Umeme wakatisha maisha ya vichanga Hospitalini Muhimbili

Hayo ni maelezo ya kina mama wako quoted wewe, soma juu vizuri. The point is, iwe dakika kumi au ishirini, why? why not immediately as usual? kwani ingekuwa si jenereta la automatic mambo yangekuwa ni kama hili janga lililotokea sasa. Lakini kabla ya hapo hatukusikia ina maana jenereta lipo na ni automatic, what was the real problem? mimi conclusion yangu ni uzembe wa watendaji pale Muhimbili na si JK. Upo hapo ulipo?

Hii Hospital si iko chini ya yule waziri anayeunda tume kuchunguza tume ? na hata matokeo ya tume ya kuchunga tume huwa hayatoi hadharani? sintoshangaa mh huyu akiunda tume kuchunguza tume na tume ambayo itakuwa inachunguza tume zilizopita..kazi kweli kweli, pole wa wafiwa wa watoto wao jamani....inauma lakini ni Tanzania yetu
 
Hayo ni maelezo ya kina mama wako quoted wewe, soma juu vizuri. The point is, iwe dakika kumi au ishirini, why? why not immediately as usual? kwani ingekuwa si jenereta la automatic mambo yangekuwa ni kama hili janga lililotokea sasa. Lakini kabla ya hapo hatukusikia ina maana jenereta lipo na ni automatic, what was the real problem? mimi conclusion yangu ni uzembe wa watendaji pale Muhimbili na si JK. Upo hapo ulipo?

Wakizungumza na mwandishi wa habari hii hospitalini hapo jana, baadhi ya akina mama wanaouguza watoto wao (majina yanahifadhiwa) walisema kwamba, umeme ulikatika majira ya saa 9 usiku wa kuamkia jana.

Akina mama hao walisema, baada ya umeme kukatika, walizuiwa kwenda kuwanyonyesha watoto wao kutokana na giza nene kutanda katika maeneo mbalimbali, ikiwamo chumba walichokuwa wamelazwa watoto hao hospitalini hapo.

Walieleza kwamba baada ya kukaa gizani kwa muda wa dakika 10, umeme wa jenereta uliwaka ambapo waliruhusiwa kwenda kuwanyonyesha watoto wao.

Hata hivyo, walisema baada ya kufika, walikuta baadhi ya vitanda walikolazwa watoto vimezungushiwa mapazia ya kijani.

Umeme ulikatika majira ya saa tisa. Tukakaa gizani kwa muda wa dakika 10. Ndipo umeme wa jenereta ukawashwa. Tulipokwenda kuwanyonyesha watoto wetu, tukakuta vyumba vitano vimezungushiwa mapazia ya kijani huku wenzetu wakilia kwa uchungu wa kupoteza watoto wao, alisema mmoja wa akina mama hao.

Baadhi ya madaktari wa watoto hospitalini hapo, walikiri kwamba, kitendo cha umeme kukatika ndani ya dakika 10, ni hatari kwa afya ya mgonjwa yeyote anayepumua kwa kutumia mashine na kwamba, kwa watoto wachanga ni hatari zaidi japo hawajafahamu kama kweli vifo vyao vimetokana na kukatika kwa umeme.

Madaktari hao pia walikiri kwamba watoto hao walikuwa wachanga na wengine walizaliwa wakiwa njiti na kusisitiza kuwa kinachosababisha waweze kuishi ni mashine.


Una hakika gani kuwa jenereta iliyokuwepo ni automatic? Kwa kuongezea, mashine sensitive za karne hii, jenereta haitoshi. Kutosikia taarifa kama hizi si ushahidi kuwa havitokei. Watanzania hawana kawaida ya kulalamika. Ndiyo tulivyo. Ukisoma majibu ya madaktari ni ya kujihami. Sitoshangaa kesho kusikia kuwa halikuwa tatizo la kukatika umeme.

Nakubaliana nawe kuwa kuna dalili za uzembe katika suala zima. Kwa kawaida mashine zakisasa zinahitaji UPS ambayo inahakikisha kuwa hakuna downtime hata ya sekunde moja. Na hizi si vile vinavyowekwa chini ya meza kwenye maofisi yetu. Lakini pengine hizo mashine za kupumilia hazihitaji hizo UPS. Hilo nakiri sijui.

Kinachonisikitisha zaidi ni kuwa haya yanatokea Muhimbili. Je huko ambako waandishi wa habari hawafiki? Wangapi wanapoteza maisha kutokana na uzembe?

Mimi matatizo yangu ni hao madaktari na wataalamu wengine. Sijawahi kuwasikia wakifanya mgomo kulalamikia mazingira ya kufanyia kazi.Mazingira haya yanajumuisha pia vitendea kazi vya kuaminika. Wao ni mishahara tu. Ninavyoona mimi, mazingira ni muhimu zaidi. Sidhani kama nimemtaja JK kwenye hili!
 
"Tuunde tume, kuna tume imeundwa, tusubiri matokeo ya tume, tume yatembelea vijjij kukusanya maoni, tume yafanya majadiliano, tume tume tume'!

Tume ya Muhimbili kuchunguza upasuaji, tume ya Raisi ya Madini, tume ya uchunguzi BOT, tume ya Dawasco, tume uratibu wa tume!

This is what our government has become. everything has a tume that is given a time frame that allows last minute uhujumu!

Okay, kwanza ni pole kwa wafiwa.

Pili je ni nini kilichotokea?

  • Je ni kwa nini umeme wa Tanesco ulikatika? ni sababu za kiufundi, kiutendaji, uzembe, ajali au...?
  • Je kwa nini ilichukua dakika 10 kwa Muhimbili kuanza kutumia umeme wa jenereta? je fundi alikuwa amelala, walikuwa hawana mawe kwenye kurunzi kuona swichi ilipo? je mafuta yalikuwa yamepungua kina cha kuwasha jenereta? je walisubiri mhandisi mkuu aongee na mkurugenzi mkuu wapate kibali cha kuwasha jenereta na kutumia mafuta ya dharura?
  • Yameshatokea, je ni mipango gani itfanyika kuhakikisha kuwa patakapotokea tatizo kama hili wakati mwingine, ile mitambo ya kisasa inayojiwasha katika sekunde moja itakuwa ipo na inafanya kazi?
  • Je hospitali na sehemu nyingine nyeti zina mipango gani madhubuti ya kuwa na mitambo ya kisasa kuhakikisha kuwa panapotokea matatizo kama haya, basi kuna back na recovery inafanyika katika sekunde na si dakika?
  • Je Tanesco hawana powersource maalumu ambazo zitalisha sehemu nyeti daima kwa kualternate hata kama powersource moja imepata shida?
Tunadai uwajibikaji, je ni nani awajibike? Mhandisi mkuu, fundi wa zamu, mganga mkuu, wakurugenzi wakuu Muhimbili na Tanesco?, Waziri wa Afya, waziri wa Nishati, waziri mkuu, Raisi?

Kwa kuwa awamu ya nne imejijengea sifa ya kufanya mambo at ease, na kujivuta, sishangai ghadhabu za wana JF kudai ni uzembe wa Serikali hata kudai Rais awajibike. Iwapo Raisi angekuwa anafanya maamuzi mengine swiftly bila kuonekana na kigugumizi au kutafuta "win-win situation" inayoishia kumuonyesha kuwa hana uwezo wa kufanya maamuzi ya kuwajibisha watu, tusingekuwa na malezi komau ya watu na watendaji wasiojituma na kuwajibika bila kusukumwa!
 
Una hakika gani kuwa jenereta iliyokuwepo ni automatic? Kwa kuongezea, mashine sensitive za karne hii, jenereta haitoshi. Kutosikia taarifa kama hizi si ushahidi kuwa havitokei. Watanzania hawana kawaida ya kulalamika. Ndiyo tulivyo. Ukisoma majibu ya madaktari ni ya kujihami. Sitoshangaa kesho kusikia kuwa halikuwa tatizo la kukatika umeme.

Nakubaliana nawe kuwa kuna dalili za uzembe katika suala zima. Kwa kawaida mashine zakisasa zinahitaji UPS ambayo inahakikisha kuwa hakuna downtime hata ya sekunde moja. Na hizi si vile vinavyowekwa chini ya meza kwenye maofisi yetu. Lakini pengine hizo mashine za kupumilia hazihitaji hizo UPS. Hilo nakiri sijui.

Kinachonisikitisha zaidi ni kuwa haya yanatokea Muhimbili. Je huko ambako waandishi wa habari hawafiki? Wangapi wanapoteza maisha kutokana na uzembe?

Mimi matatizo yangu ni hao madaktari na wataalamu wengine. Sijawahi kuwasikia wakifanya mgomo kulalamikia mazingira ya kufanyia kazi.Mazingira haya yanajumuisha pia vitendea kazi vya kuaminika. Wao ni mishahara tu. Ninavyoona mimi, mazingira ni muhimu zaidi. Sidhani kama nimemtaja JK kwenye hili!

Fundi,

Watalalamikije kuhusu mazingira na vitendea kazi wakati kuna uwezekano wanavihujumu? Alipokuwepo Daudi Trigonometry, walilalamika sana kuwa jamaa ni mkoloni, mkali ananyanyasa.

Lakini Daudi alikuwa akifanya kazi kuhakikisha kuwa hospitali ina zana za kutosha na nidhamu ya kazi inarudi. Walichokimbilia kulalamika si kuhusu utendaji wa Daudi bali ni marupurupu anayolipwa.

Tumemfukuza Trigonometry, tumewaleta "wenzetu". Tumeanza majungu tena, ooh sijui ni Mchaga, hana Digrii za kutosha za upasuaji, kila mtu kafungulia bomba la kula na kubangaiza maana mkoloni kaondoka na malalamishi mengi.

Sijui tena ni ni nini ambacho tunahitaji kama Taifa tunawajibika kukifanya kuhakikisha kuwa tunaachana na uzubafu ambao unatuondolea ufanisi na upevu wa kufanya mambo kwa kujituma na kuwajibika!

Tutadai mishahara zaidi kama wenzetu wa Botswana, huku kusoma chati kuuliza jina la mgonjwa vinatushinda!
 
......hayo ndio matatizo ya serikali kuuuuuuuuuubwa kama dunia!!
Hizo ndio zinaitwa bureaucratic nightmare, hii siyo issue ya JK ila hapo muhimbili inabidi mtu awajibike. hii kitu imekaa kama mchezo wa kuigiza.
 
Apa kwanza waziri wa afya awajibike pamoja na na uyo aliyepewa rungu la kusimamia iyo hospitali.

Hospitali kubwa kama muhimbili mnakosa standby Generator wakati nowdays ni kitu cha kawaida.

Utasikia soon tume itaundwa kuchunguza ilo na uku generator likiwa bado ni tatizo.

Kwa mtu makini TANESCO sio wa kuwategemea kabisa mimi mwenyewe kwangu tuu siwategemei sembuse hosp kubwa kama muhimbili.

Mbona kila kona kona watz tunaonekana hatuko seriuous wapi sasa tutakuwa serious jamani?

Someone has to pay the cost of of our beloved children who have passed away.

My their souls rest in peace.Amen
 
Kamwambie aliyekutuma, wanaJF wanauliza hivi huko jikoni ni wapi ili tuje tumsaidie kutafuta dawa?


Hivi miaka yote JK aliyo kaa serikalini hakuwahi kujua nini hasa matatizo ya Tanzania ? Uliutaka wa kazi gani kama hakujua lolote la Nchi ? Hebu acha kutuptezea muda kusema JK kaurithi wakati JK ni mmoja wa hawa walio lete matatizo haya .
 
dar Es salaam hapa vipi hujasema jk asifiwe ? Mbona unaacha hoja na kumshambulia jamaa ? Nilitegemea utaendeleza kumwaga sifa kwa jamaa kwamba anachapa kazi .

kasome thread kuanzia mwanzo ujue nimesema nini, usikurupuke.
 
Ahsante kwa kuniikumbuka, nimefika.

Jee, kama genereta lipo tatizo ni JK? ingekuwa genereta hakuna hapo ndio tungemshutumu Mkuu.

Haya ni makosa ya watendaji na inabidi hatuwa za haraka zifanyike na wachukuliwe hatua za kisheria na kinidhamu kwa makusudi kabisa.

Uozo wa utendaji Muhimbili unaonyesha kukomaa, (nikikumbuka na kisa cha kizembe kabisa cha kuchanganya wagonjwa).

Laiti ungekuwa unazitazama vizuri posts zangu kwa muono mpana ungenielewa vizuri kabisa.

Kumbuka uozo wa hii nchi kaurithi JK, na hivi sasa yupo jikoni kuutafutia dawa. Kwanza tumeona ameanza na rushwa, ubadhirifu na ufisadi na hivyo ndio vyanzo vya matatizo yote haya. Halafu yanafatia haya ya uzembe, kumbuka aliwekwa Muingereza pale Muhimbili kuiendesha, akapikiwa majungu mpaka akatimka, kwa nini? kwa kuwa alikuwa anawajibika ipasavyo na kuna wengi pale wakaona wanazibiwa njia zao za ubadhirifu na ufisadi na matokeo ndio hayo.

Uzembe huu (wa Muhimbili in particular) ni confined within Muhimbili na haujaanza leo na inabidi ushughulikiwe kikamilifu.

Hau-expect kuwa Rais wa nchi akumbushe mpaka mafuta ya genereta!

Hii itakuwa si kumtendea Rais haki, kabisa.

Kama mimi sijaelewa kinachozungumzwa nadhani na wewe hujaelewa kabisa nnchozungumza mimi, simply, Jee, unataka kumlaumu JK kwa kucheleweshwa kuwashwa genereta muhimbili? Ukisha jibu hilo itakuwa umeelewa nichozungumza.

Kuhusu maswala ya ufisadi na rushwa nadhani unajuwa ni nini JK anachokifanya kwa uozo alioukuta. Sina haja yakurudia rudia, tume zipo na kazi zinazofanyika zinajulikana kwa wanaotaka kuona.

Kuhusu kuwajibisha mawaziri wake, duhhh, unanishangaza, yaani hata mwezi haujapita, haujayaona ya kina Lowassa, karamagi na msabaha. Wacha kuwajibisha mawaziri. JK kaweka history ya kumuwajibisha waziri mkuu.

Kuhusu kuto-kufanya kazi zake, na hili pia unanishangaza sana tena sana, wewe unaujuwa uozo aliouruthi JK? au huujuwi? kama unaujuwa sina haja ya kuanza kukutajia mmoja mmoja, kama huujuwi niambie nikutajie na nikujulishe anaushghulikia vipi kama hujui.

Kwa hili Mkuu Rufiji nakuunga mkono mia kwa mia.

Kuna watu wantaka kupotosha kuwa genereta ilikuwa hakuna, nawashangaa sana, yaani hamkuisoma ile post ya mwanzo? inasema hivi:

" ...Walieleza kwamba baada ya kukaa gizani kwa muda wa dakika 10, umeme wa jenereta uliwaka ambapo waliruhusiwa kwenda kuwanyonyesha watoto wao...

Jenereta lipo, tatizo ni kwa nini liwake dakika 10 baadae?


Ingekuwa ni hivyo usemavyo wewe basi kila siku tungesikia tatizo hilo.

Hayo ni maelezo ya kina mama wako quoted wewe, soma juu vizuri. The point is, iwe dakika kumi au ishirini, why? why not immediately as usual? kwani ingekuwa si jenereta la automatic mambo yangekuwa ni kama hili janga lililotokea sasa. Lakini kabla ya hapo hatukusikia ina maana jenereta lipo na ni automatic, what was the real problem? mimi conclusion yangu ni uzembe wa watendaji pale Muhimbili na si JK. Upo hapo ulipo?

Ungekuwa unaweza ungewahi wewe jikoni.

dar Es salaam hapa vipi hujasema jk asifiwe ? Mbona unaacha hoja na kumshambulia jamaa ? Nilitegemea utaendeleza kumwaga sifa kwa jamaa kwamba anachapa kazi .

Kwa kukurahisishia nimekuwekea posts zangu zote kuhusu thread hii hapa ili usisumbuke kuzitafuta. Halafu sasa tuanze na maswali yako, kama hayana majibu kwenye hizo post.
 
Kuna watu wantaka kupotosha kuwa genereta ilikuwa hakuna, nawashangaa sana, yaani hamkuisoma ile post ya mwanzo? inasema hivi:

" ...Walieleza kwamba baada ya kukaa gizani kwa muda wa dakika 10, umeme wa jenereta uliwaka ambapo waliruhusiwa kwenda kuwanyonyesha watoto wao...

Jenereta lipo, tatizo ni kwa nini liwake dakika 10 baadae?


Labda lilichelewa kuwaka kwa sababu lilikuwa linasubiri kuundiwa Kamati Teule!
 
kwi kwi kwi kwi kwi...

kamati teule na baada ya hapo iundwe tume ya kuchunguza kamati teule!

kama ile kamati teule tuliyoiunda kutaka kamati ya ushindi KiTETO ichunguzwe ilishindwaje? au sio? Ha ha ha ha haaaaaaaaaaa ha!
 
kama ile kamati teule tuliyoiunda kutaka kamati ya ushindi KiTETO ichunguzwe ilishindwaje? au sio? Ha ha ha ha haaaaaaaaaaa ha!

Cha kuchekesha hapa ni kipi sasa! Watu walisha-move on kutoka Kiteto na sasa kuna miziki mipya inawekwa hapa JF na wewe unaleta kifafa hapa!

tik tak tik tak!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom