ya pato lako) hivyo kwa mwaka utakua na Tsh 732,000 badala ya Tsh 366,000
Hapa utaona kwa kuondoa matamanio yako(matumizi yasio ya lazima) unaweza ku "double" pato lako la mwaka

Nafikiri kanuni rahisi ni hii
Hapo utakua umepata mtumwa /mfanyakazi wako wa kwanza mwenye thamani ya Tsh 732,000 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja tu

Hivi ndiyo jinsi ya kuajiri pesa,tunaajiri pesa kwa kuweka akiba

3.Funzo la tatu nililojifunza ni jinsi sasa ya kuipatia kazi ya kufanya pesa yetu tuliyo iajiri
Hapa tunakua na wazo lolote lile la biashara(kumbuka hii ni biashara ambayo hatutafanya sisi)
Lengo sio sisi kufanya kazi,tayari tuna mfanyakazi Mr Tsh 732,000 atakaye fanya hii kazi

Baada ya kupata wazo letu,tuseme labda (Mgahawa wa chakula cha asubuhi)
Tunatafuta watu wenye uzoefu na aina hii ya biashara ili kupata ushauri kutoka kwao,watu wenye uzoefu ni mara zote watu waliofanikiwa kwenye biashara husika

Baada ya kupata ushauri kutoka kwao,pia tunahakikisha tunatafuta wahudumu wenye uzoefu

Baada ya kupiga hesabu na kuhakikisha hatupo kwenye risk ya mpoteza mfanyakazi wetu Mr Tsh 732,000 hapa ndipo tunapo mtuma akafanye kazi
Kwa kila faida atakayo ingiza kwa siku,tunaitumia kuajiri pesa nyingine,nayo tutaipa kazi na chochote itakacho ingiza tutaitumia kuajir nyingine kwa hekima ile ile ya kwanza

4.Funzo la nne,ni kuwa na moyo wenye uthubutu wa kufanya jambo,kuwa na nia ya kweli,na tamaa ya mafanikio

5.Tuzione changamoto kama fursa(roho ya mtu huru),kuliko kuziona kama matatizo(roho ya mtumwa)

6.Tuzungukwe na marafiki waliofanikiwa na watakao weza kutupa ushauri

7.Tusijitese sana,kuna mda tukate kiu ya matamanio yetu,bila kuathiri kipato chetu

Hayo ni machache kati ya mengi niliyojifunza
 
The Richest man in Babylon is one good book that I would advise anyone to endorse himself/herself.The problem is that most of the time we study these books and add them to our book collection with little application.

Very true. We read some amazing books, with lots of knowledge.
The story ends up there. Literally we rarely take the lessons and apply anywhere in our lives.
Sometimes I think meditation can help us manage the transition between learning something and doing. I don't do meditation myself
 
Chukuwa kopi yako kwa kiswahili
timizamalengo_bookshop_20210419_115956_0.jpg
 
Hayo maisha uliyoyapitia kuna watu wanayapitia sasa ivi unaposema hii comment

Wengine hawana access ya huu uzi wa Red Giant
Tujifunze kuwa walimu wa wenzetu,
I hope mkuu hutoruhusu hicho kipindi kijirudie
Naahidi kuwa mwalimu muzur kwa vijana!! maana vijana wengi wanajitoa uhai kwa mazira wanayopitia!!

Hawana pa kujifunza!! na Kuna watu wanauwezo wa kufundisha, lakini wanajiuliza "nitapata nn nikimfundisha" wengine wanasema " mtu mwenyewe hanihusu"
Kumbe tungeondoa ubinafisi Kama red giant tungeokoa roho nyingi sana!!
Mungu aendelee kutuinulia watu Kama red giant. Nisi pia tujifunze kushea vipawa vyetu na wengine!
 
Hivi ukiwa unasoma kitabu chenye lugha ya kiingereza Pdf kuna uwezekano ukibadili kiwe lugha ya kiswahili maana huwa nachokaga kuaangalia maneno magumu kwenye dictionary mwisho simalizi kitabu
 
Sijaelewa kidogo hapo anaposema inatakiwa ujilipe 10% ya mapato yako. Je ansmaanisha ndani ya hiyohiyo 10% ndio uweze kumudu matumizi ya kila siku? Na nyingine uwekeze izalishe ndani ya hiyohiyo 10%?. Na vipi kuhusu 90% inayobaki?. Mlioelewa tafadhali mtueleweshe sisi wa Std 4.
Amesema asilimia kumi ya kipato unaweka na asilimia tisini ndio unafanya matumizi .kanuni kuu hapa ni kusave hela kabla ya matumizi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom