Mimi na rafiki yangu siku moja tulifedheheka vibaya, ilikuwa hivi; Enzi zile tukiwa shule, Wakati wa likizo nilikwenda kwa rafiki yangu kumtembelea kwao. Home kwao kulikuwa na nyumba kubwa na kila mtu na chumba chake. Jamaa shule tulikuwa tukimwita pastor like boy, kumbe jamaa anazuga. Baba yake alikuwa mchungaji pale kijijini kwao. Mchana wa siku ya pili tulikuwa peke yetu pale kwao, tukala chakula,kumbe jamaa ana vibotro vichache chini ya uvungu wa kitanda. Tukashushia. Mtoto wa kaka yake mkubwa kumbe aliona vile vibotro, akauliza nini hiki baba mdogo,akajibiwa haya ni maji. Dogo akatulia.
Jioni wakati tuko mezani karibu familia nzima tunakula, mzee akaomba aletewe maji ya kunywa, kale katoto kakachomoka fasta kwenda chumbani kuchukua maji ya ilala. Sisi tulishasahau kuwa tulikalia bomu. Kakafika pale kumpa babu yake ashushie. Kisia nini kilitokea?
Yule mzee alisema, kijana( yaani mimi) unaniharibia mwanangu. Usiku ulikuwa mrefu sijapata kuona, sijakanyaga pale mpaka leo. :angry:
Jioni wakati tuko mezani karibu familia nzima tunakula, mzee akaomba aletewe maji ya kunywa, kale katoto kakachomoka fasta kwenda chumbani kuchukua maji ya ilala. Sisi tulishasahau kuwa tulikalia bomu. Kakafika pale kumpa babu yake ashushie. Kisia nini kilitokea?
Yule mzee alisema, kijana( yaani mimi) unaniharibia mwanangu. Usiku ulikuwa mrefu sijapata kuona, sijakanyaga pale mpaka leo. :angry: