Umeme wakatisha maisha ya vichanga Hospitalini Muhimbili

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Na hii ndio hospitali yetu ya rufaa! Nilidhani sehemu nyeti kama hiyo umeme ukizimika tu basi majenereta yanaanza kazi mara moja, kumbe sivyo! Wafungue kesi dhidi ya Muhimbili

Posted Date::2/28/2008
Umeme wakatisha maisha ya vichanga Hospitalini Muhimbili
*Ni baada ya kukatatika usiku wa manane
*Watano wadaiwa kufariki kwa kukosa hewa

Na Jackson Odoyo

WATOTO watano waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), jijini Dar es Salaam, wanahofiwa kufariki dunia baada ya kukosa hewa kutokana na kukatika kwa umeme hospitalini hapo.


Habari kutoka hospitalini zinaeleza kuwa kabla ya tukio hilo, watoto hao walikuwa wakipumua kwa kutumia mashine kutokana na matatizo mbalimbali ya kiafya, ikiwamo wawili waliozaliwa wakiwa njiti.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hii hospitalini hapo jana, baadhi ya akina mama wanaouguza watoto wao (majina yanahifadhiwa) walisema kwamba, umeme ulikatika majira ya saa 9 usiku wa kuamkia jana.

Akina mama hao walisema, baada ya umeme kukatika, walizuiwa kwenda kuwanyonyesha watoto wao kutokana na giza nene kutanda katika maeneo mbalimbali, ikiwamo chumba walichokuwa wamelazwa watoto hao hospitalini hapo.

Walieleza kwamba baada ya kukaa gizani kwa muda wa dakika 10, umeme wa jenereta uliwaka ambapo waliruhusiwa kwenda kuwanyonyesha watoto wao.

Hata hivyo, walisema baada ya kufika, walikuta baadhi ya vitanda walikolazwa watoto vimezungushiwa mapazia ya kijani.

Umeme ulikatika majira ya saa tisa. Tukakaa gizani kwa muda wa dakika 10. Ndipo umeme wa jenereta ukawashwa. Tulipokwenda kuwanyonyesha watoto wetu, tukakuta vyumba vitano vimezungushiwa mapazia ya kijani huku wenzetu wakilia kwa uchungu wa kupoteza watoto wao, alisema mmoja wa akina mama hao.

Baadhi ya madaktari wa watoto hospitalini hapo, walikiri kwamba, kitendo cha umeme kukatika ndani ya dakika 10, ni hatari kwa afya ya mgonjwa yeyote anayepumua kwa kutumia mashine na kwamba, kwa watoto wachanga ni hatari zaidi japo hawajafahamu kama kweli vifo vyao vimetokana na kukatika kwa umeme.

Madaktari hao pia walikiri kwamba watoto hao walikuwa wachanga na wengine walizaliwa wakiwa njiti na kusisitiza kuwa kinachosababisha waweze kuishi ni mashine.

Kutokana na hali hiyo, walisema hawawezi kupinga wala kukubali kufariki kwa watoto hao kwani hawakuwa zamu ya usiku siku hiyo na kukiri kwamba umeme ulikatika.

Hebu fikiria. Ukiwa ndani ya lifti, halafu umeme ukatike ndani ya dakika 10 au zaidi utakuwa kwenye hali gani? Sasa, kumbuka kwamba wale ni watoto na ni wagonjwa. Wataweza kuishi? Kama kweli walikufa kwa kukosa hewa, inabidi tumshukuru Mungu kwa kuwanusuru wagonjwa wengine waliokuwa katika hatari hiyo,? alisema daktari mmoja kati yao.

Naye Afisa Uhusiano wa MNH, Aminieli Aligahesha akizungumza na mwandishi wa habari hii ofisini kwake, alikiri kukatika kwa umeme hospitalini hapo na kukiri kwamba kuna baadhi ya maeneo yaliyoathirika kazi hazifanyiki, lakini sehemu muhimu wanatumia umeme wa jenereta.

Alisema baada ya umeme kukatika, mafundi wao walitumia dakika 10 kuunganisha umeme katika maeneo yote ya muhimu, ikiwemo wodi ya watoto na kwamba walipowasiliana na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) waliambiwa kuwa kuna kifaa cha kusambazia umeme kina tatizo na umeme huo umekatika sehemu nyingi za Jiji na si Muhimbili peke yake.

Aligahesha alisema baadhi ya maeneo yaliyoathirika baada ya umeme kukatika hospitali hapo, ni jengo jipya la watoto (OPD), maabara maalum ya watoto, vyumba vya upasuaji, wodi namba 36 inayotumika kuhifadhi watoto waliozaliwa njiti ni wadi 'A' na 'B', vyumba vya wagonjwa mahututi (ICU) na vyumba vya kuhifadhia maiti (mochwari) na kwamba kwa sasa wanatumia umeme wa jenereta.

Mbali na maeneo hayo yaliyoathirika na tukalazimika kutumia umeme wa jenereta, maeneo mengine yaliyoathirika na tukalazimika pia kubadilisha mfumo wa huduma kama vile sehemu za usajili wa wagonjwa ambapo awali tulikuwa tunatumia kompyuta ila kwa sasa tunatumia usajili wa kawaida, alisema Aligahesha.

Hata hivyo, Afisa Uhusiano huyo hakukiri wala kukanusha kufariki kwa watoto hao, badala yake alimtaka mwandishi wa habari hii kuwasiliana naye baadaye baada ya kuwasiliana na wahusika wa wodi hizo.

Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hii umebaini kuwa maeneo mengine yaliyoathiriwa na tatizo hilo, ni Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) ambako wamelazimika kutumia umeme wa jenereta.

Afisa Uhusiano wa MOI, Almas Jumaa alikiri na kusema japo umeme ulikatika, lakini maeneo ya muhimu yote hayakuathirika kwa sababu jenereta yao ni kubwa na imeunganishwa moja kwa moja kiasi kwamba umeme ukikatika ndani ya sekunde mbili unawaka tena.

Mkurugenzi Mkuu wa Muhimbili, Profesa Leonard Lema jana jioni alikataa kuzungumzia suala hilo kwenye simu na kusema kwamba kama gazeti linahitaji taarifa mwandishi amfuate ofisini.
 
Na hii ndio hospitali yetu ya rufaa! Nilidhani sehemu nyeti kama hiyo umeme ukizimika tu basi majenereta yanaanza kazi mara moja, kumbe sivyo! Wafungue kesi dhidi ya Muhimbili

Posted Date::2/28/2008
Umeme wakatisha maisha ya vichanga Hospitalini Muhimbili
*Ni baada ya kukatatika usiku wa manane
*Watano wadaiwa kufariki kwa kukosa hewa

Na Jackson Odoyo

WATOTO watano waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), jijini Dar es Salaam, wanahofiwa kufariki dunia baada ya kukosa hewa kutokana na kukatika kwa umeme hospitalini hapo.


Habari kutoka hospitalini zinaeleza kuwa kabla ya tukio hilo, watoto hao walikuwa wakipumua kwa kutumia mashine kutokana na matatizo mbalimbali ya kiafya, ikiwamo wawili waliozaliwa wakiwa njiti.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hii hospitalini hapo jana, baadhi ya akina mama wanaouguza watoto wao (majina yanahifadhiwa) walisema kwamba, umeme ulikatika majira ya saa 9 usiku wa kuamkia jana.

Akina mama hao walisema, baada ya umeme kukatika, walizuiwa kwenda kuwanyonyesha watoto wao kutokana na giza nene kutanda katika maeneo mbalimbali, ikiwamo chumba walichokuwa wamelazwa watoto hao hospitalini hapo.

Walieleza kwamba baada ya kukaa gizani kwa muda wa dakika 10, umeme wa jenereta uliwaka ambapo waliruhusiwa kwenda kuwanyonyesha watoto wao.

Hata hivyo, walisema baada ya kufika, walikuta baadhi ya vitanda walikolazwa watoto vimezungushiwa mapazia ya kijani.

Umeme ulikatika majira ya saa tisa. Tukakaa gizani kwa muda wa dakika 10. Ndipo umeme wa jenereta ukawashwa. Tulipokwenda kuwanyonyesha watoto wetu, tukakuta vyumba vitano vimezungushiwa mapazia ya kijani huku wenzetu wakilia kwa uchungu wa kupoteza watoto wao, alisema mmoja wa akina mama hao.

Baadhi ya madaktari wa watoto hospitalini hapo, walikiri kwamba, kitendo cha umeme kukatika ndani ya dakika 10, ni hatari kwa afya ya mgonjwa yeyote anayepumua kwa kutumia mashine na kwamba, kwa watoto wachanga ni hatari zaidi japo hawajafahamu kama kweli vifo vyao vimetokana na kukatika kwa umeme.

Madaktari hao pia walikiri kwamba watoto hao walikuwa wachanga na wengine walizaliwa wakiwa njiti na kusisitiza kuwa kinachosababisha waweze kuishi ni mashine.

Kutokana na hali hiyo, walisema hawawezi kupinga wala kukubali kufariki kwa watoto hao kwani hawakuwa zamu ya usiku siku hiyo na kukiri kwamba umeme ulikatika.

Hebu fikiria. Ukiwa ndani ya lifti, halafu umeme ukatike ndani ya dakika 10 au zaidi utakuwa kwenye hali gani? Sasa, kumbuka kwamba wale ni watoto na ni wagonjwa. Wataweza kuishi? Kama kweli walikufa kwa kukosa hewa, inabidi tumshukuru Mungu kwa kuwanusuru wagonjwa wengine waliokuwa katika hatari hiyo,? alisema daktari mmoja kati yao.

Naye Afisa Uhusiano wa MNH, Aminieli Aligahesha akizungumza na mwandishi wa habari hii ofisini kwake, alikiri kukatika kwa umeme hospitalini hapo na kukiri kwamba kuna baadhi ya maeneo yaliyoathirika kazi hazifanyiki, lakini sehemu muhimu wanatumia umeme wa jenereta.

Alisema baada ya umeme kukatika, mafundi wao walitumia dakika 10 kuunganisha umeme katika maeneo yote ya muhimu, ikiwemo wodi ya watoto na kwamba walipowasiliana na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) waliambiwa kuwa kuna kifaa cha kusambazia umeme kina tatizo na umeme huo umekatika sehemu nyingi za Jiji na si Muhimbili peke yake.

Aligahesha alisema baadhi ya maeneo yaliyoathirika baada ya umeme kukatika hospitali hapo, ni jengo jipya la watoto (OPD), maabara maalum ya watoto, vyumba vya upasuaji, wodi namba 36 inayotumika kuhifadhi watoto waliozaliwa njiti ni wadi 'A' na 'B', vyumba vya wagonjwa mahututi (ICU) na vyumba vya kuhifadhia maiti (mochwari) na kwamba kwa sasa wanatumia umeme wa jenereta.

Mbali na maeneo hayo yaliyoathirika na tukalazimika kutumia umeme wa jenereta, maeneo mengine yaliyoathirika na tukalazimika pia kubadilisha mfumo wa huduma kama vile sehemu za usajili wa wagonjwa ambapo awali tulikuwa tunatumia kompyuta ila kwa sasa tunatumia usajili wa kawaida, alisema Aligahesha.

Hata hivyo, Afisa Uhusiano huyo hakukiri wala kukanusha kufariki kwa watoto hao, badala yake alimtaka mwandishi wa habari hii kuwasiliana naye baadaye baada ya kuwasiliana na wahusika wa wodi hizo.

Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hii umebaini kuwa maeneo mengine yaliyoathiriwa na tatizo hilo, ni Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) ambako wamelazimika kutumia umeme wa jenereta.

Afisa Uhusiano wa MOI, Almas Jumaa alikiri na kusema japo umeme ulikatika, lakini maeneo ya muhimu yote hayakuathirika kwa sababu jenereta yao ni kubwa na imeunganishwa moja kwa moja kiasi kwamba umeme ukikatika ndani ya sekunde mbili unawaka tena.

Mkurugenzi Mkuu wa Muhimbili, Profesa Leonard Lema jana jioni alikataa kuzungumzia suala hilo kwenye simu na kusema kwamba kama gazeti linahitaji taarifa mwandishi amfuate ofisini.

Hongera sana ndugu JK . Nategemea ndugu Dar Es Salaam utafika hapa kumpa Hongera ndugu Rais kwa mambo yake makubwa haya .Mungu awarehemu hawa watoto .
 
Mimi hapa ndo ninapowambia wananchi hatuna serikali hata kidogo
Hivi inakuwaje sehemu nyeti kama hospitalini hawana automatic standby Generata jamani?
Mbona tunatia aibu jamani
Haya kikwete hangalia uzembe huu, unaofanya watu wanakufa hovyo kwa kukosa generate za uhakika, halafu pesa mnakula na kukumbatiana,
Narudia tena na nitasema siku zote, Serikali chini ya CCM ambayo ni chini ya hawa Mafisadi ni Huozo mtupu na inanuka.

Kikwete ebu jione haibu, hizo pesa mnazoiba mtazipeleka wapi? mtakufa mtaziacha tu, ila mtaenda kukutana na fimbo ya moto, na wewe utakuwa na maswali mengi ya kujibu, kwa sababu vifo vingi vinakuhusisha moja kwa moja, ni uzembe wa raisi ndo maana watu wanakufa kila mara
Mungu wapumzishe kwa amani,

Haya yanatokea wakati tume zikiundwa kurekebisha sijui nini vile?
 
...Mimi si mtetezi wa JK. Lakini nadhani hapa JK hausiki. Ni uzembe wa viongozi waliopewa dhamana ya kuongoza hii hospitali ya muhimbili. Uongozi wa hospitali inabidi uwajibike. Hii ni kashfa. Tunatakiwa kuandamana kuprotest uzembe wa hawa viongozi katika hospitali ya muhimbili. Juzi juzi aliyepaswa kupasuliwa mguu, kapasuliwa kichwa. Aliyepaswa kupasuliwa kichwa kapasuliwa mguu.

Wakati umefika sasa uongozi mzima wa hospitali ya muhimbili uwajibishwe kwa maslahi ya umma. Tulioandamana kupinga ujio wa raisi bush tanzania, naomba tujimwage tena mtaani. Hizi ndizo issue zinazotugusa moja kwa moja sisi kama watanzania. Waliokufa ni watoto zetu, ambao kesho na kesho kutwa wangelikuwa ni madaktari bingwa wa kuchunguza afya zetu wakati tunatembelea mikongojo.
 
Walilipa Bili..?

Mwana wa Kijijini hapa ni kwamba ni umeme ulikatika katika maiahs yetu ya kila siku ya umeme kukata na kurudi baada ya dakika 10 watoto wetu wamekufa kwa uzembe tu .

Kuna mtu anamsifia sana JK nimemuona naona imemchukua muda kuja kusifia na hapa kwa kazi nzuri ya kuua hawa malaika .
 
...Mimi si mtetezi wa JK. Lakini nadhani hapa JK hausiki. Ni uzembe wa viongozi waliopewa dhamana ya kuongoza hii hospitali ya muhimbili. Uongozi wa hospitali inabidi uwajibike. Hii ni kashfa. Tunatakiwa kuandamana kuprotest uzembe wa hawa viongozi katika hospitali ya muhimbili. Juzi juzi aliyepaswa kupasuliwa mguu, kapasuliwa kichwa. Aliyepaswa kupasuliwa kichwa kapasuliwa mguu.

Wakati umefika sasa uongozi mzima wa hospitali ya muhimbili uwajibishwe kwa maslahi ya umma. Tulioandamana kupinga ujio wa raisi bush tanzania, naomba tujimwage tena mtaani. Hizi ndizo issue zinazotugusa moja kwa moja sisi kama watanzania. Waliokufa ni watoto zetu, ambao kesho na kesho kutwa wangelikuwa ni madaktari bingwa wa kuchunguza afya zetu wakati tunatembelea mikongojo.

kama JK hausiki katika mambo kama haya ambayo yanatokea hapo Dar sijui ni wapi atahusika. Kumbuka kuwa kuna makampuni kibao yanalipwa pesa na serikali kuzalisha umeme ili mambo kama haya yasitokee.
 
Jamani hawa watoto malaika!!!!

Uwiii!!!!!!!

Naona uchungu sana! Watoto wazuri sana na chanzo cha furaha ktk jamii!

Naona ni uzembe zaidi kwa Uongozi wa Hospitali!
 
Jamani hawa watoto malaika!!!!

Uwiii!!!!!!!

Naona uchungu sana! Watoto wazuri sana na chanzo cha furaha ktk jamii!

Naona ni uzembe zaidi kwa Uongozi wa Hospitali!

ongezea viongozi wa serikali kuu inayoongozwa na ccm ambao ndio wametuletea richmond, IPTL, kiwira, songas ambazo zinalipwa hata bila ya kuzalisha umeme!

Damu imo mikononi mwao na wao wako bize nchi za nje kujaribu kuweka happy faces!
 
kama JK hausiki katika mambo kama haya ambayo yanatokea hapo Dar sijui ni wapi atahusika. Kumbuka kuwa kuna makampuni kibao yanalipwa pesa na serikali kuzalisha umeme ili mambo kama haya yasitokee.

Mwafrika na BabaH. Mnachoongea ni sahihi. Ni kweli pia kuwa mkubwa ni jalala. Napenda nieleweke wazi kuwa mimi sio mtetezi wa kikwete pamoja na mawaziri wake. Naomba mnielewe hivyo.

Viongozi wa hospitali ya muhimbili wanatakiwa kuwa na plan B katika issues kama hizi. Sasa wenyewe wanategemea umeme wa TANESCO bila kuwa na plan B. Wakisema kwamba kikwete aliwakataza kununua "standby" generators hapo nitawaelewa. Vinginevyo huu ni uzembe.

Mwafrika huwezi kulala giza na wanao kwa kukosa umeme nyumbani kwako simply because mumeo hajanunua mafuta ya taa, pindi dharura itakapotokea. Umeme unapokatika ghafla washa vibatari. Kasheshe ni kesho yake. Unatakiwa umtie kibano mumeo kwa nini ameshindwa kulipa bila ya umeme (kama bili ya umeme ndio ilikuwa ni chanzo cha dhahma hiyo).

Vita dhidi ya mafisadi, sio kigezo cha kuzembea kutimiza wajibu wetu. Hayo ni mawazo yangu.


 
Mwafrika na BabaH. Mnachoongea ni sahihi. Ni kweli pia kuwa mkubwa ni jalala. Napenda nieleweke wazi kuwa mimi sio mtetezi wa kikwete pamoja na mawaziri wake. Naomba mnielewe hivyo.

Viongozi wa hospitali ya muhimbili wanatakiwa kuwa na plan B katika issues kama hizi. Sasa wenyewe wanategemea umeme wa TANESCO bila kuwa na plan B. Wakisema kwamba kikwete aliwakataza kununua "standby" generators hapo nitawaelewa. Vinginevyo huu ni uzembe.

Mwafrika huwezi kulala giza na wanao kwa kukosa umeme nyumbani kwako simply because mumeo hajanunua mafuta ya taa, pindi dharura itakapotokea. Umeme unapokatika ghafla washa vibatari. Kasheshe ni kesho yake. Unatakiwa umtie kibano mumeo kwa nini ameshindwa kulipa bila ya umeme (kama bili ya umeme ndio ilikuwa ni chanzo cha dhahma hiyo).

Vita dhidi ya mafisadi, sio kigezo cha kuzembea kutimiza wajibu wetu. Hayo ni mawazo yangu.



Huu ni ukweli kabisa Mwanamalundi, lakini pia kumbuka kuwa hospitali ya Muhimbili ni ya serikali na inaendeshwa na serikali kuu. Kama Kikwete haguswi na hao wanaokufa hapo hospitali basi yeye anaguswa na nini?
 
Huu ni ukweli kabisa Mwanamalundi, lakini pia kumbuka kuwa hospitali ya Muhimbili ni ya serikali na inaendeshwa na serikali kuu. Kama Kikwete haguswi na hao wanaokufa hapo hospitali basi yeye anaguswa na nini?

.. Mwafrika, kikwete hawezi kukwepa lawama kama hizi. Na ndio maana katika nchi za magharibi mambo kama hayo yanapotokea anayewajibika ni waziri anayehusika na hiyo sekta.

Lakini tujitizame na sisi wenyewe tunapofanya kazi. Je tunatimiza wajibu wetu??? Nadhani unakumbuka ulipokuwa Mlimani mkuu wa idara alikuwa anaweza kuikalia dissertation yako kwa miezi kadhaa kabla ya kupelekwa kwa external examiners. Sasa jamani, hapa kweli tatizo ni la waziri wa elimu ya juu au mkuu wa idara???

Kimsingi, nakubaliana na wewe kwamba kikwete hawezi kukwepa hizi lawama. Lakini uongozi wa hospitali unawajibika kwa huu uzembe.
 
.. Mwafrika, kikwete hawezi kukwepa lawama kama hizi. Na ndio maana katika nchi za magharibi mambo kama hayo yanapotokea anayewajibika ni waziri anayehusika na hiyo sekta.

Lakini tujitizame na sisi wenyewe tunapofanya kazi. Je tunatimiza wajibu wetu??? Nadhani unakumbuka ulipokuwa Mlimani mkuu wa idara alikuwa anaweza kuikalia dissertation yako kwa miezi kadhaa kabla ya kupelekwa kwa external examiners. Sasa jamani, hapa kweli tatizo ni la waziri wa elimu ya juu au mkuu wa idara???

Kimsingi, nakubaliana na wewe kwamba kikwete hawezi kukwepa hizi lawama. Lakini uongozi wa hospitali unawajibika kwa huu uzembe.

Shhhhh usiongee kwa sauti kabla Kitila Mkumbo hakusikia na akazuia pepa yangu ya disertation....lol.

Ndugu yangu, katika hili mimi niko radhi kuzuiwa pepa yangu kuliko watu kutumia mabilioni kulipa makampuni ya umeme yasiyo na huduma za hakika na katika hili JK na serikali yake wako full responsible.
 
Kisheria hawa wenye watoto waende mahakamani wadai damages za mabilioni ya pesa kutokana na uzembe wa hospitali na serikali!
 
Kwa mfumo wa Tanzania wa uongozi chini ya CCM
Ni vigumu sana kwa viongozi wa Taasisi fulani kuwa na plan B

Si kweli. Ni uzembe tu. Mbona wana plan B katika familia zao??? Hawa unaowatetea kuwa hawana akili ya kuwa na plan B, ndio hao hao wenye hospitali binafsi, ndio hao hao wanaokusanya pesa kituo cha mabasi ubungo, etc. And here I simply mean private properties. Sasa, iweje inapokuja kwenye issues za umma washindwe kuwa na plan "B".

Ni vigumu sana kwa viongozi wa Taasisi fulani kuwa na plan B kama serikali haijaamua na haioni kama kuna manufaa (kwa wao)

Nadhani hii nimeijibu hapo mwanzoni

na ninaomba ikumbukwe kuwa serikali hii kila kinachofanyia watu wanataka kutumia mwanya huo kujitajilisha, hivyo kama mtu anaota kununua standaby gerenata atapa kitu, hivyo hanunui,
.

Ndio maana nikauliza pale mwanzo, je tunatimiza wajibu wetu??? nadhani jibu unalo


Mimi naomba kuwaeleza hivi, bila hii serikali kufumuliwa na kutengenezwa upya tutakuwa tunapiga mikelele tu hapa, hakuna taratibu za kuongoza serikali na taasisi zake.

Hilo si suluhisho. Kinachotakiwa ni "change in the mindset". Otherwise, there is no shortcut.
 
Si kweli. Ni uzembe tu. Mbona wana plan B katika familia zao??? Hawa unaowatetea kuwa hawana akili ya kuwa na plan B, ndio hao hao wenye hospitali binafsi, ndio hao hao wanaokusanya pesa kituo cha mabasi ubungo, etc. And here I simply mean private properties. Sasa, iweje inapokuja kwenye issues za umma washindwe kuwa na plan "B".



Nadhani hii nimeijibu hapo mwanzoni



Ndio maana nikauliza pale mwanzo, je tunatimiza wajibu wetu??? nadhani jibu unalo



Hilo si suluhisho. Kinachotakiwa ni "change in the mindset". Otherwise, there is no shortcut.

Mwanamalundi, kuhamisha lawama (shift blames) katika hili hapa si kazi rahisi. Ukitaka kila mtu awe responsible kwa kiasi hiki basi kuna haja ya kutoa madaraka yote na uwajibikaji wa serikali katika kuendesha nchi.

Haiwezekani kuwa these guys wachukue pesa ya kodi, wasainie mikataba ya kuuza nchi kwa manufaa yao binafsi na wageni, wasaini mikataba ya kipuuzi kama IPTL na Richmonduli then ikija wakati wa kuwa responsible for their actions basi somebody else abebeshwe lawama.
 
Shhhhh usiongee kwa sauti kabla Kitila Mkumbo hakusikia na akazuia pepa yangu ya disertation....lol.

Ndugu yangu, katika hili mimi niko radhi kuzuiwa pepa yangu kuliko watu kutumia mabilioni kulipa makampuni ya umeme yasiyo na huduma za hakika na katika hili JK na serikali yake wako full responsible.

Mwafrika wewe endelea kunivunja mbavu tu hapa. Lakini tusipokuwa makini tunapoelekea ni kubaya zaidi. Maana hata wahasibu katika wizara ya afya sasa hivi wanapindisha mahesabu yao usiku kucha ili kesho na kesho kutwa wambebeshe lawama zote kikwete. Na wana haki ya kufanya hivyo. Lakini wahasibu hao hao wanaendelea kuporomosha magorofa msasani penisula. Kesho, umeme ukikatika muhimbili, jibu rahisi na la haraka watakalokupa ni RICHMOND.
 
Mwafrika wewe endelea kunivunja mbavu tu hapa. Lakini tusipokuwa makini tunapoelekea ni kubaya zaidi. Maana hata wahasibu katika wizara ya afya sasa hivi wanapindisha mahesabu yao usiku kucha ili kesho na kesho kutwa wambebeshe lawama zote kikwete. Na wana haki ya kufanya hivyo. Lakini wahasibu hao hao wanaendelea kuporomosha magorofa msasani penisula. Kesho, umeme ukikatika muhimbili, jibu rahisi na la haraka watakalokupa ni RICHMOND.

Nakuhakikishia kuwa kama hao wahasibu unaosema wangeona Kikwete akiwachukulia hatua mafisadi katika serikali basi wangejua kuwa hakuna mchezo.

Kama Kikwete mwenyewe anaacha mapapa wa wizi wakipeta kwa wizi katika serikali (anza na Chenge) unategemea nani atakuwa serious katika chochote.

Nasisitiza kuwa kama Kikwete haguswi na watoto wachanga wanaokufa hostpitali kwa kutegemea kuwa kuna watendaji huko basi this is beyond hali ya kawaida ya ubinadamu.

Katika hili I hold Kikwete na serikali yake ya ccm responsible kwanza kabla ya kutafuta mchawi au wale wanaoshikilia pepa za wanafunzi kule mlimani.
 
Hongera sana ndugu JK . Nategemea ndugu Dar Es Salaam utafika hapa kumpa Hongera ndugu Rais kwa mambo yake makubwa haya .Mungu awarehemu hawa watoto .

Ahsante kwa kuniikumbuka, nimefika.

Jee, kama genereta lipo tatizo ni JK? ingekuwa genereta hakuna hapo ndio tungemshutumu Mkuu.

Haya ni makosa ya watendaji na inabidi hatuwa za haraka zifanyike na wachukuliwe hatua za kisheria na kinidhamu kwa makusudi kabisa.

Uozo wa utendaji Muhimbili unaonyesha kukomaa, (nikikumbuka na kisa cha kizembe kabisa cha kuchanganya wagonjwa).
 
Back
Top Bottom