Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,739
- 155,433
- Thread starter
- #21
SwalamaUmeamkaje mkuu
SwalamaUmeamkaje mkuu
Asante sanaSwalama
SwadaktaAsante sana
Kama unawasiliano nae mwambie anirushie majini yake PMNakumbuka miaka ya nyuma kulikiwa na mkuu wa mkoa mwanamke jijini Dar es Salaam. Huyu mama hakuwa mwingine ila Mary Chipungahelo au waweza mama Chips.
Huyu mama alikuwa ni mbabe haswa, asiyeyumbishwa wala kuburuzwa wala kupelekeshwa. Ameshawahi kumzingua kichizi Jenerali Ulimwengu.
Basi kipindi hicho nilikuwa naishi Kijitonyama Kisiwani, asubuhi na mapema nikatembelewa na mgeni, mdada wa haja, kapanda, ana bonge la shepu na sura nzuri.
Dada akaanza kunikumbusha kwamba tuliishi wote zamani tukiwa wadogo huko Nkajha kwa Kisugujhila.
Nikamkumbuka, akaaza kunipa kisa cha maisha yake. Akasema yeye ameolewa mitala, yeye ni mke mdogo.
Mumewe ni tajiri wa Kiarabu na alikutana naye Zanzibar ambapo alikuwa anafanya kazi ya uuguzi katika hospitali moja binafsi.
Kutokana na utajiri wa huyo Mwarabu, binti akaona abadili dini ili aweze kuolewa mke wa pili kisheria.
Bi mkubwa hakupenda, hapo ndio visa na mikasa ya kiganga ikaanza.
Dada akatumiwa majini yamuuwe, lakini dada naye alikuwa vizuri,majini hayakuwez kumuua ila kumtesa tu.
Siku hiyo alipokuja home, kuna dada mmoja alikuwepo na tulikuwa na mihadi ya kukutana na dada mwingine, Lulu Peter Muga.
Tukiwa tumekaa sebuleni, tukasukia mlango ukigongwa, ikajua Lulu anakuja, nikainuka kwenda kufungua. Lakini yule dada mke wa Mwarabu akasema usiende, hilo ni jini linautafuta. Ukienda hutoona kitu ila kuku, kimoyomoyo usinizingue. Nikaenda. Kweli sikukuta mtu ila kuku. Nikarudi ndani, nikaulizwa umeona nini? Nikajibu nimeona kuku.
Basi tukaendelea na mazungumzo huku akiendelea kutusimulia mikasa ambayo amekuwa akifanyiwa na majini.
Hodi ikapigwa tena, nami nikaenda kufungua. Akaniambia getini utawakuta wanafunzi wanataka maji, beba jug na vikombe kabisa. Nikampuuza, nilipofika getini nikakuta kuna waafunzi wanaomba maji, nikarudi ndani kwa aibu, nikachikua jug na vikombe nikaenda kuwapa watoto maji.
Hodi ikapigwa tena, akasema huyo ni mgeni wako kampokee. Kweli, alikuwa Lulu Peter Muga. Nikamkaribisha ndani.
Dada aliendelwa na story zake za kusisimua na kuogopesha sana za majini wanaoitaka roho yake.
Geti likagongwa tena, akasema huyo mtu anayekuja ni mchafu. Nikaenda kufungua, alikuwa Chips mtoto wa mkuu wa mkoa.
Chips alikuwa ametoka kuvuta bangizake, na bangi na majini havipatani.
Dada mashetani yakapanda, akavua nguo zake zote, na cheni, na Pete zake za dhahabu, akatoka mbio, alikuwa na nguvu za ajabu, hatukuweza kumdhibiti.
Baada ya wiki mbili, nikiwa naangalia taarifa ya habari, nikasikia geti likigongwa. Nilipoenda kufungua, alikuwa yule binti amekuja, ameng'aa yuko na mama yake, wenge hana tena.
Mama yake akaeleza kuwa walienda kwenye maombi, sasa binti yuko safi.
Nikawapa nguo zao, pochi, simu, fedha na mikufu na Pete zake za dhababu.
Tukala, wakaondoka.
Wiki ijayo ndio tunaenda ku finaliseKama unawasiliano nae mwambie anirushie majini yake PM
Harafu chief ile story yako ya baba mkwe iliishia wapi?
Ngoja tusubiri mrejesho utanitonya.Wiki ijayo ndio tunaenda ku finalise