SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,257
Ni tangazo la biashara linalooneshwa kwenye tv na linaibua hisia za mahusiano
kati ya mume na mke, na ndio maana naweka hii thread hapa na si penginepo.
Maudhui ya tangazo yako hivi:
Mume anaingia nyumbani akiwa taabani kwa uchovu. Anajilaza kwenye kochi lililosheheni
mito ya kujipumzisha. Mara anatokea mwanamke (bila shaka mkewe) na bila hata ya kumpa
pole wala nini, anamkumbusha: "Umechukua zile fedha toka benki?" Jamaa anakurupuka
kwenda benki kwa mbio za kimarathon kufuata hela.Anakumbana na madhila ya kunyeshewa
mvua na hela hapati kwani alikuta benki zimefungwa.
Kwa maoni yangu waliobuni tangazo hili, hawakuzingatia uhalisia wa mahusiano kati ya mke na mume.
Mume alipowasili nyumbani nilitarajia mkewe ampokee kwa bashasha ambayo ingehitimishwa
angalau na juisi au kinywaji kingine kidogo. Lakini eti mwanamke anamkaribisha mumewe kwa kumkumbusha
akafuate hela.
Tangazo hili limekosewa sana na watangazaji wa hiyo biashara ya fedha, na ninapata hisia kwamba
they are gender insensitive.
Mlioliona tangazo hili mwasemaje?
kati ya mume na mke, na ndio maana naweka hii thread hapa na si penginepo.
Maudhui ya tangazo yako hivi:
Mume anaingia nyumbani akiwa taabani kwa uchovu. Anajilaza kwenye kochi lililosheheni
mito ya kujipumzisha. Mara anatokea mwanamke (bila shaka mkewe) na bila hata ya kumpa
pole wala nini, anamkumbusha: "Umechukua zile fedha toka benki?" Jamaa anakurupuka
kwenda benki kwa mbio za kimarathon kufuata hela.Anakumbana na madhila ya kunyeshewa
mvua na hela hapati kwani alikuta benki zimefungwa.
Kwa maoni yangu waliobuni tangazo hili, hawakuzingatia uhalisia wa mahusiano kati ya mke na mume.
Mume alipowasili nyumbani nilitarajia mkewe ampokee kwa bashasha ambayo ingehitimishwa
angalau na juisi au kinywaji kingine kidogo. Lakini eti mwanamke anamkaribisha mumewe kwa kumkumbusha
akafuate hela.
Tangazo hili limekosewa sana na watangazaji wa hiyo biashara ya fedha, na ninapata hisia kwamba
they are gender insensitive.
Mlioliona tangazo hili mwasemaje?